Serikali Tuachieni wana CCM tupambane na TEC

Serikali Tuachieni wana CCM tupambane na TEC

Naishauri Serikali yangu isihangaike na TEC; hili suala tuangeachiwa CCM tunajua fitina za kushughulika na hawa watu sisi ndio chama Dume tuliyopigania na kudumisha uhuru wa nchi hii kwa miaka zaidi ya 60.

Maendeleo mnayoyaona hayakuja kwa bahati mbaya ni mipango madhubuti ya Chama Cha Mapinduzi. Hili suala tuachiwe sisi naona kama serikali itajipa majukumu mepesi wakati mambo ya kufanya ni mengi.

CCM Oyeee.

CCM wenyewe mnategemea mbeleko ya vyombo vya dola, sasa sijui ni TEC gani mtapambana nayo. Kwa taarifa yako nchi hii ni masikini hivi kwa kuendelea kuwa chini ya CCM. Wala nyie kukaa muda wote huo madarakani sio kwa sababu ya ubora, bali ni kwakuwa wananchi wengi ni makondoo.
 
Serikali haina dini na taasisi za kidini zijitenge kabisa na siasa. Vyama vya siasa vifanye kazi yao na makanisa yafanye kazi zao. Kuruhusu dini kuingilia ingilia mipango ya serikali ni utovu wa nidhamu.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
Serikali inawaumiza waumini kwa hiyo wakae kimya kama kondoo anayekwenda kuchinjwa?
 
Yes vinarekebishika kwenye HGA...
Sasa wale Maaskofu na usomi wao wameshindwa kuelewa nini??
Karekebisheni kwanza mkataba wa gas ya Mtwara, ndio muaminike kwenye mkataba wa huu wa bandari. Mikataba ya madini Magufuli aliivaa kichwa kichwa, leo hii kesi kibao ziko mahakamani na zote tunashindwa.
 
Uhuru mliupigania au mlienda kupewa kutumia kijana wenu MH. MWALIMU???
 
Serikali haina dini na taasisi za kidini zijitenge kabisa na siasa. Vyama vya siasa vifanye kazi yao na makanisa yafanye kazi zao. Kuruhusu dini kuingilia ingilia mipango ya serikali ni utovu wa nidhamu.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
Kama hujui kuwa suala la bandari sio siasa, kuna kitu chochote utakijua?
 
Yes vinarekebishika kwenye HGA...
Sasa wale Maaskofu na usomi wao wameshindwa kuelewa nini??
Mahakama haiwezi ikasema inapinga, Mahakama imeumia lugha ya Mwamuzi aliyepelekewa shauri alitolee maamuzi. Pi, Mahakama imekanganya, ndiyo maana walalamikaji hawajaridhishwa na hukumu hiyo na hivyo wamelipeleka mbel zaidi.
kIngine, Maadkofu hawajapinga uwekezaji, wamepinga aina ya Mkataba, na hicho unachosema Mahakama imesema 'Kurekebishika', maana yake na yenyewe imeona Mkataba huo una Mapungufu na ndiyo madai yaliyopo. So technically, hata Mahakama imepuma inaona una mapangufu, kinyume cha hapo ingetupilia mbali na kuwataka wafungua shauri kulipa gharama za kezi.

Sijui unaifuatilia hiyo flow vizuri?
 
Hahahaha! Chongolo kasitisha kuitetea DP Tulia anasema na yeye ni mwanasheria na kasoma sana dhidi ya wale wengine Sasa naloona hapa ni kama Kuna mikataba miwili yenye vipengele tofauti.

Yaani mkataba uliopitishwa bungeni sio ule unaodadavuliwa na akina Shivji, madeleka, Lisu, Nshala, Mwambukusi na wengineo ikiwamo TEC.
Nje kidogo ya mada, tutaludi. Kuna fujo fulani zinazoendana na barehe katika umri wa kijana.

Back to mada;
kuna fujo za hawa viongozi vijana zinazoshabihiana na zile za vijana katika lika la barehe. Fujo hizi ni barehe ya kimadaraka kwa hawa jamaa. Hii huenda sambamba na muda wao katika uongozi na shauku ya kuendelea kulamba asali. Kwenye kundi hili mweke Nape na Tulia. Matatizo ya fujo za kibarehe yanatatuliwa kwa kuwapumzisha hawa wahusika kwanza na kama bado wako tuwe nao makini fujo zao zitatuyumbisha. Ni hatari sana kuwapa madaraka ya juu hawa 'barehe kimadaraka'
Hao wawili ni mfano tu wako na walikuwako wengi. Mtoa mada pia yumo katika kundi hili. Kuna mambo yahitaji hekima kutatua sio kuimba ccm mbele kwa mbele. Sa100 angalia safu zako za washauri, unaweza kuwa na vichwa vyenye mvi lakini vina barehe ya kimadaraka. Sasa wote tulipita lika hili. Dawa yake mnaijua, vile vile itambulike "one mistake one goal"
 
CCM wenyewe mnategemea mbeleko ya vyombo vya dola, sasa sijui ni TEC gani mtapambana nayo. Kwa taarifa yako nchi hii ni masikini hivi kwa kuendelea kuwa chini ya CCM. Wala nyie kukaa muda wote huo madarakani sio kwa sababu ya ubora, bali ni kwakuwa wananchi wengi ni makondoo.
Haya matusi yenu kwa wananchi huwa yana wacost sana chadema ila hamjifunzi. Unawaita wananchi kondoo halafu hapo hapo unaomba kura? Ikulu nyie mtaisikilizia kwenye radio tu.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Wewe ulisoma hukumu ya mahakama??
Manake hivyo vipengele vyote vimejibiwa na mahakama
Mahakama hii inayoteuliwa viongozi na washika madaraka wa kisiasa. Mahakama hii inayosita kuroa hukumu kupisha ujio wa rais Mbeya. Hii hii...... !!!!! iliotaka kumtundika Mbowe na tuhuma za ugaidi na kumwachia pale rais alipotaka. Endelea wewe kuiamini mimi binafsi naiona kama tawi la ccm nukta
 
Unaweza kuta nyuma ya TEC kuna beberu USA sasa kama mnavyojua USA na mwarabu ugomvi wao ni wa karne.
 
Back
Top Bottom