Selfika na JF: Snap it. Show it


Niliwahi kuingia nao kwenye taharuki mwaka 2016, yaani nipo sehemu nimekaa na washikaji kitaa mida saa tano asubuhi, tukashangaa ghafla defender imetia breki.

Kamanda wao akaamrisha tuingie kwenye gari kwa kosa la kunywa pombe ( bia) kabla ya muda ( enzi hizo haikuruhusiwa kunywa mpaka ifike saa kumi jioni). Nilishangaa sana maana tulikuwa tumekaa tu kumbe kuna tupu ( chupa) ya bia iko pembeni na sisi.

Wenzangu wakakubali kuingia mi nikakataa maana sikuwa na kosa, sijakaa sawa akaja mmoja eti anataka kunikamata, nikamdaka mkono na kimsukuma huko! Basi bhana sijakaa sawa wakaja wawili nikawadaka wote! Akarusha ngumi mmoja nikakwepa nikamrukia yule mwingine nikamtwisha hook punch.

Walikuwa kama nane hivi wengine walikuwa na chuma( SMG/ak 47).
Nikamvuta mmoja tena nikachana shati lake ( hakuvaa sare). Mzuka ukapanda niliwachezeshea mkono. Wale wenye bunduki wakakaa standby wakaniamuru nijisalimishe ( wala hawakuweka chamber risasi) nikawatukana.

Raia walijazana huku wakiwazomea hao polisi. Akaja mmoja tunafahamiana akaniomba niache. Akili ikarudi kuwa nimeharibu, nikapanda kwenye gari wakataka kuanza kunishambulia nikawaambia nitawavunjavunja na hizo silaha zenu ( wakatulia huku wamechakaa vumbi)

Tumefika kituoni nikaamuliwa kuvua mkanda ili niwekwe sero, nilipoutoa tu wakaanza mkanda huu umetoa wapi? Nikaawambia kwani unapatikana wapi?

Wakanywea; hahaha wakaniachia bure na knuckles wamekula.
Nice one
 
Screenshot_20220115-060520.jpg
 
Back
Top Bottom