JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
Mhe. Dkt Dugange ameyasema hayo wakati wa akijibu swali Mhe. Venant Daud Protas Mbunge wa Jimbo la Igalula katika kipindi cha maswali na majibu aliyeuliza “Je, Serikali haioni haja ya kuongeza umri kwa Vijana wa kiume wanaopata mikopo ya Halmashauri kufikia miaka 50.” katika Bunge la bajeti linaloendelea Jijini Dodoma.
Amesema, Mikopo ya asilimia 10 inatolewa kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa Sura 290 kifungu cha 37A ya Mwaka 2018 na Kanuni za Usimamizi na Utoaji wa Mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu za Mwaka 2024.
Amesema pia, Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa mikopo hii kwa mujibu wa sheria na kanuni, na kufanya maboresho pale itakapohitajika ili kuhakikisha ufanisi na uwiano katika utoaji wa fursa hizi.