Serikali yakiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudi tena

The Evil Genius

JF-Expert Member
Mar 21, 2014
5,462
17,278
Juzi hapa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao huwa hawarudi tena.

Maana yake ni kuwa sisi Tanzania kila mwaka tunategemea watalii wapya, hatuwezi kuwatuliza(keep) ama kuwahakikishia watalii wa zamani kurudi tena Tanzania kufurahia vivutio vyetu vya utalii.

Retention yetu ya watalii ni chini ya 20%. Maana yake ukuaji wa utalii wetu bado una changamoto kubwa sana.

Nikitoa my personal experience, nilitembelea Kisiwa cha Saa Nane, Mwanza, tukakutana na tour guide wa kike, wote tuliofika pale siku hiyo hatuwezi kutamani kurudi tena, mimi na wenzangu siku hiyo tulikuwa disappointed, siwezi kutamani hata kwa bunduki kutembelea tena hiyo hifadhi.

Nimewahi kwenda Serengeti National park mara 2, kwa pale niko tayari kurudi maana mategemeo yangu yalikamilika kwa zaidi ya 80%.

Je, unadhani ni kwanini watalii wa nje hawarudi tena baada ya kutembelea Tanzania.

=============

ARUSHA
Wamiliki wa makampuni ya watalii, wadau ya sekta ya utalii nchini Tanzania ikiwemo wahifadhi wastaafu wameelezea sababu tano zinazowafanya watalii waliotembelea nchini wasirudi kwa mara ya pili.

Sekta ya utalii inachangia asilimia 17.5 ya pato la Taifa pia asilimia 25 ya mapato ya fedha zote za kigeni nchini ambapo kwa sasa inatembelewa na watalii milioni 1.2. Serikali inalenga mpaka 2025, Tanzania inatakiwa kupokea angalau watalii milioni tano na kukuza mapato ya fedha za kigeni kutokana na utalii mpaka dola bilioni 6 kutoka dola bilioni 2.5 kwa mwaka.

Wakiongea na gazeti la Citizen, washika dau wameainisha sababu kama gharama kubwa ambazo watalii wanaingia wakitembelea Tanzania, huduma kwa wateja isiyoridhisha kwenye mahoteli na watoa huduma wengine.

Kulingana na wao, miundombinu mibovu, makampuni ya watalii yanayoshindwa kutimiza ahadi zao walizowapa wateja na wafanyakazi kukosa uadilifu ikiwemo kuwalangua watalii. Akiongea na Citizen, mhifadhi mstaafu, Erastus Lufungilo ambae kwa sasa ni mkurugenzi wa kampuni ya utalii ya Burudika amesema watalii walilazimika kutumia fedha zaidi kutokana na kukosekana kwa ndege za moja kwa moja kutoka kwenye nchi zao ikiwemo Ulaya na Marekani kuja Tanzania. "Utalii ni gharama, hii ni kwasababu kutembelea Tanzania kwasasa ni gharama kuliko kutembelea Kenya au Afrika kusini" Alieleza.

Kulingana na yeye, makampuni mengi ya utalii yana mapungufu katika kuendesha biashara na kuongoza watalii kunakosababishwa na upungufu wa wafanyakazi wataalam na kusababisha matatizo.

"Baadhi ya waongoza watalii wanachukua hela kutoka kwa watalii lakini chaajabu huwezi kuwakuta uwanja wa ndege kuwapokea watalii. Hata wakijitokeza kuwapokea ambao wanalipwa hela nyingi, hawatoi huduma bora" Alisema Lufungilo

Kwa upande wake, mwenyekiti wa chama cha waongoza watalii(TTGA) amesema wingi wa kodi zinazotozwa kwa makampuni ya watalii na waongoza watalii imesababisha watalii kutomudu gharama kwa watalii wengi ambao wanashindwa kuitembelea tena Tanzania.

"Kuna kodi nyingi sana na kila siku kodi mpya zinatangazwa na kuwalazimu wamiliki kupandisha gharama ili kupata faida. Alisema ndugu Mollel. Alihoji kwanini baadhi ya mashrika ya ndege kuchaji dola 500 zaidi kwa tiketi safari kutoka Ulaya kuja Tanzania ikilinganishwa na viwanja vingine vya ndege kwenye nchi za jirani.

Akifungua mkutano wa mwaka kwa wahariri na waandishi waandamizi kwenye sekta ya utalii, katibu mkuu wizara ya Utalii na maliasili, Aloyce Nzuki amewataka wanahabari wafikiri kwa makini kwanini asilimia 20 pekee ya watalii wanaitembelea tena Tanzania.

Dr. Nzuki amevitaka vyombo vya habari nchini kutoa taswira nzuri ya nchi kabla na baada ya watalii kutembelea Tanzania

20210103_104846.jpg
 
Nadhani tunatangaza vitu tunavyoita vivutio lakini hata wenyewe sisi watz havituvutii......

Unajua ili uweze kumvuta mtalii ni vema ujue nae ni mwanadamu kama sisi, na anavutiwa na vile vitu tunavyoweza vutiwa navyo pia.

Inabidi tuongeze creativity ya kuweka vivutio ambavyo hata watu wa ndani pia wapo interested. Hebu tazama Malaysia kwa mfano, kule kuna wanawake wazuri, chakula kizuri, hoteli safi, culture profile ya kueleweka. Sasa mzungu anapokwenda kule inakuwa ni sehemu ya kutalii kweli kweli na kufurahia maisha.

Wazungu nao ni watu kama sisi, wanapokuja wanataja kuenjoy maisha ambayo sisi pia tuna enjoy sio kuwa igizia maisha ambayo hatuyaishi. Imagine mzungu anakuja unamuwekea ngoma za asili, hivi hizo ndizo ngoma unazosikiliza kila siku miaka hii?!

So hebu tutafiti kwa wenzetu Dubai na Malaysia........ Tujifunze then tuestablish.
 
Juzi hapa katibu mkuu wa wizara ya utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kua zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania hua hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao hua hawarudi tena...
Mm nimetembelea mbuga nying sn ila serenget sijawah fika kinachofanya watalii wasirud ni management mbovu mfano ukienda ruaha mapokez ni pa kiswahili vyoo ni vya kiswahili refreshment ndio kabisa uswahili swahili tu afu mbuga kubwa wanyama wachache yaan mnatafuta wanyama kwa mbinde chui, simba ndio balaa hawapatikan kuna haja ya kujenga good management wagen wasipate usumbufu mbuga pekee ambayo angalau niliifurahia ni manyara ipo poa sn japo na penyewe pana changamoto yake ilaa kwa serenget naamin ipo juu maana ndio best of all in africa
 
Asante kwa mrejeshonyuma.

Binafsi napenda kufahamu: Mambo yapi hayakukuvutia ulipotembelea kisiwa cha Saanane:ni huyo mwongoza watalii wa kike?Kipi alifanya kinyume na matarajio yako(yenu)?

Ama kisiwa cha Saanane hakina mandhari au vivutio vyenye kuridhisha hata uone thamani ya pesa yako (value for money)?
 
Juzi hapa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao huwa hawarudi tena...
Katika utafiti wako uligundua nn kinachangia tatizo hilo
 
Juzi hapa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii alikutana na wafanyakazi wa wizara hiyo katika kujadili masuala ya utalii na changamoto zake alikiri kuwa zaidi ya 80% ya watalii wanaotembelea Tanzania huwa hawarudu tena, wakishakuja mara moja wengi wao huwa hawarudi tena...
Mdogo mdogo ipo siku mtasema tu ukweli wote kuwa zile 85% zilikuwa za Lissu.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Mwaka jana nilipanda mlima Kilimanjaro na huko niliongea na baadhi ya watalii wakutoka nje. Wengi wanalilimikia ukubwa wa kodi. Kwa mtu mmoja kodi ilikuwa dola 800 kwa mujibu wa maelezo yao. Hiki ni kiwango kikubwa sana kwa mtu wa kawaida.

Serikali ipunguze kodi na iongeze promo.
 
Katibu mkuu analalamika badala ya kutoa suluhisho kwanza gharama zetu sio rafiki ukiondoa watalii wachache matajiri watalii wengi ni watu waliojinyima kwa muda mrefu lakini wakija huku gharama wanakuta ni kubwa mno hawawezi kuja tena.

Customer care mbovu. Tunaweka mazingira yaleyale kama kwao wakati wao wanapenda kuona vitu vipya lakini kuanzia chakula kila kitu cha kwao
 
Back
Top Bottom