Serikali yasema Wananchi 2,102 wanaanza kulipwa fidia ya kuhamishwa Bonde la Mto Msimbazi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Mratibu wa Miradi ya Ushirikiano kati ya Benki ya Dunia na TARURA, Eng. Humphrey Kanyenye amezungumzia kinachoendelea kuhusu mchakato wa mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam.
152b844d-ab3f-4945-9f04-33d82eb95d54.jpg

Msimbazi.jpg
Anasema “Tulianza zoezi la maandalizi ya Mradi huo muda kidogo na ili mchakato ukamilike kulihitajika kuhamisha watu kwenye eneo la bonde, tumefanya zoezi hilo kwa ufanisi tangu Mwaka 2022, tulipata watu takribani 2,592 ambao ndio walikuwa waathirika.

“Kati ya hao tuliofanikiwa kuwapata na kuingiza taarifa zao kwenye Daftari la Fidia na kupata ruhusa ya Serikali walikuwa ni watu 2,329, kati ya hao waliolipwa mpaka sasa ni 2,102.

“Sababu ya waliosalia 227 kutolipwa zipo kadhaa ikiwemo migogoro ya Kifamilia wameshindwa kukamilisha taratibu za ndani za miradhi na wapo ambao hawakujitokeza tena.

“Pia kuna watu 184 ambao waligoma kulipwa kutokana na kiwango ambacho tulikionesha kwao wakidai fidia ni ndogo, hivyo hawakusaini, wengine 186 hatukuwafikia kutokana na mazingira, kuna sehemu watoa tathimini hawakufika maeneo husika na wengine walifika kwenye nyumba lakini hawakukuta wahusika.

“Kuanzia Jumatatu ya wiki hii (Februari 5, 2024) mchakato umeanza kwa wale wengine ambao hawakupatikana kulipwa fidia, tunategemea hadi mwisho wa Februari Daftari litakuwa limemfikia Mthamini Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuendelea na malipo.”

Waliogomea
Timu inafanya kazi kwa ajili ya kukamilisha Daftari ili limfikie Mtathimini Mkuu wa Serikali.

Ikumbukwe kuwa kwenye Mradi huo hatujalipa ardhi kwa kuwa hiyo seheu Wananchi hawakupaswa kujenga, Rais aliamua kwa wale waathirika (wenye nyumba) walipwe Shilingi Milioni 4 kila mmoja kama kifuta jasho na waweze kupata sehemu nyingine.”

Amesema malipo hayo yanatarajiwa kuanza kuingia leo Februari 7, 2024 na kuwa wahusika wametakiwa kubomoa wenyewe nyumba zao ili kuokoa baadhi ya vitu na mali zao.

Amesema "Watakaoshindwa kubomoa wenyewe sisi tutanza kulitekeleza zoezi hili ndani ya wiki mbili zijazo."

Pia, soma: TAMISEMI mbona mnachelewa kufidia watu wa bonde la mto Msimbazi?


View: https://youtu.be/fl0VTMZPULo?si=-0Rrmdj4B3yUS8OI
 
Nakumbuka World Bank ilishatoa hela kipindi cha Jiwe huku Mkuu wa Mkoa Dar akiwa Bashite. Hela zilitolewa kwa kuwalipa fidia na kugeuza hayo maeneo kuwa Gardens ikiwa ni pamoja na kuziba kwa juu huo mto tena ilikuwa Dar nzima. Kwa maeneo ya Vingunguti viwandani ule mto unaobeba kemikali za sumu kuingia mto mzinga,mto umejengwa kingo zake kuanzia Vingunguti mpaka mto Mzinga maeneo ya Mtongani lakini wananchi hawakupewa fidia wala kuhamishwa kama WB walivyotaka. Bashite anajua hela walipeleka wapi yeye na muuaji mwenzake Jiwe.
 
Mratibu wa Miradi ya Ushirikiano kati ya Benki ya Dunia na TARURA, Eng. Humphrey Kanyenye amezungumzia kinachoendelea kuhusu mchakato wa mradi wa Uendelezaji wa Bonde la Mto Msimbazi Jijini Dar es Salaam.
Anasema “Tulianza zoezi la maandalizi ya Mradi huo muda kidogo na ili mchakato ukamilike kulihitajika kuhamisha watu kwenye eneo la bonde, tumefanya zoezi hilo kwa ufanisi tangu Mwaka 2022, tulipata watu takribani 2,592 ambao ndio walikuwa waathirika.

“Kati ya hao tuliofanikiwa kuwapata na kuingiza taarifa zao kwenye Daftari la Fidia na kupata ruhusa ya Serikali walikuwa ni watu 2,329, kati ya hao waliolipwa mpaka sasa ni 2,102.

“Sababu ya waliosalia 227 kutolipwa zipo kadhaa ikiwemo migogoro ya Kifamilia wameshindwa kukamilisha taratibu za ndani za miradhi na wapo ambao hawakujitokeza tena.

“Pia kuna watu 184 ambao waligoma kulipwa kutokana na kiwango ambacho tulikionesha kwao wakidai fidia ni ndogo, hivyo hawakusaini, wengine 186 hatukuwafikia kutokana na mazingira, kuna sehemu watoa tathimini hawakufika maeneo husika na wengine walifika kwenye nyumba lakini hawakukuta wahusika.

“Kuanzia Jumatatu ya wiki hii (Februari 5, 2024) mchakato umeanza kwa wale wengine ambao hawakupatikana kulipwa fidia, tunategemea hadi mwisho wa Februari Daftari litakuwa limemfikia Mthamini Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuendelea na malipo.”

Waliogomea
Timu inafanya kazi kwa ajili ya kukamilisha Daftari ili limfikie Mtathimini Mkuu wa Serikali.

Ikumbukwe kuwa kwenye Mradi huo hatujalipa ardhi kwa kuwa hiyo seheu Wananchi hawakupaswa kujenga, Rais aliamua kwa wale waathirika (wenye nyumba) walipwe Shilingi Milioni 4 kila mmoja kama kifuta jasho na waweze kupata sehemu nyingine.”

Amesema malipo hayo yanatarajiwa kuanza kuingia leo Februari 7, 2024 na kuwa wahusika wametakiwa kubomoa wenyewe nyumba zao ili kuokoa baadhi ya vitu na mali zao.

Amesema "Watakaoshindwa kubomoa wenyewe sisi tutanza kulitekeleza zoezi hili ndani ya wiki mbili zijazo."

Pia, soma: TAMISEMI mbona mnachelewa kufidia watu wa bonde la mto Msimbazi?
Safi kabisa, mji unakuwa mchafu mchafu kwa sababu ya watu kujijengea hovyo; wakimaliza hapo wawaondoshe na bodaboda na bajaji katikati ya mji
 
Nakumbuka World Bank ilishatoa hela kipindi cha Jiwe huku Mkuu wa Mkoa Dar akiwa Bashite. Hela zilitolewa kwa kuwalipa fidia na kugeuza hayo maeneo kuwa Gardens ikiwa ni pamoja na kuziba kwa juu huo mto tena ilikuwa Dar nzima. Kwa maeneo ya Vingunguti viwandani ule mto unaobeba kemikali za sumu kuingia mto mzinga,mto umejengwa kingo zake kuanzia Vingunguti mpaka mto Mzinga maeneo ya Mtongani lakini wananchi hawakupewa fidia wala kuhamishwa kama WB walivyotaka. Bashite anajua hela walipeleka wapi yeye na muuaji mwenzake Jiwe.
Frank utakuwa mnafiki au hujui kitu kuhusu hii issue au utakuwa unataka kuaminisha ubwya ya Makonda kisa humpendi.

Kwa ufupi hii project nakumbuka na files zipo haikuanza wkt wa JPM, so kaa kwa kutulia.
 
Nakumbuka World Bank ilishatoa hela kipindi cha Jiwe huku Mkuu wa Mkoa Dar akiwa Bashite. Hela zilitolewa kwa kuwalipa fidia na kugeuza hayo maeneo kuwa Gardens ikiwa ni pamoja na kuziba kwa juu huo mto tena ilikuwa Dar nzima. Kwa maeneo ya Vingunguti viwandani ule mto unaobeba kemikali za sumu kuingia mto mzinga,mto umejengwa kingo zake kuanzia Vingunguti mpaka mto Mzinga maeneo ya Mtongani lakini wananchi hawakupewa fidia wala kuhamishwa kama WB walivyotaka. Bashite anajua hela walipeleka wapi yeye na muuaji mwenzake Jiwe.
Chuki zako zitakuchelewesha

Ile projects ilikuwepo hata kabla ya Jiwe
 
Back
Top Bottom