kwenda21
JF-Expert Member
- Mar 11, 2014
- 3,420
- 3,391
MABASI KUTEMBEA KWA SAA 24
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson ameishauri Wizara ya Mambo ya Ndani kuangalia upya amri inayokataza mabasi ya abiria kutembea barabarani baada ya saa 6 usiku.
"Nafikiri hili jambo nimewahi kulisemea mahali pengine, ni muhimu Serikali ilitazame kwa ujumla wake. Tunazuia magari saa 6 kwa sababu ipi? Kwa sababu madereva ni walewale wanaotuendesha sisi na wanao endesha hayo magari mengine, madereva wanapitia masomo yaleyale. Kama kuna mahali pana mapungufu tuyafanyie kazi hayo mapungufu"
Ameongeza, "Lakini kuzuia abiria halafu anakaa hapo halafu gari inaondoka baada ya saa 4 labda saa 10 inaondoka au saa 11 inaondoka, sasa sijui tunakuwa tumezuia nini, hasa katika kapindi hiki ambacho Serikali inafanya juhudi kubwa sana ya kuboresha miundombinu ya barabara."
---
Naona Spika anasisitiza hili suala kuwa basi zisafiri usiku, mimi nasema hapana, kwanza atuambie sababu ya yeye kusisitiza hili jambo ni kwanini hasa na kuna nini?
Pili anajua ugumu wa night shift? Anajua madhara ya kutokulala usiku? Je, barabara zetu zina traffic light za kutosha Dar kwenda mikoani? Usalama wetu utakuaje?
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson ameishauri Wizara ya Mambo ya Ndani kuangalia upya amri inayokataza mabasi ya abiria kutembea barabarani baada ya saa 6 usiku.
"Nafikiri hili jambo nimewahi kulisemea mahali pengine, ni muhimu Serikali ilitazame kwa ujumla wake. Tunazuia magari saa 6 kwa sababu ipi? Kwa sababu madereva ni walewale wanaotuendesha sisi na wanao endesha hayo magari mengine, madereva wanapitia masomo yaleyale. Kama kuna mahali pana mapungufu tuyafanyie kazi hayo mapungufu"
Ameongeza, "Lakini kuzuia abiria halafu anakaa hapo halafu gari inaondoka baada ya saa 4 labda saa 10 inaondoka au saa 11 inaondoka, sasa sijui tunakuwa tumezuia nini, hasa katika kapindi hiki ambacho Serikali inafanya juhudi kubwa sana ya kuboresha miundombinu ya barabara."
---
Naona Spika anasisitiza hili suala kuwa basi zisafiri usiku, mimi nasema hapana, kwanza atuambie sababu ya yeye kusisitiza hili jambo ni kwanini hasa na kuna nini?
Pili anajua ugumu wa night shift? Anajua madhara ya kutokulala usiku? Je, barabara zetu zina traffic light za kutosha Dar kwenda mikoani? Usalama wetu utakuaje?