Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Waziri wa Fedha, Philip Mpango amesema Serikali iliunda timu ya Kitaalamu inayochambua jambo hili kiumakini, na kipaumbele cha Serikali ni kukinga watohuduma za afya na Wananchi
Amesema kwa makadirio ya awali katika kipindi cha Machi hadi Septemba mwaka huu zinahitajika Tsh. Bilioni 382.5 kwa ajili ya kukabiliana na #COVID19 na hadi sasa Hazina imetoa Tsh. Bilioni 15.49 pamoja na nusu Bilioni zilizoenda Zanzibar
Ameeleza kuwa Serikali inaangaliza zaidi upatikanaji wa vifaa vya kujikinga (PPE), kuwakinga watoa huduma za afya, dawa, vifaa tiba, kuongeza vitanda, ventilators (mashine za kupumulia), magari ya wagonjwa na kuimarisha kambi za wagonjwa
Aidha, amesema wametoa ridhaa ya kusamehewa kodi kwa vifaa takriban 15 vinavyotumika kujikinga na #CoronaVirus kama alivyoomba Waziri wa Afya na vifaa hivi vitasamehewa ushuru wa forodha na VAT
Pia amesema "Tumefanya kazi ya kuchambua mafungu mbalimbali ambayo matumizi yake yanaweza kuahirishwa ili kuelekeza fedha hizo kwenye matumizi ya dharura"
Kukabiliana na Corona ni kipaumbele cha juu kabisa cha dharura cha awamu ya 5, hakuna serikali makini inayoweza kupuuza nguvukazi, watu wake fa ndi maana tunalipa umuhimu mkubwa jambo hili
Amesema kwa makadirio ya awali katika kipindi cha Machi hadi Septemba mwaka huu zinahitajika Tsh. Bilioni 382.5 kwa ajili ya kukabiliana na #COVID19 na hadi sasa Hazina imetoa Tsh. Bilioni 15.49 pamoja na nusu Bilioni zilizoenda Zanzibar
Ameeleza kuwa Serikali inaangaliza zaidi upatikanaji wa vifaa vya kujikinga (PPE), kuwakinga watoa huduma za afya, dawa, vifaa tiba, kuongeza vitanda, ventilators (mashine za kupumulia), magari ya wagonjwa na kuimarisha kambi za wagonjwa
Aidha, amesema wametoa ridhaa ya kusamehewa kodi kwa vifaa takriban 15 vinavyotumika kujikinga na #CoronaVirus kama alivyoomba Waziri wa Afya na vifaa hivi vitasamehewa ushuru wa forodha na VAT
Pia amesema "Tumefanya kazi ya kuchambua mafungu mbalimbali ambayo matumizi yake yanaweza kuahirishwa ili kuelekeza fedha hizo kwenye matumizi ya dharura"
Kukabiliana na Corona ni kipaumbele cha juu kabisa cha dharura cha awamu ya 5, hakuna serikali makini inayoweza kupuuza nguvukazi, watu wake fa ndi maana tunalipa umuhimu mkubwa jambo hili