Sheria ya salamu ya "Shikamoo"

Sheria ya salamu ya "Shikamoo"

Naamini mko poa humu ndani.

Leo mida ya asubuh wakati naelekea kwnye miangaiko yangu ya hapa na pale bhana, nikapita mita ya karibu na nyumba anayoishi Mzee wetu mwenye nyumba.

Sasa kikukweli alikua mbali sana kiasa cha distance ya kama mita 25 au thelathini tokea nipokua napita Mimi.

Nikaona hapa kama ni kutoa salam ili aiskie bs nipaze sauti sana ndo tuskilizane...basi nikaona sio kesi nikapita kikauzu

Sasa kumbe yeye kanichora tu.

Nimerudi sa hv geto nimemkuta nje ya nyumba yetu aliotupangisha anafanya Fanya usafi.........nikamsalimia...akanikaushia....nikarudia tena kumsalimia aiseee..

Nikashangaa Mzee kawaka "unanisalimia nin wakat asubuhi umenipita bila salam,, siku hz umekua na dharau sana, hvo vimiambili mia mbili vinakuchanganya"

Yani kwa kifupi aliongea kinoma....nikaona niingie zangu ndani tu, ile nimeshangaa sana,

Sasa sijui nyie watu wa humu ndani katika swala LA kutoa shikamoo mnakua mmejiwekea utaratibu gani.
Mana mim mtu akiwa mbali sana siwezaji kupaza sauti kumsalimia kama natangaza salam bhana.



Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ni wazee wafuate tu, jishushe. Kikubwa zaidi msome unayemsalimia yeye ni wa namna gani, kama ni wa kumpungia mkono kwa mbali mpungie tu. Kama ni wa kumfuata jongea kwake.
 
Yeah niko tanga na hiki usemacho huku ndio utamadun kiasi nimezoea,sasa wengine ukiwaambia hiyo salam wanakuona unewadharau wanataka shikamoo wakat haina mana
Tamko "shikamoo" halileti dhambi wala thawabu ni utamaduni uliyojengeka katika sisi miongoni mwa wanajamii, kwa wengine lina maana kwa wengine halina maana. Ndivyo jamii ilivyo, cha msingi ni kutambua mahala husika.

Samahani kama nimekukwaza. Siku njema.
 
Tamko "shikamoo" halileti dhambi wala thawabu ni utamaduni uliyojengeka katika sisi miongoni mwa wanajamii, kwa wengine lina maana kwa wengine halina maana. Ndivyo jamii ilivyo, cha msingi ni kutambua mahala husika.

Samahani kama nimekukwaza. Siku njema.
Sidhani kama umeelewa ulochonikwot! Relax sjakwazika.
 
Siku Rais Magufuli akiwa Morogoro akampigia Dr. Kitila Mkumbo kwa simu huku tukisikia mazungumzo kwenye loud speakers, nakumbuka Mkumbo alimuamkia shikamoo, kuna maswali mengi nilijiuliza toka siku ile.

Nitarudi baadae kujiekezea zaidi.

Majadiliano ya namna hii ni muhimu sana kwenye jamii zetu, tusiyabeze.
 
Niliwahi kuchumbia Mwanza... Eti kisa mchumba wangu ni mdogo ndio nalazimishwa kumwamkia kaka yake katoto kadogo hakalingani hata na mdogo wangu wa 3!

Nikamwambia huyo aliyewaletea hiyo shikamoo aliwapa masharti kwa mdogo amwamkie mkubwa sasa nitaanzaje kukuamkia wewe mdogo wangu wa 4?

Sent from my TECNO-M3 using JamiiForums mobile app
Teh teh teh. Mkuu hilo la kuamkua shemeji yako mdogo lina ukakasi.

Sasa nikuulize, sazingine wanaume huwa tunajitupa tu bila kuangalia urefu wa shimo, kwamba vyovyote itavokuwa!

Sasa unakatokea kasichana moja matata sana, kana sifa unazozitaka wewe awenazo mwanamke.

Unaka'fall in love' na kukachumbia mazima, ni katoto yatima kanaishi kwa baba yake mdogo.

Huyo bamdogo, ambaye ndiyo mkweo mtarajiwa analingana makamo na mwanao wa kwanza.
Shikamoo hutatoa hutoi! Ninakuuliza, utatoa hutoi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paku hama hapo!!!! utakuta nyumba nyingine ndio balaa kabisa akina mama walio na umri mchanganyiko, wanapiga soga mlangoni mwako kelele vicheko na vijembe!! kwenda chooni hapaendeki ndio karibu na walipoweka kijiwe!!! ukisalimia ndio unabadilika kuwa topic ya mjadala ukiuchuna ndio balaa!!!! uswahili ni kazi
 
Hiyo issue shikamoo,umenikumbusha kipindi hicho ndio nimekuja Mwanza, niliwakuta wazee wa kabila kisukuma wamekaa wengi wengi wanaongea story zao, mie sasa nikawaamkia "SHIKAMOONI WAZEE", wale wazee wakaniangalia kwa dharau na mshangao, na mie nikawashangaa. Wakaniita, wee binti hebu njoo hapa, nilivyofika wakanihoji "SISI UMETUONA NI TENGA LA NYANYA ETI?" nikamuuliza kwanini mzee unasema hivyo? akajibu "hivi sisi unaweza kutupatia shikamoo ya jumla kwa wote?"

Kumbe walitaka niwasalimie mmoja mmoja, tena kwa kupiga magoti, kwa mfano:

1. Shikamoo Mzee Mabula
2. Shikamoo Mzee Manoni
3. Shikamoo Mzee Mpuya
4. Shikamoo Mzee Masanja

yaani hadi wote waishe kila mmoja na shikamoo yake, tena kwa kumtaja jina!!!! (ukiwa umepiga magoti)
et matenga ya nyanya....daaahh kweli kila sehemu na taratibu zake....sasa ndo kama unawahi basi stendi ndo linakupigia honi itakuaje hizo salam mpka uzimalize!
 
Kama ni wazee wafuate tu, jishushe. Kikubwa zaidi msome unayemsalimia yeye ni wa namna gani, kama ni wa kumpungia mkono kwa mbali mpungie tu. Kama ni wa kumfuata jongea kwake.
Inategemeana na mda huo ni mda gani na unaelekea wapi? Wengine mishe mishe zetu zina depend sana time....ukichelewa sekunde tu unalala njaaa
 
Tamko "shikamoo" halileti dhambi wala thawabu ni utamaduni uliyojengeka katika sisi miongoni mwa wanajamii, kwa wengine lina maana kwa wengine halina maana. Ndivyo jamii ilivyo, cha msingi ni kutambua mahala husika.

Samahani kama nimekukwaza. Siku njema.
Aiseee
 
Siku Rais Magufuli akiwa Morogoro akampigia Dr. Kitila Mkumbo kwa simu huku tukisikia mazungumzo kwenye loud speakers, nakumbuka Mkumbo alimuamkia shikamoo, kuna maswali mengi nilijiuliza toka siku ile.

Nitarudi baadae kujiekezea zaidi.

Majadiliano ya namna hii ni muhimu sana kwenye jamii zetu, tusiyabeze.
Kwa nini ushangae mkuu.....hiyo ndo asili sahihi ya neno shikamoo...."nipo chini ya miguu yako" ...... Shikamoo hutegemea pande mbili, kiutamaduni wetu ni katika umri mdogo kwa mkubwa, lakin waanzilishi walimaanisha katika upande wa......yule aliekuzid cheo au maisha au anaekutawala kivyovyote vile mpe shikamoo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom