Sheikh wa Wilaya Bagamoyo amkana Lowassa

Sheikh wa Wilaya Bagamoyo amkana Lowassa

lol! Mbali na ufisadi kumbe pia Lowassa ni muongo! Dah! Kazi kweli kweli! tabia zake zimefanana sana na DHAIFU, "Pesa za Escrow si pesa za Serikali."

Unajuaje kama hii taarifa haijaandaliwa na Nape!!???
 
Huu ni mwaka wa kuvuna hata kama hukupanda
 
Written By Mohamed Said on Sunday, March 22, 2015 | 11:27 AM




[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD]
Moh%27dSaid_Ramiya_120912_IMG_1367.jpg
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Sheikh Abdulkadir bin Sheikh Mohamed Ramiyya
Sheikh wa BAKWATA wa Wilaya ya Bagamoyo
na Khalifa wa Tariqa Kadiriyya[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Filamu ya Masheikh wa Bagamoyo ilikuwa ishafikia mwisho na wao kama jeshi lilikuwa lishateka nchi na sasa linaondoka likielekea kunakozama jua baada ya kuangamiza adui.

Hii ndiyo ilikuwa staili ya Hollywood kumaliza senema na baada ya mbabe kuelekea machweo ya jua ndipo inatokea ile "The End."

Enzi hizo mimi kijana mdogo niko Empire Cinema macho nimekodoa kwenye, "screen." Senema zetu zilikuwa za mchana siku ya Jumamosi na Jumapili.

Nakumbuka kwa masikitiko makubwa starehe niliyokuwa napata mwisho wa senema kumuona mbabe anondoka juu ya farasi wake kwa ushindi.

John Wayne au Clint Eastwood...


Hii senema ya Masheikh wa Bagamoyo ilikuwa kama vile wameshinda na ni wababe wanaondoka Dodoma kwa ushindi wanatokomea machweo ya jua la Maghrib, lile jua la rangi ya udhurungi.

Haikuwa.

Ghafla mlio wa risasi unasikika.

Kamanda aliyekuwa katangulia na jeshi lake linamfuata nyuma kuelekea machweo ya jua kapigwa risasi ya kichwa kaanguka.

Kinachofatia ni taharuki ya askari wake waliokuwa wanamfuata nyuma.

Risasi nyingine zinaanza kuvuma kila upande jeshi linashambuliwa na askari mmoja baada ya mwingine wanapigwa risasi mfululizo na kuanguka huku wakitoa vumbi kubwa.

Tahamaki jeshi zima limemalizwa.
Hapo ndipo senema inakwisha na ile "The End," inatokea...


Khalifa wa Qadiriyya Sheikh Abdulkadir Ramiyya anazungumza na waandishi wa habari na kuwapa taarifa ya BAKWATA kuwa hawatambui masheikh waliokwenda Dodoma kuonana na Lowassa...

Khalifa kapiga, "ambush."

Watazamaji senema wanapoondoka kuelekea majumbani wanalaumu wanasema, "Mbona hii senama imemalizika vibaya.

"Mimi sipendi mbabe anakufa," mmoja wa waliotazama senema analalamika.
Mimi najiuliza imekuwaje hii "script," imefanywa hivi?

Huyu Muongozaji Filamu anataka kutoa ujumbe gani?
Najisemea kirohoroho.

"Hapendi senema zenye kumalizika kwa furaha?" Jamaa mmoja anasema kwa mshangao.

"Huyu "director," mimi namjua senema zake zote yeye ni "tradegedies," tu. Hapendi kufurahisha watazamaji. Mara kazamisha meli, mara mchumba wake mbabe kanywa sumu, kagongwa na nyoka kafa ili muradi ni "director," mtata sana huyu..."

Kwani nani huyu - Oliver Stone au Spielberg?
Mtu mwingine anauliza.

Bla bla bla bla bla bla...

IMG-20150322-WA0047.jpg



Picha ya Chini: Sheikh Abdulkadir Akizungumza na TV Azam Kuhusu
Masheikh wa Bagamoyo Waliokwenda kwa Lowassa Dodoma


unnamed%2B(72).jpg
 
Huyu mzee akishika nchi si ndo tutanunuliwa na mataifa mengine? Tutauzwa huku tukishangilia
 
hela za lowasa zinaliwa kirahisi sana ! kumbe hata wewe ni mshauri wake ?
Mkuu mimi sio shabiki wa Lowasa na CCM yake kwa ujumla, ukiachilia mbali kuwa mshauri.
Nilikuwa tu najaribu kuangalia mapungufu ya ule waraka wa shehe, unaokanusha taarifa zilizoandikwa na magazeti.
 
Basi lowasa mjinga sana kwanini anafanya mambo ya hovyo kiasi hiki,

Anataka kuipeleka wapi nchi akipata huo urais,

Hajatosheka na ufisadi anafanya uminga mwingine mpuuzi sana.
Hata wewe wamponda Kada wa chama chako? Kwa maana hii pia wakiponda chama chako mwenyewe kilichomkataza kufanya kampeni za chini chini, akapuuza, na kimeshindwa kumuadhibu! Unafikiri mambo haya yanaleta afya kwa chama au magonjwa? Anyway nimejiuliza tu, unaweza nipotezea vilevile.
 
Kweli uhuni ni maelfu wa kutengeneza na sio masheikh
 
we mzee kwa kurembesha maneno tu huna mfano nowe.point yako haikutakiwa kuzidi hata mistari mitatu.hata hivyo asante kwa taarifa.
 
Kweli uhuni ni maelfu wa kutengeneza na sio masheikh
 
...labda kutaka kujionyesha kwamba ana support toka kwa fisadi mwenzie AKA DHAIFU....Urafiki wao si wa kukutana barabarani. Saa hizi watakuwa busy kupanga mikakati ya kupangua hii aibu nyingine kubwa dhidi ya huyu fisadi Lowassa.

Ni aina fulani ya utapeli which in my opinion is criminal. Kwanini Lowasa akachagua Bagamoyo? Eti anaamini wametumwa na rais!
 
...labda kutaka kujionyesha kwamba ana support toka kwa fisadi mwenzie AKA DHAIFU....Urafiki wao si wa kukutana barabarani. Saa hizi watakuwa busy kupanga mikakati ya kupangua hii aibu nyingine kubwa dhidi ya huyu fisadi Lowassa.
Siamini kwamba msafara ule ulikuwa na baraka za Jakaya.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kama Mtu anajiundia "Mashehe" Wake , Then Mashehe hawa wakamuunga Mkono HUYU MTU SI WA KUOGOPA KAMA UKOMA?
 
Hayahayahayaaaaaaaaa namuona sasa komando anaamka tena baada ya kumminiwa risasi kama sabini hivi,

Huyo ndiyo lowasa bwana najiuliza wanafunzi walijuaje kuwa leo atakuwa idodomia hivyo wakajiandaa kumtokezea?

Na je kesho atakuwa wapi ili mapadri na wachungaji wamtokezee, labda itakuwa mbeya,ngoja tuone
 
Back
Top Bottom