Sheikh Ponda akamatwa Dar!

Sheikh Ponda akamatwa Dar!

Mbona watu mnajifanya hampendi udini alafu comments zenu zimejaa udini.

Mimi ni mkristo kutokana na imani ya wazazi na naamini wengi wapo hvyo kwenye imani zao ni wachache sana waliochagua imani zao kidini wengi wamerithi.so divide and rule bdo inatumika.wameleta dini,wameleta vitabu we belive tu.

Hatujui wametoa wapi tunaadithiwa tu.tenda mema tu ndo msingi wa binadamu bora .kabla hawajaja babu zetu waliishi bila hz imani zao sijui mtawahukumu vp?

Ila walikua na adabu na miiko na utu.ndo misingi ya ubinadam.tusigawanywe

Kibwagizo

Divide.jpg
 
Ninachokiona mimi:

(i) Waislamu kwa kiasi kikubwa wamegawanyika sana wao kwa wao. Hakuna ushirikiano hata wa kutekeleza yale yanayoweza kuwasaidia wao kama taasisi. Haiwezekani kwa taasisi kubwa kama ya kiislamu na yenye watu wenye uwezo wawe na chuo kimoja tu na kisichokua (Morogoro). Resources zilizopo mikononi mwa Waislamu ni nyingi sana za kufanya mambo makubwa na kwa muda mfupi – just not organized and if organized, basi zinaishia kujenga miskiti na madras ambazo haziwakomboi waislamu sana kutoka hapo walipo. Makanisa mengi yakijengwa, the next thing ni shule.

(ii) Waislamu, kwa kuwa wako nyuma zaidi kielimu, walipaswa kuishinikiza serikali kutoa elimu bure na bora nchi nzima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne na wakati huo huo kuwashawishi waumini wao kwenda shule. Mwalimu akikosekana shuleni au vifaa visipokuwepo, wadai. Mie sidhani kama on equal education opportunities, swala la nafasi chache serikali litakuwa issue tena. Uganda has tried and is doing very well. Tatizo la wenzetu ni kutukuza elimu ahera na kuidharau elimu dunia, huku wanawake wakipewa nafasi ya mwisho kabisa.

(iii) CCM iache kutumia dini kama mtaji wa kisiasa. Yanayotokea sasa hivi ni matokeo ya CCM kwa nyakati tofauti, kuanzia mwaka 2000 (CUF) na 2010 (CHADEMA) kutumia dini ya kiislamu kama mtaji (both pro and against the opposition). Amani ikikosekana nchini, CCM haiwezi kukwepa lawama. Ukiangalia vita ya Rwanda na Burundi, uhasama haukuanzia miaka ya 1990. Ulikuwepo tangu miaka ya 1930 wakati wa Wabeljiji walipoweka vitambulisho vyenye kuegemea ukabila na kutoa fursa kufuatana na ukabila. Ni jukumu la chama kulichopo madarakani kujenga taifa moja na kuangalia jinsi ya kutoa fursa sawa badala ya kutumia udhaifu uliopo kwa faida ya wachache.
 
Ninachokiona mimi:

(i) Waislamu kwa kiasi kikubwa wamegawanyika sana wao kwa wao. Hakuna ushirikiano hata wa kutekeleza yale yanayoweza kuwasaidia wao kama taasisi. Haiwezekani kwa taasisi kubwa kama ya kiislamu na yenye watu wenye uwezo wawe na chuo kimoja tu na kisichokua (Morogoro). Resources zilizopo mikononi mwa Waislamu ni nyingi sana za kufanya mambo makubwa na kwa muda mfupi – just not organized and if organized, basi zinaishia kujenga miskiti na madras ambazo haziwakomboi waislamu sana kutoka hapo walipo. Makanisa mengi yakijengwa, the next thing ni shule.

(ii) Waislamu, kwa kuwa wako nyuma zaidi kielimu, walipaswa kuishinikiza serikali kutoa elimu bure na bora nchi nzima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne na wakati huo huo kuwashawishi waumini wao kwenda shule. Mwalimu akikosekana shuleni au vifaa visipokuwepo, wadai. Mie sidhani kama on equal education opportunities, swala la nafasi chache serikali litakuwa issue tena. Uganda has tried and is doing very well. Tatizo la wenzetu ni kutukuza elimu ahera na kuidharau elimu dunia, huku wanawake wakipewa nafasi ya mwisho kabisa.

(iii) CCM iache kutumia dini kama mtaji wa kisiasa. Yanayotokea sasa hivi ni matokeo ya CCM kwa nyakati tofauti, kuanzia mwaka 2000 (CUF) na 2010 (CHADEMA) kutumia dini ya kiislamu kama mtaji (both pro and against the opposition). Amani ikikosekana nchini, CCM haiwezi kukwepa lawama. Ukiangalia vita ya Rwanda na Burundi, uhasama haukuanzia miaka ya 1990. Ulikuwepo tangu miaka ya 1930 wakati wa Wabeljiji walipoweka vitambulisho vyenye kuegemea ukabila na kutoa fursa kufuatana na ukabila. Ni jukumu la chama kulichopo madarakani kujenga taifa moja na kuangalia jinsi ya kutoa fursa sawa badala ya kutumia udhaifu uliopo kwa faida ya wachache.
Umewahi kujiuliza ni kiasi gani makanisa hupewa fedha kutoka bajeti ya serikali ya ELIMU na AFYA kutoka mikopo ya nje (Ujarumani).. Watashindwa vipi kujenga shule nyingi ikiwa wao ni sehemu ya serikali acha mbali zinazotoka Vatican na michango mingine duniani. Waislaam wanasubiri hadi mfadhili ajitokeze na akiwa kutoka nchi za Kiarabu tayari siasa zitaingia na atanyimwa kibali..Shule zao ni private hawana msaada wowote kama Shule ya Mwaiposa au Hospital ya Kariuki. Bado unataka ushahidi upi? jamani what wrong with you guyz.. Hivi wewe unaweza kunambia Chadema wanaweza kushindana na CCM ktk uwekezaji?
 
Huo ni uzushi !!!! Kama nchi akitawala Muislamu inakuwa haina amani , mimi sikubaliani na wewe, kikubwa ni kujua hawa Waislamu wanataka nini? Kuna mambo kama ya :-
1.Baraza la Mitihani (NECTA) pamekutwa madudu mengi yamefanywa(Sipendi kuyarudia)
2. Waislamu kutaka wao wajiunge na OIC (Wakristo mpaka leo hamtaki, ila Vatcan ina Ubalozi hapa na misaada mingi inapata toka huko kwa maendeleo ya kanisa)
3. Suala la kadhi mnapinga
4. kuna fungu kubwa la fedha linakwenda kusaidia makanisa na Taasisi zake, waislamu hata sh. 1,000/=
hawapewi
.Hivi kama wewe ungekuwa ni muislamu unaweza kustahamili hali hii? Hatupendi amani ivurugike ila sio kubeza unahitaji mjadala wa kitaifa , HAWA WAISLAMU WANATAKA NINI WAFANYIWE? HAUTASIKIA TENA MALALAMIKO



Kwa hayo ndio wanaenda kuchoma makanisa.
 
tatizo lenu hamuujui uislam bali mnabwabwaja tu na haya yote allah keshatuambia katika quran (hawatokuwa radhi mayahudi na wakristo mpaka muwe kama wao) so tatizo letu hatuko kama nyie ndicho kinachowauma na haitotokea kamwe,mfano nyie dini yenu mnaruhusiwa usenge (ushoga) sisi hatuko ivo. aya nyingine allah anasema (hamtoabudu ninachokiabudu, nyinyi mna dini yenu na sisi tuna dini yetu) kwa mfano mnaabudia sanamu sisi tunamuabudu allah pekee

dini yetu hairuhusu udini kwani hata mtume s a w alikuwa anaihi na makafiri bila kuwabagua, tusiingiliane tu kwenye ibada zetu,
hairuhusu mauaji wala maasi ya aina yoyote kama ushoga n.k, lakini pia hairuhusiwi kudhulumu wala kudhulimiwa
my take: ujueni uislam ndipo mta argue kitu mnachokijua


Hivi kuna wanaohusudu ushoga kuliko kina yakheeee? nani asiyejua ya Tanga,Zanzibar,na Mombasa?
 
Umewahi kujiuliza ni kiasi gani makanisa hupewa fedha kutoka bajeti ya serikali ya ELIMU na AFYA kutoka mikopo ya nje (Ujarumani).. Watashindwa vipi kujenga shule nyingi ikiwa wao ni sehemu ya serikali acha mbali zinazotoka Vatican na michango mingine duniani. Waislaam wanasubiri hadi mfadhili ajitokeze na akiwa kutoka nchi za Kiarabu tayari siasa zitaingia na atanyimwa kibali..Shule zao ni private hawana msaada wowote kama Shule ya Mwaiposa au Hospital ya Kariuki. Bado unataka ushahidi upi? jamani what wrong with you guyz.. Hivi wewe unaweza kunambia Chadema wanaweza kushindana na CCM ktk uwekezaji?

Mkuu wangu sikuelewi,sijuhi ni kukaa ughaibuni kwa muda mrefu ndiko kunasababisha kuwa na fikra za aina hii ama ni chuki!! Wakristo wa Tanzania ya sasa wanajihamasisha wenyewe kujenga shule na zahanati,hawasubiri tena wafadhili wa nje! Huduma za jamii zinazopata ruzuku toka serikalini ni zile zinazohudumia jamii kwa ujumla wake. Mfano ni hospitali teule za wilaya na rufaa na vyuo vya elimu ya juu! Inasikitisha mtu mwenye uelewa wa juu kama wewe unapoongea kama akina Sheikh Ponda!
 
waarabu tunamini kuwa MTI WENYE MATUNDA NDIO UNAORUSHIWA MAWE.

Hongera sana radio Iman, gazeti la An Nur na Ismael Jussa. hakika mpo juu na wengi mnawanyima usingizi.

keep it up na Mola yu nanyi daima.


We mwarabu umefuata nini tanzania? rudi kwenu
 
waarabu tunamini kuwa MTI WENYE MATUNDA NDIO UNAORUSHIWA MAWE.

Hongera sana radio Iman, gazeti la An Nur na Ismael Jussa. hakika mpo juu na wengi mnawanyima usingizi.

keep it up na Mola yu nanyi daima.

Nina mashaka na mheshimiwa fulani uliemtaja hapo juu.
 
Mkuu wangu sikuelewi,sijuhi ni kukaa ughaibuni kwa muda mrefu ndiko kunasababisha kuwa na fikra za aina hii ama ni chuki!! Wakristo wa Tanzania ya sasa wanajihamasisha wenyewe kujenga shule na zahanati,hawasubiri tena wafadhili wa nje! Huduma za jamii zinazopata ruzuku toka serikalini ni zile zinazohudumia jamii kwa ujumla wake. Mfano ni hospitali teule za wilaya na rufaa na vyuo vya elimu ya juu! Inasikitisha mtu mwenye uelewa wa juu kama wewe unapoongea kama akina Sheikh Ponda!
Wewe unayo shule? umejenga hata moja au unazungumza tu ili mradi unataka kufurahisha baraza. Ebu nipe majina ya shule hizo halafu utamjua Mkandara nani haswa katika maswala haya. Nimefanya Homework yangu na kama unakumbuka nilikuwa mbishi sana hapa JF wakati Game Theory akizileta mada hizi hapa lakini nilikwenda deep na kujua ukweli hivyo siongei tu ili mradi..fanya utafiti wako kwanza halafu njoo tujadili na sii kudhania dhania..

Na umesema huduma zote zinazohudumia jamii kwa ujumla ebu nambie shule gani na Hospital gani haihudumii jamii kwa ujumla maana unasema ovyo hata Agakhan au Hindu Mandal zinahudumia jamii zote na hawapati ruzuku.. Tafuta jingine..
 
Hacha kulalamika, waislaam hata mkipewa hela mtaishia kuoana na kuponda starehe kama afanyavyo mzee kijana katuharibia kila kitu kwa sababu ya tamaa na udhaifu wake, mwisho mnaishia kukaa vijiweni na kulala misikitini. Sijui wakristo wakihamua nao kuchoma hiyo misikiti mtalala wapi???
 
M4c imeshasahaulika. Nashuru mungu ilikuwa upepo
 
HAKI unaipigania kwa kuchoma kanisa?kuna mkristo yeyote alishawah kuja kwako akakudhuru?mimi nachukulia hayo maneno yako km wivu wa kike tu,ukimuona mwanamke mwenzio ana kazi,nzuri,anapendeza unammaind bila kisa..Jipangeni,adui wa umaskini wenu au ugumu wa maisha umeletwa na serikali na wala c wakristo coz ugumu wa maisha tunaupata wote wala haubagui.au masoko mnayoenda nyie wakristo hawaendi?

Asante kwa ujumbe wako. Mie sipo kwenye kutukanana. Muke,suala la kanisa kuchomwa ni matokeo ya tukio fulani ambalo linakuwa limefanywa na watu wa Imani hiyo. Kwanza kabisa nikuweke sawa haipo kisheria wala kibinadam kuchoma nyumba ya Ibada ya mtu wa Imani nyingine hilo liko wazi. Tatizo linakuja je nani kasababisha makanisa yachomwe? nadhani kwa mzalendo hili litakuwa swali la msingi sana. Kwa ninavyofaham mimi waislam baada ya tukio la yule kijana wa form2 kukojolea Qur'an wala hawakwenda moja kwa moja kuchoma makanisa,mtoto alipelekwa kwenye vyombo vya sheria na kule ndiko udwanzi/uzembe ulikofanyika mpaka yakatokea yaliyotokea.
Sasa mimi na wewe tulitakiwa kwa pamoja kwanza tuchukizwe na kitendo alichokifanya huyo kijana na tukemee kwa vijana wengine wa kikirsto wasije wakakitenda tena, kwani kinaibua migongano ya kiimani baina yetu na umoja wetu kuporomoka na chuki baina yetu kuwa kubwa, ama pili kwa pamoja tuilaumu police kwa kila siku kukosea katika kuyaendea mambo ya kijamii.

Ushauri wangu kwa viongozi wa kiroho:
Matukio ya kuchana ,kukojolea,kuemea mate, kukanyaga na matusi kwa waislam ni vitendo ambavyo mazingira yake huonesha viongozi pia wanahusika kwa kuwafundisha zaidi waumini wao chuki dhidi ya waislam, nashauri waache kwani pakivurugika na wao watakuwa wahanga.
Mie sijawahi sikia hata siku moja eti muislam kadhihaki biblia. Naomba mtu yeyote anayejua vurugu zozote zilizowahi tokea zinazogusa mambo ya kiimani na chanzo cha vurugu hizo wakawa ni waislam anikumbushe.
 
Serikali yetu inafanya kazi kwa mtindo wa zima moto. Yakiisha ya Mbagala, hakuna mwenye busara ya kutabiri yatakayotokea Kigogo.

Ponda sio chanzo cha tatizo, tatizo ni kubwa zaidi ya Ponda.
 
Acheni kudanganya wenzenu enyi majirani zetu. Ponda akikamatwa, au akifanyiwa uhalifu wowote hata kwa bahati mbaya. Kitakachotokea matahadithia kwa miaka hamsini mingine kwa wale watakao kua hai.

Kumbekeni nini kilitokea mombasa baada ya kupigwa risasi kwa sheikh aboud rogo, na watu eti wasiojulikana. Vijana wa kiisalamu walichukua mwili wa marehemu na kwenda kumzika kimya kimya. Walipo rudi, nadhani mlisikia nini kilichotokea. Ilibidi waombwe wazazi wa kiislamu kuwazuia watoto wao.

Yaani kama kuna maadui wa kiislamu wanaojidai kupambana na uislamu, basi jueni vijana wa kiislamu wao wamepinda zaidi. Endeleeni kuwachokoza. Kama uliangalia vizuri, zile vurugu za mbagala ziliongozwa na watoto wa madrasa tu.

Sasa mkamateni sheikh ponda, ndio mtawajua kaka zao wale watoto wa madrasa.

Ponda hayuko juu ya sheria. Anaweza kuitwa kuhojiwa wakati wowote ili kuweka jambo bayana. Hivyo mnavyo shangilia kua kakamatwa huo upotofu wa taarifa.

Ponda haongei uchochezi. Anaongea kwa hoja na ndio maana sheria haiwezi kumtia hatiani. Kuweni waelewa.

Kama ponda angekamatwa kwa staili hiyo, saa hizi tungekua tunaongea habari nyingine. Waislamu wote tunajua wajibu wetu katika kuwalinda viongozi wetu.
Wako tunao tumia busara katika hili, lakini wapo vijana wao ni kazi pale wanapo amrishwa.

Hii nchi tusipo kua na adabu na nidhamu, juu ya imani na tofauti zetu, basi msishangae tukigawana milango na madirisha.

Hatupendi tufike huko, lakini hatuko tayari kua second citizen katika nchi tulio ipagania. Mlicho tufanyia ni sawa sawa na kumtu kukuomba lifti, na wewe unampa kwa roho mmoja kama binadamu mwenzako, kumbe ni jambazi. Bahati nzuri tumeshtuka, before it is too late.

Sasa ukitaka kujua ladha ya sumu onja.

Mkuu, hata mkichoma makanisa yote hakuna siku mtaona mkristo anaenda kuchoma msikiti in revenge. It is below their dignity, na dini yao imekataza revenge 'as revenge belongs to the Lord'.

Hata mkiwaburuza wakristo na kuwauwa au kuchoma nyumba zao na biashara zao, hakuna siku mtaona wakristo wakifanyia waislamu maovu. it is below their dignity. You are mistaken ku assume ya kwamba kila mtu asiye kuwa muislam ni mkristo, ati chochote kikifanywa na mtu asiye kuwa muislam kitakuwa ni mkristo amekifanya kwa hiyo lazima wakristo to suffer for it. That is petty and uonevu.

Duniani kuna imani nyingi na watu wengi zaidi hawafuatilii imani za kidini. Waislamu kuwa wanawachukulia wakristo kama adui siku zote ni kitu hakielezeki, it makes no sense. Labda utueleze wewe kwa kuwa unaonekana kuna kitu unachokifahamu. Nyie mnao hubiri fujo mtawatoa waislamu wapenda amani kwenye hiyo dini. Hakuna siku mtaona wakristo au dini yeyote ikiandamana against waislamu au dini nyingine. Inafaida gani? Mkristo hana ubaguzi lakini nyie mna leta kwamba dunia yote is against Islam. For what? Kwani kuna mtu amekatazwa kuwa muislam kama akiona inafaa?

Amani Tanzania is at risk kwasababu ya watu kama wewe. Ni bora vita vya ukabila kuliko vya dini na wanaofaidi hizi fujo sio waislamu au wakristo, ni walala hoi ambao hata dini hawaijui na hawana kazi za kufanya ila kutafuta nafasi za kufanya looting. Acheni chuki isio kuwa ya kibinadamu na isio kuwa na sababu za msingi.
 
Asante kwa ujumbe wako. Mie sipo kwenye kutukanana. Muke,suala la kanisa kuchomwa ni matokeo ya tukio fulani ambalo linakuwa limefanywa na watu wa Imani hiyo. Kwanza kabisa nikuweke sawa haipo kisheria wala kibinadam kuchoma nyumba ya Ibada ya mtu wa Imani nyingine hilo liko wazi. Tatizo linakuja je nani kasababisha makanisa yachomwe? nadhani kwa mzalendo hili litakuwa swali la msingi sana. Kwa ninavyofaham mimi waislam baada ya tukio la yule kijana wa form2 kukojolea Qur'an wala hawakwenda moja kwa moja kuchoma makanisa,mtoto alipelekwa kwenye vyombo vya sheria na kule ndiko udwanzi/uzembe ulikofanyika mpaka yakatokea yaliyotokea.
Sasa mimi na wewe tulitakiwa kwa pamoja kwanza tuchukizwe na kitendo alichokifanya huyo kijana na tukemee kwa vijana wengine wa kikirsto wasije wakakitenda tena, kwani kinaibua migongano ya kiimani baina yetu na umoja wetu kuporomoka na chuki baina yetu kuwa kubwa, ama pili kwa pamoja tuilaumu police kwa kila siku kukosea katika kuyaendea mambo ya kijamii.

Ushauri wangu kwa viongozi wa kiroho:
Matukio ya kuchana ,kukojolea,kuemea mate, kukanyaga na matusi kwa waislam ni vitendo ambavyo mazingira yake huonesha viongozi pia wanahusika kwa kuwafundisha zaidi waumini wao chuki dhidi ya waislam, nashauri waache kwani pakivurugika na wao watakuwa wahanga.
Mie sijawahi sikia hata siku moja eti muislam kadhihaki biblia. Naomba mtu yeyote anayejua vurugu zozote zilizowahi tokea zinazogusa mambo ya kiimani na chanzo cha vurugu hizo wakawa ni waislam anikumbushe.
Pole sana. Upande wa pili ungekuwa na busara kama zenu za munkari amani ya nchi hii ingekuwa imeshatoweka muda mrefu. Tatizo waislam mnajiona kama mna leseni ya kukashifu dini za watu wengine na mkiambiwa mnasema mnawaelimisha. Yule Salman Rushdie mlitaka kumfanyaje alipotoa kitabu chake cha Satanic verses? Sasa imagine kiongozi yeyote wa kikristo awe padre/mchungaji aanze kufanya mihadhara na kuchambua Qoran hadharani labda na kusema kuna aya za shetani...waislam mta react vipi? Lakini kwenu nyie hakuna tatizo kwa shehe kusimama na Biblia mkononi na kuanza kuitafsiri anavyojua yeye...mara oh Yesu siyo Mungu na mambo mengine. Sijui mtu ukishakuwa muislam automatically unapata hitilafu kwenye mfumo wa kufikiri maana ni waislam wachache sana wenye busara ya kuheshimu dini za wengine. Pita mwenge , ubongo na manzese uone mashehe wenu wanavyofanya...najua utasema wanaelimisha...
 
Mnaongea sana, wengine mnakejeli sijui waislamu wavivu, hawajasoma, wanalala misikitini tu,wanafundisha elimu akhera, ongeeni mtakachosema lkn. Swali ni Waislamu wanataka nini?
 
Umewahi kujiuliza ni kiasi gani makanisa hupewa fedha kutoka bajeti ya serikali ya ELIMU na AFYA kutoka mikopo ya nje (Ujarumani).. Watashindwa vipi kujenga shule nyingi ikiwa wao ni sehemu ya serikali acha mbali zinazotoka Vatican na michango mingine duniani. Waislaam wanasubiri hadi mfadhili ajitokeze na akiwa kutoka nchi za Kiarabu tayari siasa zitaingia na atanyimwa kibali..Shule zao ni private hawana msaada wowote kama Shule ya Mwaiposa au Hospital ya Kariuki. Bado unataka ushahidi upi? jamani what wrong with you guyz.. Hivi wewe unaweza kunambia Chadema wanaweza kushindana na CCM ktk uwekezaji?



Sie toka tukiwa wachanga tunafundishwa KANISA LITAJENGWA NA WENYE MOYO,
maana ikitokea issue zinazohusu Nyumba ya Mungu au kazi yoyote ya Mungu hata mtoto mdogo anachangia, hayo yako hata kwenye vitabu vyetu vya dini ... Pamoja na UPENDO ambayo niyo amri yetu iliyokuu ndo maana unaona vitu vinaendaa... waambie wachome tu makanisa hela tunayo tutaijenga madhabahu ya Bwana kwa SIKU TATU..
MUNGU TUNAE, NA MUNGU WETU NI TAJIRI ... SIJUI MISIKITI NAYO IKIANZA KUCHOMWA ITACHUKUA MUDA GANI KUJENGWA?

ANYWAY VITA VYETU SI VYA NYAMA NA DAMU NI VYA KIROHO ZAIDI... NA PALE MUNGU ATAKAPO TUTUMA TUKAPIGANE NANYI TUTASHINDA KWANI HATUTUMII SILAA NI MATARUMBETA TU KUTA ZINAPASUKA NA MAPAMBIO TU MAGEREZA YANAFUNGUKA.
 
Halafu kinachoshangaza wanapigia dini debe la nje... Dini ya mtu ni ndani ya moyo wake, huwezi kumlazimisha mtu awe muislamu kwa kuchoma makanisa ... Ndo kwanza hata wale walioingia wataona walifanya uchaguzi usio sahihi..... Hao wakristo mnaowachukia wengi wao ndo wanaowatibu, wanaowafundisha, wanao walisha, waliowaajiri.. Hata tukiwapa hospital zote na shule zote zitakufa...
Mnadanganywa na watu wachache bila kupima mambo...
 
umewahi kujiuliza ni kiasi gani makanisa hupewa fedha kutoka bajeti ya serikali ya elimu na afya kutoka mikopo ya nje (ujarumani).. Watashindwa vipi kujenga shule nyingi ikiwa wao ni sehemu ya serikali acha mbali zinazotoka vatican na michango mingine duniani. Waislaam wanasubiri hadi mfadhili ajitokeze na akiwa kutoka nchi za kiarabu tayari siasa zitaingia na atanyimwa kibali..shule zao ni private hawana msaada wowote kama shule ya mwaiposa au hospital ya kariuki. Bado unataka ushahidi upi? Jamani what wrong with you guyz.. Hivi wewe unaweza kunambia chadema wanaweza kushindana na ccm ktk uwekezaji?

ulishawahi kwenda kutibiwa huko au kupeleka mtoto kusoma huko ukaulizwa cheti cha kubatizwa?? Serikali inatoa ruzuku pale ambapo kama hospital imeanzishwa na dini yeyote ina hadhi ya kuitwa hospital ya rufaa au wilaya ili serikali isiangaike kujenga nyingine ina weka waganga wake pale na kusaidiana kwenye uendeshaji... Sasa nyie ziko ngapi ili tuzipigie kelele bungeni zipewe ruzuku???
Wenzako inakuwepo then unapewa ruzuku... Wewe unataka serikali ijenge halafu uiite ya bakwata???
 
Back
Top Bottom