Duuh mimi sitasahau mwaka fulani kuna siku nilikuwa gerezani pale usiku, ilikuwa msimu wa mvua na kama unavyojua huu mkoa mvua zikinyesha, mafuriko na foleni kila kona plus shida ya usafiri mwee
Mimi nilikuwa natoka gerezani naenda morocco, sasa siku hiyo sijui waliamua kutukomoa abiria wa morocco, mwendokasi zote za morocco wakazipeleka kimara na mbezi yani tulipangishwa foleni tu
Nahisi waliona abiria wa morocco ni wachache hivyo wakatuweka pending kwanza, basi abiria wa kimara na mbezi nao hawapoi ilikuwa ni bumper to bumper, ikijaza moja iking'oa inayofuata nayo haikai dakika mbili inajaza inang'oa
Hapo unasikia wanatangaza abiria kituo cha kwanza Ubungo Terminal na bado imejaa dadeki, maana yake hiyo ni express ninyi mnaoshuka katikati hapo sijui Fire hadi Shekilango msipande, maana haishushi kiumbe
Daah yani katika siku nilizowahi kupanda mwendokasi nikakutana na kadhia ile siku sitakaa niisahau asee