Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 23,283
- 33,881
Yamakagashi,Hivi wewe mzee haunaga stori nyingine zaidi ya hizi ,kila siku waislamu na uhuru .....Waliofanya mapinduzi Zanzibar ni kina nani ? Mbona haijawahi kutokea Rais wa Zanzibar Mkristo ?
Yaani unavyo ongelea hili swala la Waislamu na uhuru utafikiria nchi hii haikuwa na watu wa dini nyingine walikuja baada ya kupata Uhuru sijui ulioletwa na Waislamu
Sijui kizazi chako utakuwa umewalisha sumu kiasi gani
Mbona unaanza kwa lugha kali isiyo na adabu na kujawa na ghadhabu?
Ikiwa ushakiri kuwa mie ni mzee wajibu wako wewe ikiwa ni kijana ni
staha si matusi.
Nina stori nyingi sana mbali na mchango wa Waislam katika uhuru wa
Tanganyika.
Nimealikwa kwingi duniani kuzungumza historia hii ambayo wewe kwa
bahati mbaya inakuchoma.
Na hii kuchomwa na historia hii hauko peke yako.
Miaka 50 iliyopita palifanyika njama ya kuifuta kabisa historia hii isiwe
historia ya Tanganyika.
Hawa walikuwa wakichonotwa na historia hii kama wewe hii leo hapa
inavyokutaabisha.
Lakini huna sababu ya wewe kujiumiza nafsi yako.
Ikiwa wewe unakereka na historia hii pita usisome kwani hujalazimishwa
na mtu yoyote kunisoma.
Lakini ukweli utabakia kuwa historia hii inapendwa sana na wengi na ndiyo
pita utaona ikiwa sijatokea watauliza Mzee Mohamed mbona yuko kimya?