Serikali imeninyang'anya korosho zangu

Serikali imeninyang'anya korosho zangu

Baba yangu jee ulikuwa na leseni ya biashara??????????????
Kisheria inawezekana kuwa wewe ni mlanguzi kwa sababu huna shamba wala leseni ya biashara hiyo.
Ninadhani mwisho wa siku mtalipwa ila jamani tujifunze kufuata sheria na taratibu zake.
mkuu kuwa na akili kidogo.......


biashara ya mazao haina leseni.........
 
Baba yangu jee ulikuwa na leseni ya biashara??????????????
Kisheria inawezekana kuwa wewe ni mlanguzi kwa sababu huna shamba wala leseni ya biashara hiyo.
Ninadhani mwisho wa siku mtalipwa ila jamani tujifunze kufuata sheria na taratibu zake.
Mkuu labda wewe Ni mgeni wa biashara lakini hakika ungelijua yanayoendelea huko mashambani usingeshangaa hili wafanyabiashara wanaonunua mazao asilimia 90 hawana leseni iyo kumi iliyobaki ndo wanaleseni tena Ni wale wakubwa ambao wengi husafirisha nje ya nchi
 
Baba yangu jee ulikuwa na leseni ya biashara??????????????
Kisheria inawezekana kuwa wewe ni mlanguzi kwa sababu huna shamba wala leseni ya biashara hiyo.
Ninadhani mwisho wa siku mtalipwa ila jamani tujifunze kufuata sheria na taratibu zake.
Hivi mnatetea hata uozo huu ?!. Kama hana shamba si wamuachie korosho zake zimuozee au ajibangulie ?!. Haya mambo yamezoeleka sasa. Wavuvi wamefanywa hivi hivi.
 
Amevunja odi ya korosho. Kamtimua waziri wa viwanda eti wameshindwa kufanya wajibu wao kwa wakulima wa korosho
Then kateua bodi mpya... Ila yanayotokea sasa
Ni kama alitaka kuwainua juu lakini anawapiga mateke kurudi nyuma

Tuna rais wa ajabu mno
 
Serikali badala ya kutaifisha hizo bora wangewaambia wananunua za wakulima tu ili wafanyabiashara wakatafute masoko yao. Kutaifisha si kitu sahihi...
 
Haya mambo ni wengi wanalia..... Waulizeni walio sambaza mbolea za Ruzuku 2015/2016 2016/2017.....
 
japo sikubaliani na magufuli mambo kadhaa ila kwa hili niko nae.

vyama vya msingi vipo kwa ajili ya kukopesha pembejeo kwa wakulima, huku vikisubiri mkulima arejeshe korosho/tumbaku/kahawa ili wao wakate pembejeo zake na kumpa chake mkulima.

wewe ulipo enda wasaidia wakulima kwa malipo ya korosho ulikuwa unapunguza urejeshaji wa deni kwa chama maana mkulima angepeleka ama kushindwa kupeleka korosho hivyo kulaza deni na kuwagharimu wana kikundi kama si chama kizima.

alafu vyama vya msingi huuza kwa namba (mkulima anakuwa na namna ya uanachama baada ya kuhakiki shamba lake na uwezo wake wa kuzalisha)

wewe hukuna navyo, wewe ni kirusi katika ukuaji wa ushirika. sijaona kosa katika ilo.

alafu mambo ya kusema wakulima walikuwa na njaa sana siamini sana maana nafahamu vyama huwa vinawapa wakulima mikopo ya kuokoa mazao yao (inatumika pia kujikimu)

kama ambavyo sikubaliani na ww ndivyo ambavyo sikubaliani na magufuli kutaka wakulima walipwe moja kwa moja bila ya kukatwa madeni ya pembejeo ( mikopo mingine )

ivi kwani ukimkopa mkulima pesa lazima akulipe korosho kwa nini asikulipe pesa baada ya kuuza korosho zake.

ushauri wangu kwa wahanga kama wewe. fanya janja janja tafuta mkulima aliye kuuzia/mnaye elewana mpe izo korosho ye ataonesha shamba mtagawana iyo pesa.
 
Habari yenyewe inaonekana ya kutunga na ya uchochezi. Eti mstaafu kanionea huruma kanikopesha million 10? Nani anaweza kukukopesha million 10 bila dhamana! Acha uongo hii story yako ya uongo
Kwani kuna sehemu amesema kuwa amekopeshwa bila dhamana??
 
Habari yenyewe inaonekana ya kutunga na ya uchochezi. Eti mstaafu kanionea huruma kanikopesha million 10? Nani anaweza kukukopesha million 10 bila dhamana! Acha uongo hii story yako ya uongo

Nini mkopo wa millioni 10, watu wanakopeshana mamilioni mengi bila ya mkataba. Uaminifu ndio asset ya maana.
 
japo sikubaliani na magufuli mambo kadhaa ila kwa hili niko nae.

vyama vya msingi vipo kwa ajili ya kukopesha pembejeo kwa wakulima, huku vikisubiri mkulima arejeshe korosho/tumbaku/kahawa ili wao wakate pembejeo zake na kumpa chake mkulima.

wewe ulipo enda wasaidia wakulima kwa malipo ya korosho ulikuwa unapunguza urejeshaji wa deni kwa chama maana mkulima angepeleka ama kushindwa kupeleka korosho hivyo kulaza deni na kuwagharimu wana kikundi kama si chama kizima.

alafu vyama vya msingi huuza kwa namba (mkulima anakuwa na namna ya uanachama baada ya kuhakiki shamba lake na uwezo wake wa kuzalisha)

wewe hukuna navyo, wewe ni kirusi katika ukuaji wa ushirika. sijaona kosa katika ilo.

alafu mambo ya kusema wakulima walikuwa na njaa sana siamini sana maana nafahamu vyama huwa vinawapa wakulima mikopo ya kuokoa mazao yao (inatumika pia kujikimu)

kama ambavyo sikubaliani na ww ndivyo ambavyo sikubaliani na magufuli kutaka wakulima walipwe moja kwa moja bila ya kukatwa madeni ya pembejeo ( mikopo mingine )

ivi kwani ukimkopa mkulima pesa lazima akulipe korosho kwa nini asikulipe pesa baada ya kuuza korosho zake.

ushauri wangu kwa wahanga kama wewe. fanya janja janja tafuta mkulima aliye kuuzia/mnaye elewana mpe izo korosho ye ataonesha shamba mtagawana iyo pesa.
Pumbavu kabisa hujui inavyouma
 
Ndugu mbona huu utaratibu zamani haukuwepo?wa kuulizwa shamba?
Huu ni unyonyaji
Hizi njema hazina hela. Walijua misele ya Mzee wa Msoga ughaibuni ilikuwa kula bata kumbe jamaa anatafuta mtonyo watoto wasife njaa. Sasa huyu bwana hana kitu ana tafuta upenyo kwa yoyote yule amkamue hasa hawa anawaowaita wanyonge.
 
Pole sana Mkuu..ila hiyo uliyokuwa unafanya ndio KANGOMBA..yaani unanunua korosho kwa mkulima kwa shilingi 1000 ili wewe uje kuuza kwa 3300. Japo umesema hukuwa unawalazimisha ila ulitumia shida za wakulima kujinufaisha. Suala lako linafanana na utetezi wa kufanya mapenzi na binti chini ya miaka 18, hata kama ulimtongoza na kukubaliana lakini sheria itakuambia umebaka.
Hata ww unapoenda dukani kununua mchele au sukari unaenda kwa shida zako

Na hata unapoenda hosiptal unaenda kwa shida zako, biashara ni shida za mtu
 
Back
Top Bottom