Serikali Ifanye Hili Kabla ya kuruhusu Mabasi Kusafiri Kwa Saa 24, Vinginevyo Mtaua Watu Wengi

Boss la DP World

JF-Expert Member
Dec 12, 2021
1,997
7,551
Serikali imesema hivi karibuni itaruhusu mabasi kusafiri kwa saa 24, ni jambo jema sana endapo jambo hili muhimu litafanyiwa kazi.

Jambo lenyewe ni kufunga taa kwenye barabara kuu zote, fungeni taa zinazotumia solar panels ili kuongeza mwanga barabarani, kwa wanao endesha usiku watakubaliana namimi kuwa mwanga wa taa za gari pekee hautoshi kuonesha kila kitu barabarani hasa kipindi cha kupishana.

Nadhani wapo watakaohofia wizi wa taa, well zipo taa ambazo zina camera zenye uwezo wa kudetect mpaka alama za macho, napendekeza zifungwe hizo pia wakuu wa wilaya waambiwe kuwa ikitokea taa hata 1 imeibiwa kwenye eneo lako basi kibarua chako kimeota nyasi na utakatwa mafao yako kufidia.

Nadhani vyombo vya ulinzi vitaongeza umakini kulinda miundombinu hiyo badala ya kukimbizana na wanasiasa huko Ngorongoro. Hii nchi ni tajiri, msiue raia wenu kisa taa za barabarani. Anzeni na barabara ya Dar-Dodoma kisha barabara nyingine za kuunga mikoa yote.
 
Kuweka taa za barabarani kwa km zaidi ya mia nne ni matumizi mabaya ya fedha. Aidha taa hizo haziwezi kuwa jibu ya vyombo vya kusafiri usiku kutopata ajali.

Cha msingi ni kuweka taa hizo kilomita karhaa(1 au 2) barabara inapokaribia kuingia kwenye kitongoji mji au mkoa na wakati wa kutoka sehemu hizo.

Hii itakuwa kama tahadhali kwa vyombo hivyo kuwa sasa unaingia sehemu yenye watumizi wengi wa barabara. Na sio kulenga mabasi tu!

Ikumbukwe kuwa safari za usiku/saa 24 zilishakuwepo miaka ya nyuma. Na sababu ya kuzifuta haikutokana na kutokuwepo na taa za barabarani...
 
Yaani uweke taa barabara zote ili tu mabasi ambayo pia yanataa yasafiri usiku?

Mkuu Dp world, naona fedha ulizowapa serikali ni nyingi sana hivyo unaanza kuwapangia matumizi .

Kifupi kwa sasa kuna gari zinakupa mwanga kadiri ya giza unalokutana nalo barabarani na umbali wa kutosha huku zikiji adjust kadiri ya object/gari unayokutana nayo barabarani.

Hivyo trafik wazingatie ubora wa taa za mabasi.
 
Kuweka taa za barabarani kwa km zaidi ya mia nne ni matumizi mabaya ya fedha. Aidha taa hizo haziwezi kuwa jibu ya vyombo vya kusafiri usiku kutopata ajali.

Cha msingi ni kuweka taa hizo kilomita karhaa(1 au 2) barabara inapokaribia kuingia kwenye kitongoji mji au mkoa na wakati wa kutoka sehemu hizo.

Hii itakuwa kama tahadhali kwa vyombo hivyo kuwa sasa unaingia sehemu yenye watumizi wengi wa barabara. Na sio kulenga mabasi tu!

Ikumbukwe kuwa safari za usiku/saa 24 zilishakuwepo miaka ya nyuma. Na sababu ya kuzifuta haikutokana na kutokuwepo na taa za barabarani...
Waweke nchi nzima, sisi si maskini kihivyo, sisi ni matajiri tunao ongozwa na matapeli.
 
Yaani uweke taa barabara zote ili tu mabasi ambayo pia yanataa yasafiri usiku?

Mkuu Dp world, naona fedha ulizowapa serikali ni nyingi sana hivyo unaanza kuwapangia matumizi .

Kifupi kwa sasa kuna gari zinakupa mwanga kadiri ya giza unalokutana nalo barabarani na umbali wa kutosha huku zikiji adjust kadiri ya object/gari unayokutana nayo barabarani.

Hivyo trafik wazingatie ubora wa taa za mabasi.
Mkuu ukipata nafasi nenda marekani, canada na uk au germany uone. Halafu uje hapa useme wao ambao ndiyo waundaji wa magari kwanini wana taa na kila mara wanaweka taa latest kwenye barabara zao.

Kunakuwaga na emergency pia taa zinazima ghafla utafanyaje ukiwa kwenye speed kali?
 
Back
Top Bottom