Series (Special thread)

Upo sahihi kiasi fulani. Ila kwa mtu ambaye hapendi kupoteza muda na MBs, reviews za IMDB zinasaidia sana.
 
Upo sahihi kiasi fulani. Ila kwa mtu ambaye hapendi kupoteza muda na MBs, reviews za IMDB zinasaidia sana.
Mhhhh! Nakwambia ivo maana mimi nimeingia cha kike sana kule mpaka leo sifuatilii.
Swali rahisi tangu tuwe hapa na nakujua upo humu kitambo na unajua series ushawahi sikia mtu anasema series ya Planet earth Kali? Maana iyo ndio inayoongoza kuwa na highest rate kuliko series zote au ushawahi ona mtaani watu wanaizungumzia?

 
Hiyo Planet Earth ni documentary, mimi sio mpenzi wa documentary series, ndio maana sijawahi kuiangalia mpaka leo. Ila top ten ya IMDB ukiondoa documentaries, nimeshazitazama, na kwa mtazamo wangu hawajakosea katika "kuzirank". Kuna wakati huwa nafikiri sisi "Wabongo" huwa hatujui TV Series nzuri, hiyo nahisi inachangiwa na level of INTELLIGENCE, Wabongo tunapenda TV series ambazo zina matukio mepesi kuyachakata, ndio maana Wabongo wengi ni wapenzi wa action movies/series, ndio maana ni rahisi kukuta mtu anakuambia Money Heist ni kali kuliko The Wire au Strike Back ni kali kuliko Breaking Bad, wakati ukweli ni kuwa The Wire na BB ni kati ya TV series kali kabisa kuwahi kutengenezwa hapa duniani. TV series karibia zote ambazo zinachukuliwa kama kali kuwahi kutengenezwa, sio "popular" mtaani au humu jukwaani, tukiondoa mapenzi binafsi, sababu ni hiyo niliyokuambia hapo juu (Level of intelligence).
 

Kweli umesema vizuri ndugu yangu series nyingi zinahitaji uelewa mzuri ili kuifaidi vizuri maana utaelewa kila kitu kinachoendelea, binafsi kwenye movie ukiachana na plot huwa napenda zile minor issues kama conversations, zile savage replies, quotes na comebacks huwa nafurahi sanaβ€’

baadhi ya shows zinahitaji background nzuri uwe unajua labda Law hata kigogo kwa series kama Suits na nyingine utakuta uwe una background ya physics kidogo mfano Scorpion, Salvation kuna nyingine za Medical dramas ni tamu huwa napenda kujifunza vitu mfano The resident, Grey’s Anatomy, New Amsterdam pamoja na The Good doctor hizi series zipo za auna tofauti kulenga wahitaji tofauti, kuna wengine wanapenda series zile za crazy actions watu wanabondana tu basi iko hivyoβ€’

Leo ni Premier ya F9 (Fast and Furious) mzigo Theatre Century Cinemax baadae ni mwendo wa kula radha ya Crazy actions
 
Tuseme ni maoni mzee maana hata wao ni binadamu so ni maoni yao ndio wanaamua kuzipa series Hii iwe kubwa na hii iwe na rate ndogo.
Ukizungumzia kuhusu kuangalia series za action hapo sipo pa1 na wewe maana mimi naangalia zote hata series za Tyler Perry ni nzuri na hazipewi rate kubwa ila zinamfanya jamaa kuwa bilionea maana people wengi hawaangalii kule IMDB wanaangalia story ya series ipoje na hatujutii kupoteza MB zetu na hapo siioni game of thrones wala la casa de la paper hata 7 bora ila zimeuza sana na angalia kiu ya watu walivyokuwa wanazisubiria dunia nzima so watu wote hao wangekuwa wanaamini IMDB izo filamu zingangaliwa kweli au kuuzika? Au kitu kinapendwa na wengi ni kibaya?....hapana sio kweli πŸ˜† So wale ni binadamu na wana maoni yao mzee na yamenikuta huko sina hamu wakati nipo chuo 🀣🀣🀣
 
Leo ni Premier ya F9 (Fast and Furious) mzigoTheatre Century Cinemax
Sasa ndio umwambie Mbongo kuna movie inaitwa Inception, ni kali kuliko Fast and Furious zote. Akienda kuicheki akirudi, lazima akuone "mwehu".
Mzee kacheki hicho "chuma", akina sisi tuna subiri mpaka itoke "clean version" katika pirate sites tuishushe.
 
Kweli mzee ila series zote ulizotaja zina rate ya ngapi IMDB?πŸ˜†πŸ˜†
 
Kumbe tupo wengi tusioenda cinema utafikiri kuna bei ya juu ila wapi watu tunasubiri pirates tushushe πŸ˜†πŸ˜†
 
Hizo series za Tyler Perry nimejaribu kuicheki "The Oval" nikachemka. Kwangu mimi sijawahi kuona movie au TV series ambayo iko na positive reviews nyingi nikaikuta haiko vizuri, kifupi IMDB haijawahi kuniangusha.
Hapa inabidi tukubaliane kutofautiana tu, ni binadamu sisi, hatuwezi fanana kimtazamo.
Lakini mmmmh, ebu ngoja kwanza!
Mkongwe, unataja "La Casa De Papel", seriously!? Yaani unategemea uione "La Casa De Papel" katika top ten ya best TV series of all time?
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Nafikiri unatania!
 
Nashauri mtu asiangalie hizi series Tehran, Treadstone na revolution utapoteza muda maana wamezicancel so hakuna muendelezo tena
Hivi Tehran ndo ishafika mwisho...

Sema kuna series huwa wanazicancel mpka roho inauma..
Niliangalia The Bodyguard, kila siku nachungulia kama wametoa season 2
 
Hivi Tehran ndo ishafika mwisho...

Sema kuna series huwa wanazicancel mpka roho inauma..
Niliangalia The Bodyguard, kila siku nachungulia kama wametoa season 2
Yeah mzee Tehran ilikatishwa na kuhusu roho kuuma kuna jamaa nilikuwa nampa iyo series si akaanza kunimind mimi baada ya kumwambia imekatishwa sasa sijui kosa langu lilikuwa nini? 🀣🀣
 
Labda point ya juu kwamba tunatofautiana kila kitu ila ukiangalia money heist ina fans wengi dunia nzima labda wewe tu uiponde na point yangu ni kuwa hao watu wangekuwa wanaangalia rates za IMDB izo series za Money heist zisingekuwa na fans wengi na pia hata tuzo zisingepewa maana haina rates kubwa watu wangebaki kuangalia series zenye rates kubwa kama Chernobyl au The Mandarolian?.
Unafikiri hamu ya watu wanavyoisubiri Money heist ndio wanavyoisubiri series inaitwa Oz ile ya mapunga gerezani au The Mandarolian? Maana hizo zina rate kubwa.....KweliπŸ˜†?
 
Hivyo vyuma alivyotaja huyo mdau, hakuna hata kimoja ambacho kina alama chini ya 7 katika ratings za IMDB. vyote vyuma kwelikweli.
Sasa hapa ndio unanichanganya maana kama hizi series unasema ni vyuma alafu unasema Money heist nayo si series nakuwa natania wakati kwenye IMDB yako ina rate ya 8.3 so hiki sio chuma ni NONDO au?πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
Ila kitu haujui sometimes kinachofanywa na hizi sites zinazofanya rates ni fitina na watu wengi wamemind ilo suala ndio maana watu wanaangalia reaction ya watu wameipokeaje, mauzo na tuzo ngapi imebeba au kuwa nominated kuhusu izo movies na series na sio rates.
Soma hapa πŸ‘‡πŸ‘‡ utajifunza kitu iwe wewe na wengine wanaongalia rates then wanashusha series





 

Money Heist haiwezi kuwa G.O.A.T acha msihara na ubishi usio na maana na kuhusu njia za kuangalia Movie kila mtu ana jinsi yake wengine wanaangalia Plot, wengine trailer pamoja na cast na wengine wanaangalia ratings kama hivyo basi kikubwa maisha yaende
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…