Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Nawaombeni wote mtafute muda mkaisome kwa makini hiyo inayoitwa rasimu ya tatu ya katiba iliyowasilishwa na Andrew Chenge iliyojengwa katika msingi wa muundo wa serikali mbili! Wonders will never cease!
 
Ouuuuuchh!!! naaam!

Mkuu kuna siku nilishangaa sana jamaa mmoja ni Phd holder alikaa na kusema kuwa Zanzibar ina mafuta, na alisema ukienda pemba mafuta yanaonekana juu juu kabisa. Na hiyo ndio sababu iliyowafanya waamue kusema mambo ya madini yaondolewe kwenye suala la muungano........

JK amabaye has first hand info kuhusu map ya miamba ya Tanzania kwenye ukanda wa pwani (give the knowldge he aquired from being waziri wa nishati na madini), kwa furaha kabisa alikubali hoja hiyo kwa wazanzibar kwa kuwa aliona ni wazo na aimani ya kitoto.
 
Ndugu,
Tatizo la watu kama wewe mnaziangalia siasa za Uingereza mkiwa nje na kuanza kujenga hoja ambazo hazina ukweli kiuharisia na kimantiki. Unatakiwa uzichambue kwanza katika historia yake na hali ilivyo kwa sasa.

Bila kufanya uchambuzi fasaha unajenga hoja kama hii hapa chini kutaka kuwaaminisha wanaJF,

Waliokuwa wanataka uhuru kamili ni viongozi wa SNP ambao walijiunga na wananchi wengine katika mwanvuli wa harakati wanaouita Scottish nationalism.

Hoja ya Mamlaka kamili ilikataliwa na wananchi wengi katika kura ya maoni. Wewe bado unaongelea Mamlaka Kamili.

Hoja yako haitofautiani na madai ambayo yamekuwa yanatolewa na baadhi ya wanasiasa nchini walionukuliwa katika mikutano ya hadhara wakidai wanataka Zanzibar na Tanganyika zipewe MAMLAKA KAMILI.

Baadhi ya wanasiasa wa kikundi kinachojiita UKAWA walinukuliwa wakisema,



Kuanza kujenga hoja katika msingi wa kitaifa na kuondoa uchama kwenye siasa za Uingereza ni kupotosha au kutokuzifahamu siasa za Uingereza.

David Cameron hakukubali kufanyika Kura ya maoni kwa sababu ya kusukumwa na mstakabali wa kitaifa bali kwa sababu ya kupambana na chama cha Labour.

Chama cha Labour ambao ni waanzilishi wa devolution nchini Scotland hawakutaka kufanya kura ya maoni badala yake waliamua kuwapa madaraka zaidi lakini waendelee kuwa sehemu ya Muungano kwa sababu Scotland ni ngome yao katika maamuzi ya Westminster.

Kwanza lazima uelewe kuwa chama cha conservative kina mbunge mmoja tu anayetoka Scotland katika Bunge (Westminister) wakati Labour wana Wabunge kama 40, kwa maana kuwa chama cha conservative hakikubaliki Scotland.

Kujitenga kwa Scotland kungenufaisha chama cha Conservative katika bunge la Westminister zaidi ya Labour Party, ndiyo maana kwa sasa unamsikia David Cameron akisema anapenda kuwepo na English votes for English laws, kwa maana kuwa, masuala ya England yawe yanaamuliwa na wabunge wa England ambao kiuharisia, wabunge zaidi ya 40 wa Labour kutoka Scotland hawataruhusiwa kuamua masuala hayo. Kama hili litakubaliwa, basi chama cha Labour hakitakuwa na wabunge wengi watakao weza kupitisha maamuzi ya serikali itakayoundwa na chama cha Labour.

Chama cha Conservative kilikuwa na win win situation katika matokeo ya Kura ya Maoni na siyo kusema kilisimama katika msingi wa utaifa. Conservative walisimama katika msingi wa kichama, vivyo hivyo, Labour nao walisimama katika msingi wa Uchama ndiyo maana wanasiasa kutoka Labour ndiyo walikuwa wanapigana kihoja kwa hali na mali ili Scotland ibakie katika Muungano huku wanasiasa wa Conservative wakiwa wamekaa pembeni wakichekelea mtifuano.

Kinachofanyika katika suala la Scotland ni party politics ambazo kwa mtu asiye chambua kwa undani hawezi kuelewa.

Unafahamu kinachoendelea kwa sasa kuhusu suala hili kwenye Mkutano Mkuu wa Labour huko Manchester?
Mheshimiwa
Hotuba ya Cameron tumeiweka hapo. Vyombo vyote vya habariduniani tumesoma maoni yao. Ukweli unabaki kuwa D.Cameron ameeleza kamakiongozi wa taifa.
Kwa Tanzania, ukimtazama au kusoma hotuba ya Cameron na jinsianavyo handle hili suala, utagundua black and white na bogus wengine dunianiwanaojiita viongozi
Soma Historia ya Uingereza na siku za karibuni kuhusu JohnMajor. Thatcher, Blair na Cameron. Scotland imekuwa mwiba bila kujali uchama nandio maana hata wajumbe waliotuliwa kusimamia mageuzisi wa vyama.
Lazima tukubali handling ya wenzetu ni bora sana kulikoviongozi wetu ambao si kuwa wamebofoa bali tuna wasi wasi kama wanajua kwaninini viongozi.
Kiongozi amebadili misimamo Zaidi ya mara 3, akisema hilileo, kesho lile, keshokutwa lingine n.k.
Ukimweka katika mizani na D. Cameron utafahamu kwaniniTanzania ni masikini.

N.B
Please check the spelling and don't confuse between the bestand the bogus
 
Mkuu kuna siku nilishangaa sana jamaa mmoja ni Phd holder alikaa na kusema kuwa Zanzibar ina mafuta, na alisema ukienda pemba mafuta yanaonekana juu juu kabisa. Na hiyo ndio sababu iliyowafanya waamue kusema mambo ya madini yaondolewe kwenye suala la muungano........

JK amabaye has first hand info kuhusu map ya miamba ya Tanzania kwenye ukanda wa pwani (give the knowldge he aquired from being waziri wa nishati na madini), kwa furaha kabisa alikubali hoja hiyo kwa wazanzibar kwa kuwa aliona ni wazo na aimani ya kitoto.
Hawa watu walisikia kuna madebe 37 wakakimbia BLW kuatungia shariaya kuyaondo katika muungano
Wakiyapata hata kusikia neno Tanganyika kule kwao itakuwa niharamu na kosa la jinai.

Huyo anayesema mafuta yanaelea ni sehemu ya jamii tunayoishinayo, tv za rangi na umeme wa meli, ndio maana tunasema , hapana! Tunataka Tanganyikayetu
JK alichokifanya ni kuwafurahisha bila kujua anaudhi wenyemuungano
Leo nguvu ya Tanganyika ni kubwa sana kuliko wakatimwingine.

Na kadri yanavyotokea kama ya rasimu ya Sitta na CCM ndivyo hasira zaWatanganyika zinapanda Zaidi.

Kamsikilize Cameron halafu umsikilize JK katika issue yamuungano!
Sisi si masikini wala si nchi masikini, tuna umasikini wauongozi wa nchi
 
Nguruvi3,
Mkuu wangu wewe na Mchambuzi mumeamua kuwapotosha wananchi vibaya sana na kwa sababu hawaelewi wamekubali kuwa misukule wakitumikia wasichokielewa.

Swala la Scotland linafanana sana na swala letu kwa madai ya nchi ya Scotland japo sisi tuko mbele yao kidogo na hivyo ni serikali ya England kujifunza kutoka kwetu. Changes zitakazo fanyika sisi tayari zimekwisha fanyika na ndizo zinawatpa taabu kwa sababu Scotland walichotaka ni kuondosha mamlaka ya serikali kuu kukusanya kodi badala yake wapewe wao kisha wachangie mfuko wa taifa.

Scotland walichotaka pia ni wao kuwa wasimamizi wa shughuli zote zinazohusiana na huduma za wananchi wake (social welfare) mamlaka ambayo yapo chini ya serikali kuu hivyo hizi changes hazina mahusiano yoyote na kuundwa kwa serikali ya shrikisho ama kuwa na serikali 5 zinazounda UK. Na kwa nini Scotland wametaka hivyo? - ni kutokana na kuwepo mafuta na gas nchi mwao hivyo wanachokitaka kwa kila pato la kodi zao mfano corporate tax wawe na asilimia yao, halafu wachangie mfuko wa Taifa badala ya fedha zote kuwa mfuko wa Muungano kisha wakatiwe baada ya kuzingatia mahitaji ya nchi nne zilizopo katika muungano. Na haya ndio pia yalopelekea Zanzibar kuendeleza madai zaidi juu ya mapato yatokanayo na gas na mafuta jambo ambalo wao wanadai hawapewi kitu kutoka bara.

Nimekwisha kukwambia ni rahisi sana kuwalalamikia Zanzibar kwa haya lakini haya yalifanyika baada ya makubaliano baina ya CCM na serikali ya Zanzibar kupewa mamlaka hayo (kina Cameron wetu) jambo ambalo sisi tulitakiwa kulizungumzia toka mwaka 2010 bungeni na sio vinginevyo. Na wala matatizo yake hayakuanza jana ila toka mwaka 1984 tulipobadilisha mfumo wa kiuchumi kutoka Ujamaa kwenda Ubepari tukapotea kuunda mfuko wa pamoja kukusanya mapato ya taifa, hivyo Zanzibar wasingeweza kuchangia kitu ambacho hakipo wala hakuna sheria inayosema watachangia asilimia ngapi ya makusanyo yao.

Tofauti na sisi Ungereza wakifanya hivyo wataweka tofauti ya mifuko hivyo Scotland watalazimika kuchangia moja kwa moja mfuko huo wa pamoja kwa silimia itakayo wekwa na vile vile yawezekana likaondolewa ktk sheria mama ili kila upande utakusanya kodi zake na kuchangia mfuko wa Pamoja ni swala la maridhiano kwa washirika wote yatafuatia. Na hakuna kigumu hapa kabisa ikiwa kesho bunge letu la katiba litakubaliana kuweka asilimia fulani kwa kila kodi kuingia mfuko wa pamoja halafu kila upande utajadili na kupanga asilimia yake.

Tuacheni hizi habari za Siasa kutumia jukwaa hili kutangaza vitu ambavyo vitawapotosha wananchi na kuwa misukule ya chama badala ya kutazama mustakabali wa Taifa letu. Tujifunze kwa mema badala ya kuzua uhasama usokuwa na maana kabisa kwani kesho maneno haya yatakuja wahukumu nyie mlowalisha wananchi haramu hizi.
Mkuu Mkandara , D Cameron ni mwingereza Zaidi kuliko wewe

"So, just as Scotland will vote separately in theScottish Parliament on their issues of tax, spending and welfare, so tooEngland, as well as Wales and Northern Ireland, should be able to vote on theseissues - and all this must take place in tandem with, and at the same pace as,the settlement for Scotland."
Anaendelea
"And I want Wales to be at the heart of thedebate on how to make our United Kingdom work for all our nations.
"In Northern Ireland, we must work toensure that the devolved institutions function effectively.
I have long believed that a crucial part missing from this national discussionis England.

"We have heard the voice of Scotland - andnow the millions of voices of England must not go ignored
Mkandara kama unahitaji tafsiri ya Kiswahili tafadhalitueleze kwanza kabla hujajibu,
Pili, kama umeelewa alichosema Cameron tufafanulie
.
Tatu, tumeweka hoja zetu katika mabandiko 6 ili kuwezakuchambuliwa na kila mmoja. Hujajibu hoja hata moj, hivi unapata wapi ushujaawa kusema tunapotosha?

Mfano, tumeuliza kuhusu unitary na federal system, tuelezewapi ilianza federation ikaja unitary
Nne, hotuba ya Cameron hiyo hapo, kama wewe ni mwingerezakuliko yeye mjibu basi tukusikie.
 
Tetty naungana na wewe sema pia kwa uwezo hawa jamaa walionao siku wakijiexpose bado maisha yao yatakuwa hatarini..

Tusisahau sisi hatuna viongozi ila tuna watawala.
Mtawala anaua na kuharibu yoyote asiyefuata matakwa yake! poor Tanzania.

Ni kweli,lakini tutaogopa mpaka lini?Ninajua kuwa wachache wetu wanaopata ahueni kutokana na hali ilivyo na wengi tunaoumia siyo sababu tumekosa mahali pa kulala,kula,au kutibiwa bali wale wengi wanaokosa huduma hizi muhimu.Leo tunataka mpaka miaka 100 ijayo tuwe tuna viongozi/wabunge ambao ni iliterrate,je ni kweli ndicho tunachokihitaji?Hivi ni mpaka lini watakoma kutudharau watanzania ambao hatuna nasaba na viongozi wa siasa au watawala hawa?

Tatizo lingine viongozi wetu wa DINI waliwapakata hawa wakapokea na pesa zao zilijaa damu na leo wanaamka wanasema wamekiuka sheria ya Katiba etc,hivi na hawa pia mbona wamesahau shuka na mpaka asubuhi ndiyo wanakumbuka kuwa hawajajifunika.Je huu ni uwoga au tumekosea wapi?
 
Mkuu Mkandara , D Cameron ni mwingereza Zaidi kuliko wewe

Anaendelea

Mkandara kama unahitaji tafsiri ya Kiswahili tafadhalitueleze kwanza kabla hujajibu,
Pili, kama umeelewa alichosema Cameron tufafanulie

Tatu, tumeweka hoja zetu katika mabandiko 6 ili kuwezakuchambuliwa na kila mmoja. Hujajibu hoja hata moj, hivi unapata wapi ushujaawa kusema tunapotosha?

Mfano, tumeuliza kuhusu unitary na federal system, tuelezewapi ilianza federation ikaja unitary
Nne, hotuba ya Cameron hiyo hapo, kama wewe ni mwingerezakuliko yeye mjibu basi tukusikie.

Ujue katika sisi kuna wale ambao hata ukimwambia jambo lenye ukweli sababu hataki kuelimika utajisumbua bure kumwelimisha.Hawa ndiyo wale wachache ninaowaongelea ,wanaofaidika na UFISADI,WIZI na RUSHWA kubwa kubwa hivyo hata siku moja hata penda kusikia kuna kitu kinaitwa masikilizano kwenye jamii.Hatuhitaji USAWA bali kila mtanzania japo kidogo afaidi matunda ya TAIFA lake.

Kuna wengine wameishi nje miaka nenda rudi na wamezeekea huko Ulaya lakini leo ukiona mchango wake kwenye hoja yenye mashiko utalia maana hata ile exposure kidogo aliyonayo angetusaidia kutupatia au kuwapatia hawa watawala wetu,lakini sababu ni mmoja kati yao hawezi kuuona ukweli wala kuuogopa.Na ndiyo maana sioni mantiki ya wanaojiita DIASPORA wakitanzania kuwa wanaweza kutusaidi kutuinua hapa tulipo bali naona ndiyo kwanza wamekuwa wachumia tumbo zaidi.
 
Absolutely right, hatuna viongozi tuna watawala.

Viongozi wanaongoza, watawala wanatumia FFU na mbinu za kilaghai ili kuendelea kutawala.

Ndio maana nasema, sisi si masikini, ni masikini wa viongozi.

Cameron ameonyesha uongozi, je viongozi wetu wameonyesha nini tofauti na uzezeta?

Kaka zangu mtakubaliana nami kwamba hawa wenzetu wakiwa wanatumia BUSARA,ELIMU yao na UZALENDO wao ili kusukuma maendeleo ya nchi zao ndiyo wakwanza kutuletea MADERAYA,na SILAHA kali za kivita ili tumalizane.Na ndiyo wakwanza kuwatetea hawa watawala.

Leo watawala wetu wanakuwa wepesi kusema wapinzani wanapata nguvu kutoka nje,au hiki kipo sababu ya MAADUI zetu kutoka nje.Ni lini itabidi tuwaambie wasiendelee tena kutudanganya kwani MAADUI hatuna nje,maadui wa MAENDELEO yetu ,maadui wa AMANI yetu na UHURU wetu,Maadui wa mshikamano wetu ni wao WATAWALA wetu wanaojiita VIONGOZI.Ni hawa wanaotoa pesa za maendeleo kwa ajili ya Mtanzania maskini zikaliwa na viongozi lakini bado wanaendelea kuzitoa.Ni hawa wanaotao pesa nyingi kwa ajili ya kufadhili misafara mirefu ya viongozi/watawala kwenda nje ya nchi kutumia,semina na sitting allowance zisizokwisha.

Wafadhili hawa nao inabidi tuwaambie ukweli hatuhitaji kuwaficha pia.
 
Kuwepo wa Tanganyika ni swala la sisi wenyewe kujitangaza kama England inavyofanya. Tuwe na wana michezo wetu, ligi yetu iitwe ligi ya Tanganyika, taifa Stars ijulikane kama ni ya Tanganyika na mengineyo mengi ambayo tunaweza kuyatenganisha kiasi kwamba wewe kesho ukiulizwa unatoka wapi sema Tanganyika. Lakini tukubali pia Wazanzibar wawe na timu zao na wanamichezo wao kuiwakilisha Zanzibar kama tunaona ni sifa kwetu.

Mbona Waingereza (England) wameweza wakati hawana serikali yao kiasi kwamba huku duniani tunaiita UK nzima ni Uingereza, Sisi tunashindwa nini hadi kudai serikali kana kwamba serikali ndio kutupa jina. Nani huko Bongo anajua kuna serikali ya Wyoming Marekani? sii mpaka wapekue ramani..na hata ukiijua nani mwenye kutaka kuijua na ili iwe nini? Jina Marekani linatosha ni jina kubwa zaidi ya nchi zake..
Kama Wazanzibar wanajiita wao Wazanzibar, am good with Mtanzania maana ndiyo yenye jina kubwa huko nje kuliko Zanzibar ama Tanganyika, am proud of it - Mtanganyika limekaa kama Mgagagigikoko! lol!

Yaani hata ww mkuu unamezeshwa maneno na watawala yakwamba Tanganyika imekufa,,,,!!!! duuh,,,,!! Unasema tunaweza hata kuanzisha ligi yetu ya tanganyika.fyn bt.sinilazima Serikali icmamie ss itasimamia.vip ikiwa wanatandaza FFU barabarani kwa lengo lakuzuia fikra mpya,,Nimejifunza jambo moja mtu acpoeleimika anakuwa chakula ya wasomi
 
Hawataki kusikia ukweli, wanaongozwa na utashi.

Leo wanaendelea kujidanganya na kuwadanganya Watanzania.

Cameron aliwaeleza watu wake ukweli, sijui lini tutapata Cameron wetu.

Tanzania si masikini, umasikini wetu ni kutokuwa na viongozi na hao waliopo hawana maarifa, ni majuha, mazezeta. Kiongozi anayehamisha magoli kila dakika heshima yake ni kama haipo.

Waingereza wajivunie akina Cmaeron

Hivi hawa watawala wetu wana siri gani au ndiyo vichwa vyao vimefungwa hata kujifunza haviwezi? Humu huwa hawapiti kuona mawazo huru ya kujenga kama haya? Ila time will tell
 
Tunachokosa Tanzania ni viongozi wakweli...Wengi ni waongo na wanapenda kupeleka mambo kwa namna ambavyo wao wanaona inafaa.
 
Nguruvi3 nakubaliana na wewe kwamba kilichotokea scotland sio kukataa mabadiliko ila ni kukataa kutengana na kwao mabadiliko ykiwepo yenye tija kwao ndani ya muungano wao ni vyema zaidi.

Nafikiri ni ugumu wa viongozi wetu kwenye kukubaliana na ushauri wa wananchi. Unajua nikionacho mimi wanasiasa wetu wanajiona wanaakili zaid ya raia na tena wanadiriki kutuonyesha kwamba wao wanajua vitu kuliko raia wa kawaida na hapo ndipo shida inapokuja.

Mathalani maneno ya rais wetu kusema kwamba yeye hawez kukubali S3 unless awe ameshatoka madarakan yanamaana gani kwetu sis kama wananchi?
na je tujiongeze kidogo alipounda tume ya Warioba akaipa mamlaka ikusanye maoni alitegemea watu wakusanye maoni yaliyotoka kwenye kichwa chake?
ama je mwenye akili atasema ile tume basi ilikuwa batili meaning haikuwa halali na kama ndivyuyo iweje hazina iidhinishe mamilion ya pesa kwenye matumiz ya tume isiyo kuwa halali? ama je nani anayelipa garama za haya?
Nachukuia sana nikiona sisi tunadharauliwa kama raia ilihali wanasiasa wetu hawana hata huo utashi tunaodhani wanao.
 
Last edited by a moderator:
KURA YA 'HAPANA' SCOTLAND NI USHINDI KWA TUME YA JAJI WARIOBA NA WANANCHI.

Kumekuwepo na upotoshaji mkubwa kutoka kwa baadhi ya makada wa ndani ya chama Chetu (CCM) juu ya nini ni maana ya matokeo ya kura ya "hapana" Scotland. Tumewasikia na kuwasoma makada hao kwenye media, lakini pia tunazidi kuwasoma kwenye mitandao ya kijamii, na kuna kila dalili Kwamba Orodha hii itazidi kuongezeka. Mbali ya kupotosha umma juu ya tafsiri ya matokeo ya kura ya Scotland, pia mbinu zinaandaliwa kupotosha umma zaidi Kwamba kura ya hapana Scotland ni Anguko au pigo takatifu la rasimu ya tume ya warioba, hasa Kwamba maoni Yale hayakutokana na wananchi. Lakini uongo huu hauna mileage ya kutosha, Vinginevyo:

1. Serikali ya CCM isingefunga tovuti ya tume kuzuia umma usione yaliyomo. Kwani Kama ni kweli Kwamba content ya utafiti na uchambuzi wa tume ungekuwa na mapungufu ambayo CCM inayasema, Jambo la busara lingekuwa ni kuachia umma uone hiyo content Ili uwe ni ushahidi wa CCM kwa wananchi juu jinsi gani maoni yake hayakuwa ya wananchi Bali ya tume. Hilo halijafanyika, na halitafanyika kwa sababu ni upotoshaji na CCM inajua Hilo.

2. Ushahidi mwingine Kwamba CCM ni waongo na tuhuma zao Kwamba maoni ya rasimu ya tume hayakuwa ya wananchi Bali ni ya kina mzee warioba ni Kwamba - Makada wa CCM wameshindwa kwenda kuisemea tume kwa wananchi au kuichapisha na kuisambaza kwa umma ili ujionee wenyewe Kwamba yaliyomo sio yake waliyoyasema Mbele ya tume. Pia Hilo, CCM haijafanya na haitafanya kwa sababu inajua Fika Kwamba chama hakisemi Ukweli.

Ni kwa mantiki hii, baadhi yetu ambao ingawa ni wanachama hai wa CCM tutaendelea Kupinga wale wote ambao wanahatarisha uhai wa muungano na taifa letu kwa ujumla kwa kuweka maslahi ya chama Mbele ya maslahi ya taifa. Mwendelezo wa kupotosha umma juu ya uhalali wa rasimu iliyowasilishwa na tume ya jaji warioba hautavumiliwa.

Baada ya kusema hayo, sasa niingie moja kwa moja kwenye mada - kujadili kwanini kura ya maoni ya Scotland ni Ushindi kwa tume ya warioba na wananchi.

Moja ya hadidu za rejea kwa tume ya mabadiliko ya katiba ilikuwa ni kulinda na kuboresha muungano, sio kuudhoofisha na kuvunja muungano. Tume ilitekeleza Hilo kwa uadilifu mkubwa, na nitoe Mifano michache:

1. Sura ya kwanza inaelekeza kuwepo kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

2. Sura ya tano inaelekeza Kwamba uraia ni wa nchi moja, nao sio mwingine Bali uraia mmoja wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Hivi karibuni, viongozi wa CCM wamekuwa wakizunguka na hoja Kwamba "kura ya Scotland ni ushahidi Kwamba muungano ni Jambo muhimu kuliko utengano". Wengine wamekuwa wakikejeli rasimu ya tume Kwamba inalenga kuvunja muungano. Lakini Kama tulivyokwisha ona, hakuna Ukweli juu ya Madai haya.

Makada wa CCM wanasema Kwamba 55% ya kura ya hapana Scotland maana yake ni Kwamba muungano ni suala muhimu. Lakini hoja ya msingi ambayo baadhi yetu tumekuwa tukiwasilisha haipingani na Hilo. Hoja Hapa sio juu ya umuhimu wa muungano, kwani tangia Shule ya msingi, sote tunajua Kwamba "umoja ni Nguvu, utengano ni udhaifu". Lakini baada ya kupevuka akili na kuondokana na utoto, tume jifunza kitu kingine muhimu zaidi, nacho ni Kwamba - pamoja na Ukweli Kwamba umoja ni Nguvu, utengano ni udhaifu, nguvu haiwezi kupatikana katika mazingira ya kutegeana na kunyonyana. Ikitokea Hali hii ya kutegeana na bado tukasema Kwamba eti umoja huo ni Nguvu, Huko ni kujidanganya.

Katika hoja zao za upotoshaji juu ya matokeo ya kura ya Scotland, makada wa CCM wanaendelea kujadili Kwamba - kura hii ni fundisho kwa Zanzibar ambayo inataka kujitenga. Makada hawa wanaenda Mbali na kusema Kwamba - kura hii ni ushahidi juu ya "ubora wa serikali Mbili", Huku Wakisema Kwamba eti hata England haina serikali yake nje ya muungano wa UK, ingawa Scotland wanayo serikali Yao Kama Zanzibar. Kwa mantiki hi, wanahitimisha Kwamba muungano wa UK ni sawa na muungano wa Tanzania, hivyo hakuna mabadiliko yanayohitajika.

Kwa manufaa ya muungano na taifa kwa ujumla, ni muhimu tukasahihisha upotoshaji huu unaofanywa na makada kadhaa wa CCM mapema Kabla ya Hali haijawa Mbaya zaidi.

Tuanze kwa kuangalia hotuba ya waziri mkuu wa UK, David Cameroon ambayo aliitoa muda mchache baada ya matokeo ya kura ya maoni kutangazwa. David Cameroon alisema hivi:

"Just at the people of Scotland will have more power over their affairs, so it follows that the people of England, wales and Northern Ireland must have a bigger say over theirs".

Tafsiri isiyo Rasmi ni Kwamba:

"Kama ambavyo Scotland itakavyokuwa na mamlaka zaidi juu ya mambo Yao, Vivyo hivyo watafuata Watu wa England, Wales na Northern Ireland kuwa na kauli juu ya mambo Yao".

Hapa tunaona Kwamba makada wa CCM hawasemi Ukweli juu ya mabadiliko yanayokuja UK kufuatia kura ya maoni Scotland. Makada wa CCM hawasemi Ukweli Kwamba kwa kauli hii, sasa serikali ya England itajitenga au itajivua koti la muungano. Swali linalofuata ni je:

•Kauli hii ya David Cameroon inapishana vipi na kazi ya tume ya mabadiliko ya katiba pamoja na matamshi mbalimbali ya mzee wetu jaji warioba ambae alifanya kazi yake kwa uadilifu na uzalendo mkubwa?

Kama alivyofanya Jaji warioba, David Cameroon ametambua Kwamba haiwezekani kuwepo kwa muungano imara iwapo muungano huo Unatoa Nguvu au mamlaka zaidi kwa mshirika mmoja wa muungano. Kuendekeza Hali hiyo ni kujenga chuki, uhasama baina ya pande Mbili za muungano, na hatimaye kuvunja muungano.

Katika hotuba yake, pia David Cameroon Alitamka Kwamba:

"I have long believed that a crucial part missing from this national discussion is England. We have heard the voice of Scotland and now the millions of voices of England must not be ignored".

Tafsiri isiyo Rasmi ni Kwamba:

"Kwa muda mrefu, nimekuwa nikiamini Kwamba suala muhimu linalokosekana Katika mjadala wa kitaifa, ni suala la England". Tumesokia sauti za wa-Scotland na sasa sauti za mamiloni na waingereza haziwezi kupuuzwa"

Katika Hilo pia, jaji warioba na tume yake waliweka bayana Kwamba kuna manung'uniko mengi ya wananchi juu ya Mfumo wa muungano wa serikali Mbili. Jaji warioba Alisema Kwamba kwa upande wa Zanzibar, yapo malalamiko makuu matatu, na kwa upande wa Tanzania bara, yapo malalamiko makuu manne. Jaji warioba akaonya Kwamba iwapo watawala watayazibia masikio malalamiko haya, matokeo yake itakuwa ni kuzidi kuudhoofika kwa muungano. Muhimu Hapa pia ni Kwamba, Kama alivyofanya David Cameroon kutaja jina la England na umuhimu wake kujivua koti la muungano, jaji warioba pia nae alijadili haja ya kuizindua Tanganyika pamoja na umuhimu wake wa kujivua koti la muungano. Kwa maana nyingine, kwa manufaa ya muungano, Kama ilivyokuwa muhimu kwa sauti za mamiloni wa Uingereza Kuanza kusikilizwa, Vivyo hivyo ni kwa sauti za mamilioni ya watanganyika.

Tunachojifunza kutoka kwa David Cameroon na Jaji Warioba ni Kwamba wadau wakubwa Katika suala la Mfumo wa Utawala ni wananchi, sio viongozi au Wanasiasa.

Katika hotuba yake ya kukabidhi rasimu ya pili pale viwanja vya karimjee, jaji warioba alisema Kwamba - "kuendelea kwa serikali Mbili kulihitaji ukarabati mkubwa ambao haiwezekani kufanyika."

Kauli hii ya jaji warioba haipishani na waziri mkuu wa zamani wa UK, Gordon Brown aliyoitoa mwezi Juni mwaka huu wa 2014. Gordon brown alisema Kwamba:

"Westminster's claim to undivided authority over the county? dead and buried".

Tafsiri isiyo Rasmi ni Kwamba:

"Madai ya Westminster juu ya mamlaka ya nchi yasiyogawanyika? Madai hayo yamekufa na kuzikwa".

Hapa tufahamu Kwamba Gordon Brown na David Cameroon ni viongozi wa vyama viwili Vikubwa vyenye upinzani mkubwa sana nchini UK, lakini Katika suala muhimu Kama Mfumo bora wa muungano wenye maslahi kwa taifa na muungano wenyewe, wameona Kwamba kuna haja ya kuweka pembeni itikadi za vyama, hasa iwapo suala husika wadau wake wakubwa ni wananchi. Gordon Brown amewahi kunukuliwa akisema Kwamba yeye sio Mpenzi wa Dhana ya shirikisho la Britain, lakini Mfumo huo sasa ni "necessary & inevitable". Huu Ndio uongozi! Kwanini Tanzania Tunakosa viongozi wa aina hii? Moja ya sofa kubwa ya uongozi ni uwezo wa kuingoza mabadiliko. Sisi viongozi wetu wanaogopa kuongoza mabadiliko. Je tutafika? Kwa Tanzania, kitendo cha ukawa kuwa nyuma ya maoni ya wananchi kwa mtindo ule ule wa UK, baadhi ya makada wa CCM wanafanya mzaha Katika suala nyeti Kama hili na kuendelea kuchakachua rasimu ya wananchi Kule Dodoma.

Kuna haja ya kuacha kupotosha wananchi juu ya nini maana ya kura ya maoni Scotland. No vote in Scotland haikumaanisha No Change. Kwa maana nyingine Rahisi - the ni vote has preserved the union, but has not preserved the status quo. Nitafafanua:

Katika kampeni za Gordon Brown juu ya "no vote" to Scotland's independence, tulisikia kampeni hizi zikiambatana na ahadi nyingi juu ya mabadiliko makubwa ya Mfumo wa Utawala wa nchi iwapo Scotland watakataa kujitenga na Uingereza. Brown alienda Mbali zaidi na kusema Kwamba - England, Wales, na Northern Ireland pia zitapewa mamlaka zao Kama Scotland. Haya hayasemwi na makada wa CCM wanaotumia matokeo ya kura Scotland kuhalalisha "No Change in Status Quo" in Tanzania. Kwa kufanya hivyo, pengine hawajui Kwamba ni kuingiza muungano wetu kwenye Giza nene.

Tukiendelea kujenga hoja kwanini kura ya hapana Scotland ni Ushindi kwa tume ya warioba na wananchi, Ahadi Za akina Gordon Brown zilizolenga kulinda muungano wa UK zinafanana sana na kazi iliyofanywa na tume ya warioba. Kwa mfano, kina Gordon Brown waliahidi Kuanza mchakato wa kuleta shirikisho la UK. Walienda Mbali na kusema Kwamba watafanya mabadiliko makubwa Kama vile kuzuia wabunge wa Scotland kutoshiriki kwenye bunge la westminster - kwenye mijadala na maamuzi juu ya mambo ya England kwa vile hayawahusu. Msimamo huu ulitokana pia na chama cha Conservatives chini ya David Cameroon ambacho kilidai madaraka Kama hayo kwa England (yani England nao kuingia kwenye bunge la Scotland). Kwetu Tanzania, ilitakiwa CCM iwe na msimamo sawa na ukawa Kama ilivyopendekeza tume, kwa maslahi ya muungano na taifa kwa ujumla.

Hoja za tume ya jaji warioba na kina Gordon Brown Wakati wa kampeni za "no vote to Scotland's independence zinafanana sana kuhusiana na washirika wa muungano kuwa na serikali zao, mabunge Yao, kuwa na mamlaka nje ya muungano. Kwa maana nyingine, Pendekezo la viongozi wa UK linafanana na lile la tume ya warioba juu ya shirikisho la serikali Tatu ambapo Tanganyika na Zanzibar zitakuwa na serikali zake na mabunge yake juu ya masuala Yao ambayo hayataingiliana na masuala ya muungano Kama ilivyo sasa chini ya serikali Mbili.Hata ziboreshwe kwa miaka Mia moja, bila ya serikali Tatu, muungano utazidi kudhoofika.

Kuna umuhimu wa makada husika wa CCM kuacha kupotosha umma, na hii itakuwa kwa faida ya chama kwani wananchi wa Leo ni waelewa, sio wale wa miaka 50 iliyopita. Dhana ya kwenda kwa Wakati ndani ya chama ni lazima iendane na Dhati ya kuzingatia mahitaji ya Wakati uliopo, kwa mfano shirikisho la serikali Tatu.

Wanapojadili matokeo ya kura ya maoni Scotland, makada husika wa CCM wana haja pia ya kujadili kwanini matokeo ya Scotland yamekuwa hivyo, na hii pia ni faida kwa chama, hasa kuanzisha utamaduni wa kusimamia masuala ya kitaifa Kama wenzetu UK Katika masuala nyeti Kama haya ya Mfumo wa Muungano badala ya kuweka maslahi ya chama Mbele, huku muungano na taifa kwa ujumla vikiwekwa Katika hatari ya kusambaratika.

Kujadili Ushindi wa UK kwenye kura ya maoni Scotland bila ya kichambua na kujadili sababu za Ushindi wa kura hiyo haiwezi kukisaidia hata chama (CCM) Katika mikakati yake ya Ushindi na kutumikia wananchi. Kwa mfano, kujadili Ushindi bila uchambuzi wa sababu za Ushindi Ni sawa na chama kujadili Ushindi wake kwa mfano kwenye jimbo la uchaguzi au kata ya udiwani bila ya kujali kuchambua au kutathmini sababu juu ya kwanini chama kimeshinda kiti husika. Vile vile ni sawa na chama kuanguka kiti cha ubunge au udiwani na kuacha kujadili sababu za kuanguka Huko kwa manufaa ya kujipanga Mbeleni. Sidhani Kama CCM imepungukiwa hivyo kifikra, kwahiyo nadhani nitakuwa sahihi kusema Kwamba CCM Inaacha kujadili sababu za matokeo ya hapana Kule Scotland, kwa makusudi Kabisa, na kwa sababu hazina maslahi kwa muungano na taifa Bali CCM peke yake.

Tanzania nchi ya Watu wote bila ya kujalisha itikadi zao za vyama. Kati ya watanzania milioni 45, wanachama wa CCM hawazidi milioni tano, ambayo ni sawa na asilimia isiyozidi kumi na moja (11%) ya watanzania wote. Ni sababu hizi Ndio zinafanya baadhi yetu Kama wanachama wa CCM kuwa waangalifu Katika kuweka misimamo baina ya Ile yenye maslahi ya chama na Ile yenye maslahi ya muungano na taifa kwa ujumla. Tunaamini Kwamba hivyo Ndio tutaweza kuendelea kuwepo Katika siasa za nchi yetu hata Kama itatokea tukapoteza uchaguzi ngazi ya urais. Vinginevyo kuweka maslahi ya chama kwa kukandamiza maslahi ya taifa hakutatuwezesha kuongoza kwa ridhaa ya wananchi (the 90% ya watanzania ambao sio wana CCM), badala yake tutakuwa tukiongoza kwa hila na vitisho, masuala ambayo hata baba wa taifa aliyakemea Katika vitabu vyake vya "tanu na Raia" na "tujisahihishe" (1962).

Kuna haja ya makada wa CCM Kujifunza kutoka kwa vyama vya siasa UK, hasa kwa kuangalia mfano jinsi gani UK inaelekea kwenye Mfumo wa shirikisho kwa manufaa ya wananchi wa UK Kama tulivyojadili. Ni muhimu ieleweke Kwamba
matokeo ya kura ya hapana Scotland ni ahadi waliyopewa na vyama vyote Vikuu vya Uingereza juu ya mamlaka zaidi, mabadiliko makubwa ya kikatiba Kukidhi haja ya devolution kwa washirika wote wa muungano, na muhimu zaidi, safari ya kwenda kwenye "federation of the United Kingdom" na vision ya shirikisho (federalism). Kama wapo wasiokubali juu ya haya, basi watafute Nyaraka inayoitwa "a pledge for Scottish Voters". Nyaraka hii ilitiwa Saini na viongozi wote wakuu wa vyama vya siasa England: Cameroon (Conservatives), Ed Millband (Labour), na Nick Clegg (Liberal democrats), bila ya kujadili itikadi Zao za vyama. Nyaraka hii ilikuwa ni ahadi kwa wananchi wa Scotland Kabla ya kura ya maoni Kwamba wakipiga kura ya hapana na kubakia kwenye muungano, watapewa more executive powers juu ya Utawala wao wa ndani. Pia waliahidiwa Kwamba watakuwa na kauli ya mwisho (mamlaka) ya kuamua juu ya masuala mbalimbali yanayohusiana na maendeleo ya jamii - elimu, afya, Ajira n.k, Katika jurisdiction Yao.

Mbali ya Hilo, Scotland pia walipewa ahadi ya kuwa na mamlaka (baadhi ya ahadi zikiwa tayari zinatekelezwa kwenye baadhi ya kodi) mamlaka ya kuamua masuala Mbali Mbali yanayohusiana na kodi na matumizi Yao - kibajeti (fiscal autonomy). Kwa mfano, suala la income tax, capital gains tax, VAT etc. Muda sio mrefu, Mfumo wa kibajeti UK utabadilika kufuatia kura ya hapana Scotland kwani hata northern Ireland and Wales (washirika Wengine wa muungano wa UK), nao wanaelekea kwenye fiscal autonomy.

Ni hitimishe kwa kusisitiza Kwamba:
"no vote" haina maana "no change" in Scotland. Kwa maana nyingine, the vote has preserved the "union", but has not preserved the "status quo".

Kwa tathmini ya tume ya jaji warioba, baada ya kuwasikiliza wananchi, tume iliona Kwamba ni dhahiri Pendekezo la kuifanya Zanzibar isionekane Kama kwa kuificha Tanganyika lisingekubika kwenye kura ya maoni. Kama ilivyo kwa tume ya warioba, viongozi wa UK waliona Hilo kwa Scotland zaidi ya miaka kumi iliyopita, na kuamua kuachana na siasa za vyama na bada yake kuweka maslahi ya taifa Mbele ili kulinda muungano. Hivyo ndivyo historia itamwandika mzee warioba. Lakini legacy yake itatokana na kuzinduliwa kwa Tanganyika, suala ambalo tofauti na miaka 50 iliyopita ambapo lilikuwa haliwezekani, Leo mtazamo umegeuka kuwa, kuzinduka kwa Tanganyika ni suala la muda tu, kwani, contrary to popular belief ndani ya CCM, rasimu ya tatu ya katiba ambayo ni Kinyume na Sheria ya mabadiliko ya katiba 2011, rasimu hii Ndio itakuwa kichocheo cha uzinduzi wa Tanganyika.


Tanzania kwanza, Tanganyika Kabla.


Sent from my iPhone using JamiiForums

Cc MwanaDiwani, chama, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, ZeMarcopolo
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara , D Cameron ni mwingereza Zaidi kuliko wewe

Anaendelea
Mkandara kama unahitaji tafsiri ya Kiswahili tafadhalitueleze kwanza kabla hujajibu,
Pili, kama umeelewa alichosema Cameron tufafanulie
.
Tatu, tumeweka hoja zetu katika mabandiko 6 ili kuwezakuchambuliwa na kila mmoja. Hujajibu hoja hata moj, hivi unapata wapi ushujaawa kusema tunapotosha?

Mfano, tumeuliza kuhusu unitary na federal system, tuelezewapi ilianza federation ikaja unitary
Nne, hotuba ya Cameron hiyo hapo, kama wewe ni mwingerezakuliko yeye mjibu basi tukusikie.
Mkuu wangu kama umenisoma hapo juu huna sababu ya kusema maneno mengi ambayo unarudia lugha ile ile. Tulichokitaka sisi tanzania ni kuondoa mamlaka makubwa ya serikali ya CCM (serikali kuu) kuwapa wananchi wenyewe na muda wote hapa nimekuwa mpiga debe wa kuondosha mamlaka hayo toka CCM na sio swala la Zanzibar wamepewa nini kwa sababu sisi tayari tax zetu zinakusanywa na TRA kwa ajili ya Tanganyika (Tanzania Bara) na ZRB kwa ajili ya Zanzibar na kilichoelezwa na tume ya katiba ni kwamba hata yale mambo ya muungano ni mambo ya Tanganyika.

Matumizi ya Bara yanatokana na kodi hayatokani na vitu vingine zaidi ya hapo bara tumeteka mali zote za mashirika ya Umma zilizoanzishwa chini ya serikali ya Muungano hapakuwa na mgawanyo. CCM wameteka mali zote zilizokuwa chini ya serikali ya TANU ambayo iliwahusu wananchi wote chini ya Ujamaa na hayakufanyika marekebisho kuelekea vyama vingi. Dovolution gani zaidi unayoitaka wewe ikiwa bado yapo mambo mengi chini ya utawala wa CCM ambayo Zanzibar hawana mamlaka nayo. CUF wameliona hili na wanajenga hoja zao kuyaondoa mikononi mwa CCM na kuyapeleka kwa wananchi wake, mijinga kina sisi tunajivuruga tu wenyewe. Tumeona swala la OIC na hata michezo Zanzibar hairuhusiwi kuunda timu zake kushiriki kimataifa tofauti na Scotland.

Swala hapa ni sisi wananchi kuyadai mamlaka zaidi kwa mikoa yetu, kama ni swala la Ulinzi, Katiba iainishe wazi ni vitengo gani viko chini ya serikali kuu - Kwa mfano JMTZ na FFU lakni Polisi wabakie kwa nchi zake na hata mikoa yake. Polisi wa Mkoa wa Mwanza awe chini ya mkuu wa mkoa RC ambaye atachaguliwa na wananchi (anaweza kuwa mgombea binafsi) hivyo kuondoa nguvu ya CCM kuamrisha Polisi kuvamia maandamano ama mikutano. kama tunaondoa nafasi ya RC basi Polisi iwe kitengo kinachojitegemea kwa kushirikiana na Meya. Meya na halmshauri za miji hawana mamlaka ya kutosha vile vile ukilinganisha na nchi nyinginezo.

Haya maswala ya kusema Zanzibar hivi ama vile ni uroho wa fisi kula nyama mbichi, wakati bado kabisa devolution haijafanyika vya kutosha ili demokrasia ifanye kazi inavyotakiwa ni kujidanganya wenyewe kwa sababu Leo hii Chadema wakishinda uchaguzi Mkoa wowote, jimbo lolote bado hawana nguvu ya kiutawala kwa jimbo hilo hata kama wana madiwani karibu wote, meya akiwa wa CCM tayari nguvu hawana na watapigwa na polisi kama wezi hata mgombea Urais ama mwenyekiti wa chama ni mtu mdogo sana haheshimiwi nje ya chama chake.

Tuitazame picha hii kwa mapana zaidi ya kuitazama Zanzibar wala wenzetu huko UK hawakujenga Chuki bali wametazama interest zao kwanza mbele ya kujitenga na ndio maana maamuzi yamekuwa tofauti. Sisi na chuki hizi itatulazimu tufanye maamuzi ya kichuki ambayo mwisho wa siku hakuna aloshinda bali tumevunja udugu wa asili kwa ujinga wa siasa za majitaka. yapo mambo muhimu ya kupigania sio Uzanzibar na Utanganyika hii ni tabia chafu ya Kibaguzi ambayo ina asili kubwa na mtu mweusi kutojiamini.

Isome rasimu vizuri kisha jenga hoja yako kwa kuyadai mamlaka ambayo bara ingetakiwa kuwa nayo badala ya kudai kuendesha serikali mbili, mabunge mawili na mahakama mbili ambayo ni mzigo mkubwa kwa wananchi walipa kodi. Kwa kila mnachokidai ni lazima muwaambie wananchi kwamba ni kodi zao ndizo zitakazo gharamia matumizi ya mihimili mnayoitaka.
 
HITIMISHO

....Tunajiuliza, Waafrika tuna laana gani?

Miaka 50 ya kujitawala hatuwezi kujivunia viongozi wetu wenyewe.

Ile thamani ya Tanzania iliyojijengea sasa imeyeyuka.

Hatuna watu wa kutuweka pamoja kama taifa. Tunakwenda kama nguruwe mwituni.

Hili la kuua Tanganyika yenye urithi wake na kupendelea Zanzibar si suluhisho.

Na wala picha ya Karume katika coin ya sh 500 haitamaliza tatizo, ni suluhu za wapumbavu na wehu tu.

Uhuni unaoendelea Dodoma ni hatari kwa taifa.


Ahsanteni


Mkuu Nguruvi3 Umemaliza kila kitu kwa maneno hayo machache. Siku hizi tuna viongozi wako Ikulu wanamsaidia Rais wanaotoa majibu ya kijinga yasiyo na busara utafikiri majuha. Wengi wao wanasema watagombea urais, akiulizwa kwanini unataka kuwa Rais, anajibu "kwani ni dhambi, nimepata simu tano za wananchi wangu wananiomba nigombee-shi.t!" Badala ya kutuelezea vision yake nini anataka kufanya akiwa Rais ili Taifa lipige hatua, yeye anataka kwenda kukaa Ikulu kwa sababu rafiki zake wamemtaka afanye hivyo!

Mpaka sasa wote wanaotaka urais sijaona hata mmoja akielezea nini atatufanyia watanzania akiwa Rais. Huu mtindo wa kusema wa majibu mepesi mepesi ya kihuni waandishi wa habari lazima mjifunze jinsi ya kuuliza maswali ya kuwabana watu hawa.

...Sijui waafrika tumelogwa na nani!
 
Mchambuzi na Nguruvi3 nazidi kuwapa like nyingi kwa mabandiko yaliyojaa hekima na maarifa ya kutosha.

Binafsi nasema hivi jamani kama kusema tumesema sana na bado tunazidi kusema lakin yatupasa sasa tuanze kufanya mabadiliko kwenye fikara zetu.

Kuna jambo baya sana naliona kwa vijana wa taifa hili weni wetu tumekuwa wapenda pesa, tumepoteza uadilifu tumepoteza kaliba ya kuwa na uthubutu kusema haya hadharani ili yaeleweke. Imagine kila siku CCM inakaa kusema kwamba tume ya warioba sio halali ama sijui hawakwenda kukusanya maoni ya wananchi bali wamekusanya ya kwao. sasa hebu sisi kama raia tuamue tuseme iyo rasimu kama ilivyo irudishwe kwetu alafu tuipigie kura baada ya kuisoma tuone je imewakilisha mawazo yetu ama laa.

nakumbuka jinsi tulivyokuwa tunashinda kwenye madarasa na lekcha rums kuijadili pengine tulinyeshewa mvua na jua kutuwakia ili tutoe maoni alafu leo tunaambiwa eti sio maon yetu??

ivi kwanza naomba Mh. Warioba aseme kwa kauli yake tena kweli ile rasimu iliyobeba maoni ndiyo aliyoipelek ama alipeleka ingine? kama ndiyo ile basi serikali ituambie kwann hawataki kusikia sauti zetu bali wanataka tusikie sauti zao.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 Umemaliza kila kitu kwa maneno hayo machache. Siku hizi tuna viongozi wako Ikulu wanamsaidia Rais wanaotoa majibu ya kijinga yasiyo na busara utafikiri majuha. Wengi wao wanasema watagombea urais, akiulizwa kwanini unataka kuwa Rais, anajibu "kwani ni dhambi, nimepata simu tano za wananchi wangu wananiomba nigombee-shi.t!" Badala ya kutuelezea vision yake nini anataka kufanya akiwa Rais ili Taifa lipige hatua, yeye anataka kwenda kukaa Ikulu kwa sababu rafiki zake wamemtaka afanye hivyo!

Mpaka sasa wote wanaotaka urais sijaona hata mmoja akielezea nini atatufanyia watanzania akiwa Rais. Huu mtindo wa kusema wa majibu mepesi mepesi ya kihuni waandishi wa habari lazima mjifunze jinsi ya kuuliza maswali ya kuwabana watu hawa.

...Sijui waafrika tumelogwa na nani!
Hili ni tatizo kubwa sana ambalo waandishi wa habari ni sehemu yake.
1. Tunapata watu wenye nia za kugombea hata wasio na sifa kwasababu ile hadhi ya Ikulu imeondoka.
2. Huu utamaduni wa kutumwa na watu''nimeambiwa na viongozi wa dini, wapiga kura n.k.'' ni njia ya wendawazimu kuwadanganya wananchi.

Tunasikia mtu anadai achaguliwe ili alete maendeleo. Hivi maendeleo ni makontena ya mitumba au ubuyu yanayopaswa kusafirishwa kutoka bandarini hadi kwa wananchi!!

Wenzetu wanachagua viongozi ili wawatumikie. Cameron ameanza kufanyia kazi madai ya pande zote, hasubiri hadi aondoke mwakani. Hawa ndio viongozi, siyo viongozi wetu wanaoongozwa na hisia, kila siku wanabadilika hata kinyonga ana afadhali.
 
Back
Top Bottom