Nsaji Mpoki
JF-Expert Member
- Nov 5, 2007
- 396
- 65
RIP Sheikh Gorogosi!
Duh GT mkuu hata kama humpendi kiasi hicho haifai ndugu yangu.. Tunajua Bakwata ni sumu ya Waislaam lakini inapofikia kifo mkuu wangu basi hata sema - Bwana ndiye aliyetupa, Bwana ametwaa (Ina Lillah wa ina Ilaihi Rajiun) inatosha...
Mungu aiweke roho ya Marehemu Sheikh Gorogosi mahali pema peponi.Amen. TBC 1 wametangaza katika habari kwa ufupi ya saa 10 kamili.
bwana Muyaka anaendelea kusema hivi:Thread inahusu taarifa ya kifo..wengine badala yake wanafanya hii kuwa sehemu ya swearing kana kwamba wao hawataonja mauti.
haya hebu tuonyeshe wapi watu wameswear?
GT, surely unaweza kutafuta sehemu nyingine to settle the score, hpa ni kushoto kidogo mkuui HOPE SERIKALI HAITOTUMIA KODI ZETU KUGHARAMIA MAZISHI YAKE MAANA HAKUAJIRIWA NA SERIKALI
WAPO AKINA MENGI AMBAO NAJUA WATAJITOLEA KWA KILA HALI INCLUDING KUONYESHA MAZISHI LIVE KWENYE ITV
G.T,kwa waislam siku yake ya peponi bado kwa sababu itabidi kwanza afufuliwe siku ya kiama kisha asomewe mashtaka yake hapo ndio itaamuliwa ataenda FIN'AARI JAHANAM au vipi
the bottom line huyu huwezi kumfananisha na al Marhum sheikh NURDIN SHADHLY au HEMED BIN JUMAA BIN HEMED kwani pamoja na mambo mengine wao walikuwa wamebobea kwenye EI'LM tofauti na Gorogosi
Thanks mkuu, hii ungeituma kama report tungeifanyia kazi haraka kuliko kuandika kama post.Halisi/Invi..rekebisha opening sentence, kifo kisomeke tangu mwanzo
unaanza ku sound kama mgala mambo haya umeyaanza lini?
thanks a lot for the news!_____________________________
Reported Earlier:
Kuna taarifa kuwa Sheikh Gologosi kapata ajali mbaya muda si mrefu. Hatuna uhakika wa maisha yake, tuombe Mungu. Tunafuatilia usahihi wa taarifa husika.
_____________________________
Update 1.
Confirmed:
Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki katika ajali mbaya akiwa katika safari kusini mwa Tanzania. Aliondoka Dar leo kwa ndege kwenda Lindi kupitia Mtwara, akashuka na ndege mtwara kwenda Lindi gari ikapasuka tairi la mbele.
Mwenye miwani ndiye marehemu Sheikh Suleiman Gologosi akiwa kwenye mahafari ya shule ya Sekondari Jitegemee Oktoba 2007
Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiwa kwenye mkesha wa Maulid katika viwanja vya Mnazi Mmoja usiku wa kuamkia leo. Kulia ni kaimu Mufti Sheikh Suleiman Gologosi.
********************
Update 2.
Marehemu alikuwa akitokea Mtwara kwenda Lindi na kwenye gari walikuwa watatu, marehemu na abiria mwingine mmoja pamoja na derava wao aliyetambulika kwa jina la Maguo aliyewahi kuwa mfanyakazi wa Bandari (Mtwara).
Marehemu alifariki papo hapo na abiria mwingine na dereva walikimbizwa kwenda Hospitali.
Gari walilokuwa wanatumia ni T968ARC Toyota Land Cruiser Prado ambalo liliacha njia na kupinduka.
********************
Update 3.
Aliyekuwa anaendesha gari (dereva) ndiye mmiliki wa gari hilo na aliwahi kushiriki mchakato wa kugombea kiti cha ubunge Lindi kwa ticket ya CCM mwaka 2005 na akashindwa kwenye kura za maoni na mpaka sasa alikuwa anafanya kampeni za chinichini kujiimarisha ili agombee tena.
Majeruhi mwingine (abiria) ametambulika kwa jina la CPT Aboubakar Fundi lakini haijathibitishwa kama bado ni askari wa JWTZ au kishastaafu.
Bado haijathibitika majeruhi wamekimbizwa hospitali ya Mission Nyangao au ile ya mkoa wa Lindi.
Mwili wa marehemu umeondolewa dakika chache zilizopita kwenye eneo la tukio na askari polisi na inaelekea wanaupeleka Hospitali ya mkoa wa Lindi.
Marehemu alikuwa pia ndiye Sheikh mkuu wa mkoa wa Lindi.