Selfika na JF: Snap it. Show it

Tuko pamoja naye katika kipindi hiki kigumu

Sent using Jamii Forums mobile app
 

maskini duuh pole sana kwake Mungu aitie nguvu familia kwa kipindi hiki kigumu kwao
 
Pole sana kwake Saint Anne
Huyu mkuu amekua mdau mzuri sana kwenye uzi wetu huu na nyuzi nyingine pendwa pamoja na salamu za pole yunzotoa napendekeza tufanye chochote kinachowezekana kumfariji

Nashauri Heaven Sent au mkuu Mshana Jr mtusaidie kuli organise hili kama itawapendeza
 
Ooooh JAH awape wafiwa wote faraja na uvumilivu mkubwa wa kuweza kupambana na kipindi hiki kigumu kwao cha kuondokewa na mpendwa wao,

Mpendwa huyo baba apumzike kwa amani, bwana alitoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.

Raha ya umpe eeeh bwana, na mwanga wa milele umuangazie
Mpendwa Baba yetu astarehe kwa amani, AMEEEEN.
 
aisee pole sana kwake....Mungu amlaze baba mahali pema peponi

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Limepokelewa hili
 
Too bad nipo safarini, so nakuwa on and off, sina utulivu. Ngoja tuone litakalowezekana kufanyika

 
Aisee, pole yake na kwa familia yake yote, Mungu amtie nguvu katika kipindi hiki kigumu..hakika sisi sote njia yetu moja.
 
Pole sana Anne jamani Mungu amtie nguvu sana yeye pamoja na familia yake

Mama mchungaji tulio mbali basi tutumiwe no hata tumfariji kwa pole
 
Ooh! Habari za hovyo kabisa hizi...

Kama binadamu hatuna la kufanya isipokuwa kumuombea marehemu pumziko jema na lenye heri. Na kwa wapendwa walioachwa; hebu Roho Mtakatifu Ajulikanaye pia kama Mfariji Mkuu Akawapoze mioyo yao na kuwapa faraja na matumaini katika kipindi hiki chenye giza na maumivu makali.

Na kwenu Heaven Sent na/au Mshana Jr. Saint Anne ni memba mwenye mahusiano mema na watu wengi; na anajulikana sana hapa. Anzisheni uzi kamili wenye taarifa hii ili habari hizi ziweze kuwafikia watu wengi. Na cha muhimu zaidi, toeni mwongozo wa jinsi ya kutoa rambirambi ili tunaoweza kufanya hivyo tufanye hivyo mara moja.

Asanteni na poleni
 
Ok sawa ngoja nifanye hivyo .. Nitapost kule mchanganyiko
 
Ooh pole kwake na kwa familia yote.
Mungu awe nae na kuwepo mkakati wa namna ya kumsaidia mwenzetu.
Lakin madame vizuri upost kama uzi wa kipekee ili iwe wepesi watu kujua
Nilishindwa kuanzisha uzi kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu. At last nimefanikiwa kuwasiliana naye so tunaweza kuendelea na mengineyo.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…