Una uhusiano gani na huyo mtu uliyemwamini kukuandikia recommendation letter? Kama ni profesa alikufundisha una uhakika bado anakukumbuka? Mara ya mwisho uliwasiliana naye lini au mtu hamjawasiliana tangu uondoke chuo na leo ndiyo umekurupuka tu kumtafuta baada ya kuomba kazi inahitaji recommendation.
Tujenge tabia ya kuwa karibu na watu wachache tunaojua kuwa ni wa muhimu katika maisha yetu; na tusiwatafute tu pale tunapokuwa tunawahitaji. Hili ni jambo la muhimu sana maishani.