james chapacha
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 939
- 200
Kama waliberali walikasirika kiasi hicho sipati picha wangekuwepo CDM lazima kingewaka tu....
CDM wangekuwepo lazma wangerushiwa bomu!
Kama waliberali walikasirika kiasi hicho sipati picha wangekuwepo CDM lazima kingewaka tu....
Kwani alishapona ule ugonjwa wake wa kulia(hysteria)?anaumwa nini waziri mkuu wetu?
Kama kuagwa si angeagwa kitambo yaani miaka kibao imepita ndio wanamuaga, hapa maana yake 2015 asigombee tena ikiwa kama atakuwa bado yupo interested na siasa zetu (kama vile wamefanya hivyo ili aone noma kugombea)Hiyo ndo CCM ya wachovu wa mawazo aliyoyasema Nyerere kwenye kitabu chake cha "Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania"
Yaani Sitta naye anakubali kufanyiwa sherehe ya kuagwa? Je hizo nazo ni fedha za walipa kodi au michango yao binafsi? Wamesahau kwamba watoto wanakaa chini hakuna madawati na walimu wanawadai, na wagonjwa wanalala wanne wanne kwa kila kitanda? "ama kweli akili za kuambiwa changanya na zako!"
Jana kulikuwa na sherehe za kumuaga Samweli Sitta ,Spika za zamani wa Bunge zilivurigika baada ya Spika wa Bunge na Pinda kuamuru zipigwe nyimbo za Komba na mmojawapo uliopigwa ni ule wa ....wapinzani wakija tuwachanechane tuwatupe... Wimbo huu uliamsha hasira za wabunge wa CUF ambao waliamua kuondoka kwenye sherehe hizo bila kula chakula kilichokuwa kimeandaliwa.
Mbatia naye alitaka kuondoka ila akashikwa mkono na wabunge wa CCM naye bila aibu alirejea kwenye sherehe hizo , ila wabunge wa CUF waliamua kuondoka moja kwa moja pamoja na zawadi waliyokuwa wamemwandalia Sitta.
wabunge wa Chadema ,hawakuwepo hata mmoja.
----------------------------
![]()
Hawa watu wameiharibu kweli CCM! Unaweka wimbo wapinzani wakija tuwachanechane tuwatupe, huku mkielewa bado kuna utata juu ya wahusika wa mlipuko wa bomu huko Arusha lilowachanachana kiongozi wa chama hicho huko Arusha na watoto wadogo. Enzi za mwalimu aliyeamuru wimbo huo upigwe angesahaurika. Mnamuaga Sitta au mnampongeza mlipuaji wa bomu?. Siamini na wala sitaamini kuwa wabunge wote wa CCM hamna akili.Tatizo sio wimbo wa nani ila ni maudhui ya wimbo na hadhira kusudiwa, hivi unaendaje kuweka wimbo wa wapinzani wakija tuwachanechane tuwatupe , kwenye sherehe za kuaga spika aliyekuwa na wabunge wa upinzani na hao wa Ccm? Huu ni ujinga uliopindukia , sasa waliachiwa chakula chao walifurahia kula chote wenyewe?
same to me tangu juz nasoma ishu ya kaugonjwa,liugonjwa,sasa najiuliza anaumwa nini?
Aibu ilioje .... .... ...... zawadi ya television kutoka kwa pesa za walipa kodi? Halafu wanaitangaza kama vile ni kitu cha maana sana, hivi kweli katika karne ya 21 zawadi kama hii inatolewa na kuonyeshwa kwa mamillioni ya walipa kodi wakati huyu Mr. 6 alishindwa kutekeleza wajibu wake na kuiacha serikali kuendelea kutapanya pesa za walipa kodi! Je, alifanya kitu gani cha maana zaidi ya kusimamia kujiuzulu kwa richimonduli na kujirizisha kwa woga? Je, lile hekalu alilojengewa ni zawadi ya aina gani? This country has gone to the dogs.
Huku ndiko kukosa dira ya nini kifanyike kuwawezesha walipa kodi kuinua maisha yao, viongozi wanajipongeza wakati hakuna la maana wanalolifanya bali kujilimbikizia utajiri kutoka migongo ya walipa kodi.
Kuna mtu anaweza kusema ni kwanini CCM wanamuaga Spika (waliyemnyima' kuendelea kukalia kiti cha uspika - kwa sababu za kijinsia) miaka takribani mitatu?
Tangu mwaka 2011 walikuwa wapi? Na kama waliona anafanya kazi nzuri, kwanini walimuondoa?