Serikali inapokosolewa kwa Constructive Criticism, je, Ifuate Ushauri? Hongera Bunge letu tukufu kufuata ushauri na kutuondolea ubatili huu

Barua ya marekebisho bila Shaka iliandikwa baada ya wiki 2 kupita, lakini tarehe ikawa hiyo hiyo 6 January! Kwa maana hiyo, hiyo ni barua ya kughushi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Hapana, ile sio barua ya kughushi, kama mwandishi ni wewe, ukiandika mwanzo, ukakosea, uka withdraw na kupeleka barua sahihi, sio kughushi, hoja za kisheria kuhusu barua ile nimeizungumza kupitia kitu kinachoitwa, halali, batili na batilifu. Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge?
Barua ya kwanza ilikuwa batilifu, kwenye ubatilifu ubatilifu ukiondolewa inakuwa halali bila kughushi chochote!.
P
 
Kwa ni sawa serikali kusema uongo mahakamani? Huoni kuwa ni hatari nchi kuongozwa na viongozi wanaokosa uadilifu kiasi cha "kutengeneza" barua ya uongo na kuipeleka mahakamani?
No sio barua ya uongo, ni barua ya ukweli, kwasababu hakuna yoyote aliyeiona ile barua ya mwanzo zaidi ya kuhadithiwa kwenye ile press release ya Bunge. Mahakama inafanyia kazi, kile kitu kilicholetwa mbele yake, kilicho pelekwa mbele ya mahakama ni barua, bonafide genuine.
P
 
Asante sana Mayalla kwa udadavuzi wako kwa Katiba ya Jamhuri...

Pamoja na kwamba shauri la Mbatia lilitupwa ila binafsi naona Mbatia ndio mshindi maana amewafanya wafanye vile katiba inataka.
 
No sio barua ya uongo, ni barua ya ukweli, kwasababu hakuna yoyote aliyeiona ile barua ya mwanzo zaidi ya kuhadithiwa kwenye ile press release ya Bunge. Mahakama inafanyia kazi, kile kitu kilicholetwa mbele yake, kilicho pelekwa mbele ya mahakama ni barua, bonafide genuine.
P
Mahakamani kuna sheria tu, ukweli na haki havipatikani mahakani. Swali ni je ile press release ya bunge ilitolewa na mwendawazimu? Kwanini sasa wanazidoa kwenye website yao? Wanasheria mnapenda kujiita wasomi ila msomi asiyejiuliza maswali ni mjinga japo amekaa darani
 
Mahakamani kuna sheria tu, ukweli na haki havipatikani mahakani. Swali ni je ile press release ya bunge ilitolewa na mwendawazimu? Kwanini sasa wanazidoa kwenye website yao? Wanasheria mnapenda kujiita wasomi ila msomi asiyejiuliza maswali ni mjinga japo amekaa darani
Mkuu Gulwa, kwanza heshima kitu cha bure, makosa ya kibinaadamu ni kitu cha kawaida kwenye maisha, usiite watu wendawazimu kwa human mistakes hata Press Release za Ikulu sometimes zinamakosa madogo madogo.

Ile Press Release ya Bunge iliyosema barua imepelekwa CCM ndicho Chanzo cha yote, hivyo baada ya marekebisho, hiyo taarifa lazima iondolewe, hivyo imeisha ondolewa kwenye Website ya Bunge.
P
 
Wanabodi,
Hii ni Nipashe ya Leo, 30.01.2022
View attachment 2100761
Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa huteremka na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" leo ni swali na pongezi. "Serikali inapokosolewa kwa constructive criticism, kama ushauri uliotolewa ni ushauri nzuri wenye maslahi kwa taifa, jee serikali ifuate ushauri huo, au iupuuzie kwa kushupaza shingo?. Hongera sana Bunge letu Tukufu kwa kufuata ushauri na kutuondolea ubatili katika Barua ya kujiuzulu Spika JYN!.

Kikawaida ni a being, ila sio human, hivyo serikali haiwezi kukosea jambo lolote, lakini serikali inaendeshwa na watu na inaongozwa na watu, human beings, watu hao wanaoongoza serikali ni binadamu na sio malaika, hivyo wanaweza kukosea, watu hao wanapokosea, inahesabika kuwa ni serikali ndio imekosea, hivyo serikali inapokosea au kwa kukosea yenyewe au kwa kukoseshwa, lazima ikubali kuwajibika kwa makosa hayo. Japo nimesema serikali kama serikali haiwezi kukosea, ila watendaji ndio wanaokosea na kuikosesha serikali.

Kila serikali inapofanya makosa, sometimes huwa kunatokea watu wenye jicho tunduizi, ambao wanaona makosa hayo na kuikosoa serikali kwa kutumia ukosoaji wa ujengaji (constructive criticism) ambao hufanyika kwa kuonyesha kosa lililofanyika na wakati huo huo kutoa mapendekezo ya jinsi ya kurekebisha makosa na kushauri a way forward kurekebisha makosa yaliyofanyika yasijirudie na maisha yaendelee. Naishauri serikali yetu tukufu, pale inapokosolewa kwa makosa ya wazi, kwanza isikasirike, pili ifuate ushauri na kurekebisha makosa na kujitahidi makosa kama hayo yasijirudie. Kitendo cha serikali kukubali kosa, not expressly but impliedly kwa kurekebisha kosa bila kukiri kosa, kwa kupokea ushauri, sio udhaifu ni uimara, na kuonyesha serikali yetu ni serikali sikivu.

Moja ya makala yangu ya nyuma, nilishauri, viongozi wa kisiasa na wa serikali, wanapofanya makosa ya wazi na kuifanya serikali ionekane imekosea, wanapaswa kwanza kukubali makosa, kuomba msamaha na kuwajibika. Hiki ndicho kilichofanyika kwa Spika aliyejiuzulu, Mhe. Job Ndugai, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kwanza alikubali makosa, kisha akaomba msamaha, japo msamaha wenyewe ulikuwa ni msamaha batili Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu!
akidhani atasamehewa, na baada ya kuomba msamaha huo batili, sisi waona mbali tukashauri, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away? na baada ya shinikizo, ndipo JYN akakubali kujiuzulu ila huku nako alikurupuka na kuandika barua batili, hatukukaa kimya, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Taarifa ya kujiuzulu uspika ya Spika Mhe. Job Ndugai kwa vyombo vya habari, iliyosambazwa na ofisi ya Bunge, ni hii
View attachment 2100870
Taarifa hii ya Ofisi ya Bunge kwa vyombo vya habari, illionyesha Spika Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu na kuilekeza kwa Katibu Mkuu wa CCM na nakala ofisi ya Bunge. Msemaji wa Katibu Mkuu wa CCM akakiri kuipokea barua hiyo, na Ofisi ya Bunge ikakiri kupokea nakala ya barua hiyo kutoka CCM.

Taarifa hiyo ya kujiuzulu ilisababisha mjadala mkubwa wa kwanini ipelekwe CCM badala ya ofisi ya Bunge kama katiba inavyoelekeza. Mjadala huo ulihitimishwa na taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa alichokifanya Spika Ndugai kuandika barua CCM badala ya Bungeni ni sawa tuu. Mimi nami nikaweka ukosoaji wangu ila ukosoaji wangu ulikuwa ni a constructive criticism kwa kukosoa na kushauri kitu sahihi cha kufanyika. Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge?

Mimi nilisema jambo fulani likielekezwa na katiba namna ya kufanyika, hakuna tena mjadala lifanyikeje, ni lazima lifanyike kwa jinsi ile ile katiba ilivyoelekeza, likifanyika kinyume, linakuwa ni batili au batilifu. Hivyo nilionyesha kifungu cha katiba kinachoekeza Spika akijiuzulu barua yake ya kujiuzulu inaandikwa kwa nani.

Ibara hii ya 149 1 (c) ya Katiba imeelekeza Spika akijiuzulu, ataandika barua kuliarifu Bunge. Kitu kikiishwa elekezwa na katiba namna ya kufanyika, kikifanyika kwa namna nyingine yoyote kinyume cha katiba, kitu hicho ni batili. Kujiuzulu halali ni kuandika barua kwa mamlaka yako ya uteuzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Spika kwa vyombo, imearifu ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na copy kwa Katibu wa Bunge. Katiba imeelekeza barua ya kujiuzulu Spika, itatumwa kwa Bunge. Kitendo cha Spika kuandika barua na kuituma kwa CCM kabla ya Bungeni, kumeifanya Barua ya Spika kuwa Batilifu, Bila huo ubatilifu kuondolewa, then barua hiyo imekuwa ni barua barua batili!. Katibu Mkuu wa CCM ametoa taarifa ya kupokea barua ya kujiuzulu Spika na tayari ameliarifu Bunge kuhusu kujiuzulu huko, na Bunge limeipokea taarifa hiyo b
atilifu hivyo hivyo ubatili wake na kuikubali. Huu ni ubatili!. Kama Bunge ndio mhimili wa kutunga sheria, Bunge lisipofuata katiba kwa kuukubali ubatili, nani atafuata katiba?.

Haki ya CCM Kupokea barua ya kujiuzulu, ni kama Mhe Spika JYN angejiuzulu uanachama wa CCM, hivyo kupoteza ubunge wake na uspika, ndipo CCM ingeliarifu Bunge.

Jee tuliruhusu Bunge letu tukufu kukumbatia ubatili katika madogo, jee ubatili huu ukihamia katika makubwa, nani atakuwa na jeuri ya kulihoji Bunge?
Hivyo nilitoa ushauri ufuatao
  1. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, kufuatia taarifa kupelekwa mahali kusikohusika, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu tuu, yaani Spika Ndugai ameishajiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua yake ya kujiuzulu uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
  2. Kwa vile tayari CCM imeisha kiri kuipokea barua ile batilifu, Bunge nalo limekiri kuipokea barua kutoka CCM, marekebisho ya kuondoa ubatili huu, yafanyike kimya kimya. Spika mstaafu aelekezwe kuandika barua nyingi na Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, for filing kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Kufuatia ubatili huu, Kiongozi wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, amefungua shauri Mahakama Kuu kuupinga ubatili huu, serikali ikaleta mahakamani barua rasmi ya Spika Ngugai kujiuzulu Uspika, ambayo imeonyesha Spika Ndugai, amejiuzulu kwa mujibu wa katiba, ni hii
View attachment 2100876
Barua hii ni utekelezaji wa ule ushauri wangu wa iandikwe barua nyingine kimya kimya na kuireplece ile barua batili. Barua yenyewe rasmi sasa ndio hii, na ndiyo iliyopelekea shauri la Mbatia kutupwa!. Japo ile taarifa ya kujiuzulu batili imeoishaondolewa kwenye website ya Bunge, lakini taarifa za CCM kuipokea barua batili ile ziliishatolewa na Bunge kuipokea barua batili ile ziliisha tolewa, ila ukienda kwenye files, hukuti tena barua batili, sasa utakutana na barua halali.

Natoa wito wa dhati kwa Serikali yangu, kukosea makosa madogo madogo is not a sin, to err is a human nature, kunapotokea makosa madogo madogo kama haya, na serikali kukosolewa, ni vitu vido tuu vya kurekebisha makosa na maisha yakaendelea. Serikali yetu ingekuwa inakubali makosa na kufuata ushauri, hii sintofahamu yote hadi kufikishana mahakamani, tusingefika huku kote. Hili jambo lilikuwa ni jambo dogo tuu, baada ya Bunge kutoa taarifa ya kujiuzulu kwa Spika Ndugai ikionyesha ameandika barua CCM, badala ya Ofisi ya Bunge, Bunge lingetoa taarifa ya pili kuonyeshea kulifanyika kosa dogo kwa barua kuelekezwa CCM, badla ya Ofisi ya Bungena kuonyesha kuwa Barua imeandikwa kwa Katibu wa Bunge na copy ndio kupalekwa CCM.

Unapokosoa kwa kuandika na kushauri, kitu cha kufanyika, halafu ukaona ushauri wako umefuatwa kama ulivyo, na makosa yamerekebishwa kama ulivyoshauri, huna budi kuandika tena na kutoa pongezi kwa serikali yetu kuwa ni serikali sikivu na kuuondoa ubatili ule, hivyo hapa nalipongeza Bunge letu Tukufu kwa kuondoa ubatili wa Barua ya Kujiuzulu kwa Spika Ndugai sasa imefuata katiba. Hongera sana kwa hili.

Sasa kumebakia ubatili mmoja tuu wa Naibu Spika, ajiuzulu kwanza nafasi ya unaibu Spika kabla ya kugombea Uspika na akiisha jiuzulu uNaibu Spika, ndipo angombee Uspika.

Nawatakia Jumapili Njema.
Wasalaam

Paskali
Mkuu, kwamba mahakama imepata nyaraka iliyofichika ambayo. Hata Job ndugai hailewi.. imewasilishwa na nani?
Kwa kifupi mahakama ingetakiwa ifanye kazi kikatba then spika hakiri kutokufuata utaratibu wa kujiuzulu .... na hapewe nafasi upya ya kuita press. Ndipo harusiwe kujiuzulu mamna sheria inavyotaka ..
Wenda ndugai haelewi taratibu, namna spika anavyojiuzulu .
 
Mkuu, kwamba mahakama imepata nyaraka iliyofichika ambayo. Hata Job ndugai hailewi.. imewasilishwa na nani?
Kwa kifupi mahakama ingetakiwa ifanye kazi kikatba then spika hakiri kutokufuata utaratibu wa kujiuzulu .... na hapewe nafasi upya ya kuita press. Ndipo harusiwe kujiuzulu mamna sheria inavyotaka ..
Wenda ndugai haelewi taratibu, namna spika anavyojiuzulu .
Ni kuchanganyikiwa tuu,
na tuliisha muombea msamaha Msameheni bure Job Ndugai, amechanganyikiwa baada ya kuomba msamaha batilifu uliokataliwa! Barua yake ya Kujiuzulu nayo pia ni batilifu!
hayo marekebisho yamefanywa na JYN mwenyewe ila hawakuandaa Press Release nyingine, the document is authentic bonafide genuine.
P
 
Wanabodi,
Hii ni Nipashe ya Leo, 30.01.2022
View attachment 2100761
Kama kawaida yangu, kila nipatapo fursa huteremka na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" leo ni swali na pongezi. "Serikali inapokosolewa kwa constructive criticism, kama ushauri uliotolewa ni ushauri nzuri wenye maslahi kwa taifa, jee serikali ifuate ushauri huo, au iupuuzie kwa kushupaza shingo?. Hongera sana Bunge letu Tukufu kwa kufuata ushauri na kutuondolea ubatili katika Barua ya kujiuzulu Spika JYN!.

Kikawaida ni a being, ila sio human, hivyo serikali haiwezi kukosea jambo lolote, lakini serikali inaendeshwa na watu na inaongozwa na watu, human beings, watu hao wanaoongoza serikali ni binadamu na sio malaika, hivyo wanaweza kukosea, watu hao wanapokosea, inahesabika kuwa ni serikali ndio imekosea, hivyo serikali inapokosea au kwa kukosea yenyewe au kwa kukoseshwa, lazima ikubali kuwajibika kwa makosa hayo. Japo nimesema serikali kama serikali haiwezi kukosea, ila watendaji ndio wanaokosea na kuikosesha serikali.

Kila serikali inapofanya makosa, sometimes huwa kunatokea watu wenye jicho tunduizi, ambao wanaona makosa hayo na kuikosoa serikali kwa kutumia ukosoaji wa ujengaji (constructive criticism) ambao hufanyika kwa kuonyesha kosa lililofanyika na wakati huo huo kutoa mapendekezo ya jinsi ya kurekebisha makosa na kushauri a way forward kurekebisha makosa yaliyofanyika yasijirudie na maisha yaendelee. Naishauri serikali yetu tukufu, pale inapokosolewa kwa makosa ya wazi, kwanza isikasirike, pili ifuate ushauri na kurekebisha makosa na kujitahidi makosa kama hayo yasijirudie. Kitendo cha serikali kukubali kosa, not expressly but impliedly kwa kurekebisha kosa bila kukiri kosa, kwa kupokea ushauri, sio udhaifu ni uimara, na kuonyesha serikali yetu ni serikali sikivu.

Moja ya makala yangu ya nyuma, nilishauri, viongozi wa kisiasa na wa serikali, wanapofanya makosa ya wazi na kuifanya serikali ionekane imekosea, wanapaswa kwanza kukubali makosa, kuomba msamaha na kuwajibika. Hiki ndicho kilichofanyika kwa Spika aliyejiuzulu, Mhe. Job Ndugai, Viongozi wetu wanapofanya makosa ya wazi waishie tu kuomba msamaha kisha 'life as usual', au tujenge utamaduni wa kuwajibika kama enzi za Nyerere? kwanza alikubali makosa, kisha akaomba msamaha, japo msamaha wenyewe ulikuwa ni msamaha batili Ndoa halali, ndoa batili na ndoa batilifu. Je, wajua pia kuna msamaha halali wa kweli, msamaha batili na msamaha batilifu? Msamaha ule ni batilifu!
akidhani atasamehewa, na baada ya kuomba msamaha huo batili, sisi waona mbali tukashauri, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away? na baada ya shinikizo, ndipo JYN akakubali kujiuzulu ila huku nako alikurupuka na kuandika barua batili, hatukukaa kimya, Baada ya maneno haya ya Rais Samia, kama ni timamu, je, tumshauri to do "The needful?" au akomae nao, till they do him away?

Taarifa ya kujiuzulu uspika ya Spika Mhe. Job Ndugai kwa vyombo vya habari, iliyosambazwa na ofisi ya Bunge, ni hii
View attachment 2100870
Taarifa hii ya Ofisi ya Bunge kwa vyombo vya habari, illionyesha Spika Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu na kuilekeza kwa Katibu Mkuu wa CCM na nakala ofisi ya Bunge. Msemaji wa Katibu Mkuu wa CCM akakiri kuipokea barua hiyo, na Ofisi ya Bunge ikakiri kupokea nakala ya barua hiyo kutoka CCM.

Taarifa hiyo ya kujiuzulu ilisababisha mjadala mkubwa wa kwanini ipelekwe CCM badala ya ofisi ya Bunge kama katiba inavyoelekeza. Mjadala huo ulihitimishwa na taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa alichokifanya Spika Ndugai kuandika barua CCM badala ya Bungeni ni sawa tuu. Mimi nami nikaweka ukosoaji wangu ila ukosoaji wangu ulikuwa ni a constructive criticism kwa kukosoa na kushauri kitu sahihi cha kufanyika. Je, wajua haramu isipoharimishwa inageuka halali? Na batili isipobatilishwa inageuka halali. Je, tuhalalishe ubatili huu kwa mhimili wetu wa Bunge?

Mimi nilisema jambo fulani likielekezwa na katiba namna ya kufanyika, hakuna tena mjadala lifanyikeje, ni lazima lifanyike kwa jinsi ile ile katiba ilivyoelekeza, likifanyika kinyume, linakuwa ni batili au batilifu. Hivyo nilionyesha kifungu cha katiba kinachoekeza Spika akijiuzulu barua yake ya kujiuzulu inaandikwa kwa nani.

Ibara hii ya 149 1 (c) ya Katiba imeelekeza Spika akijiuzulu, ataandika barua kuliarifu Bunge. Kitu kikiishwa elekezwa na katiba namna ya kufanyika, kikifanyika kwa namna nyingine yoyote kinyume cha katiba, kitu hicho ni batili. Kujiuzulu halali ni kuandika barua kwa mamlaka yako ya uteuzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Spika kwa vyombo, imearifu ameandika barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na copy kwa Katibu wa Bunge. Katiba imeelekeza barua ya kujiuzulu Spika, itatumwa kwa Bunge. Kitendo cha Spika kuandika barua na kuituma kwa CCM kabla ya Bungeni, kumeifanya Barua ya Spika kuwa Batilifu, Bila huo ubatilifu kuondolewa, then barua hiyo imekuwa ni barua barua batili!. Katibu Mkuu wa CCM ametoa taarifa ya kupokea barua ya kujiuzulu Spika na tayari ameliarifu Bunge kuhusu kujiuzulu huko, na Bunge limeipokea taarifa hiyo b
atilifu hivyo hivyo ubatili wake na kuikubali. Huu ni ubatili!. Kama Bunge ndio mhimili wa kutunga sheria, Bunge lisipofuata katiba kwa kuukubali ubatili, nani atafuata katiba?.

Haki ya CCM Kupokea barua ya kujiuzulu, ni kama Mhe Spika JYN angejiuzulu uanachama wa CCM, hivyo kupoteza ubunge wake na uspika, ndipo CCM ingeliarifu Bunge.

Jee tuliruhusu Bunge letu tukufu kukumbatia ubatili katika madogo, jee ubatili huu ukihamia katika makubwa, nani atakuwa na jeuri ya kulihoji Bunge?
Hivyo nilitoa ushauri ufuatao
  1. Japo Spika Mhe. JYN tayari ameisha jiuzulu uspika, kujiuzulu huko, japo ni kujiuzulu batilifu, kufuatia taarifa kupelekwa mahali kusikohusika, lakini kujiuzulu ni kujiuzulu tuu, yaani Spika Ndugai ameishajiuzulu, lakini kwa kuheshimu katiba, lazima ubatili katika barua yake ya kujiuzulu uondolewe kwa kuandikwa barua rasmi kwa mujibu wa katiba.
  2. Kwa vile tayari CCM imeisha kiri kuipokea barua ile batilifu, Bunge nalo limekiri kuipokea barua kutoka CCM, marekebisho ya kuondoa ubatili huu, yafanyike kimya kimya. Spika mstaafu aelekezwe kuandika barua nyingi na Bunge lipokee kimya kimya barua mpya ya kujiuzulu kwa Spika iliyoandikwa kwa mujibu wa katiba, for filing kisha Bunge ndio litoe copy kwa CCM.
Kufuatia ubatili huu, Kiongozi wa NCCR Mageuzi, James Mbatia, amefungua shauri Mahakama Kuu kuupinga ubatili huu, serikali ikaleta mahakamani barua rasmi ya Spika Ngugai kujiuzulu Uspika, ambayo imeonyesha Spika Ndugai, amejiuzulu kwa mujibu wa katiba, ni hii
View attachment 2100876
Barua hii ni utekelezaji wa ule ushauri wangu wa iandikwe barua nyingine kimya kimya na kuireplece ile barua batili. Barua yenyewe rasmi sasa ndio hii, na ndiyo iliyopelekea shauri la Mbatia kutupwa!. Japo ile taarifa ya kujiuzulu batili imeoishaondolewa kwenye website ya Bunge, lakini taarifa za CCM kuipokea barua batili ile ziliishatolewa na Bunge kuipokea barua batili ile ziliisha tolewa, ila ukienda kwenye files, hukuti tena barua batili, sasa utakutana na barua halali.

Natoa wito wa dhati kwa Serikali yangu, kukosea makosa madogo madogo is not a sin, to err is a human nature, kunapotokea makosa madogo madogo kama haya, na serikali kukosolewa, ni vitu vido tuu vya kurekebisha makosa na maisha yakaendelea. Serikali yetu ingekuwa inakubali makosa na kufuata ushauri, hii sintofahamu yote hadi kufikishana mahakamani, tusingefika huku kote. Hili jambo lilikuwa ni jambo dogo tuu, baada ya Bunge kutoa taarifa ya kujiuzulu kwa Spika Ndugai ikionyesha ameandika barua CCM, badala ya Ofisi ya Bunge, Bunge lingetoa taarifa ya pili kuonyeshea kulifanyika kosa dogo kwa barua kuelekezwa CCM, badla ya Ofisi ya Bungena kuonyesha kuwa Barua imeandikwa kwa Katibu wa Bunge na copy ndio kupalekwa CCM.

Unapokosoa kwa kuandika na kushauri, kitu cha kufanyika, halafu ukaona ushauri wako umefuatwa kama ulivyo, na makosa yamerekebishwa kama ulivyoshauri, huna budi kuandika tena na kutoa pongezi kwa serikali yetu kuwa ni serikali sikivu na kuuondoa ubatili ule, hivyo hapa nalipongeza Bunge letu Tukufu kwa kuondoa ubatili wa Barua ya Kujiuzulu kwa Spika Ndugai sasa imefuata katiba. Hongera sana kwa hili.

Sasa kumebakia ubatili mmoja tuu wa Naibu Spika, ajiuzulu kwanza nafasi ya unaibu Spika kabla ya kugombea Uspika na akiisha jiuzulu uNaibu Spika, ndipo angombee Uspika.

Nawatakia Jumapili Njema.
Wasalaam

Paskali
Hii the so called Barua rasmin ni Ubatili Mtupu
Imeandikwa baada ya Mbatia ku file kesi, tena huenda hata hakaandika Ayubu Mwenyewe
 
Ile Press Release ya Bunge iliyosema barua imepelekwa CCM ndicho Chanzo cha yote, hivyo baada ya marekebisho, hiyo taarifa lazima iondolewe, hivyo imeisha ondolewa kwenye Website ya Bunge.
P
Sema walikosea.
Na walirekebisha baada ya kukosolewa.
Chukua credit were due.
Tusonge mbele kuisaka Katiba Bora!
 
Ile Press Release ya Bunge iliyosema barua imepelekwa CCM ndicho Chanzo cha yote, hivyo baada ya marekebisho, hiyo taarifa lazima iondolewe, hivyo imeisha ondolewa kwenye Website ya Bunge.
P
Press release ilipaswa kueleza barua imewasilishwa kwa katibu wa Bunge

Bunge lina wanasheria waliopaswa kumshauri Spika Ndugai nini cha kufanya katika mkanganyiko

Mh Mbatia alieleza nia ya kwenda Mahakamani kufuatia press release. Katika mazingira ya kawaida kama barua ilikuwepo ingetolewa bila kusubiri na kupoteza muda wa kuitoa Mahakamani

Hata kama Ndugai angechelewa kuipeleka , busara ilikuwa kutoka na kuomba radhi, au basi kueleza tu kuwa amepeleka tena kwa katibu wa Bunge katika tarehe tofauti.
Kumbuka 'Ndugai had nothing to lose''

Kwa ushauri wako bw. Pascal ni mzuri kwa nchi zisizofauta taratibu kama Tanzania.

Laiti ingalikuwa nchi nyingine tayari kungekuwa na harufu ya ''forgery' kwa maana kwamba uchunguzi ulitakiwa kubaini ni lini barua ilisajiliwa kwa Katibu wa Bunge

Kama ingebainika hakuna tatizo umma ungejulishwa.

Ingebainika kuna 'ushauri wa pascal uliofanyiwa kazi'' watu wangepukutishwa akiwemo katibu wa Bunge kwa kukubali barua iliyoghushiwa tarehe ya usajili na pengine kutumika mahakamani.

JokaKuu
 
Hivi Ndugai kesho akigeuka na kusema yeye hajawamhi kujiuzuru uspeaker,

Ya lipumba Yana weza jirudia.

Nadhani hizi barua zote wameandika kitengo.


Sema mafao ni makubwa mno kwa speaker kuleta choko choko.
 
Hii the so called Barua rasmin ni Ubatili Mtupu
Imeandikwa baada ya Mbatia ku file kesi, tena huenda hata hakaandika Ayubu Mwenyewe
Barua ya mwanzo ndio ilikuwa na ubatili, barua hii ya sasa is perfekt.
Kuondoa ubatilifu kunaweza kufanywa vyovote.
P
 
LOL! This's so funny, brother...

Man, hili ni suala la Kikatiba, Kanuni za Bunge na Sheria zilizotungwa na Bunge!! Wakati msingi wa suala zima ndo huo niliousema, wewe katika kujenga hoja zako, umeunga unga tu maneno kwa kutumia hisia badala ya kuangalia katiba/sheria/kanuni zinasemaje!

Na hata ulipojaribu kutumia katiba, umeeleza tofauti na katiba inavyosema.
Mkuu Chige

Mkuu Chige, kwanza asante sana kwa mchango wako huu elimishi, maana ni kupitia michango kama hii, hutoa fursa ya kuelimisha wengine walio wengi wasiojua, kama jinsi wewe na hata Mwanasheria Mkuu wa serikali, asivyojua!. Lugha ya Kiswahili, ina upungufu mkubwa wa vocabulary, hivyo kunapotokea utata wa neno lolote la katiba ya Kiswahili,
Kwa hili ndugu yangu HAKUNA upungufu wowote wa misamiati!
tafsiri rasmi huchukuliwa kwenye katiba ya Kiingereza. Hivyo neno "taarifa" kwenye katiba ya Kiswahili, sio taarifa yoyote, maana kutoa taarifa hata kwa mdomo tuu, ni taarifa, neno "taarifa" tafsiri ya taarifa kutoka katiba ya Kiingereza ni "notice", hivyo notice has to be in black and white!, yaani lazima iwe ni kwa maandishi!. Hiyo taarifa ya maandishi, ndio barua ya kujizulu, hivyo kusoma kwako koote katiba, hujaona neno barua, ila umeona taarifa, hivyo darasa la kwanza kwako na wengine wa type yako, taarifa ndio barua!.
Nani kasema "taarifa yoyote" na hata ya mdomo ni taarifa?!

Hicho unachoona kwamba ni sahihi kwa mujibu wa maelezo yako hapo juu, ndicho nimefanya, unless kama HUKUSOMA post yangu, au kama hukuisoma kwa vituo!

Nimekuambia, na hapa narudi kwamba, kwenye katiba HAKUNA popote palipoandikwa neno BARUA bali TAARIFA! Na nikaendelea kukuambia kwamba,
na newest version ambayo ipo kwa lugha ya mabeberu imesema NOTICE of Resignation!!
Na ibara mzima inasema:-
SWAHILI VERSION:-
Mtu yeyote mwenye dhamana ya kazi yoyote iliyoanzishwa na Katiba hii (pamoja na kazi ya Waziri, Naibu Waziri au Mbunge, isipokuwa Mbunge ambaye ni Mbunge kwa mujibu wa madaraka ya kazi yake, aweza kujiuzulu kwa kutoa
taarifa iliyoandikwa na kutiliwa sahihi kwa mkono wake
, kwa kufuata masharti yafuatayo: iwapo mtu huyo ni Spika au Naibu wa Spika wa Bunge, basi taarifa hiyo ya kujiuzulu ataiwasilisha kwenye Bunge;

ENGLISH VERSION:-
Any person holding any office established by this Constitution (including the office of Minister, Deputy Minister, or Member of Parliament, except an ex-officio Member of Parliament) may resign by giving notice in writing and signed by him, in accordance with the following procedure: if that person is the Speaker or Deputy Speaker of the National Assembly, the notice of resignation shall be submitted to the National Assembly; and

Haya, niambie sasa hilo neno BARUA umelitoa kwenye katiba ipi? Unaweza kuweka ibara husika hapa?!

Au unaamini kabisa kwamba hakuna msamiati wa neno NOTICE, na ndo maana Kiswahili Version imeandika TAARIFA, kumbe according to you, NOTICE SIO TAARIFA BALI BARUA... Ndicho unachojaribu kusema?

Au Notice inakuwa barua pale inapotolewa kwa maandishi na kuwekwa sahihi kwa mkono? Hicho ndicho unachojaribu kutuelimisha?!

To be honest, siwezi kuwa na ujasiri wa kukupinga moja kwa moja kwamba sio kweli, na ndo maana kwenye post yangu nilikueleza kwamba:-
So, utakuwa sahihi endapo BARUA = TAARIFA=NOTICE!
Can you SINCERLY AND PUBLICLY declare kwamba Notice ni Barua?

Hebu angalia screenshot ulizoweka mwenyewe... screenshot ya kwanza na ya pili! Hivi hata kwa kuangalia tu huwezi kujua hapo taarifa ni ipi na barua ni ipi?

REMEMBER: Kama hoja ni nyaraka husika kutolewa kwa maandishi na kuwekwa sahihi kwa mkono, ZOTE hizo zimetolewa kwa maandishi na kuwekwa sahihi!

Kabla hatujaendelea na hayo mengine, hebu jibu hayo maswali hapo juu, manake nachelea nikiandika sana, utashindwa kunisoma kwa vituo kama inavyoonesha hukufanya hivyo kwenye post yangu ya msingi!
 
Mkuu Gulwa, kwanza heshima kitu cha bure, makosa ya kibinaadamu ni kitu cha kawaida kwenye maisha, usiite watu wendawazimu kwa human mistakes hata Press Release za Ikulu sometimes zinamakosa madogo madogo.

Ile Press Release ya Bunge iliyosema barua imepelekwa CCM ndicho Chanzo cha yote, hivyo baada ya marekebisho, hiyo taarifa lazima iondolewe, hivyo imeisha ondolewa kwenye Website ya Bunge.
P
Mwana haramu ameishapita
 
Kwa ushauri wako bw. Pascal ni mzuri kwa nchi zisizofauta taratibu kama Tanzania.

Laiti ingalikuwa nchi nyingine tayari kungekuwa na harufu ya ''forgery' kwa maana kwamba uchunguzi ulitakiwa kubaini ni lini barua ilisajiliwa kwa Katibu wa Bunge

Kama ingebainika hakuna tatizo umma ungejulishwa.

Ingebainika kuna 'ushauri wa pascal uliofanyiwa kazi'' watu wangepukutishwa akiwemo katibu wa Bunge kwa kukubali barua iliyoghushiwa tarehe ya usajili na pengine kutumika mahakamani.

JokaKuu
Mkuu Nguruvi3, kwa vile barua rasmi ya kujiuzulu was not a public document, bandiko hili ni la Hypothetical situation only kwamba barua ni authentic bonafide genuine, ila ile Press ya JYN ndio ilikosewa, CCM ikakosea kusema imepokea barua badala ya kupokea copy na Bunge likasema imepokea copy kutoka CCM badala ya barua kutoka kwa Spika, kwa vile mahakama inafanya kazi na document iliyowasilishwa mezani, then document ya kujiuzulu uspika iliyowasilishwa mezani ndio document halisi, an authentic copy of the original, bonafide genuine.
P
 
LOL! This's so funny, brother...

Man, hili ni suala la Kikatiba, Kanuni za Bunge na Sheria zilizotungwa na Bunge!! Wakati msingi wa suala zima ndo huo niliousema, wewe katika kujenga hoja zako, umeunga unga tu maneno kwa kutumia hisia badala ya kuangalia katiba/sheria/kanuni zinasemaje!

Na hata ulipojaribu kutumia katiba, umeeleza tofauti na katiba inavyosema.

Kwa hili ndugu yangu HAKUNA upungufu wowote wa misamiati!

Nani kasema "taarifa yoyote" na hata ya mdomo ni taarifa?!

Hicho unachoona kwamba ni sahihi kwa mujibu wa maelezo yako hapo juu, ndicho nimefanya, unless kama HUKUSOMA post yangu, au kama hukuisoma kwa vituo!

Nimekuambia, na hapa narudi kwamba, kwenye katiba HAKUNA popote palipoandikwa neno BARUA bali TAARIFA! Na nikaendelea kukuambia kwamba,

Na ibara mzima inasema:-
SWAHILI VERSION:-

ENGLISH VERSION:-

Haya, niambie sasa hilo neno BARUA umelitoa kwenye katiba ipi? Unaweza kuweka ibara husika hapa?!

Au unaamini kabisa kwamba hakuna msamiati wa neno NOTICE, na ndo maana Kiswahili Version imeandika TAARIFA, kumbe according to you, NOTICE SIO TAARIFA BALI BARUA... Ndicho unachojaribu kusema?

Au Notice inakuwa barua pale inapotolewa kwa maandishi na kuwekwa sahihi kwa mkono? Hicho ndicho unachojaribu kutuelimisha?!

To be honest, siwezi kuwa na ujasiri wa kukupinga moja kwa moja kwamba sio kweli, na ndo maana kwenye post yangu nilikueleza kwamba:-

Can you SINCERLY AND PUBLICLY declare kwamba Notice ni Barua?

Hebu angalia screenshot ulizoweka mwenyewe... screenshot ya kwanza na ya pili! Hivi hata kwa kuangalia tu huwezi kujua hapo taarifa ni ipi na barua ni ipi?

REMEMBER: Kama hoja ni nyaraka husika kutolewa kwa maandishi na kuwekwa sahihi kwa mkono, ZOTE hizo zimetolewa kwa maandishi na kuwekwa sahihi!

Kabla hatujaendelea na hayo mengine, hebu jibu hayo maswali hapo juu, manake nachelea nikiandika sana, utashindwa kunisoma kwa vituo kama inavyoonesha hukufanya hivyo kwenye post yangu ya msingi!
Mkuu Chige, usikuze mambo, notice ni barua!.
Hata kama katiba haijasema neno barua, the notice of Resignation ni barua ya kujiuzulu.
P
 
Mkuu Chige, usikuze mambo, notice ni barua!.
Hata kama katiba haijasema neno barua, the notice of Resignation ni barua ya kujiuzulu.
P
Kukuza mambo tena?!

Ukileta mambo ya eti usikuze mambo ndo unaishia kutoa maoni yako binafsi tofauti na maandiko yanavyosema!

Anyway, mimi sio mtaalamu wa haya mambo, na sikuona yeyote wa kumuuliza anifafanulie, zaidi ya Google. Huko nikitafuta source ambayo inaonekana kuwa decent traffic kwa imani yangu kwamba, a source with crap contents haiwezi kuwa na decent traffic.

Kwavile nimefundishwa na kuandika barua tangu shule ya msingi, nikalazimika kuuliza tu hivi FORMAT ya NOTICE inakuwaje kuwaje hasa, na nikajibiwa hivi:-
Notice.png


Haidhuru hata hkama hutaki kukuza mambo, na kwavile notice ni barua, je unaweza kueleza hapa hiyo hapo juu pia ndo format ya barua? Au haya mambo ya format haya-determine kama nyaraka husika ni barua au vinginevyo, na kwahiyo ili mradi nyaraka husika imeandikwa na kusainiwa, basi automatically inakuwa barua.

Ngoja niendelee kukuza mambo kidogo kwa kuwa-refer wenye Kiingereza chao:-
Notice-Kamusi.png


NOTICE NI BARUA....
 
Back
Top Bottom