Ni wazi kamati kuu ya CCM ilikaa kwa dharura kujadili kauli ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Kauli aliyotoa Makamu wa kwanza wa Rais alipokuwa Pemba ilikuwa kauli nzito iliyoashiria kuvunjika kwa mashirikiano yaliyopo. Kauli ile ilieleza wazi dhamira yake ya kutoendelea na madaraka kwenye kundi la watu wasioridhika na ambao hawana uchungu na watu kufa, kuwa vilema nk. Alihoji watu wanatafuta madaraka ya Nini? Wameua na kuumiza watoto ikiwemo ubakaji lakini bado awajaridhika, Wakati vidonda vikiwa vibichi watu wale wale kwa kutumia tume ile ile wanakwenda tenda kwa wahanga walewale wakuiba uchaguzi. Wanatafuta Nini?

Bila kuficha hisia zake aliwaomba waislam wakae na watafakari namna ya kuponya majeraha na kwamba anakubaliana na Serikali ya Kitaifa kwa 100% ila yeye hatokuwa sehemu ya Serikali hiyo.

Naamini kauli ile kwa uzito wake na kwa ninavyo mfahamu ndugu yangu Zitto haikuwa kauli ya chama Bali msimamo binafsi na kwa kutambua hilo Zitto amekaa kimya kwa muda mrefu bila kuwa na harakati za siasa mitandaoni kama kawaida.

Lakini waliosumbuka zaidi ni Chama cha Mapinduzi na kupelekea kuitana kwa dharura na kisha kumwelekeza mgombea aliyepita bila uhalaali ajiuzulu Jambo ambalo amelitekeleza. Lakini kwa upande mwingine ili kuficha uchafu wa tume ya uchaguzi na uchafu wa CCM barua iliyotolewa na kiongozi wa CCM ndugu Shaka inadai Mbunge huyo amejiuzulu kwa sababu za kifamilia na wananchi wawe wavumilivu.

Unajiuliza huyo Mbunge kaongeza Mke, kashikizwa na familia au kafanyaje. Haya ni mambo yasiyopaswa kufanywa na watu waliopewa dhamana, usanii tunaoona ndio unaoendelea Hadi kwenye miradi ya maendeleo na mikataba ya rasilimali zetu. Kila Jambo wizi tu.
 
Huyo mbunge naye yaani unashindwa kutatua changamoto ya familia mpaka unajiuzuru.

Sizan kama angeweza ata kwa 2% tu kutatua changamoto za jimbo lake.
 
Tuliwaambia kina Zitto, Urafiki na CCM ni mgumu mno ku exist, huwezi kushiriki uchaguzi tume ile ile, watu walewale, mbinu zilezile, police walewale, mazingira yaleyale yet ukategemea kupata positive results - never under CCM. Nafikiri sasa kaamini.
 
Wameshindwaje kumununua IPI asijiudhuru. Au wamemnunua ili ajiudhuru kulinda Umoja wa kitaifa. Huyu aliyetamka tumekukaribisha sebuleni wataka uingie chumbani kafanyweje?
 
makamu wa kwanza wa rais ni mtu ambae hayumbishwi, alipochaguliwa tuu, nikasema haya weee sasa kweli ACT wazalendo wamepata kiungo, na CCM kwa huyu siyo kwa kuambiwa yakhe yakhe,

huyu jamaa alisimama na hoja zake na msimamo wake kwenye bunge la muungano kama yeye binafsi wakati alikuwa mwanasheria mkuu wa zanzibar, jambo ambalo liliwashtua sana CCM, inakuwaje wanasheria mkuu alochaguliwa na serikali akasimama na hoja zake binafsi kwa maslahi ya zanzibar, asiungane na wenzake? kichwa chake huyu jamaa hakiyumbishwi kabissaaa.

Sasa ilipotokea kadhia ya konde, nikasema enhe, kama mambo hayatobadilika jamaa ataachia ngazi hivi hivi na wala asiwe na habari kabisa, ni kweli hasemezeki huyu mbele ya haki, na mtu alokuwa mpole na hana tamaa ya madaraka kabisaaa.
Na inawezekana kuonyesha nini alilosema kwenye mkutano,

CCM nahisi alivyoona reputation yake na alivyo, walijua fika analolisema ndio analosimama nalo, bora nusu shari kuliko shari kamili.
nahisi wakapeana moyo CCM wakamwita mgombea aseme uongo kama kawaida, ila wakaandaa ni mikakati ipi ya kutiana adabu, maana CCM ni kama mmtoto wa shaytain ukimkanyaga bahati mbaya tuu njiani hujamuona, heee, cha mtema makuni utakiona, mama wa mtoto na jamaa zake, kila wakikuona watakutia adabu wewe na familia yako, utakuwa hujui nini sababu kumbe ulimkanyaga mtoto wao.
 
Huyo mbunge naye ni f☆la tu, yaani unashindwa kutatua changamoto ya familia mpaka unajiuzuru.
Sizan kama angeweza ata kwa 2% tu kutatua changamoto za jimbo lake.
Kwani alikuwa hajui kama ana changamoto za kifamilia
Ubunge si umgemaliza hizo changa moto kwa mishahara na maposho ya ubunge.

kuna jambo limefichwa.

Ukweli ukidhihiri uwongo hujitenga
 
Bila kuficha hisia zake aliwaomba waislam wakae na watafakari namna ya kuponya majeraha na kwamba anakubaliana na Serikali ya Kitaifa kwa 100% ila yeye hatokuwa sehemu ya Serikali hiyo.
Hii lugha ni ngumu kuielewa.
Msomaji anaweza akasema ni ubabaishaji usiokuwa na maana yoyote.
 
Bara wanataka katiba mpya na Zanzibar wakitaka katiba mpya ujuwe ccm itakuwa na wakati mgumu. Sasa itabidi mtoto apewe pipi(ACT Wazalendo) ili mtoto mmoja anyamaze.


Lunatic
 
Kauli aliyotoa Makamu wa kwanza wa Rais alipokuwa Pemba ilikuwa kauli nzito iliyoashiria kuvunjika kwa mashirikiano yaliyopo. Kauli ile ilieleza wazi dhamira yake ya kutoendelea na madaraka kwenye kundi la watu wasioridhika na ambao hawana uchungu na watu kufa, kuwa vilema nk. Alihoji watu wanatafuta madaraka ya Nini? Wameua na kuumiza watoto ikiwemo ubakaji lakini bado awajaridhika, Wakati vidonda vikiwa vibichi watu wale wale kwa kutumia tume ile ile wanakwenda tenda kwa wahanga walewale wakuiba uchaguzi. Wanatafuta Nini?

Bila kuficha hisia zake aliwaomba waislam wakae na watafakari namna ya kuponya majeraha na kwamba anakubaliana na Serikali ya Kitaifa kwa 100%
Unajiuliza huyo Mbunge kaongeza Mke, kashikizwa na familia au kafanyaje. Haya ni mambo yasiyopaswa kufanywa na watu waliopewa dhamana, usanii tunaoona ndio unaoendelea Hadi kwenye miradi ya maendeleo na mikataba ya rasilimali zetu. Kila Jambo wizi tu.
 
Kauli aliyotoa Makamu wa kwanza wa Rais alipokuwa Pemba ilikuwa kauli nzito iliyoashiria kuvunjika kwa mashirikiano yaliyopo. Kauli ile ilieleza wazi dhamira yake ya kutoendelea na madaraka kwenye kundi la watu wasioridhika na ambao hawana uchungu na watu kufa, kuwa vilema nk. Alihoji watu wanatafuta madaraka ya Nini? Wameua na kuumiza watoto ikiwemo ubakaji lakini bado awajaridhika, Wakati vidonda vikiwa vibichi watu wale wale

Hawa jamaa bila ushupavu wa kuchukua maamuzi magumu, itakuwa bado sana!
 
Kauli aliyotoa Makamu wa kwanza wa Rais alipokuwa Pemba ilikuwa kauli nzito iliyoashiria kuvunjika kwa mashirikiano yaliyopo. Kauli ile ilieleza wazi dhamira yake ya kutoendelea na madaraka kwenye kundi la watu wasioridhika na ambao hawana uchungu na watu kufa, kuwa vilema nk. Alihoji watu wanatafuta madaraka ya Nini? Wameua na kuumiza watoto ikiwemo ubakaji lakini bado awajaridhika, Wakati vidonda vikiwa vibichi watu wale wale kwa kutumia tume ile ile wanakwenda tenda kwa wahanga walewale wakuiba uchaguzi. Wanatafuta Nini?

Bila kuficha hisia zake aliwaomba waislam wakae na watafakari namna ya kuponya majeraha na kwamba anakubaliana na Serikali ya Kitaifa kwa 100% ila yeye hatokuwa sehemu ya Serikali hiyo.

Naamini kauli ile kwa uzito wake na kwa ninavyo mfahamu ndugu yangu Zitto haikuwa kauli ya chama Bali msimamo binafsi na kwa kutambua hilo Zitto amekaa kimya kwa muda mrefu bila kuwa na harakati za siasa mitandaoni kama kawaida.

Lakini waliosumbuka zaidi ni Chama cha Mapinduzi na kupelekea kuitana kwa dharura na kisha kumwelekeza mgombea aliyepita bila uhalaali ajiuzulu Jambo ambalo amelitekeleza. Lakini kwa upande mwingine ili kuficha uchafu wa tume ya uchaguzi na uchafu wa CCM barua iliyotolewa na kiongozi wa CCM ndugu Shaka inadai Mbunge huyo amejiuzulu kwa sababu za kifamilia na wananchi wawe wavumilivu.

Unajiuliza huyo Mbunge kaongeza Mke, kashikizwa na familia au kafanyaje. Haya ni mambo yasiyopaswa kufanywa na watu waliopewa dhamana, usanii tunaoona ndio unaoendelea Hadi kwenye miradi ya maendeleo na mikataba ya rasilimali zetu. Kila Jambo wizi tu.

Great Thinking mkuu
 
Back
Top Bottom