Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,300
Reaction score
38,450
"2. USIMAMIZI WA ARDHI: Chadema itaanzisha mfumo wa umiliki wa ARDHI ambapo kila MWANANCHI atamiliki ardhi na rasilimali zake JUU na CHINI ya ARDHI hiyo. TOFAUTI na CCM, Chadema HAKIAMINI katika KUFUKUZA watanzania kwenye ARDHI YAO kufuatia UGUNDUZI wa MADINI."
===========================

Chadema hili swala la ardhi litawamaliza, Kama Baba wa Taifa angefuata hii sera yenu leo kungekuwa na mtu mmoja mwenye uwezo wa kumiliki mkoa mzima na kila kitu kilichomo ndani yake.

Naona mnataka kutupeleka Zimbabwe kwa hii sera yenu.

Screenshot_20180928-112112_Twitter.jpeg
 
pint ya halima mdee hapo ni kuwa serikali inatumia kigezo cha ardhi kuwa chini yake kuwadhulumu wananchi hasa pale paapotokea maliasili chini ya ardhi hiyo.mwananchi anayeishi hapo wengi wao huwa wanadhulumiwa hapa fidia hawapewi
 
Mkuu @idawa,kwa heshima yako humu hustahili kuandika hivi. Umeandika kitoto sana. Ulipaswa kueleza jambo la maana
Mkuu nimeweka screen shot ya Twitter Mbunge Halima mdee sera ya Chama kuhusu Ardhi naona kwa wengine haionekani....
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.
Nchi kama Kenya hiyo ndo Sera yao, mbona hakuna vita ya kugombea ardhi ?
 
idawa nadhani utakua haujamuelewa vizuri Halima Mdee, sheria ya Ardhi nchini inampa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumpa/kumnyang'anya/kumuongezea hati ya umiliki/kubatili haki ya umiliki kwa mtu yoyote anaemiliki ardhi kwa ridhaa/bila ridhaa yake, na kwa kumlipa fidia au bila kumlipa fidia.

Mara nyingi Ardhi inapogundulika kua ina madini au rasilimali nyingine chini, wananchi hua wanahamishwa kwa kulipwa fidia ya ARDHI tu (na si fidia za rasilimali iliopo katika ardhi yake au thamani ya kiwanja baada ya kugundulika kwa hizo rasilimali).

Mfano,

Una kiwanja, umekinunua Sh Milioni 1, kikagundulika kina madini ya dhahabu chini, utapewa hela ulionunulia hicho kiwanja na maendeleo uliofanya katika hicho kiwanja tu (kama vile kujenga nyumba, kupanda miti n.k) ila hautapewa fidia ya thamani ya hicho kiwanja baada ya ugunduzi wa hayo madini. Kawaida kiwanja hupanda thamani baada ya kugundulika kua kina rasilimali.
 
Mkuu nimeweka screen shot ya Twitter Mbunge Halima mdee sera ya Chama kuhusu Ardhi naona kwa wengine haionekani....
Hapana mkuu tatizo ni premise uliyoitumia ku set premise yako. Hiyo ni sera jaribu kufanya deep analysis katika kuchambua athali zake badala ya ulivyofanya.
 
View attachment 880155
Chadema hili swala la ardhi litawamaliza, Kama Baba wa Taifa angefuata hii sera yenu leo kungekuwa na mtu mmoja mwenye uwezo wa kumiliki mkoa mzima na kila kitu kilichomo ndani yake.

Kwa Tanzania sera ya ardhi imejitosheleza,
Idawa hayo ni maoni yako lakini ingekuwa vema kama ungefafanua vizuri kile kinachokufanya uiogope sera hiyo!
 
Back
Top Bottom