Mganguzi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2022
- 1,032
- 2,769
Niliingia mahabusu moja nikalala usiku mmoja ,sikuamini kama nipo Tanzania ,watu wanahojiwa kwa kupigwa na vyuma na wanavunjwa mifupa ,mtu analetwa akiwa mzima na anatoka akiwa mlemavu!
Jeshi la polisi halina mbinu nyingine ya kipelelezi lazima watumie virungu? Interjensia inayosemwa kila siku iko wapi ? Watu wanavunjwa kende anatoka polisi ni hanithi, na asilimia kubwa ya hawa wanaovunjwa miguu ni watoto wa maskini wasio na kitu ,ni wale wanaotuhumiwa tu na bado mahakama haijathibitisha kama ni kweli wengi wao ni wenye vikesi vidogo vidogo ,kama kukutwa anakunywa gongo ,kutembea usiku ,wizi wa simu au vibaka na wadokozi wa vimiamia.
Lakini huko serikalini tunasikia mafisadi na wezi wa mabilioni na mabilioni ,hawaguswi hata na ncha ya njiti ya kiberiti ,wale wanaomiliki ardhi mahekali na mahekali kwa njia za utapeli wapo tu na mavx mitaani ,kwanini viongozi wa juu hawataki kufuatilia kinachotendeka vituo vya polisi ?
Waziri Masauni umewahi kufanya tathmini ya walemavu walioupata ulemavu wao wakiwa wanahojiwa na polisi? Ni lini sheria itatungwa ya kumlinda raia na uonevu wa polisi na watapataje fidia pale wanapopata ulemavu wakiwa kwenye vituo vya polisi?
Tafadhali kama kuna mtu sasa anaweza kuwa miongoni mwa wahanga wa mateso ya polisi wakiwa centre police tuungane kudai haki ya kulipwa fidia ,wanasheria wawasaidie waathirika waliosababishiwa ulemavu na polisi na hawana la kufanya ,wakati mwingine maisha ya polisi yanakuwa magumu sana kwa sababu ya laana za wananchi ,tuamke polisi sio miungu!
Jeshi la polisi halina mbinu nyingine ya kipelelezi lazima watumie virungu? Interjensia inayosemwa kila siku iko wapi ? Watu wanavunjwa kende anatoka polisi ni hanithi, na asilimia kubwa ya hawa wanaovunjwa miguu ni watoto wa maskini wasio na kitu ,ni wale wanaotuhumiwa tu na bado mahakama haijathibitisha kama ni kweli wengi wao ni wenye vikesi vidogo vidogo ,kama kukutwa anakunywa gongo ,kutembea usiku ,wizi wa simu au vibaka na wadokozi wa vimiamia.
Lakini huko serikalini tunasikia mafisadi na wezi wa mabilioni na mabilioni ,hawaguswi hata na ncha ya njiti ya kiberiti ,wale wanaomiliki ardhi mahekali na mahekali kwa njia za utapeli wapo tu na mavx mitaani ,kwanini viongozi wa juu hawataki kufuatilia kinachotendeka vituo vya polisi ?
Waziri Masauni umewahi kufanya tathmini ya walemavu walioupata ulemavu wao wakiwa wanahojiwa na polisi? Ni lini sheria itatungwa ya kumlinda raia na uonevu wa polisi na watapataje fidia pale wanapopata ulemavu wakiwa kwenye vituo vya polisi?
Tafadhali kama kuna mtu sasa anaweza kuwa miongoni mwa wahanga wa mateso ya polisi wakiwa centre police tuungane kudai haki ya kulipwa fidia ,wanasheria wawasaidie waathirika waliosababishiwa ulemavu na polisi na hawana la kufanya ,wakati mwingine maisha ya polisi yanakuwa magumu sana kwa sababu ya laana za wananchi ,tuamke polisi sio miungu!