Serikali hoi kifedha, Sasa kukopa...

Serikali hoi kifedha, Sasa kukopa...

Usimsingizie Nyerere wa watu muache apumzike huko aliko! Kama mlifahamu nchi hii ilifirisika tangu zamani kwanini mlituongopea Mwaka 2005 "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA!?" hamkuishia hapo mkaendelea kutuongopea "ARI MPYA, NGUVU MPYA NA KASI MPYA" viko wapi!? Hivi si ndiyo nyinyi mlituletea sera ya KILIMO KWANZA!? Kimeleta faida gani!?

= Ilifilisika

Ilifilisika wakati wa Nyerere, Mwinyi akaja kuitoa huko na kuirudisha kwenye chart.

Maisha bora ni ukweli kabisa. Leo unaenda siokoni uanchaguwa ule maharage ya Mbeya au ya Arusha. Leo una matumaini ya kuishi miaka zaidi ya 62. Wakati wa Nyerere alikuwa 43, Mwinyi akaipandisha 45, Mkapa akafikisha 49, leo Kikwete kwa miaka yake 9 tu unamatuamaini yakuishi zaidi ya miaka 62. Unajuwa maana yake ni nini? ni maisha bora hayo.

Leo unaweza kuingia kwenye mtandao ukabwabwaja, unajuwa maana yake ni nini? ni maisha bora hayo.

Leo unaweza kwenda dukani ukachaguwa unataka mswaki upi na dawa ipi ya kusafisha kinywa chako, ni maisha bora hayo.

Thubutu yote hayo uyaone wakati wa Nyerere.
 
Umeona tu kipindi cha Nyerere?
Na kipindi cha Mzee Ruksa mbona usemi au kwa kuwa ni kaka yako!
Sema awamu zote tatu nchi ilifilisika bila kusahau hii awamu ya nne.
Sababu kubwa ya kufilisika kwa awamu zote tatu ni kutolipwa madeni ya nje (ya kimataifa).
Ebu Faiza tuambie from the bottom of your heart, sababu ya kufilisika kwa hii awamu ya nne ni nini hasa?

Mzee Ruksa, ni hero wa Watanzania mpaka leo hii, na hilo jina ulilomwita linathibitisha hilo.

Alitutoa kwenye lindi la umasikini wa Nyerere na kila kitu chema kwake kikawa RUKSA. Tukaanza mpaka kuiona dunia kwenye TV ambazo hatujawahi kuziona wakati wa Nyerere.
 
Nikuambie kitu dada yangu..kuna masuala ambayo ccm na serikali yake haibebeki..ni mwendawazimu tu anaweza kuwatetea au kuitetetea..kila kitu kiko wazi..nakushauri ukiona thread kama hizi wewe sepa..usi comment ..watu hawatakuelewa na watakushukia kama mvua!utakufa kwa presure..mafisadi wenyewe wanafaidi..lbd na wewe ni moja wao!

Haitetei ccm na serikali yake , huyo anamtetea Kikwete ndugu. Msome vizuri huyo bibi utaelewa anatetea nini.
 
Huu uzi nusu ya comments zake ni kwa hisani ya FaizaFoxy !

Naam, nilikwambia kwenye zile nyuzi zako za uongo uliolishwa na kuja kuutapika humu, kila mtapokuja na uongo wenu mtanikuta. Na sitowapa pumzi hata chembe, ntawaonesha ukweli ni upi.

Mpaka mtie akili muwe mnakuja na ukweli, hapo ntawatembelea kule MMU kwenda kujitia pressure kidogo.
 
Naona sasa umekosa hoja. Watanzaia 80% juzi wamaichaguwa CCM.

Myinyi hasira zanu za kubwagwa mnakuja hapa kubwabwaja, kwanza muelewe Serikali siku hizi si ya ujamaa, uchumi upo mikononi mwa raia, au wewe ndiye umefilisika? unaanza kubwabwaja na kulalama bila mpango?

Hasira za kipigo kitakatifu mtabwabwaja sana, lakini tupo hapa, uongo wenu hauna nafasi.
Wamaichagua=wameichagua
Myinyi=nyinyi
Zanu=zenu
wewe ndiye umefilisika?=wewe ndiye uliyefilisika?
 
Huu uongo wenu hauwasaidii kitu unazidi kuwaumiza roho zenu tu.

Watanzania leo hii tukipewa choice tunataka Kikwete aendelee kutuongoza kwa miaka mingine 10.

Hakuna Rais Tanzania hii wa kabla ya Kikwete aliyeyafanya hata nusu ya mema kwa Tanzania hii kama alivyofanya Kikwete.

Nioneshe ni yupi na lipi au changanya wote kwa pamoja.
Mermermerko
 
Labda kama tuna matatizo mengine, fedha zilizozuiliwa na wafadhili, sio ile General Budget Support kupitia Busket Funding, ni development budget, hivyo zile sio fedha za kulipia mishahara!. Hata fedha za MCC pia sio fedha za kulipia mishahara!.
Kama ni kweli Watumishi wa umma wamekosa mishahara, then tuna tatizo kubwa kuliko tunavyo jidhania!.

Pasco.
Pasco bhana yani unaongea kama vile sio mjanja tena; hivi kukiwepo na fedha kwenye deposit account haziwezi kuhamishwa kwenda reccurrent account kuokoa jahazi na makusanyo yakiingia zikarudishwa deposit account? sasa kama deposit ni kweupe serikali ikope wapi kuboost recurrent kama sio kwenye mabenki?
 
Ilifilisika wakati wa Nyerere. Wakati hatuna hata cha kukila.

Leo mambo swaaafi kabisa, na wala hamumstui mtu humu, Serikali iliyofilisika unaijuwa wewe ulikuwepo wakati wa Nyerere au unausikia tu?
Unausikia=unasikia
 
Hiyo hali mbaya ya kifedha wewe imekuathiri nini? ulikosa mchele dukani? ulikosa unga dukani? ulikosa maharage dukani?

Wacha porojo. Ngoja siku ukose vyote hivyo ndiyo uje humu kubwabwaja. Hamjakuwepo wakati hii nchi imefilisika tuulizeni sisi tuliokuwepo wakati wa Nyerere.

Ulikosa=umekosa
Hamjakuwepo=hamkuwepo
 
Hiyo hali mbaya labda unayo wewe si nchi. Wakati hii nchi ilipokuwa na hali mbaya tulikuwepo. Wacha porojo.

Nchi ingekuwa na hali mbaya wewe ungeweza kuingia mtandaoni? hayo mafuta ya kukuwashia mitambo ya umeme ungeyatowa wapi? fikiri, wacha kulishwa uongo na wewe kama msukule unaamini tu.

Ungeyatowa=ungeyatoa
 
unh kumbe mishahara yote ya wafanyakazi wa serikali ni 300 bilioni. zile pesa za escrow zinazosemakana kuchotwa.. zingelipa wafanyakazi kwa mwezi huu? how ironic

Umeelewa kweli analichokiandika mdau hapo au umeamua kujitoa akili!? Soma kwa makini kabla hujareply comment ya mtu
 
Back
Top Bottom