Sensa: Hotuba ya Rais Kikwete, yatokanayo

Nimemsikiliza na nimemwelewa vizuri,yaani JK hana msimamo kabisa, anajikanyaga kwenye mambo ya msingi kama haya, mara ilikuwa wakati wa ukoloni wanahesbu raia kwa dini na makabila yao mara serikali imejipanga kwa muda mrefu na sasa ndugu tafsiri yake ni nini kama si kwamba kwa sasa haiwezekani suala hilo kuingizwa kutokana na muda? hana msimamo huyu DHAIFU, kamsikilize tena tbccm lazima watarudia hotuba yake, nahisi wataifanyia editing kwai yale madudu siyo kabisa!
Hakuwa na jinsi kwani hoja za Waislamu si nyyepesi kama wengi wanavyodhani.
Serikali ilifanya makosa makubwa kukubali na kuachia taasisi zake kama idara ya utalii kuweka katika website yao asilimia ya watanzania kwa misingi ya dini,na hapa ndipo ambapo Waislamu wamemshika pabaya.
JK si dhaifu kama tunavyowaza ila anajua kwenda na wakati.Kumbuka alipo diffuse tension ya Zanzibar wkt isivyotarajiwa akamteua Ghrib Bilal kuwa mgombea mwenza.
Angalia alivyokubali kuandaa katiba wakati haikuwa katika ilani yake.
Angalia alivyowapeleka kina Mramba mahakamani hata kama watatoka yeye keshanawa mikono.
 
Huyu bwana ndiye kinara wa mambo haya ya udini .Angekuwa kongozi makini angewakemea ndugu zake siku ile ile wamelianzisha hili swala .Leo ni kuwa anawatuliza ndugu zake kuwa alitaka kuwasaidia kuingiza kipengele cha udini ila viongozi wenzake wamempinga. Jk kwa maoni yangu si mtu makini na mara zote anafanya mzaha na maswala yanayohitaji umakini .
JK analigharimu taifa, anagharimu amani yetu, anagharimu umoja wetu kwa ujumla CCM imeshafanya makosa mengi sana lakini hili la kutupatia JK ni kosa kubwa sana maana mtu huyu ataliangamiza taifa, MUNGU atusaidie kutuondolea hili jiwe.
 
Imaan fm hata yeye ndiyo radio yake ya uhakika ndiyo maana haifungiwi. Ni kama kioo ukivunja huwezi kutoka nje. In short haifungiwi
 
yaani huyu JK haeleweki namshangaa mpaka akaanza kuongelea mambo ya Dinosaur aliyeko Berlin Germany sijui jamaa huwa anaongea mambo hajui kuunga dot
 
Kati ya radio IMANI na gazeti la MWANAHALISI kimi kinahusika kutoa habari za uchochezi?
We mdada tofauti ni kubwa sana. Redio Imaani haiongei habari za uchochezi bali huwa inaongea matatizo yaliyopo ktk jamii,na hiyo ndiyo kazi ya media,media haitakiwi ifiche yaliyo ktk jamii. What do u mean unaposema uchochezi?. Kilichomkwanza kubenea alikuwa anaingilia uhuru wa mahakama. Na kilichomuuwa zaidi ni kesi ya dr uli. Sasa we mdada unapoitaja redio imaani kwa lipi hasa.
 
Ni rahisi sana kumpuuza Kikwete kwa kila anachosema au kufanya, lakini ninaweza kukuhakikishia sio mjinga hivyo kama wengi wetu tunavyodhania, na kama kweli ameongea hivyo usidhani ni mjinga, Kikwete ni mwanasiasa na anajua anachokifanya na mwisho wa siku utaona nani ni dhaifu yeye au sisi tunaopinga sensa kwa maana mwishowe wote tutahesabiwa na kubaki kuapia tu kwamba Sensa ijayo haki hapa patachimbika hatahesabiwa mtu,kama vile tunavyosema we ngoja 2015 ndio watatujua, ikifika 2015 oktoba tutaandamana kidogo tutasahau tutamkubali raisi mpya wa CCM na kuanza tena we ngoja 2020 ni kiama cha CCM hawatoki tumeshachoka! Lakini mwisho wa siku Kikwete gets what he wants, sasa sijui dhaifu ni nani?



Mkuu nlikuwa nimeanza kukuunga mkono mpaka ulipoanza kuzungumzia habari za 2015..hapo uliingia chaka.
 
Katika hotuba yake kwa Taifa kuhusu masuala ya sensa Rais Kikwete amekiri kwamba amekuwa akiwasikiliza waislamu wakihamasishana kutoshiriki katika sensa kupitia Radio yao (Radio Imani).

Radio hiyo imekuwa ikilalamikiwa kwa kuchochea chuki kati ya Wakristo na waislamu. Kwanini isifungiwe kama gazeti la Mwanahalisi?

huu ndio udhaifu wa jk
 
Umepona?
We mdada tofauti ni kubwa sana. Redio Imaani haiongei habari za uchochezi bali huwa inaongea matatizo yaliyopo ktk jamii,na hiyo ndiyo kazi ya media,media haitakiwi ifiche yaliyo ktk jamii. What do u mean unaposema uchochezi?. Kilichomkwanza kubenea alikuwa anaingilia uhuru wa mahakama. Na kilichomuuwa zaidi ni kesi ya dr uli. Sasa we mdada unapoitaja redio imaani kwa lipi hasa.
 
Mkuu nlikuwa nimeanza kukuunga mkono mpaka ulipoanza kuzungumzia habari za 2015..hapo uliingia chaka.
Nimeandika kutokana na uzoefu wangu na jamii yetu, siku zote tunafanya mambo yale yale na kutegemea matokeo tofauti, uchaguzi ulopita ilikuwa hivyo, kwanza tangu enzi za Mrema tunaongea sana ikifika siku ya vitendo hatuonekani aidha tuko bize na mambo mengine au sijui nini.

Mimi nina jamaa zangu wengi sana ni CHADEMA damu ukiwasikia wakiongea unaweza ukasema kweli hapa CCM hawatoki, siku ya Uchaguzi ilipofika kisia kilichotokea, hakuna hata mmoja alieenda kupiga kura na wote ukiwauliza walikuwa na visingizio ambavyo wao waliviona ni muhimu kuliko kupiga kura, Kikwete amekuwa Raisi malalamiko yamerudi palepale nikikaa nzo kijiweni ni mambo yale yale we ngoja 2015 lazima CCM tuwatoe!

Sasa ni vitu kama hivyo vinanisukuma kuandika hivyo, vinginevyo napenda mabadiliko lkn shida ni aina ya watu ambao wanataka hayo mabadiliko yaani sisi je tuko serious kweli au tunaongea mwisho wa siku tuna kitu muhimu zaidi cha kufanya zaidi ya kupiga kura!

Kama kweli tungekuwa serious na mabadiliko leo CCM isingekuwepo kabisa kwani haipaswi kuongoza nchi kabisa, lakini bado ipo na bado inakomandi kubwa tu!
 
naanza kunusa harufu ya udini Tanzania, umoja na nchi ya bila udini vilivyo mchukua mwl nyerere miongo 2.5 kuvijenga,,leo JK anaviua kwa masaa tu? kweli kujenga ni kazi kuliko kubomoa
 
udhaifu wa jakaya umejidhihirisha zaidi leo wakati anahutubia taifa juu ya sensa, alijichanganya aliposema kuwa serikali ilishafanya maandalizi ya sensa kwa kipindi kirefu hivyo kwa muda huu si rahisi kuingiza kipengele cha dini, wakati awali alishasema kuwa serikali haipangi maendeleo kwa kufuata dini wala kabila za watu na kwamba wakoloni ndio walikuwa wanahesabu watu kwa makabila yao na dini zao. Wanajamii jk anaamanisha nini juu ya hili suala mbona anazidi kudhihirisha udhaifu wake?
ina maana anasema wamechelewa au kipengle kilisahaulika.
Hapa kuna mawili;
ama ana maanisha tz bado haijasilimu
au anaukwepa mzigo wa kuwasaliti waislamu wenzie kiaina. N kwa maana hiyo anajua 2015 rais ajaye atamuachia vipengele vitakavyowezesha udini uweze kuingiza kwenye katiba na hivyo iwe rahisi kuingiza dini ktk sensa. Watz tuwe macho na hasa wasio waislamu hapa lazima kuna namna ya kuendelza maslahi ya oic kinamna . Na tuna tujua oic haipo kiuchumia bali kiislamu zaidi. Mwenye ubavu alikuwa mwalimu?
 
Waislam wameshakata shauri kutohesabiwa imedhihiri bakwata kwa waislam sawa na uvccm kwa vijana (hakuna ushawishi kwa jamii inayowakilisha).mpaka sasa sheikh wa bakwata wilaya za Arusha na Mbeya wamefukuza kwa kukataa kuburuzwa na mufti wa ccm.pamoja na urasim wa vyombo vya habari alhamdulillah taarifa zimefika kila kijiji na kesho ni utekelezaj tu. Shime waislam kesho hakuna kuhesabiwa wakilazimisha wape taarifa za kutengeneza!
 
ni kina nani walisema hawatashiriki sensa mpaka mjusi aliyeko ujerumani arudishwe?
 
Waislam wameshakata shauri kutohesabiwa imedhihiri bakwata kwa waislam sawa na uvccm kwa vijana (hakuna ushawishi kwa jamii inayowakilisha).mpaka sasa sheikh wa bakwata wilaya za Arusha na Mbeya wamefukuza kwa kukataa kuburuzwa na mufti wa ccm.pamoja na urasim wa vyombo vya habari alhamdulillah taarifa zimefika kila kijiji na kesho ni utekelezaj tu. Shime waislam kesho hakuna kuhesabiwa wakilazimisha wape taarifa za kutengeneza!

mkuu unakijua kiswahili?
 
mkuu unakijua kiswahili?

waislam wenyewe waaelewa as kwako ndo ngeni hizo jargon,kama sijui kiswahili imekuaje swali lako umelileta katika lugha hiyohiyo,tembelea kamusi ujifunze maneno mageni kama shime lililokuchanganya!
 
"Kuna wanao kataa kuhesabiwa mpaka mjusi aliyetoroshwa arudishwe na washangaa kuhusisha mjusi huyo na sensa tena ni mabaki ya mifupa ya mjusi- jk"
 
Back
Top Bottom