Serikali hoi kifedha, Sasa kukopa...

Serikali hoi kifedha, Sasa kukopa...

Ni kweli, haya Wabunge hawajalipwa mishahara yao na posho za Bunge lililopo ya nadhani. Kuna rafiki yangu kachukua tenda ya kuweka kifusi kwenye barabara maeneo Mbagala mpaka leo anapigwa Kiswahili tu.
Benno Ndulu alionya kuwa hutolewaji wa pesa zilizokuwa kwenye akaunti ya Escrow kunaweza kuyumbisha uchumi wetu, lakini majizi hayakutaka kumsikiliza yakalazimisha pesa zitoke na kugawana haraka haraka.
Hali mbaya kweli, kama hakutakuwa na chochote kuna hatari mishahara ya walimu na Polisi ikaanza kupigwa kalenda.
Ova
Hao police na walimu wasipopewa mishahara ni sawa tu.kwanza ndio wanaoisaidia ccm kuiba kura na hivyo kuendelea kuwepo madarakani kwa hila zao,pili Jk alikataa kura zao still wakampa-Big up Jk-Kaza uzi zaidi
 

Kwenye kila budget zetu zote zina sehemu mbili, budget ya recurrent na budget ya development. Budget ya recurrent, ni budget ya matumizi ya kawaida, hii ni budget tunayojitegemea kutoka vyonzo vyetu vya ndani, na nakisi kwenye recurent, tunakopa!, fedha hizi hazijazuiliwa na wala hatujazuiwa na yeyote kukopa popote!. Umasikini wetu kwa kiasi kikubwa haswa deni la taifa kumetokana na hili, kutumia kuliko uwezo wetu wa kuzalisha!.

Kubwa zaidi ni pale sio tuu tunapotumia kuliko tulichozalisha bali ni pale tunapotumia kile ambacho hatukubudget kama dharura, alafu dharura yenyewe sio majanga kama natural disasters bali sherehe, kama yale maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru!, Tangu ile siku tunapata uhuru, ilijulikana kabisa miaka 50 itakuwa ni lini, lakini we did not budget!, tukaifanya ni dharura!, ni dharura kama hizi, ndizo zinaingilia recurrent na kuifanya kumegwa kwa matumaini itafidiwa baadae!. Hivyo kama ni kweli, wafanyakazi wamekosa mishahara this time, sababu inaweza kuwa ni ile dharura ya ugonjwa ambayo hii ni dharura kweli!.

Budget ya pili ndio ile development, hii ni fedha ambayo haipo, ila tunaibudget according to projections na commitments za nchi wafadhili kugharimia miradi ya maendeleo, na hii ndio tunawatemea zaidi nchi wahisani, wafadhili, mikopo na fedha za ndani. Kusitishwa kwa misaada kwa kiasi kikubwa kutaathiri hii miradi ya maendeleo!. Kwa vile na sisi tunachangia miradi hii kwa fedha zetu za ndani, in this case reallocation is inevitable na ni kitu cha kawaida, lakini siku zote fungu ambalo liko very safe serikalini, ni fedha za mishahara, fedha ambazo zinaweza zikakosekana ni zile za O/C (other charges) lakini sio mishahara!.

Bahati mbaya sina hata mtumishi mmoja wa umma, nimjuaye ambaye ningeweza kumuuliza!.

Pasco

Napenda watu wenye intelligent analysis kama PASCO. Kwa sisi tulio ughaibuni hii inakuwa food for thought.

Ila PASCO kitu kimoja huja realise uliposema fedha za mishahara ziko always safe. Tangu aje madarakani JK nadhani amechukulia serikali kama kitu chenye 'limiless resouces'. Hii ndiyo hasa dhana ya watu wasioelimika juu ya serikali. Sijui vipi yeye pia anayo hiyo. Labda kwa sababu alitegema sana wafadhili.
Pili: aina ya uongozi wake ni ule tunaouita usio na nidhamu (fiscal discipline) katika masuala ya matumizi ya fedha. Sitashangaa ameamuru kuchukuliwa fedha zilizopangiwa mambo mbali mbali ku- fund mambo mengine, aghalabu ya kiufujaji. kwa hiyo hakuna hiyo safety ya fedha za mishahara chini ya serikali ya JK.
 
Kuna CCM mbili:CCM imanini na CCM maslahi-Warioba.

Wengi wenu leo ni CCM maaslahi!

Warioba alibwagwa na Mwinyi uwaziri mkuu kwa maslahi ya Taifa.

Huyo mzee kigeugeu, nna mashaka anatumia bangi kwa wingi sana kupita kiasi.
 
hahahaha kweli kaka mabaka yakikosa mshahara itakuwa shughuli ngumu sana hawata kubali na wanajua hela hawa mafala wamekula. wanagawana eti sio za uma kama sio za uma ndo wagawane wangetudanganya basi wamelipa mikopo coz nchi ni kuomba kuomba tuu tuu. Mkubwa wa nchi mwenywe anaona hela za nchi yake za madafu wakati yeye ndo anatakiwa azipandishe ziwe za gold. Yani tulikosea saaaaana safari hii tuangalie mara mbili mbili wakati wa kufanya maamuzi ya mtu wa kutuongoza. Kwa sasa mtu ninae mwona ana maamuzi ni nywele nyeupe tu sijaona mtu mweingine anaweza shika hapo juu. Ukiangalia ukawa nao wanakuja vizuri tatizo nao bado hawajakomaa kisiasa hao wanafaa kuwajaza bungeni ili serikali ifanye kazi kwa viboko ila kusema tuwape nchi kabisa bado.
Kuna mtu anaitwa Waitara hivi yupo wapi siku hizi?Post yako imenikumbusha huyu kamanda
 
Wahaya bana, kwa kuwa mgao wa dada yako umekukosa basi unaona na wewe utolee machungu yako humu jf! duh!

Duh! Umekosea sana, mimi sio Mhaya na wala sitokei kanda ya ziwa.
Wasubiri Wahaya uje ujadili nao issue za ukabila kama watakuwa na muda.
Ova
 
Inauma sana kodi inakusanywa kidogo watu wachache wanagawana pesa then serikali kwa maksudi kabisa inakataa pesa ya escrow eti si ya umma huku wabunge wengi wa ccm wanashangilia kuwa wameshinda eti pesa si ya umma sasa wamepata nn wengine hata mgao hawajapata mfano asumpta mshana leo wafadhili wamegoma hali mbaya jamani hii nchi.
 
Kwa CCM kule natamàni Mwigulu agombee japo najua JK hatathubutu kufanya kosa hilo la kumpa nafasi Mwigulu aukwae urais.Haki ya mungu Mwigulu atawapeleka wengi magerezani akiwemo huyu Mk.were,najua namna Mwigulu anavyoumizwa na uonevu wa mafisadi dhidi ya Watanzania.Kwa Upinzani ni Dr Slaa tu ndiye atakayewanyoosha hawa mahayawani.

Mwigulu atatekeleza ilani gani ya tofauti? Hawa ni kopo na mfuniko. Chama kimeoza jumla jumla. Kinahitaji overhaul, sio repair
 
Nakwambia Kikwete angekuwa Rais wakati tunapata Uhuru, hii nchi saa hizi ingekuwa ni pepo aka mbinguni.

Yule mzee alitutoa toka nchi ya kwanza katika Afrika (alipopewa madaraka) kuuza mazao ya shambni nje mpaka kutufikisha nchi omba omba na masikini wa mwisho dunia. Alipotaifisha tu. Kwisha. Tukawa hohe hahe.

Leo mna neema ya uongozi wa Kikwete, mnaweza kuingia mtandaoni mkabwabwaja mnavyopenda , thubutu wakati wa Nyerere, TV yenyewe tulikuwa hatuna, wacha mtandao.


We dada nimekuvulia kofia..
Hivi nikwanini wafuasi wa JK niwaongo na wanafiki kiasi hiki!!?
 
Baadhi ya unayosema ni kweli, lakini kuna uhusiano gani na sasa? Tangu Nyerere aondoke ni miaka mingapi? At least yeye hakuwa mfujaji, kama unayemtetea. Alikuwa honest. Mtu kama huyo ni rahisi kumsamehe, kama ambavyo wengi tumefanya. JK alikuta hazina imefurika. Akaanza kuzitafuna kwa kuunda baraza kubwa la Mawaziri (rafiki zake) na safari za nje za gharama.
Aliachiwa Tanzania ikiwa ready for a take-off. Shule zilikuwa zinajengwa, barabara, afya......zaidi ya hayo bei za bidhaa zikuwa muwafaka- inflation chini ya 6%
Nataka unjibu: ni kigezo gani unatumia kwa rais kufeli?

Hazina gani imefurika wewe? hazina ingefurika tungelipishwa kodi? kasome takwimu, kaikuta reserve ya nchi hata miezi miwili haifiki, yeye sasa hivi ana ya miezi sita. Fikiri.

Huyo wengine hatumsamehi ndiyo aliweka misingi mibovu ya kutufikisha tukawa masikini wa mwisho duniani.
 
Uongo mtupu.

Sasa ukweli ni upi? Nenda hospital kama hujaambiwa kanunue drip duka la dawa mimi nimeenda temeke hosptl hali iko hivyooo kwani we dada unamatatizo ya akiri au? We kila kitu unaona ccm wanaonewa.
 
Hazina gani imefurika wewe? hazina ingefurika tungelipishwa kodi? kasome takwimu, kaikuta reserve ya nchi hata miezi miwili haifiki, yeye sasa hivi ana ya miezi sita. Fikiri.

Huyo wengine hatumsamehi ndiyo aliweka misingi mibovu ya kutufikisha tukawa masikini wa mwisho duniani.

Usitegemee takwimu zinazorushwa tu huku na huku. Third world inajulikana kwa uongo na ndiyo maana hawachapishi kitu. Miezi sita? Haya na alipe mishahara basi!
 
Nilizaliwa kabla ya huo uchawi wa Nyerere.

Na nimeishi wakati nchi hii ilipofilisika, najuwa kufisika nchi ni nini.

Leo mko nyuma ya keyboard zenu, umeme mnao, mmeshiba mnajambajamaba hivyo.

Hii nchi wakati wa Nyerere ilipokuwa imefilisika kiukweli, saa hizi mngekuwa kwenye foleni ya unga wa Yanga.

Mmekula unga wa Yanga nyinyi?

mwanzo nilijua wewe ni dada laaa aisee kumbe ni bibi
 
Labda kama tuna matatizo mengine, fedha zilizozuiliwa na wafadhili, sio ile General Budget Support kupitia Busket Funding, ni development budget, hivyo zile sio fedha za kulipia mishahara!. Hata fedha za MCC pia sio fedha za kulipia mishahara!.
Kama ni kweli Watumishi wa umma wamekosa mishahara, then tuna tatizo kubwa kuliko tunavyo jidhania!.

Pasco.

mkuu hujui kuwa bjeti yetu mara nyingi ni kiini macho, haya matumizi ya anasa ya serikali si lazima bajeti ya maendeleo itakua inachakachuliwa
 
Nilizaliwa kabla ya huo uchawi wa Nyerere.

Na nimeishi wakati nchi hii ilipofilisika, najuwa kufisika nchi ni nini.

Leo mko nyuma ya keyboard zenu, umeme mnao, mmeshiba mnajambajamaba hivyo.

Hii nchi wakati wa Nyerere ilipokuwa imefilisika kiukweli, saa hizi mngekuwa kwenye foleni ya unga wa Yanga.

Mmekula unga wa Yanga nyinyi?

Kweli nimeamini we ni mwendawazimu unasahau maendeleo ya sayansi na teknolojia yamekua kwa kasi usifananishe karne ya 17 na karne ya 21 yaani hata innovation hujui kweli wewe kama ulikuwepo kipindi cha nyerere na unatetea ujinga basi laana ya mwalimu inakumaliza eti kikwete kafanya mazur kuliko Rais yeyote aliyetangulia duuuuh kama kizazi chako utakuwa umekilishisha huu ujinga wako basi umeua ukoo wako wotee.naamini kwa haya unayoyafanya wewe hujafka hata miaka 40 unaxuga tuu
 
Naam, nilikwambia kwenye zile nyuzi zako za uongo uliolishwa na kuja kuutapika humu, kila mtapokuja na uongo wenu mtanikuta. Na sitowapa pumzi hata chembe, ntawaonesha ukweli ni upi.

Mpaka mtie akili muwe mnakuja na ukweli, hapo ntawatembelea kule MMU kwenda kujitia pressure kidogo.
Mkuu Faiza Foxy nisaidie.mimi ni mgeni hapa jamvini,huwa ninaona kila uzi unaoihusu serikali na Jk, wewe ndiye unakuwa mteteze mkuu na unatetea kwa nguvu zako zote either kwa kutumia pumba(big %) or mchele (less %).1.Wewe ni nani kwenye serikali yetu?2.Je umeajiriwa kwa kazi hii tu au unakazi nyingine?3.Je unapotukana watanzania (sometimes) huoni kama unaifitinisha serikali na wananchi wake?4.Je umewahi kufanya tadhimini ya kazi yako hapa jamvini?5.Matokeo uliyaonaje?6.Je huoni kama majibu na hoja zako hapa jamvini zinawafanya watu waichukie zaidi ccm,serikali na Jk?
 
Back
Top Bottom