Selfika na JF: Snap it. Show it

Kiimani zaidi

ZABURI 137
Maombolezo juu ya maangamizi ya Yerusalemu
1 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2Katika miti iliyo katikati yake
Tulivitundika vinubi vyetu.
3Maana huko waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka tuwatumbuize;
Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4Twawezaje kuimba wimbo wa BWANA
Katika nchi ya ugeni?
5Nikikusahau, Ee Yerusalemu,
Mkono wangu wa kulia na upooze.
6 Ulimi wangu na ugandamane
Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7 Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,
Siku ile Yerusalemu ilipotekwa.
Kwa namna walivyosema, Bomoeni!
Bomoeni hata misingini!
8 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,
Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,
Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…