Mchekechoni
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 279
- 19
Serikali 'baradhuli' ya JK inashambuliwa kila kona: Yaani kwa kweli ni hatari tupu jinsi wandugu wa TZ wanavyoishambulia serikali pande zote kiasi kwamba zile kelele za mlango sasa zinaleta usumbufu kiasi cha kumkosesha JK usingizi murua tofauti na ilivyokuwa enzi anaingia ikulu baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Du, hali inatisha mazee kila kona: maredioni, magazetini, makanisani, misikitini, klabuni, vijijini, mijini, maofisini, mashambani, madukani, kwenye bar, uwanjani, mpirani, mahospitalini, jeshini, UV-CCM, UWT, katika Facebook na hapa JF, kwenye NGO's, vijiweni hadi kwenye magesti, you just name it.....mh! What next..? 2015 ni mbali sana, akimaliza awamu yote ana roho ya paka au kuwe na mkono wa mtu!