Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

pint ya halima mdee hapo ni kuwa serikali inatumia kigezo cha ardhi kuwa chini yake kuwadhulumu wananchi hasa pale paapotokea maliasili chini ya ardhi hiyo.mwananchi anayeishi hapo wengi wao huwa wanadhulumiwa hapa fidia hawapewi

Fidia Juu na chini ndicho kinacholengwa kwenye hiyo sera.
So muhekezaji akija leo sio mambo ya kuhamishana, tupeeane hisa au anilipe nisepe.
 
Ni kweli ndio maana hata Halima Mdee amerusha kipande tu cha hiyo Sera, ni vyema angeiweka sera nzima kuhusu Ardhi tungeelewa zaidi... Hata hivyo hicho kipande kidogo kinaonyesha taswira nzima ya sera ya Chadema kuhusu ardhi...

Sasa kwanini umekoment kwneye kitu usichokijua?
 
Hivi mkuu ni kweli ardhi ya Tanzania inamilikiwa na Raisi? na kama ndiyo ina maana mpaka hizi zetu tunazouziana au kurithi?
Mkuu ni kweli kabisa,ardhi ya Tanzania inamilikiwa na rais ndio maana wewe umiliki wako wa ardhi ni wa miaka 33,66 au 99.Baada ya hapo hati yako ya kumiliki ardhi inakuwa imefika tamati,mpaka hapo utakapoangezewa muda mwingine tena.ili uendelee kuimiki.
 
Hili la ardhi kuwa mali ya serikali hata mimi silitaki kabisa, ardhi ni mali yangu iwe na madini, mafuta hata misitu, alaa,. Leo ukigungua madini faster usheondolewa, """BULYANGHULU"""
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.
Kwanj sasa hivi matajiri hawamiliki ardhi kubwa! Hebu tujjfunze kuelewa kinachosemwa badala ya kupelekwa na mkumbo.
 
Sera ya ardhi ya CCM imeshasababisha maafa makubwa sana kwa watanzania. Madini yote wamewagawia wazungu na wachina, gesi na mafuta wamegawa, na bado wanaendelea kupora ardhi ya wananchi bila hata fidia na kuigawa kwa wakoloni.

Sisi wenye ardhi yetu tunaonekana kama takataka kwenye hiyo ardhi, hasa pale inapoonekana ina thamani. CCM ilichoweza ni kupora ardhi yenye rasilimali na kuwapa wakoloni.

Hii sera ingetumika tangu zamani angalau kungekuwa na wenyeji wenye sauti kwenye hizo rasilimali.

Tatizo letu watanzania bado tupo kwenye ulimbukeni wa kufikiri kuwa maendeleo yanaletwa na serikali.
 
Tanaka la kuua linawaza vifo, makaburi kuua ua tu!
Hata tukichukulia kuwa hiyo sera ina mapungufu itamaanisha ndio CHADEMA ife?! ccm imekuwa na sera nyingi zisizofaa unaweza kueleza hapa kwa nini haijafa? Au unataka kutuaminisha kuwa ccm haijawahi kuwa na sera mbovu?!

Kama unaipinga, weka hapa weka hapa hoja zako badala ya kugeuka ghafla kuwa shehe Yahya.
 
"2. USIMAMIZI WA ARDHI: Chadema itaanzisha mfumo wa umiliki wa ARDHI ambapo kila MWANANCHI atamiliki ardhi na rasilimali zake JUU na CHINI ya ARDHI hiyo. TOFAUTI na CCM, Chadema HAKIAMINI katika KUFUKUZA watanzania kwenye ARDHI YAO kufuatia UGUNDUZI wa MADINI."
===========================

Chadema hili swala la ardhi litawamaliza, Kama Baba wa Taifa angefuata hii sera yenu leo kungekuwa na mtu mmoja mwenye uwezo wa kumiliki mkoa mzima na kila kitu kilichomo ndani yake.
View attachment 880155
Nchi ya Nigeria,ina sera kama hii,matokeo yake,mafuta nalipogunduliwa katika ardhi za watu,hinyo serikali haikuwa na namna ye yote ya kuweza kutwaa mafuta kwa manufaa ya wote.Wenye ardhi ambao mafuta yaligunduliwa waliwauzia wanaoweza kuzalisha mafuta kwa fedha za makubalino ya mtu muuzaji wa rasilima ardhi yenye na taasisi inayonunua ardhi na serikali kutegemea kodi tu.
Wazungu walizalisha mafuta bila kuajali athali za mazingira,wala kusaidia jamii iliyowazunguka,kwa sababu walikuwa kwenye ardhi yao,waliyoinunua kihalali.Ndio maana wakina wananchi walipolalalimika athali za mazingira,waliishia kupigwa risasi.
Kutokana na hali hii,wananchi wengi wa Nigeria waliendelea na wanaendelea kuwa maskini wa kutupwa,huku wengine wakiwa na utajiri wa kukufuru
 
Nchi ya Nigeria,ina sera kama hii,matokeo yake,mafuta nalipogunduliwa katika ardhi za watu,hinyo serikali haikuwa na namna ye yote ya kuweza kutwaa mafuta kwa manufaa ya wote.Wenye ardhi ambao mafuta yaligunduliwa waliwauzia wanaoweza kuzalisha mafuta kwa fedha za makubalino ya mtu muuzaji wa rasilima ardhi yenye na taasisi inayonunua ardhi na serikali kutegemea kodi tu.
Wazungu walizalisha mafuta bila kuajali athali za mazingira,wala kusaidia jamii iliyowazunguka,kwa sababu walikuwa kwenye ardhi yao,waliyoinunua kihalali.Ndio maana wakina wananchi walipolalalimika athali za mazingira,waliishia kupigwa risasi.
Kutokana na hali hii,wananchi wengi wa Nigeria waliendelea na wanaendelea kuwa maskini wa kutupwa,huku wengine wakiwa na utajiri wa kukufuru
Wanasahau kuwa ukisharuhusu sera kama hiyo tayari unaitoa serikali kwenye miongozo kuhusu ardhi hivyo athari zake kuwa kubwa zaidi kuliko faida.
 
shamba lako likikutwa na madini linakua Mali ya serikali. "ila" likikutwa na bangi ni Mali yako 😎
 
"2. USIMAMIZI WA ARDHI: Chadema itaanzisha mfumo wa umiliki wa ARDHI ambapo kila MWANANCHI atamiliki ardhi na rasilimali zake JUU na CHINI ya ARDHI hiyo. TOFAUTI na CCM, Chadema HAKIAMINI katika KUFUKUZA watanzania kwenye ARDHI YAO kufuatia UGUNDUZI wa MADINI."
===========================

Chadema hili swala la ardhi litawamaliza, Kama Baba wa Taifa angefuata hii sera yenu leo kungekuwa na mtu mmoja mwenye uwezo wa kumiliki mkoa mzima na kila kitu kilichomo ndani yake.
View attachment 880155
Mbona hata sasa tunamilikiwa na watu wachache!
 
idawa nadhani utakua haujamuelewa vizuri Halima Mdee, sheria ya Ardhi nchini inampa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumpa/kumnyang'anya/kumuongezea hati ya umiliki/kubatili haki ya umiliki kwa mtu yoyote anaemiliki ardhi kwa ridhaa/bila ridhaa yake, na kwa kumlipa fidia au bila kumlipa fidia.

Mara nyingi Ardhi inapogundulika kua ina madini au rasilimali nyingine chini, wananchi hua wanahamishwa kwa kulipwa fidia ya ARDHI tu (na si fidia za rasilimali iliopo katika ardhi yake au thamani ya kiwanja baada ya kugundulika kwa hizo rasilimali).

Mfano,

Una kiwanja, umekinunua Sh Milioni 1, kikagundulika kina madini ya dhahabu chini, utapewa hela ulionunulia hicho kiwanja na maendeleo uliofanya katika hicho kiwanja tu (kama vile kujenga nyumba, kupanda miti n.k) ila hautapewa fidia ya thamani ya hicho kiwanja baada ya ugunduzi wa hayo madini. Kawaida kiwanja hupanda thamani baada ya kugundulika kua kina rasilimali.
Madini agundue mwingine thamani ulipwe wewe. Muda wooote umayakalia ulishindwaje kuyagudua uithaminishe ardhi
 
Nchi ya Nigeria,ina sera kama hii,matokeo yake,mafuta nalipogunduliwa katika ardhi za watu,hinyo serikali haikuwa na namna ye yote ya kuweza kutwaa mafuta kwa manufaa ya wote.Wenye ardhi ambao mafuta yaligunduliwa waliwauzia wanaoweza kuzalisha mafuta kwa fedha za makubalino ya mtu muuzaji wa rasilima ardhi yenye na taasisi inayonunua ardhi na serikali kutegemea kodi tu.
Wazungu walizalisha mafuta bila kuajali athali za mazingira,wala kusaidia jamii iliyowazunguka,kwa sababu walikuwa kwenye ardhi yao,waliyoinunua kihalali.Ndio maana wakina wananchi walipolalalimika athali za mazingira,waliishia kupigwa risasi.
Kutokana na hali hii,wananchi wengi wa Nigeria waliendelea na wanaendelea kuwa maskini wa kutupwa,huku wengine wakiwa na utajiri wa kukufuru
Nadhani hujatafiti kiusahihi ndugu. Hebu kajichimbie tena kisha urudi kwa usahihi.
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.

Sasa kuna vita, je imesababishwa na nini? Na hata ingetokea, si kuna vyombo vya kuzima? Mbona maandamano ya Mange yalizimwa nchi nzima?
Mimi nadhani kinachomaanishwa, madini yakigundulika, kunakuwa na majadiliano kati ya serikali/Mwekezaji na mwenye mali, yaani mwananchi. Kuna ubaya gani?
 
We hujui kenyatta alitaka kukosa urais kwa ajili ya hiyo sera ikabidi arudishe sehemu ya ardhi.
Duh aliporudisha sehemu ya aridhi ndio kubadili Sera? Kwa nn mnapindisha maneno makusudi ? Au bongo zenu zimepata kiharusi nazo zikapinda?
 
Ngosha mwenyewe kachanganyikiwa analeta anayoyaita maendeleo kwa hela za mkopo lakini havutii watu. Sasa hivi anatumia madaraka yake vibaya kuhakikisha vyombo vya dola na tume vinamtangaza mgombea wa chama chake kushinda. Wananchi nao wamegoma kulazimishwa mapenzi ya kubakwa nao hawajitokezi kupiga kura. Imebaki kupika idadi ya wapiga kura ili kujifariji.

Hapo wenzake cdm hamna cha sera wala nini wanamtangenezea ajali tu, na yeye kwa hamaki lazima aiige. Si unajua kama hupendwi inabidi uiige anayependwa anatumia ushawishi gani?
Hahaha
 
Back
Top Bottom