Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
_____________________________
Reported Earlier:
Kuna taarifa kuwa Sheikh Gologosi kapata ajali mbaya muda si mrefu. Hatuna uhakika wa maisha yake, tuombe Mungu. Tunafuatilia usahihi wa taarifa husika.
_____________________________
Update 1.
Confirmed:
Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki katika ajali mbaya akiwa katika safari kusini mwa Tanzania. Aliondoka Dar leo kwa ndege kwenda Lindi kupitia Mtwara, akashuka na ndege mtwara kwenda Lindi gari ikapasuka tairi la mbele.
Mwenye miwani ndiye marehemu Sheikh Suleiman Gologosi akiwa kwenye mahafari ya shule ya Sekondari Jitegemee Oktoba 2007
Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiwa kwenye mkesha wa Maulid katika viwanja vya Mnazi Mmoja usiku wa kuamkia leo. Kulia ni kaimu Mufti Sheikh Suleiman Gologosi.
Reported Earlier:
Kuna taarifa kuwa Sheikh Gologosi kapata ajali mbaya muda si mrefu. Hatuna uhakika wa maisha yake, tuombe Mungu. Tunafuatilia usahihi wa taarifa husika.
_____________________________
Update 1.
Confirmed:
Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki katika ajali mbaya akiwa katika safari kusini mwa Tanzania. Aliondoka Dar leo kwa ndege kwenda Lindi kupitia Mtwara, akashuka na ndege mtwara kwenda Lindi gari ikapasuka tairi la mbele.
Mwenye miwani ndiye marehemu Sheikh Suleiman Gologosi akiwa kwenye mahafari ya shule ya Sekondari Jitegemee Oktoba 2007
Rais Mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi akiwa kwenye mkesha wa Maulid katika viwanja vya Mnazi Mmoja usiku wa kuamkia leo. Kulia ni kaimu Mufti Sheikh Suleiman Gologosi.
********************
Update 2.
Marehemu alikuwa akitokea Mtwara kwenda Lindi na kwenye gari walikuwa watatu, marehemu na abiria mwingine mmoja pamoja na derava wao aliyetambulika kwa jina la Maguo aliyewahi kuwa mfanyakazi wa Bandari (Mtwara).
Marehemu alifariki papo hapo na abiria mwingine na dereva walikimbizwa kwenda Hospitali.
Gari walilokuwa wanatumia ni T968ARC Toyota Land Cruiser Prado ambalo liliacha njia na kupinduka.
********************
Update 3.
Aliyekuwa anaendesha gari (dereva) ndiye mmiliki wa gari hilo na aliwahi kushiriki mchakato wa kugombea kiti cha ubunge Lindi kwa ticket ya CCM mwaka 2005 na akashindwa kwenye kura za maoni na mpaka sasa alikuwa anafanya kampeni za chinichini kujiimarisha ili agombee tena.
Majeruhi mwingine (abiria) ametambulika kwa jina la CPT Aboubakar Fundi lakini haijathibitishwa kama bado ni askari wa JWTZ au kishastaafu.
Bado haijathibitika majeruhi wamekimbizwa hospitali ya Mission Nyangao au ile ya mkoa wa Lindi.
Mwili wa marehemu umeondolewa dakika chache zilizopita kwenye eneo la tukio na askari polisi na inaelekea wanaupeleka Hospitali ya mkoa wa Lindi.
Marehemu alikuwa pia ndiye Sheikh mkuu wa mkoa wa Lindi.
Update 2.
Marehemu alikuwa akitokea Mtwara kwenda Lindi na kwenye gari walikuwa watatu, marehemu na abiria mwingine mmoja pamoja na derava wao aliyetambulika kwa jina la Maguo aliyewahi kuwa mfanyakazi wa Bandari (Mtwara).
Marehemu alifariki papo hapo na abiria mwingine na dereva walikimbizwa kwenda Hospitali.
Gari walilokuwa wanatumia ni T968ARC Toyota Land Cruiser Prado ambalo liliacha njia na kupinduka.
********************
Update 3.
Aliyekuwa anaendesha gari (dereva) ndiye mmiliki wa gari hilo na aliwahi kushiriki mchakato wa kugombea kiti cha ubunge Lindi kwa ticket ya CCM mwaka 2005 na akashindwa kwenye kura za maoni na mpaka sasa alikuwa anafanya kampeni za chinichini kujiimarisha ili agombee tena.
Majeruhi mwingine (abiria) ametambulika kwa jina la CPT Aboubakar Fundi lakini haijathibitishwa kama bado ni askari wa JWTZ au kishastaafu.
Bado haijathibitika majeruhi wamekimbizwa hospitali ya Mission Nyangao au ile ya mkoa wa Lindi.
Mwili wa marehemu umeondolewa dakika chache zilizopita kwenye eneo la tukio na askari polisi na inaelekea wanaupeleka Hospitali ya mkoa wa Lindi.
Marehemu alikuwa pia ndiye Sheikh mkuu wa mkoa wa Lindi.
Last edited by a moderator: