Sherehe za kumuaga Samweli Sitta zavurugika Dodoma

Sherehe za kumuaga Samweli Sitta zavurugika Dodoma

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2007
Posts
4,132
Reaction score
1,582
Jana kulikuwa na sherehe za kumuaga Samweli Sitta ,Spika za zamani wa Bunge zilivurigika baada ya Spika wa Bunge na Pinda kuamuru zipigwe nyimbo za Komba na mmojawapo uliopigwa ni ule wa ....wapinzani wakija tuwachanechane tuwatupe... Wimbo huu uliamsha hasira za wabunge wa CUF ambao waliamua kuondoka kwenye sherehe hizo bila kula chakula kilichokuwa kimeandaliwa.

Mbatia naye alitaka kuondoka ila akashikwa mkono na wabunge wa CCM naye bila aibu alirejea kwenye sherehe hizo , ila wabunge wa CUF waliamua kuondoka moja kwa moja pamoja na zawadi waliyokuwa wamemwandalia Sitta.

wabunge wa Chadema ,hawakuwepo hata mmoja.

----------------------------

IMG_0080.JPG
 
inaonekana wakiwa kwenye vikao vyao, mishipa ya aibu inaziba kabisa na kujitoa ufahamu.!!
 
Pinda anadhihirisha kuwa bunge sio la jamhuri, ni la ccm. Ndo maana tunaimba nyimbo za ccm na sio za serikali. Hongera mtoto wa settler cum mkulima
 
Hii nyimbo ingekuwa ni ya CUF au NCCR au TLP, DP, UDP ingekuwaje?
 
Jana kulikuwa na sherehe za kumuaga Samweli Sitta ,Spika za zamani wa Bunge zilivurigika baada ya Spika wa Bunge na Pinda kuamuru zipigwe nyimbo za Komba na mmojawapo uliopigwa ni ule wa ....wapinzani wakija tuwachanechane tuwatupe... Wimbo huu uliamsha hasira za wabunge wa CUF ambao waliamua kuondoka kwenye sherehe hizo bila kula chakula kilichokuwa kimeandaliwa.

Mbatia naye alitaka kuondoka ila akashikwa mkono na wabunge wa CCM naye bila aibu alirejea kwenye sherehe hizo , ila wabunge wa CUF waliamua kuondoka moja kwa moja pamoja na zawadi waliyokuwa wamemwandalia Sitta.

wabunge wa Chadema ,hawakuwepo hata mmoja .

Hiyo ndo CCM ya wachovu wa mawazo aliyoyasema Nyerere kwenye kitabu chake cha "Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania"

Yaani Sitta naye anakubali kufanyiwa sherehe ya kuagwa? Je hizo nazo ni fedha za walipa kodi au michango yao binafsi? Wamesahau kwamba watoto wanakaa chini hakuna madawati na walimu wanawadai, na wagonjwa wanalala wanne wanne kwa kila kitanda?
"ama kweli akili za kuambiwa changanya na zako!"
 
Hii nyimbo ingekuwa ni ya CUF au NCCR au TLP, DP, UDP ingekuwaje?
Tatizo sio wimbo wa nani ila ni maudhui ya wimbo na hadhira kusudiwa, hivi unaendaje kuweka wimbo wa wapinzani wakija tuwachanechane tuwatupe , kwenye sherehe za kuaga spika aliyekuwa na wabunge wa upinzani na hao wa Ccm? Huu ni ujinga uliopindukia , sasa waliachiwa chakula chao walifurahia kula chote wenyewe?
 
Pinda ana akili finyu sana ukichanganya na ugonjwa anaoumwa basi ndo anakuwa kama msukule kabisaaa
Wakati Pinda anakaribishwa alianza kwa kusema CCM hoyeee......mara kajishitukia akasema ila kwani hata nikisema hivyo kuna nini si ni salamu zetu? .........hiii ni dalili za wazi jinsi walivyo na chuki za ndani na watu ambao sio CCM .....
 
Nadhani sasa ugonjwa unaadhiri mfumo wa fahamu..msameheni bure...

Haya ni matokeo ya kutopima Afya za watu wanaoteuliwa bila ya kupimwa afya zao; inabidi katiba itamke wazi kuwa wale wanaoteuliwa au kugombea uongozi wa nchi ni lazima wawe wenye kuthibitisha kuwa sio wagonjwa kwa kuleta ripoti za afya zao kama wanavyofanyiwa wale wanaokwenda jeshini!! Bila hivyo tutakuwa tunazidi kushangaa na matamshi yanayotolewa na hawa viongozi wagonjwa.
 
CDM wangekuwepo wasingethubutu kupiga hizo nyimbo... Paka akiondoka, panya anatawala.
Kama waliberali walikasirika kiasi hicho sipati picha wangekuwepo CDM lazima kingewaka tu....
 
Tanzania inamatatizo makubwa ya kiuongozi kuliko tunavyofahamu.
 
Hiyo ndo CCM ya wachovu wa mawazo aliyoyasema Nyerere kwenye kitabu chake cha "Uongozi wetu na Hatma ya Tanzania"

Yaani Sitta naye anakubali kufanyiwa sherehe ya kuagwa? Je hizo nazo ni fedha za walipa kodi au michango yao binafsi? Wamesahau kwamba watoto wanakaa chini hakuna madawati na walimu wanawadai, na wagonjwa wanalala wanne wanne kwa kila kitanda?
"ama kweli akili za kuambiwa changanya na zako!"

Mimi nashangaa sana hii nchi. Hivi ingeshindikana vipi kupiga alambee kuchangia hata madawati, vifaa vya mahospitali hata kwa mkoa mmoja tu kila mwisho mwa wiki? Kweli Tz tuna watawala.
 
Back
Top Bottom