Mkazi: Siondoki Bonde la Msimbazi bila fidia ya angalau bilioni moja

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,447
7,832
Wananchi wanaoishi bonde la Msimbazi waliokumbwa na mafuriko wametoa maoni yao baada ya Rais Samia kutangaza wapewe fidia huku ya ardhi ikiwa milioni nne huku jumla wengine wakipata jumla ya milioni sita wakihoji wanaenda kufanyaje ili wapate kiwanja na nyumba huko wanapoenda.

Kijana mmoja amesema hawezi kuondoka kwake kwa fidia iliyotajwa huku mwingine akisema wameambiwa hakuna sheria inayomlazimisha Rais kulipa fidia bali ni huruma ya Rais.

Serikali ilipokea bilioni 463 kwa ajili ya mradi wa bonde la mto Msimbazi ikiwemo ujenzi wa daraja na kuboresha matumizi ya ardhi katika bonde hilo, nusu zikiwa msaada na nusu mkopo.

 
Wananchi wanaoishi bonde la Msimbazi waliokubwa na mafuriko wametoa maoni yao baada ya Rais Samia kutangaza wapewe fidia huku ya ardhi ikiwa milioni nne huku jumla wengine wakipata jumla ya milioni sita wakihoji wanaenda kufanyaje ili wapate kiwanja na nyumba huko wanapoenda.

Kijana mmoja amesema hawezi kuondoka kwake kwa fidia iliyotajwa huku mwingine akisema wameambiwa hakuna sheria inayomlazimisha Rais kulipa fidia bali ni huruma ya Rais.

Serikali ilipokea bilioni 463 kwa ajili ya mradi wa bonde la mto Msimbazi ikiwemo ujenzi wa daraja na kuboresha matumizi ya ardhi katika bonde hilo, nusu zikiwa msaada na nusu mkopo.

Ataondolewa hata Kwa bakora. Alizaliwa na hiyo Ardhi?
 
Madhara ya kuwa na nchi inayowaza hurumahuruma hadi kutaka kuifunika haki.

Huruma ni mwana

Haki ni baba

Baba asimdhulumu mtoto na mtoto asimdhulumu baba. Bali wanashirikiana.

Baba anaweza kusimama peke ake, lakini mwana anamuhujitaji baba kujikamilisha

Tujikite kwenye kuwatendea haki wananchi zaidi ya kutoa ama kutafuta huruma. Haki ndo huinua Taifa 👊
 
Back
Top Bottom