hebu tuanzie hapa jana mahakama imesema kwamba bunge la katiba linatakiwa kurekebisha katiba ya warioba tu na sio kutengeneza rasimu ingine sasa je mpaka hapo hili bunge lina uhalali wa kuendelea kuwepo?
unajua rais ameshaona moto na ukweli ni kwakua anajua hana jinsi kwasasa mambo yamemkalia pabaya na hajapata washauri wazuri kwenye mwenendo wa siasa kwa sasa.
kwanza waliposema mambo ya muungano yamekuwa sijui 14 badala ya 7, nashangaa sana kwann sisi tanganyika tuiogope zanzibar kuliko ambao ni sawa na ka mkoa kamoja ka tanganyika na kusahau mikoa yetu?
kuna mambo ambayo hatuyajui umeme zanzibar tunawalipia, maji hivyo hivyo, na hata chuo wenzetu wasoma kwa unafuu kuliko sisi lkn sisi tunakaa kimya. cha ajabu zaid wa zanzibar hawatak kuskia tunaidai tanganyika yetu wanafikiri jinsi watakavyopata tabua na kuona waendelee kukaa kwenye ndoa inayotuumiza sasa leo tumechoka mie ni miongoni mwa wanaosema wazi tunaitaka tangnyika yetu.
Ndugu,
Hukumu ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar haikusema kama ulivyoweka katika msingi wa hoja yako.
Ieleweke kuwa Pingamizi lao la kwanza la Kutaka Bunge lisimamishwe wakati kesi yao inaendelea kusikilizwa, lilikataliwa ambapo mahakama ilisema Bunge Maalum liko kisheria na katika sheria hiyo litaendelea.
Habari hiyo ililipotiwa hapa, gonga kama unataka kuisoma,
Madai ya pili ya kutaka tafsiri sahihi ya kifungu cha 25 (1-2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 yamepatiwa majibu pia na Jopo la Majaji hao watatu ambao ni Jaji Augustino Mwarija, Dk Fauz Twaib na Aloyisius Mujuluzi.
Akisoma hati ya amri ya mahakama Jaji Augustino Mwarija kwa niaba ya majaji watatu waliosikiliza shauri hilo, amesema kumekuwepo na Utata katika kifungu cha 25(1) na 25(2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 katika lugha mbili zilizotumika kuandika sheria hiyo. Na kusema kuwa kutokana na
kifungu hicho kinalipa mamlaka Bunge Maalum la Katiba kuijadili rasimu ya katiba, kubadili au kuboresha na kuwa Bunge hilo lina mipaka kwa kuzingatia kifungu cha 9(2) cha sheria ya mabadiliko ya katiba.
Akizungumza baada ya amri hiyo nje ya mahakama kuu Wakili wa Saed Kubenea, Peter Kibatala amesema wanafurahi kuona mahakama imetoa maamuzi kwa wakati na kueleza kuwa tafsiri iliyotolewa ni katika kusaidia wananchi kupata katiba iliyotokana na maoni yao.
Mipaka ya kuzingatia katika kutunga Katiba mpya kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kwenye Kifungu cha 9(2) ni kama ifuatavyo,
9(2) Katika kutekeleza masharti ya kifungu kidogo cha (1), Tume itaongozwa na misingi mikuu ya kitaifa na maadili ya jamii ya kuhifadhi na kudumisha mambo yafuatayo:
(a) kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano;
(b) uwepo wa Serikali, Bunge na Mahakama;
(c) mfumo wa kiutawala wa kijamhuri;
(d) uwepo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(e) umoja wa kitaifa, amani na utulivu;
(f) uchaguzi wa kidemokrasia wa mara kwa mara katika vipindi maalum kwa kuzingatia haki ya watu wote wenye sifa ya kupiga kura;
(g) ukuzaji na uhifadhi wa haki za binadamu;
(h) utu, usawa mbele ya Sheria na mwenendo wa sheria; na
(i) uwepo wa Jamhuri ya Muungano isiyofungamana na dini yoyote na inayoheshimu uhuru wa kuabudu.
Nakala ya hukumu hii hapa,