Serikali hoi kifedha, Sasa kukopa...

Serikali hoi kifedha, Sasa kukopa...

Mie natamani hali ya serikali, na wananchi izidi kuwa ngumu na mbaya [kwa nia njema] ili ifike mahali tujue umuhimu wa kutowachekea viongozi na watendaji wapuuzi. Kwa upuuzi unaofanywa sasa nhivi ni nguvu ya wananchi pekee ndo inayoweza kutoa ujumbe kwa viongozi kuwa tukiamua wao na familia zao hawabaki salama. Kitu kibaya, mijitu mingine hawajatambua hilo hivyo wacha tule shida wote mpaka akili itukae vizuri.

Very true, lazima watu waelewe kuwa mabadiliko ni lazima ili kuleta ufanisi wa serikali na maendeleo ya mmoja mmoja na taifa kwa jumla..... Na hakuna namna nyingine ambayo ni practical itakayowaelewesha watu ila ni kwa kuiface hali ngumu sana ambayi imezalishwa na serikali iliopo. Mi nadhani wacha maisha yawe taiti
 
Wawache na wawaache ni vitu viwili tofauti. Fikiri.

Ngoja nikupe darsa kidogo:

Wawache = uko peke yako, wako wengi nakwambia wawache.
Waache = wao wako wengi unawaambia waache wanachokifanya.
Wawaache = wao wako wengi unawaambia wawaache wengine (zaidi ya mmoja).
Wawache kiswahili cha wapi hicho?
 
Wewe ni nani usiyefikiria sawa sawa?? Nyerere alijenga nchi tuliyoikuta na mabwana zako ndio wanaiba. Reli ya Tazara ilijengwa wakati wa nyerere, reli ya kati ilikuwa inaendesha shughuli zake vyema jamaa zako wameingia wameua tazara reli ya kati na reli ya uhuru zote hazifanyi jazi leo. Wamefanya makusudi ili wafanye biashara ya malori, mabasi na vituo vya mafuta. Uchumi umeporomoka mtajuta siku ccm itakapobanwa na kushindwa kutoarushwa sijui mtaishije.
 
Mimi nimezaliwa kabla hii nchi haijapata Uhuru. Kumbuka hilo, Nyerere bado alikuwa anavaa kaptura na mimi mwenyewe nimeshamuuzia Nyerere sigereti dukani kwetu, nakumbuka zilikuwa sigara karata, ubavu na ubavu na ilipo sasa Makao Makuu ya Mkoa ya CCM.

Bravo FF, hapo umeongea ukweli mtupu. Wewe ni ajuza na hawa vijana wanatakiwa kutia adabu, wajue akili zimechoka na kila unaloandika sio lazima liwe sawa. Wanatakiwa waitikie..amina bibi yetu!
 
Yote uliyozungumza hapa uongo na upotoshaji wa hali ya juu kabisa.

Kama elimu ya washauri waliopo Lumumba na Magogoni ni kama yako ndiyo maana taasisi ya Urais ni dhaifu. Mimi nina uhakika na ninaandikacho.
Jenga hoja kukanusha.
 
Changes dont come without sacrifices, Lazima nchi ipite kwenye bonde la mauti kabla ya kufika kwenye nchi ya ahadi yenye maziwa na asali. Wasiwasi wangu ni kuwa inaweza chukua muda mrefu sana kabla ya wadanganyika kufahamu kuwa viongozi wetu ni wabinafsi sana. "GET THEM OUT!!!!!!"
 
Professionalism is your biggest problem-Ndiyo maana unachanganya mambo yenu ya kitandani na utawala wa nchi.Hivyo ni vitu viwili tofauti sana Shemeji yetu.

Kumbe unamfahamu..you nailed it. Those who know they are saying "kudo".
 
Hiyo hali mbaya ya kifedha wewe imekuathiri nini? ulikosa mchele dukani? ulikosa unga dukani? ulikosa maharage dukani?

Wacha porojo. Ngoja siku ukose vyote hivyo ndiyo uje humu kubwabwaja. Hamjakuwepo wakati hii nchi imefilisika tuulizeni sisi tuliokuwepo wakati wa Nyerere.

Wakati wa Nyerere nchi iliingia vitani na Uganda. Saizi tunapigana na nchi gani zaidi ya deni la Taifa kukua kama kuku wa broiler??
 
Kipindi hicho serikali ilikuwa inapigana vita na Nduli Iddy Amini. Saizi tunapigana na nani zaidi ya deni la taifa kukuwa kila siku??

Tulianza kuwa hohe hahe kabla hata ya vita hatujuwi ni nini, umasikini tulijitakia mwaka 1967 tulipodhulumu "taifisha".
 
Wakati wa Nyerere nchi iliingia vitani na Uganda. Saizi tunapigana na nchi gani zaidi ya deni la Taifa kukua kama kuku wa broiler??

Hukopeshwi kama huwezi kulipa. Hili kumbuka. Ukiona unakopesheka sana ujuwe na uchumi wako ni mzuri sana.

Hata USA wanakopa.
 
quote_icon.png
By FaizaFoxy Hiyo hali mbaya ya kifedha wewe imekuathiri nini? ulikosa mchele dukani? ulikosa unga dukani? ulikosa maharage dukani?

Wacha porojo. Ngoja siku ukose vyote hivyo ndiyo uje humu kubwabwaja. Hamjakuwepo wakati hii nchi imefilisika tuulizeni sisi tuliokuwepo wakati wa Nyerere.
Kuna member mmoja alikuambia 'Professionalism is your biggest problem' nafikiri alikuwa sahihi, kwa upeo wako wa kufikiri unadhani kila kitu kinajibiwa kwa ubishi.

Indicators za kushuka kwa uchumi si vyakula kukosekana sokoni bali ni uwezo wa shilingi au mtu kuvinunua hivyo vyakula.

Tulipoambiwa uchumi wa Zimbabwe umeshuka sio kwamba maharage, mkate, mchele vilikosekana madukani bali nguvu ya hela ya Zimbabwe ilipungua thamani katika kununua bidhaa hizo.
 
Badala ya kukopa benki si wamuombe tu Rugemalira atawapa bure badala ya kuhangaika na mikopo yenye riba,serikali ifungue akaunti Mkombozi benki ,kwa Rugemalira hiyo ni hela ya kauzu tu wajameni
 
Kwa huu at least nimeelewa FaizaFox ni mtu wa aina gani kisiasa. Shikamoo bibi, but bibi wengine wanalea wajukuu. We uko busy mitandaoni muda wote. Du huna wajukuu bibi. Hata mama yangu kazaliwa kabla ya usury (though hakuwahi kumuuzia Nyerere sigara). Ila kwa umri wake haezi kutukanana jf. Ni Salam tu bibi yangu.
 
Kwa huu at least nimeelewa FaizaFox ni mtu wa aina gani kisiasa. Shikamoo bibi, but bibi wengine wanalea wajukuu. We uko busy mitandaoni muda wote. Du huna wajukuu bibi. Hata mama yangu kazaliwa kabla ya usury (though hakuwahi kumuuzia Nyerere sigara). Ila kwa umri wake haezi kutukanana jf. Ni Salam tu bibi yangu.

Nani anaetukanana? mkiambiwa ukweli mnasema mnatukanwa.

Unayajuwa matusi wewe? au unajiropokea tu?

Huyo bibi'yo nna uhakika hata kompyuta hawezi kutumia ataingiaje JF? fikiri.
 
  • Thanks
Reactions: OR7
Back
Top Bottom