Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Urojo na mazaga yake unaweza kupika?
Naweza na ni rahisi sana yale mazaga yake ndio huchosha uanze kachori,nyama mayai mbogamboga crips bagia sijui nini 😁 uje kwenye rojo aisee bora uwe unapika mle wengi ila peke yako inatia uvivu kimtindo
 
Naweza na ni rahisi sana yale mazaga yake ndio huchosha uanze kachori,nyama mayai mbogamboga clips bagia sijui nini 😁 uje kwenye rojo aisee bora uwe unapika mle wengi ila peke yako inatia uvivu kimtindo
Nakuonea donge! Huku kuna sehemu nilikua nakunywa haukua mzuri kivile lakini nilikua naridhika.
 
Huenda ilikuwa ni menu maalumu kwa wageni wao

Kama una mtu DSM mwambie wakupakilie kwenye sgr, ni mwendo wa kusubiri dakika 120 tu

Naamini hotel kubwa kubwa za hapa mjini watakuwa wanapika kwa oda
Nishapata wanapouza nimewapigia simu wanao najiandaa kujilamba tu usiku

Selikavu asante nimewapigia simu wanao panaitwa Arabian mishkaki
 
Dah 🤣🤣 babu umejua kumshauri
Labda ukute anategemea kutuletea vitukuu (mama kija)

Nakumbuka kuna ujauzito fulani wa Bibi yenu, alikuwa anataka chakula fulani Kinapatikana DSM pekee na wakati huo tulikuwa Mkoani

Bahati nzuri nilikuwa na cabin crew nafahamiana naye wa shirika fulani la ndege, ndiyo nilikuwa namwagiza 🙌

Akipendacho binti.......🤗
 
Back
Top Bottom