alubati
JF-Expert Member
- May 29, 2016
- 5,684
- 12,153
Hapajui dodoma kweli huyo niko mwaka wa pili hapa muda wowote nabeba virago
Hapajui dodoma kweli huyo niko mwaka wa pili hapa muda wowote nabeba virago
Dah, upo sahihi Sana kaka, actually nipo Dodoma but Kama usemavyo ukiwa huna channel Ni jiji gumu Sana, Cha muhimu kabla ya kuja angalau uwe na pakuanzia au ujitosheleze mahitaji yote ya muhimu, mfano Kodi na mtajiTuache mzaha Dodoma kama huna chaneli pagumu sana.kule kama sio mtumishi wa umma basi angalau uwe mfanyabiashara ndio utaona nafuu.au uwe na ajira ya namna yoyote ile, mission town utakufa njaa kule,utaishia kupunga upepo Nyerere Squre tu.ukienda uwe na pa kuanzia.
Babati- Kilimo biasharaWakuu habari, mimi ni mdau wa maswala ya ujenzi (civil engineer) nataka nifanye maisha ambayo kwa kiasi kikubwa yatakuwa yanahusiana na sekta ya ujenzi.
Je, kati ya Dodoma na Babati ni mji gani utakuwa poa zaidi?
Na je gharama za maisha kwa ujumla zikoje maeneo hayo.
Pia kati ya miji hiyo miwili Fursa za Maendeleo zikoje.
Nakaribisha maoni yenu huenda uzi huu ukawasaidia wengi.
Asanteni.
Kabisa yaani ukiwa na ka biashara unawachomoa sana mpunga watumishi.Dah, upo sahihi Sana kaka, actually nipo Dodoma but Kama usemavyo ukiwa huna channel Ni jiji gumu Sana, Cha muhimu kabla ya kuja angalau uwe na pakuanzia au ujitosheleze mahitaji yote ya muhimu, mfano Kodi na mtaji
Nipo Dodoma but mwanzon nililiona jiji gumu Sana kiasi Cha kukata tamaa, Kwan me ni graduate na nilihitaji nguvu nyingi Sana ya kujipanga, kwa dodoma Kuna biashara nyingi Sana unaweza ukazifanya na ukatoboa, hasa kuku, matunda na fast foods, TRUST ME
" jua kali"Babati- Kilimo biashara
Dodoma-jua kali
Kweli aisee...Tanzania nchi kubwa sana sehemu nzuri ni pale unapopata rizki yako. Hata Dar kuna watu wako pale ukiwaona kama wanasindikiza wenzao tu maisha wanayoishi. Nchi kubwa fursa hazifanani ni juu yako wewe maana hatuwezi watu Tz tukarundikana sehemu moja kugombea kitu kimoja. Tatizo la Tz maisha yetu na biashara zetu zinafanana sana nchi kama mfano USA utakuta kila state wazuri kwa jambo fulani hawafanani na wenzao kuna state wao kamali tu, wengine mafuta zaidi, wengine viwanda vya magari tu na wengine mambo ya jeshi tu. Tz tungejenga system hiyo tungefanikiwa sana, mfano Arusha utalii tu, Mwanza labda madini tu, sujui pwani mashamba tu ukija Dodoma wine sana, Dar mambo ya biashara hivi yaani hii mifano tu lakini ungefanywa utafiti kila mkoa wazuri kwa kitu gani investment ifanywe kubwa kwa ujumla wote tunachangia TZ. Bahati mbaya tunafanana sana.
Mkuu nakushauri nenda Dodoma. Kama ulivyosema unajihusisha na maswala ya ujenzi nenda huko hutojuta. Kwasasa Jiji la Dodoma lina muingiliano wa watu wengi sana. Hata ukianzisha mgahawa au any opportunity unatoboa mapema tu.
Juzi kidogo nilale nje. Nilipata lodge maeneo ya Town. Asubuhi nikarudisha ile lodge nikijua nitamaliza shughuli Zangu pamoja na kikao mapema then nirudi Zangu Dar. Cha ajabu mambo yalienda Sivyo. Ilipofika saa Kumi na mbili nikaanza kutafuta lodge. We we we weeeee nilizunguk Town nzima vyumba vimejaaa. Ikabidi niende maeneo ya Four way barabara ya Mwanza. Huko ndiko nilikolala
Je kwa biashara za machinga panafaa?
Kilimo,ardhi yake ina rutuba,ukizama kwenye kilimo lazima uchomoke...Kuna madini gani boss
One way ipo sehem gan mkuuMachinga dodoma eneo zuri la umachinga ni one way ,Ila kupata eneo ndo mbinde sasa ,unaweza ukawa na million mbili na eneo la kupanga vitu usipate.