Serikali ya Kikwete Imefanya nini 2005-2015...

Serikali ya Kikwete Imefanya nini 2005-2015...

Kweli ni kichaa tu ambaye haoni mafanikio ya JK

Ni taahira tu anayefikri kuwa haya maendeleo yameletwa na Kikwete!! Hata kama tungekuwa na Rais mwehu kwa mikopo hii lazima anagejenga miradi mingi tu!! Huyu aliingia madarakani kukiwa na deni lisilozidi 6 trillion, sasa hivi limefikia trillion 27 na mpaka anaondoka litakuwa limefikia trillion 30. Sasa hapo kipi cha ajabu?

Namhurumia sana Rais atakayefuatia awamu hii ya zombi.e!!
 
Ni taahira tu anayefikri kuwa haya maendeleo yameletwa na Kikwete!! Hata kama tungekuwa na Rais mwehu kwa mikopo hii lazima anagejenga miradi mingi tu!! Huyu aliingia madarakani kukiwa na deni lisilozidi 6 trillion, sasa hivi limefikia trillion 27 na mpaka anaondoka litakuwa limefikia trillion 30. Sasa hapo kipi cha ajabu?

Namhurumia sana Rais atakayefuatia awamu hii ya zombi.e!!

Pesa zote hizi ni mikopo hata dawa tunazotumia zote ni za wazungu.... Nyie majinga ya SiSiEMu tuambieni serikali yenu imepunguza utegemezi wa bajeti kwa kiasi gain??? je bei ya vitu hivi ...sukari , Bati, mfuko wa simenti, Nondo, umeme wa majumbani na kadhalika bei zake zilikuwa tsh. ngapi mwaka 2010 siku JK alipoingia ikulu na Leo hii ni sh. ngapi???????
 
Kaja kujenga barabara tu -------- yule elimu hakuna kitu shule za Kata zero imekuwa kawaida
 
Nyie mmeifanyia nini Tanzania au mnamlaumu JK TU! Na wazazi wenu wamenifanya nini TZ,
 
Upuuzi mtupu hayo majengo watanzania yanawasaidia nini kama bei ya chumvi, ya sukari inapanda kila kukicha, kundi la vijana wasio na ajira linaongezeka maradufu. Sio kwamba serikal haijafanya lolote lakini yaliyofanywa hayajafika hata nusu ya yale tuliyoahidiwa mpaka tukawapa kura zetu, hivo ccm wamewataperi wapiga kura.

Acha kupoteza lengo tulia ufahamishwe jk amefanya nini usilete porojo
 
Hiilo jengo la moyo lililopo Muhimbili hakuna kinachofanyika zaidi ya kuligeuza hotel hapo badae
 
Serikali ya Kikwete imefanya vitu viwili vikubwa ni mawasiliano ya cm na usafiri wa boda boda tu! Mengine hakuna kilichonyooka.
 
imeshindwa kupunguza mfumuko wa bei yani 'inflation'
 
Kaja kujenga barabara tu -------- yule elimu hakuna kitu shule za Kata zero imekuwa kawaida
Elimu: mwaka 1961 chuo kikuu kimoja - hivi sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 44 tunaongoza wa idadi katika EAC
- miaka 10 iliyopita tulizidiwa idadi ya vyuo vikuu na Kenya na Uganda
- kabla ya utawala wa Kikwete alikuta idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu 40,000
- hivi sasa idadi ya wanafunzi ni 160,000 hii ni mara 4 zaidi
- bajeti ya %24 ya wizara ya elimu ni mikopo kwa wanafunzi hakuna nchi ya EAC iliyotoa kiwango kikubwa cha msaada kwa wananchi wake kama hivi.
- UDOM-Chuo kikuu cha serikali kikubwa zaidi katika EAC kinachukua wanafunzi 40,000 ni idadi ya uwezo wa vyuo vikuu vyote vilivyokuwepo kabla ya serikali ya Kikwete.
- Chuo kuu kikubwa cha sayansi A.Mashariki Nelson Mandela.
- kuna shule za msingi kwenye kila kata.
- Kuongezeka ajira kwenye sekta ya elimu.
- Kujenga miundombinu ya elimu


 
Hiilo jengo la moyo lililopo Muhimbili hakuna kinachofanyika zaidi ya kuligeuza hotel hapo badae
Mafanikio sekta ya Afya:
Mafanikio ya nchi yanapimwa kimataifa na hivi sasa kigezo kikubwa cha kupima maendeleo ya nchi ni malengo ya millennia.
Tanzania ni mojawapo ya nchi duniani ambayo ilitekeleza huduma za afya ya msingi kwa mafanikio makubwa sana baada ya uhuru, hii ni kauli ya Rais wa baraza kuu la 65 la UN mwaka 2011 Bw. Joseph Deiss alisema Tanzania ni nchi ya kupigiwa mfano barani Afrika.
Miongoni mwa mafanikio kwenye sekta ya afya ni:
- huduma za afya zimesogezwa karibu wananchi.
- utoaji wa chanjo za kuzuia magonjwa mbalimbali bure na chanjo kuhusu mama na mtoto.
- Kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka 5.
- Huduma ya kinga ya maambukizi ya ukimwi toka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto.
- Kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
- Kupunguza malaria kwa kugawa vyandarua vyenye dawa.
- Kupunguza magonjwa yanayosababishwa na maji, magonjwa hayo ni pamoja na kipindupindu na homa ya matumbo.
- %86 miongoni mwa kaya maskini walitumia huduma za vituo vya afya vya serikali
- Utoaji wa dawa za kupunguza makali ya ukimwi bure.
- Utoaji wa tiba ya kifua kikuu na ukoma bure.
- Kutokomeza magonjwa mbalimbali ambayo hapo awali yalikuwa ni kero.
- Kuongeza ajira kwenye sekta ya afya.
- Kujenga miondombinu ya afya.
- Hospitali Ocean roard imetangazwa na na tume ya nyuklia duniani kuwa ni mfano hospitali bora ya tiba ya kansa barani Afrika.
- Imeanzishwa tiba ya moyo nchini, kuna operesheni za moyo zaidi ya 400 zimefanyika kwa mafanikio ndani kipindi cha miaka 3 hivi sasa.

 
Pesa zote hizi ni mikopo hata dawa tunazotumia zote ni za wazungu.... Nyie majinga ya SiSiEMu tuambieni serikali yenu imepunguza utegemezi wa bajeti kwa kiasi gain??? je bei ya vitu hivi ...sukari , Bati, mfuko wa simenti, Nondo, umeme wa majumbani na kadhalika bei zake zilikuwa tsh. ngapi mwaka 2010 siku JK alipoingia ikulu na Leo hii ni sh. ngapi???????
Usiangalie bei ilikuwa kiasi gani mwaka 2010 ila linganisha bei ya vitu hivyo na majirani zetu wa EAC sisi tuna nafuu kubwa.
 
Kama sii serikali ya kikwete ,dada yako huko kijijini angekuwa housegirl mjini,leo anasoma sekondari,hata kama kuna changamoto bado zinatatulika.
 
Ahadi ya Ujenzi wa Reli mpya kwa ajili Treni iendayo kasi toka Dar hadi Mwanza imefikia wapi???

Ama huo ulikuwa ni mtindo wa kuonyesha alilemewa na Dr Slaa so akaanza kuropoka hadi ahadi ZISIZOTIMIZIKA.
 
Kama sii serikali ya kikwete ,dada yako huko kijijini angekuwa housegirl mjini,leo anasoma sekondari,hata kama kuna changamoto bado zinatatulika.
Sasa hivi ma-house girls ni form 4, kama wewe bado unapata darasa la 7 basi una bahati mbaya.
 
Nyie mmeifanyia nini Tanzania au mnamlaumu JK TU! Na wazazi wenu wamenifanya nini TZ,

Kwani huoni mafanikio ya sehemu chache ambazo cdm imeshikilia unajifanya kipofu au.jk hapa alikuwa raisi ili kutuzidishia zero tu .matokeo ya mwaka huu top 40 yote hakuna shule za serikali.pia idadi ya wanafunzi kwenda chuo imekua kwasababu hata wasichana waliopata div 3 wanaweza kuendelea na chuo pia ni matter of population growth tu
 
Pesa zote hizi ni mikopo hata dawa tunazotumia zote ni za wazungu.... Nyie majinga ya SiSiEMu tuambieni serikali yenu imepunguza utegemezi wa bajeti kwa kiasi gain??? je bei ya vitu hivi ...sukari , Bati, mfuko wa simenti, Nondo, umeme wa majumbani na kadhalika bei zake zilikuwa tsh. ngapi mwaka 2010 siku JK alipoingia ikulu na Leo hii ni sh. ngapi???????
Mkuu kwa nini una-quote bandiko langu halafu unatukana? Inakuwa kama unanitukana mimi vile wakati na mimi nayashangaa haya ma-Zombie ya CCM yanayotudanganya na maendeleo ya mikopo!!Naomba unitake radhi mkuu!!
 
Aliwambia walio iba EPA warudishe pesa, na ni Rais pekee aliye ongeza deni la Taifa kuwa kubwa zaidi
 
Back
Top Bottom