Serikali izingatie haya ili bei ya mafuta nchini ishuke

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
SERIKALI IZINGATIE HAYA SAKATA LA KUPANDA BEI YA MAFUTA NCHINI ILI YASHUKE.

Na Bwanku M Bwanku.

Jana Ijumaa Mei 06, 2022 kwenye Gazeti la TANZANIA LEO Ukurasa wa 6 nimechambua Vita ya Urusi na Ukraine ilivyopaisha Sakata la Kupanda kwa Bei ya Mafuta kwenye Soko la Dunia kulikoathiri Bei Duniani kote ikiwemo nchini kwetu ambako Bei imeendelea kupanda na kupaa mwezi hadi mwezi. Kupitia Makala hii na kwa unyenyekevu mkubwa sana, nimeishauri Serikali yangu kuzisitisha kwa muda au kuzifuta baadhi ya tozo na kodi kwenye Mafuta hasa zile zisizoenda moja kwa moja kwenye Maendeleo ili kumtua mzigo huu mzito Mtanzania wa kupaa kwa Bei ya Mafuta.

Tanzania mpaka sasa ina tozo na kodi zaidi ya 19 kwenye Mafuta hivyo licha ya Bei ya Mafuta kupanda kwenye Soko la Dunia lakini Kodi na tozo hizi zinachangia pia pakubwa kupandisha Bei nchini, hivyo Kodi kama ya TASAC, EWURA, TBS, Excise Duty na zingine kama hizo ambazo haziendi kwenye Maendeleo moja kwa moja, Serikali ichukue hatua ya kuzisimamisha kwa muda au kuzifuta kwa kipindi hiki cha mpito ambacho Dunia na Taifa linapitia kupaa kwa Bei ya Mafuta ili ku-rescue situation kwasababu Bei hizi zinavyozidi kupanda, inazidi kupandisha Bei ya bidhaa na huduma pia na kuzidi kuongeza ugumu wa maisha maana mafuta ni Runner wa Uchumi.
IMG-20220506-WA0017.jpg


IMG-20220506-WA0016.jpg
 
1 Litre of Petrol

1.Total cost CIF to Dar port 1,162
2. Wharfage 20.5
3. Railway devl levy 19.4
5. Customs processing fee 6.0
5. Weights & measures fee 5.6
6. TBS charge 10.0
7. TASAC fee 8.7
8. EWURA fee 9.0
9. Fuel making 16.0
10. Demurrage costs 8.0
11. Surveyors cost 8.00
12. Financial cost 17.0
13. Evaporation losses 6.5
14. Fuel levy 513.00
15. Excise duty 479.0
16. Petroleum fee 180.0
17. Oil marketing companies 163.0
18. Charges to executive agencies 6.0
19. Service levy to LGA 6.7
20. Retailers margin (profit) 210.5
21. Transport charges (local) 50.5

Total Levy 1,743.4
Plus TC 1,162

Total cost 2,905.4 @Wabunge wetu,huo mzigo wa 1,743.4 yote mlaji wa mwisho,Wananchi wenu wanakwenda kulipa kwa kila lita moja ya mafuta, yaani kodi ni kubwa kuliko bei halisi ya mafuta🤣 Tanzania nchi yaanguu..!
 
SERIKALI IZINGATIE HAYA SAKATA LA KUPANDA BEI YA MAFUTA NCHINI ILI YASHUKE.

Na Bwanku M Bwanku.

Jana Ijumaa Mei 06, 2022 kwenye Gazeti la TANZANIA LEO Ukurasa wa 6 nimechambua Vita ya Urusi na Ukraine ilivyopaisha Sakata la Kupanda kwa Bei ya Mafuta kwenye Soko la Dunia kulikoathiri Bei Duniani kote ikiwemo nchini kwetu ambako Bei imeendelea kupanda na kupaa mwezi hadi mwezi. Kupitia Makala hii na kwa unyenyekevu mkubwa sana, nimeishauri Serikali yangu kuzisitisha kwa muda au kuzifuta baadhi ya tozo na kodi kwenye Mafuta hasa zile zisizoenda moja kwa moja kwenye Maendeleo ili kumtua mzigo huu mzito Mtanzania wa kupaa kwa Bei ya Mafuta.

Tanzania mpaka sasa ina tozo na kodi zaidi ya 19 kwenye Mafuta hivyo licha ya Bei ya Mafuta kupanda kwenye Soko la Dunia lakini Kodi na tozo hizi zinachangia pia pakubwa kupandisha Bei nchini, hivyo Kodi kama ya TASAC, EWURA, TBS, Excise Duty na zingine kama hizo ambazo haziendi kwenye Maendeleo moja kwa moja, Serikali ichukue hatua ya kuzisimamisha kwa muda au kuzifuta kwa kipindi hiki cha mpito ambacho Dunia na Taifa linapitia kupaa kwa Bei ya Mafuta ili ku-rescue situation kwasababu Bei hizi zinavyozidi kupanda, inazidi kupandisha Bei ya bidhaa na huduma pia na kuzidi kuongeza ugumu wa maisha maana mafuta ni Runner wa Uchumi. Pata Nakala ya Gazeti letu sasa usome au soma Makala yangu na Gazeti lote kupitia Link hapo chini.

👇🏿👇🏿👇🏿👇🏿

View attachment 2214854

View attachment 2214855
Naunga mkono hoja
Huu ndio uzalendo wa kweli wa taifa lako
P
 
Na kwa kuongezea makampuni mengi makubwa ya madini na wenye mashamba makubwa saana ,

Wana nafuu kubwa katika kodi zoote ikiwemo bei za mafuta ( ambao wanapata kwa takriban sh 655 pungufu) .

Anayeumia saaana ni mwananchi wa kawaida.
Mwenye lori, mabasi, biashara woote watapandisha iwe nauli au bei za vitu.

Wananchi wa kawaida siku zoote wana beba mzigo mkubwa na hawasikilizwi illa padogo saana.
 
Back
Top Bottom