Serikali 'tukufu' ya Mh. JK inashambuliwa kila kona...!

Mchekechoni

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
279
19
Serikali 'baradhuli' ya JK inashambuliwa kila kona: Yaani kwa kweli ni hatari tupu jinsi wandugu wa TZ wanavyoishambulia serikali pande zote kiasi kwamba zile kelele za mlango sasa zinaleta usumbufu kiasi cha kumkosesha JK usingizi murua tofauti na ilivyokuwa enzi anaingia ikulu baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Du, hali inatisha mazee kila kona: maredioni, magazetini, makanisani, misikitini, klabuni, vijijini, mijini, maofisini, mashambani, madukani, kwenye bar, uwanjani, mpirani, mahospitalini, jeshini, UV-CCM, UWT, katika Facebook na hapa JF, kwenye NGO's, vijiweni hadi kwenye magesti, you just name it.....mh! What next..? 2015 ni mbali sana, akimaliza awamu yote ana roho ya paka au kuwe na mkono wa mtu!
 
wezi hawakubaliki vyo vyote vile iwavyo . Ndio matokeo yake. Utamu wa Bembea unamrudi
 
Ndugu Mchekechoni, hakuna kitu kibaya **** Mtu kuwaibia Umma anoongoza!! Inakera kupita kiasi mtu unapowaibia wananchi haki ya kuchagua waongozwe na nani hata ukajipenyeza kimazingaombwe ikulu kupitia mlango wa nyuma na kisha kuanza kujiona ni mjanja sana umewazidi watu wote akili nchini.

Dhoruba hizi zote Watanzania TUMEIBIWA CHETU na tunasema hakuna kulala mpaka kieleweke. DAMU YA MASHUJAA WA ARUSHA NA PEMBA ndio tutakayoandikia uhuru wetu wa kweli na kuwaengua mafisadi kimoja.
 
Give me a break please.............!!!!!!! serikali tukufu?? utukufu wake uko wapi????? .....you are not serious kama alivyo huyo Kikwete wako!!
  • wanaong'ang'ania madaraka ( wamechakachua ili wabaki ikulu/wamekatalia umeya wa Arusha, Mbeya, Kigoma nk) ndio unawaita watukufu?
  • Wanaotapeli kupitia Dowans ndio watukufu?
  • Wanaoua wananchi wao wanaodai haki badala ya kuwalinda na mali zao ndio watukufu?
  • Wanaoziba masikio na kufanya usanii wakati wananchi wanadai haki zao za kikatiba ndio Watukufu?
  • Wanao ongoza nchi bila dira wala utashi wa wanao ongozwa ndio unawatetea na kuwaita watukufu?
  • .........mapungufu yao ni mengi na wala hawastahiki hata kuitwa viongozi wetu!!!!
 
watu wakishakuchoka cha maana ni kukaa pembeni..akina Gbagbo wengi Africa hii.. ..Vinginevyo huyu mzee anatafuta kukimbia nchi akiondoka madarakani...So far tunaendelea kumwangalia na kuona anavyotumia busara yake.,.
 
Yaani kwa kweli ni hatari tupu jinsi wandugu wa TZ wanavyoishambulia serikali pande zote kiasi kwamba zile kelele za mlango sasa zinaleta usumbufu kiasi cha kumkosesha JK usingizi murua tofauti na ilivyokuwa enzi anaingia ikulu baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Du, hali inatisha mazee kila kona: maredioni, magazetini, makanisani, misikitini, klabuni, vijijini, mijini, maofisini, mashambani, madukani, kwenye bar, uwanjani, mpirani, mahospitalini, jeshini, UWT, katika Facebook na hapa JF, kwenye NGO's, vijiweni hadi kwenye magesti, you just name it.....mh! What next..?

Kelele za mlango hazimshtui mwenye Nyumba.
 
Naona sasa kila kiongozi yuko kivyake -- anatoa kauli kivyake. Hakuna msimamo mmoja wa serikali. Mwanzo wa mwisho!!!!
 
Yaani kwa kweli ni hatari tupu jinsi wandugu wa TZ wanavyoishambulia serikali pande zote kiasi kwamba zile kelele za mlango sasa zinaleta usumbufu kiasi cha kumkosesha JK usingizi murua tofauti na ilivyokuwa enzi anaingia ikulu baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Du, hali inatisha mazee kila kona: maredioni, magazetini, makanisani, misikitini, klabuni, vijijini, mijini, maofisini, mashambani, madukani, kwenye bar, uwanjani, mpirani, mahospitalini, jeshini, UWT, katika Facebook na hapa JF, kwenye NGO's, vijiweni hadi kwenye magesti, you just name it.....mh! What next..?


Unashangaa nini? Mbona kawaida tu. Unakumbuka enzi za mzee Mwinyi ambaye aliwatoa Watanzania katika lindi la umasikini wa njaa na udhalilishaji wa kuvaa magunia, kupanga foleni mchana kutwa kwa kilo ya unga wa muhogo aliishia kutukanwa matusi ya nguoni? Yanayompata JK yalishampa mzee rukhsa miaka 15 iliyopita.
 
Unashangaa nini? Mbona kawaida tu. Unakumbuka enzi za mzee Mwinyi ambaye aliwatoa Watanzania katika lindi la umasikini wa njaa na udhalilishaji wa kuvaa magunia, kupanga foleni mchana kutwa kwa kilo ya unga wa muhogo aliishia kutukanwa matusi ya nguoni? Yanayompata JK yalishampa mzee rukhsa miaka 15 iliyopita.
meaning what???!!!!
 
hakuna jammii yoyote hapa duniani na hata huko wanakokwenda watu kisha wasirudi wanapendezwa na wizi,unafiki,nguvu pasipotakiwa, uongo! wote kwa pamoja watasimama wima kupinga mambo hayo kwa nguvu zao zote ilimradi tu haki yao ipatikane!
 
Ukweli ni kwamba wananchi sasa wameweza kugundua kuwa wananyonywa na kulisiwa mali zao na watu wachache wanaofisadi nchi hii kana haina wengine isipokuwa wao na pengine nchi hii ilitengwa kwa ajili yao... lakini kwa sasa wakae mkao wa kuondoka maana watz wametambua udharimu wao!!
 
Yaani kwa kweli ni hatari tupu jinsi wandugu wa TZ wanavyoishambulia serikali pande zote kiasi kwamba zile kelele za mlango sasa zinaleta usumbufu kiasi cha kumkosesha JK usingizi murua tofauti na ilivyokuwa enzi anaingia ikulu baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Du, hali inatisha mazee kila kona: maredioni, magazetini, makanisani, misikitini, klabuni, vijijini, mijini, maofisini, mashambani, madukani, kwenye bar, uwanjani, mpirani, mahospitalini, jeshini, UWT, katika Facebook na hapa JF, kwenye NGO's, vijiweni hadi kwenye magesti, you just name it.....mh! What next..?


katika marais wetu watatu waliopita he is the one guy who doesnt stand for himself na nafikiri ushikaji umemponza vibaya sana. ithink hata katika mawaziri aliowachagua tangu 2005 hakuna hata mmoja anaeweza kumkemea so kwa kipindi kilichobakia anamalizia akapumzike ccm ianze kuhangaika 2015 bcs it will be broken very bad wanachi wamechoka na siasa za matapeli( i hope haitatokea serekali ya mseto sababu huo ni upuuzi mwingine unaoisumbua africa sasa hivi)
 
ndugu yakupasa kutulia,kutafakari na kisha unasema! siku zote nakushahuri ujifunze kuangalia leo yako na si jana yako, maana jana haina maana yoyote zaidi ya leo yako, na leo yako ndio inayotengeneza kesho yako!
 
Kikwete, what a hopeless leader!! He's the root of all these problems. I can not bare this a## h### anymore
 
When you are about to yake a city, fight becomes heavier. We are about to enter canaan if we keep perservering!
Just let us keep knoking and shouting for the Good of our country!!
 
Nakushangaa ndugu yangu kwanini unaita "DANGER?...HATARI TUPU?", kwanini usiseme NURU/HOPE FOR N\A NEW TANZANIA mana tushukuru mungu saiv watanzania wanaanza kufunguka macho na kuona mabaya yanayofanywa na serikali ya JK, Aluta Continua!
 
JK hajachaguliwa na waTanzania, bali kwa mujibu ya Kiravu na Makame ni asilmia 64 ya watu waliopiga kura, ambyo kwa idadi ya walipiga kura hiyo 64% ni watu chini ya milioni nane, sasa kwa nchi ya watu milioni 20 walijiandikisha kwenye daftari la kudumu, na amepata kura chini ya nusu, unategemea atamtawala nani?, na huu ni mwanzo tu baada ya miaka miwili atabwaga manyanga mwenyewe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom