Shaka amvaa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar; "Haiwezekani unahoji leo ushindi wa CCM ukiwa sehemu ya Serikali unahudumiwa kwa kila kitu''

"Kuna watu wanasema eti Dkt. Hussein Mwinyi ameshinda kwa wizi, wanasahau kuwa CCM ni Chama kikubwa, kina mipango, uratibu unaeleweka, atambue msemaji wa hayo amehifadhiwa na kusitiriwa na Serikali ya CCM na sivinginevyo"

"Haiwezekani unahoji leo ushindi wa CCM ukiwa sehemu ya serikali unahudumiwa kwa kila kitu, kula tunakupa sisi, Ving'ora vya kumsafishia njia akitembea tunampa sisi, Nguo ya kuazima......1.

Tatizo lake amekaribishwa ukumbini (sebuleni) analazimisha kuingia chumbani, wanajisahau waache chokochoko, tunataka Wazanzibar waendeleze umoja na mshikamano asiyeweza akae pembeni apishe wengine "- Mwenezi wa CCM Taifa jana Zanzibar
huyu dogo aache upumbavu, yani ni mpumbavu kweli kweli
 
Huyo makamu nadhani mind set yake haijabadilika , Bado ana act kama mwanaharakati na sio kiongozi,

Hata ishu ya masheshe wa uamsho nilishangaa sana comment yake, kwa nafasi yake alikua anahamasisha raia wachangie masheshe anasahau kwamba yeye tayari ni sehemu ya serikali ambao ndio wasimamia sheria. Afadhali angesema hata Kwa kificho ila katoa maoni hayo publicly.
 
Usitutishe!!!!😅😄😃😂😂😀😀😆😆😅
Ccm Inamfokea Mtu Hivyo
 
Huyo makamu nadhani mind set yake haijabadilika , Bado ana act kama mwanaharakati na sio kiongozi,

Hata ishu ya masheshe wa uamsho nilishangaa sana comment yake, kwa nafasi yake alikua anahamasisha raia wachangie masheshe anasahau kwamba yeye tayari ni sehemu ya serikali ambao ndio wasimamia sheria. Afadhali angesema hata Kwa kificho ila katoa maoni hayo publicly.
Kala Maharage Ya Wapi??
Ndiyo Viongozi Mizigo
 
MUULIZE ZANZIBAR NI NCHI AU SIYO NCHI.
Majibu kwa makamu wa kwanza
 
"Kuna watu wanasema eti Dkt. Hussein Mwinyi ameshinda kwa wizi, wanasahau kuwa CCM ni Chama kikubwa, kina mipango, uratibu unaeleweka, atambue msemaji wa hayo amehifadhiwa na kusitiriwa na Serikali ya CCM na sivinginevyo"

"Haiwezekani unahoji leo ushindi wa CCM ukiwa sehemu ya serikali unahudumiwa kwa kila kitu, kula tunakupa sisi, Ving'ora vya kumsafishia njia akitembea tunampa sisi, Nguo ya kuazima......1.

Tatizo lake amekaribishwa ukumbini (sebuleni) analazimisha kuingia chumbani, wanajisahau waache chokochoko, tunataka Wazanzibar waendeleze umoja na mshikamano asiyeweza akae pembeni apishe wengine "- Mwenezi wa CCM Taifa jana Zanzibar
Hao wote ni watoto wa baba familia moja
 
Huyo makamu wa rais anajielewa na sio mnafki
Alichosema ni kweli Mwinyi hakushinda
Namkumbuka kwenye bunge maalumu la katiba Mpya lililoharibiwa na maccm akiwa kama mwanasheria mkuu wa Zanzibar alipiga kura kutaka Serikali Tatu kinyume cha wanafki wengine wa ccm
 
Kazi ipo! Inawezekana huyo makamu wa rais anapewa kila kitu ila hapangiwi majukumu wala kushirikishwa mipango ya serikali, hivyo na yeye anaamua kuleta chokochoko ili akumbukwe kwamba, na yeye yupo.

Siasa ni mchezo mchafu!
 
Shaka anashindwa kutofautisha Ccm na Serikali. Huyo makamu yupo hapo kikatiba na sio kwa hisani ya Çcm. Makamu analipwa na Serikali sio Ccm.
 
Back
Top Bottom