Sheikh wa Wilaya Bagamoyo amkana Lowassa

Sheikh wa Wilaya Bagamoyo amkana Lowassa

Kuna wachumia tumbo wengine wanajiita wasomi nao wameandana leo kwenda kwa EL kumwomba agombee uraisi kesho wasomi wanaweza nao kukanusha wanasema hao walienda kwa EL leo ni wauza mkaa siyo wasomi
 
Hayahayahayaaaaaaaaa namuona sasa komando anaamka tena baada ya kumminiwa risasi kama sabini hivi,

Huyo ndiyo lowasa bwana najiuliza wanafunzi walijuaje kuwa leo atakuwa idodomia hivyo wakajiandaa kumtokezea?

Na je kesho atakuwa wapi ili mapadri na wachungaji wamtokezee, labda itakuwa mbeya,ngoja tuone

Na wakafika kwa muda mmoja, wanafunzi wa vyuo vyote na wamachinga, muda mmoja?nani alikuwa anawakusanya??

Huyu director aongeze ubunifu kidogo.
 
mwaka huu kazi ipo,tutaona kila aina ya sinema, kumbe hao masheikh hawakuwa wametumwa? sasa nani aliwaambia waende kumshauri Lowassa agombee kama Sheikh mkuu wa Bagamoyo kawakana?
 
Mungu yupo upande wetu miaka 10 ya mateso imetosha hawezi kutubebesha msalaba mwingine.

Ngoja nimualike kurugenzi ya mawasiliano ya Lowasa bwana Pasco
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri waliteta hivi
 

Attachments

  • 1427059929871.jpg
    1427059929871.jpg
    97.9 KB · Views: 1,274
Soma hapa tamko la viongozi wa dini jinsi walivyopinga juu ya upotoshwaji wa vyombo vya habari.

View attachment 236919

thanks to CCM...

nchi ishakuwa vipande vipande.

migongano kati ya imani moja dhidi ya nyingine.

ndani ya imani moja pia ni migongano.

kila mahali ni migongano tu.

...all this thanks to CCM!

CCM damu yetu na vizazi vyetu itawalilia kwa miaka 100 ijayo. Mungu aturehemu.
 
Tumesema sana hapa jf kuwa mtu huyu ni hatari na hafai. Ccm mnakazi na wasaka madaraka hasa mafisadi.
 
Tusker...,
Hapana Ahmed Rajab ni mwingine lakini tunafahamiana sana toka Uingereza.
 
Masumbuko...
Naomba nifahamishe nini BAKWATA wamefanya huko Moshi.
 
Mohamed Said,

..vipi leo uko upande mmoja na Shekhe wa Bakwata?

..kwani Mashekhe waliokwenda kwa Lowassa walisema wao ni Mashekhe wa Bakwata?

..pia sidhani kama hili ni suala la Ushekhe, kinachoendelea hapo ni SIASA na harakati za uchaguzi mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Ikumbuke kuwa si kila muislam yupo chini ya Bakwata. Pia wale hawakwenda kwa niaba ya waislam wa Bagamoyo.
 
Pamoja na hizi sinema za EL zinazoendelea kushika kasi lakini bado tunapaswa kujiuliza hao Bakwata ni nani hadi wahitajike kuwatambua masheikh?
 
Mohamed Said,

..vipi leo uko upande mmoja na Shekhe wa Bakwata?

..kwani Mashekhe waliokwenda kwa Lowassa walisema wao ni Mashekhe wa Bakwata?

..pia sidhani kama hili ni suala la Ushekhe, kinachoendelea hapo ni SIASA na harakati za uchaguzi mkuu.

JokaKuu,
Niko upande wa BAKWATA kwa vipi?
Kuhusu masheikh wa Bagamoyo kuwa BAKWATA au vinginevyo...

Inabidi ujue siasa za Bagamoyo toka enzi za kupigania uhuru 1950s
wakati Sheikh Mohamed Ramia akiwa si tu mmoja katika viongozi
wakubwa wa TANU bali alikuwa ndiye Khalifa wa Tariqa Kadiriyya.

Bila ya kujua haya hutaelewa nini kinaendelea sasa na kwa nini
Khalifa wa sasa mtoto wa Sheikh Mohamed Ramiyya kawakana
masheikh hao waliokwenda kwa Lowassa.

Ukitaka kujua ushawishi wa ukoo wa Sheikh Mohamed Ramia katika
siasa za Bagamoyo msome August H. Nimtz Jr, Islam and Politics in
East Africa, University of Miannapolis, 1980.

0


Kushoto: Idd Faiz Mafongo (Mwekahazina wa TANU), Sheikh Mohamed
Ramiyya, Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro, Haruna Taratibu.
Idd Faiz
na Sheikh Ramiyya walikuwa mabinamu.
 
hao masheikh wametambika kwanza Kaole, Caravani Selai, Kaburi la wapendanao, maji ya baraka na kuzunguka mbuyu wa kuongeza uhai huku wakitaja jina la LOWASA!
 
Pamoja na hizi sinema za EL zinazoendelea kushika kasi lakini bado tunapaswa kujiuliza hao Bakwata ni nani hadi wahitajike kuwatambua masheikh?

Mjasiria,
Ukitaka kuwajua BAKWATA na nafasi yao katika siasa za Tanzania inabidi
usome kitabu cha Abdul Sykes Sehemu ya Tatu niliyoipa anuani - "Njama
Dhidi ya Uislam."

Kwa mistari minne mitano hapa Majlis hakuna atakaeweza kuieleza BAKWATA.
 
Back
Top Bottom