Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

Sio kweli, ongea unachofahamu, sasa Wakenya wengine wanaishi wapi !!!!!!
Hiyo ni namba tuu kuonyesha ardhi ya Kenya inamilikiwa nachache, wengine wanabanana kwenye skwata. Km familia ya mkuu wa nchi inamiliki nusu ya ardhi unafikiru kitabaki nn?
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.
Sioni shida yoyote sababu sera haionyeshi kuzungumzia kupoka ardhi ila kuhakikisha wasiokuwa na ardhi wanapata na wakipata zikaandikiswa na kurasimishwa serikali ikihitaji watalipwa kwa haki. Sioni machafuko yanakujaje kama mpango wa ugawaji uko makini na usiyo na upendeleo!
 
Hiyo ni namba tuu kuonyesha ardhi ya Kenya inamilikiwa nachache, wengine wanabanana kwenye skwata. Km familia ya mkuu wa nchi inamiliki nusu ya ardhi unafikiru kitabaki nn?
Ninachofahamu ni kwamba kuna wachache wana miliki ardhi kubwa, ilhali wengi wanamiliki vipande vidogo vidogo ambavyo ni vya kwao binafsi. Hii ni tofauti na huko ambako mnasema ardhi ni mali ya umma lakini hilo linatekelezwa kwa watu wa hali ya chini pekee wakati kuna baadhi wanamilikia ardhi kwa miaka 999 !!!
 
"2. USIMAMIZI WA ARDHI: Chadema itaanzisha mfumo wa umiliki wa ARDHI ambapo kila MWANANCHI atamiliki ardhi na rasilimali zake JUU na CHINI ya ARDHI hiyo. TOFAUTI na CCM, Chadema HAKIAMINI katika KUFUKUZA watanzania kwenye ARDHI YAO kufuatia UGUNDUZI wa MADINI."
===========================

Chadema hili swala la ardhi litawamaliza, Kama Baba wa Taifa angefuata hii sera yenu leo kungekuwa na mtu mmoja mwenye uwezo wa kumiliki mkoa mzima na kila kitu kilichomo ndani yake.
Chama cha matajiri wenye sifa ya uchoyo. Unakumbuka kauli ya yule dogo wa Arumeru ambaye alishiriki kwenye mazishi ya mbwa?.
 
Idawa hayo ni maoni yako lakini ingekuwa vema kama ungefafanua vizuri kile kinachokufanya uiogope sera hiyo!
Mkuu kumbuka sera ya Taifa inasema ardhi ni mali ya serikali msimamizi mkuu akiwa Raisi...... hivyo hiyo sera mpya ya Chadema wanamaanisha ardhi itakuwa mikononi mwa wananchi wenyewe yaani ni juhudi zako kununua ardhi na kujimilikisha....bila kujali athari kwa kizazi kijacho.
 
Chama cha matajiri wenye sifa ya uchoyo. Unakumbuka kauli ya yule dogo wa Arumeru ambaye alishiriki kwenye mazishi ya mbwa?.
Hawa jamaa swala ardhi ni vyema wangeachana nalo kabisa kwenye sera yao mpya.
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.
Huwezi kujenga hoja kwa ushabiki na mihemko juu ya jambo fulani kisha ukaeleweka kwa wasio watumwa wa fikra
 
Mkuu kumbuka sera ya Taifa inasema ardhi ni mali ya serikali msimamizi mkuu akiwa Raisi...... hivyo hiyo sera mpya ya Chadema wanamaanisha ardhi itakuwa mikononi mwa wananchi wenyewe yaani ni juhudi zako kununua ardhi na kujimilikisha....bila kujali athari kwa kizazi kijacho.
Sera ya taifa haiwezi kubadilika?
 
Mkuu nimeweka screen shot ya Twitter Mbunge Halima mdee sera ya Chama kuhusu Ardhi naona kwa wengine haionekani....

Mkuu idawa kuna sera na kanuni za kutekeleza hiyo sera. Sera yao ya ardhi ni hiyo, ikifika wakati wa utekelezaji wa sera ndio utasikia kanuni na mbwembwe nyingine kama hizo. Hivi Hujawahi kuoana sheria inatungwa huku ukiambiwa ina nia njema, halafu wakati wa utekelezaji kunawekwa kanuni? Sera na jambo moja, kanuni/sheria kuitekeleza ni jambo jingine.

Mkuu hivi hujawahi kumtongoza mrembo ukajimwagia sifa za kufa mtu na miezi michache ya mwanzo ukafanya mambo makubwa. Lakini ukishamuoa ndio unamuonyesha uhalisia kwa kumpa taratibu za maisha?
 
Pamoja na yote lakini tumeona mara nyingi ardhi akitaifishwa na serikali toka mikononi mwa hao matajiri.....lakini huko kwingine huwezi kuona kitu kama hicho.!
Ninachofahamu ni kwamba kuna wachache wana miliki ardhi kubwa, ilhali wengi wanamiliki vipande vidogo vidogo ambavyo ni vya kwao binafsi. Hii ni tofauti na huko ambako mnasema ardhi ni mali ya umma lakini hilo linatekelezwa kwa watu wa hali ya chini pekee wakati kuna baadhi wanamilikia ardhi kwa miaka 999 !!!
 
Mkuu @idawa,kwa heshima yako humu hustahili kuandika hivi. Umeandika kitoto sana. Ulipaswa kueleza jambo la maana
Mbona inaeleweka..maana yake rasilimali kama madini zitamilikiwa na wachache..ingekuwa hivyo leo tanzanite isingekuwa ya tanzania..ingekuwa ya mzee Ngoma na familia yake..nilichogundua hapa ni rahisi ukiwa nje kuona makosa ndani ya uwanja..chadema hawajachukua hata nchi wameanza kuleta ubinafsi
 
Nchi kama Kenya hiyo ndo Sera yao, mbona hakuna vita ya kugombea ardhi ?
We hujui kenyatta alitaka kukosa urais kwa ajili ya hiyo sera ikabidi arudishe sehemu ya ardhi.
 
Pamoja na yote lakini tumeona mara nyingi ardhi akitaifishwa na serikali toka mikononi mwa hao matajiri.....lakini huko kwingine huwezi kuona kitu kama hicho.!
Kwa nini Serikali itaifishe ardhi, badala ya kuwafidia ?
 
We hujui kenyatta alitaka kukosa urais kwa ajili ya hiyo sera ikabidi arudishe sehemu ya ardhi.
Hiyo ni kwa sababu ya ulafi wa Baba yake ambaye alichukua sehemu kubwa ya ardhi na kuwaacha Wakenya wengi wakiwa na sehemu vipande vidogo vidogo. Mbona hakuna wanachi wengine waliambiwa kurudisha ardhi.
 
Wamepanick, ngosha kawashika pabaya. Wanajaribu kujiokoa wasisahaulike mazima.

Ngosha mwenyewe kachanganyikiwa analeta anayoyaita maendeleo kwa hela za mkopo lakini havutii watu. Sasa hivi anatumia madaraka yake vibaya kuhakikisha vyombo vya dola na tume vinamtangaza mgombea wa chama chake kushinda. Wananchi nao wamegoma kulazimishwa mapenzi ya kubakwa nao hawajitokezi kupiga kura. Imebaki kupika idadi ya wapiga kura ili kujifariji.

Hapo wenzake cdm hamna cha sera wala nini wanamtangenezea ajali tu, na yeye kwa hamaki lazima aiige. Si unajua kama hupendwi inabidi uiige anayependwa anatumia ushawishi gani?
 
Back
Top Bottom