#COVID19 Serikali ya Saudia yasema "Mwaka huu ni wale Waislamu waliopata chanjo ya COVID-19 pekee ndiyo wataruhusiwa kuhiji Makka/Madina"

Allah awabariki watawala wa Saudia, awahifadhi na awasamehe makosa yao.
Hakika MKUU,,

Haswa kwa mauaji ya kashogi ,,

na kwa dhuluma wanayoifanya kwa waislam wote duniani,,

Pamoja na wanainchi wa Yemen kwa ujumla.
 
Tuendelee kusubiri
Umoja wa ulaya ,canada na Us
Muda sio mrefu watapiga marufuku raia wa kutoka nchi yeyote dunian ambaye hajapata chanjo ya korona kuingia nchini mwao

Tujiandae
 
Yanahusiana na ukiukwaji wa haki za binadamu wa saudia.

Hawana uislam kitu..

Watalazimishaje mambo ya chanjo ambayo bado yamekuwa ni sintomfahamu ktk baadhi ya inchi ..

Kama unaona nakuumiza vaa chupi yako nenda..
Warembo wako wengi..
Nchi zipi middle east ndio zenywe uislamu kuliko saudi arabia??
 
Serikali ya Saudi Arabia leo imetoa maelekezo kuwa hakuna Muislamu atakaye ruhusiwa kwenda kuhiji kama hajapata chanjo ya Covid19
Source DW Kiswahil leo.

Kama ambavyo tumesikia makanisa ya Kikatoliki na Kilitheri yalivyotoa matamko juu ya ugonjwa huu tunasubiri tamko la Mufti Zuberi na kipenzi cha serikali hii Sheikh Alhad
 
huwezi kujitenga na Dunia - ni kujidanganya. Yaani mataifa makubwa yote yameitambua Chanjo ya COVID wewe unasema haifai - haya sasa ma-ustadhi mwaka huu hija kwa TV.
 
Saudi Arabia ni mke wa USA, yani katika mataifa ya kiislamu ni Iran pekee yake ndio mtetezi wa waislamu dhidi ha makucha ya beberu, wengi wote ni wachumba tu.

Haishangazi kuona Saudi ana toa boko kama hili maana ni kibaraka wa USA.
 
JPM akiipata hiyo

" Nimesikia ndugu zangu waislamu mmewekewa masharti kwamba mwaka huu hamuwezi kwenda kuhiji mpk uwe umechanjwa, Hao ndiyo viongozi wetu wa kiroho tulio nao leo yaani wanawazuia watu kutekeleza nguzo yao ya imani kisa ugonjwa, nilikuwa nachombeza na Mufti hapa kwani hatuwezi kujenga hiyo sehemu ya kuhiji kama ile ya Makka kule kisarawe kwa Mh Jafo ili na wao huko waje kuhiji hapa Tanzania kwa watani zangu wazaramo na fedha hizo zipo maana mambo mengine aah basi tu nisiendelee sana maana ni mambo ya imani ila ni mambo ya ajabu, ila wakiendelea kuwazuia leteni pendekezo tutajenga nasema tutajenga"
Aiseeh we jamaa kunywa soda kwanza hapo ulipo
 
Serikali ya Saudi Arabia leo imetoa maelekezo kuwa hakuna Muislamu atakaye ruhusiwa kwenda kuhiji kama hajapata chanjo ya Covid19
Source DW Kiswahil leo
Kama ambavyo tumesikia makanisa ya Kikatoliki na Kilitheri yalivyotoa matamko juu ya ugonjwa huu tunasubiri tamko la Mufti Zuberi na kipenzi cha serikali hii Sheikh Alhad
utachanjwa Nairobi au Addis Ababa wakati unasubiri connection ya kwenda Jeddah
 
Saudi Arabia ni mke wa USA, yani katika mataifa ya kiislamu ni Iran pekee yake ndio mtetezi wa waislamu dhidi ha makucha ya beberu, wengi wote ni wachumba tu.

Haishangazi kuona Saudi ana toa boko kama hili maana ni kibaraka wa USA.
Sasa kwanini na ninyi mnaenda kuhiji kwa kibaraka/mke wa USA, Kwanini msiende kuhiji kwa mtetezi wenu Irani?
 
Wengine hatuhitaji chanjo, kama hilo suala la chanjo likipitishwa basi liwe kwa wanaohitaji kuchanjwa isiwe lazima kwa kila mtu.
 
Mkuu umeuliza maswali 100 sasa sijuwi nikujibu lipi.
Maswali niliyo uliza hayafiki hata 30 wala 20. Jibu utakalo ona jepesi kwako na uwe na majibu sahihi.
Mimi nipo damamm,,,sifuatilii habari za vitabuni.
Nani amefatikia habari za vitabuni, na hiki lina nafasi gani hapa? Kuwepo Damamm siyo hoja, hoja ni kujibu maswali na kuandika ukweli kwa hija na elimu.
Zipo baadhi ya broadcast za magharibi na saudia wenyewe hawawezi kukutangazia hivyo vitu.

Naangalia..
Yemen TV.
Palestine TV.
Nk..
Hizi zote si hoja, hija ni weee ujibu maswali niliyo kuuliza kwa uadilifu na insafu. Hizi dibaji hazina nafasi hapa, naona unapoteza kuandika vitu visivyo na maana.
Kashogi alikuwa mkosoaji wa serikali ya kifalme.
Mfano,

Leo saudia kumekuwa na mambo mengi ya kimagharibi.

Ni tofauti kabisa na misingi ya kiislam.
Tuwekee jambo moja au hata mawili ambayo alikuwa anakosoa Kashogi kwa mujibu wa Uislamu.

Kisja utuambie ni mafunzo gani ya Uislamu yanaruhusu ukosoaji wa namna ile alio kuwa anaufanya Kashogi?
TV zinaonyesha wanawake wanakata mauno,,vitovu nje,,ndy uislam?
Hui siyo Uislamu na hili linasemwa sana na Wanazuoni wana likemea, na ndiyo maana tunakubali ya kuwa madhaifu yapo, ila nyie mnaandika vitu kwa dhulma na uadui, na kuzua yaani hamuongelei mambo kielimu na uadilifu. Ndiyo maana nahitimisha kwa kusema hakuna nchi inayoizidi Saudia kwa kusimamia sheria za Uislamu, hizo nchi nyingine hayo mambo hakuna ? Sasa kwanini mnalingaisha kwa mambo fulani na mengine mnayaacha?
Ukiangalia hata Iran ipo tofauti na saudia sababu msaudia kamkumbatia mmarekani ambaye ndy adui namba moja wa uislam duniani.
Swali la msingi ni je amemkumbatia katika mambo ganina je uislamu unasemaje juu ya hilo?

Pili,ni kosa la kielimu kuilinganisha Saudia na Irani, Irani si Taifa la Kiislamu, na hawana tofauti na Mayahudi na wa Marakani, na katika nchi ambayo Makafiri huitumia kuwadhuru Waislamu basi ni Irani, hizi nyingine ni filamu tu mnachezewa.
Saudia royal family ni genge la wahuni..
Haoa unathibitisha ya kuwa ulichokiandika hao awali huna elimu nacho. Sasa huu unao ufanya wewe ndiyo uhuni.
Hivi kukumbusha mwenendo wa utawala wa ufalme haupo sawa ni usaliti?
Ni usaliti na utuambie Kashogi alikuwa amekumbatiwa na kina nani na je usulubu ule ndiyo mafunzo ya Uislamu ? Huelewi na wapi na kwanini hujibu maswali ninayo kuuliza?

Au unataka kutuambia Uislamu haukufundisha namna ya kuayaendea haya mambo? Mko wapi na elimu vijana?
Nani kakwambiya kwamba adhabu ya usaliti ni kifo?
Soma katika historia ya Uislamu utaona.
Dini inasemaje kuhusu udugu wa kiislam?
--Ni yule ndugu yako ktk imani.
Sada hapa unauzungumzia undugu kati ya Muislamu na Shia au ? Hakuna undugu kati ya Uislamu na Ukafiri bali kuna muamala tu wa kuishi kwa mipaka, na udui wa Shia kwa Waislamu ni mkubwa sana, soma Historia ya Mashia na uone waichokifanya kwa Waislamu katika Dola ya Swafawiya. Kila kitu kimeandikwa.
--Au ni yule wa imani nyingie ,,, anayekuchochea ugombane na ndugu zako.
Saudia anafanya miamala na Wamarekani katika mambo ya kimiamala na kibiashara.
Dunia ya Leo hakuna vita vya jihad,,
Vilishapiganwa na mtume (S.AW)na maswahaba vikaisha.
Huu ujinga mwingine. Jihadi ni ibada ikikidhi masharti na nguzo Jihadi inapiganwa. Miongoni mwa Jihadi zilizo wahi kupigwana ni vita vya Afghanistani ila wapiganaji ndiyo walikuwa na shida, kadhalika vita vya wamogoli karne ya 13 lakini tatizo waislamu walikuwa wanaingia na mahirizi na ucjafu mwingine, wakawa wanashindwa.
wengi wanagombea matumbo yao ikiweno saudia.
Hili huna ushahidi. Unaleta habari za vijiweni.
Isitumie mgongo wa kuua watu kwa kisingizio cha usaliti,,
Swali wanao uliwa ni Waislamu au makafiri ? Hili swali mboma hulijibu ? Au wewe ni Shia nini ? Maana naona huna hoja unalalama tu. Mahafuko kaskazini mwa Yemeni yameanza miaka ya 2011,2012,2014, 2015 Saudia wakaanza kuingilia kati, mbona kipindi hicho hote mlikaa kimya ? Waislamu wanauliwa ila alipoingia Saudia kuwatetea Waislamu mnapayuka payuka...?
Soma vizuri history ya mfalme wa sasa wa saudia..
1975 King Faisal mfalme wa kipindi hicho aliuliwa na nephew wake hadharani.,,mpwa akitokea marekani alipokuwa akiishi huko.
Mfalme aliipigwa risasi hadharani,,na kufa.
Hili lina uhusiano gani na tunachokijadili hapa ?
Yote ni mipango ya marekani kuweka watu wao.
Waivuruge saudia na uislam.
Tuwekee ushahidi wa haya. Vijana msiwe mnatuletea habari za vijiweni, tena mkiwa hamna ushahidi ndiyo mkae nazo wenyewe huko.

Kazi yangu nimemaliza.
 
Back
Top Bottom