Selfika na JF: Snap it. Show it

Wanawake wanaoweza kuyavumilia hayo maisha ndiyo wale ambao hawapendi kuwapikia wala kuwafulia. Kwahiyo ni ninyi tu kuchagua mtavumilia kipi maana hakuna mkamilifu chini ya jua.
 
Lazima afeli hapo sijui kwanini
 
Kama umeamua kufanya hivi na pesa unayo na ukaamua tufunge mkanda ili mambo fulani yaende(mf.ujenzi, uwekezaji) hamna noma kwa sababu ni suala la muda tu lkn kama ni kukomeshana sio poa😀.
We si ulisema unahitaji true love😂, unajua maana ya true love? Huko si kukomeshana, hio ni interview tu kuhakikisha je? Siku nikianguka utakuwa nami? Siku nimeugua maisha yametupiga utakuwepo kuniliwaza na kunipa moyo?

Yaani nakuigizia mpaka nijiridhishe
 
Lazima afeli hapo sijui kwanini
My brother alipata mchumba, dada mmoja asili ya ki Asia, nilichoandika hapo mkuu tuliki practice in real life nakupa true story kabisa..

Jamaa ndiye alileta wazo kwa sababu anataka kumuoa huyo binti baada ya mahusiano ya uchumba..

Akanishirikisha nikamwambia haina shida😀 ni wewe tu..

Jamaa akanikabidhi funguo za gari zake 2, akamficha mchumba wake kuhusiana na status halisi aliyokuwa nayo, alimwambia gari ameuza kulipa madeni..

Walikwenda kupanga uswahilini, yule dada alikuwaga amezoea ku drive akaanza kupewa nauli kwenda chuoni, at the time alikuwa mwanafunzi anajiendeleza..

Dada kapambana sana na daladala😁, akirudi maskani ni hadithi za vituko vya kwenye daladala, basi bwana ukapita mwezi, jamaa alikuja kunieleza kwamba imetosha anaona kafaulu tayari, nikamwambia pambana na hali yako, funguo sikupi tumekubaliana miezi mitatu we mwezi mmoja tu unaanza kubadili mawazo, jamaa akanambia anamuonea sana huruma😂..

Mzee wa kushauri nilikuwa nimesimamia msimamo wangu, nikamwambia sasa anza na kumuomba pesa kabisa😂, mwambie upo broke mbaya😂

Jamaa akasafiri kwenda mkoa flani kikazi, huko akawa anampigia mchumba wake simu kwamba hali ni mbaya, hana pesa ya kula, dada anatuma pesa, jamaa anamuuliza umeiotoa wapi? anasema mama alinipatia nikatunza..

Life likasonga, mwezi wa pili, mwezi wa 3, binti alifaulu ule mtihani hata mie sikuamini kabisa😁, niliweka msimamo kwa sababu huyu msichana nishazinguana nae, angefeli ingekuwa fresh tu kwangu.., angefaulu pia ingekua fresh cause bro angekuwa amepata mwanamke sahihi..

Nilimkabidhi jamaa funguo zake akiwa na furaha kinoma, ndoa ilifungwa wiki chache baadae, siku hio nilicheza mziki ukumbini mpaka watu walinishangaa😂..

Na mie nilijipiga siku hio nikawapatia zawadi ya fridge, ngoja niangalie picha kama ipo kipindi natoa zawadi niiweke..

Basi ikawa hivyo, jamaa alinushukuru baadae, wakawa mke na mme..

Mi sio mwandishi mzuri..

Mkuu hii sio hot tea, hii kitu imenitokea na nimei practice kabisa..

Wapo kwenye ndoa miaka michache sasa, wana 2 beautiful daughters na life linasonga..
 
Wanawake wanaoweza kuyavumilia hayo maisha ndiyo wale ambao hawapendi kuwapikia wala kuwafulia. Kwahiyo ni ninyi tu kuchagua mtavumilia kipi maana hakuna mkamilifu chini ya jua.
Hilo linaitwa chujio la chuma😂

Fake na real lazima wajulikane..

Ni sawa kabisa kwa mwanamke kumuuliza mwanaume kama ataweza kum afford, huyo hana shida, huyo ni muwazi na lazima mawazo yake yaheshimiwe.. na pia ni muwazi..

Lakini waigizaji hivyo ndivyo inapaswa iende hasa suala la ndoa, ndoa ni issue very sensitive, mahusiano ya kawaida hata kama mkiwa mnakwenda Paris kuangalia show ya Ty Dolla sign for one weekend haina shida, lakini ndoa, asee unahitaji mtu sahihi..

Sio mwanamke wala mwanaume wote mnahitaji mtu sahihi, that's why wenzetu marriage ni inshu serious sana..

Kikubwa be real, kama unaona hawezi kuku afford mwambie mapema, lakini kunidanganya utakuwa nami kwenye shida na raha then later unanibadilikia hio sio poa.. we lazima upite kwenye chujio la chuma, na hakuna kitu kinauma duniani kama kutendwa na umpendaye😉
 
Sadly, kuweza kumvumilia mtu kwa shida doesn't guarantee mta-last long 🥴🥴
 
Sadly, kuweza kumvumilia mtu kwa shida doesn't guarantee mta-last long 🥴🥴
Ni kweli lakini usi take risk pasipo risk management..
Kwenye kilimo utafuata taratibu zoote na gharama itakutoka lakini huna uhakika kama utavuna, kuuza na kupata faida, waweza ishia kwenye hasara..

Lakini hata kama utaishia kwenye hasara na kujua haikwepeki, chukua hatua basi at least za kupunguza hio hasara..

Mfano wanao trade stocks wanajua kuna risk is involved, lakini Wana risk management, just in case soko limekwenda against wasipate hasara kubwa..

Hio ni same na hiki ulichosema, of course sio guarantee lakini kwa kiasi fulani itasaidia😊
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…