Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,314
- 33,808
- Thread starter
- #61
Rasimu ya Warioba imetupwa. Iliyopo ni ya CCM na Samwel Sitta.Mchambuzi na Nguruvi3 nazidi kuwapa like nyingi kwa mabandiko yaliyojaa hekima na maarifa ya kutosha.
Binafsi nasema hivi jamani kama kusema tumesema sana na bado tunazidi kusema lakin yatupasa sasa tuanze kufanya mabadiliko kwenye fikara zetu.
Kuna jambo baya sana naliona kwa vijana wa taifa hili weni wetu tumekuwa wapenda pesa, tumepoteza uadilifu tumepoteza kaliba ya kuwa na uthubutu kusema haya hadharani ili yaeleweke. Imagine kila siku CCM inakaa kusema kwamba tume ya warioba sio halali ama sijui hawakwenda kukusanya maoni ya wananchi bali wamekusanya ya kwao. sasa hebu sisi kama raia tuamue tuseme iyo rasimu kama ilivyo irudishwe kwetu alafu tuipigie kura baada ya kuisoma tuone je imewakilisha mawazo yetu ama laa.
nakumbuka jinsi tulivyokuwa tunashinda kwenye madarasa na lekcha rums kuijadili pengine tulinyeshewa mvua na jua kutuwakia ili tutoe maoni alafu leo tunaambiwa eti sio maon yetu??
ivi kwanza naomba Mh. Warioba aseme kwa kauli yake tena kweli ile rasimu iliyobeba maoni ndiyo aliyoipelek ama alipeleka ingine? kama ndiyo ile basi serikali ituambie kwann hawataki kusikia sauti zetu bali wanataka tusikie sauti zao.
Wakati bunge linaanza Sitta alisema kuna mambo mengi mazuri ya kushughulikia kama kuwapa wazanzibar nafasi zaidi katika muungano, kuwapa wafugaji na wakulima fursa zaidi ndani ya katiba.
Ukisoma rasimu ya Chenge, kila jambo alilosema Sitta ndilo limefanyika. Kuwapa wazanzibar pipi na peremende.
Wakati huo huo kuhakikisha Tanganyika inafutika.
Njia ya kuhalalisha katiba ya CCM ya mafichoni ni Sitta kukusanya maoni kwa wakulima 17 na wafugaji 23 halafu kutengeneza katiba waliyosoma jana.
Hawa watu wanatufanya majuha kama ulivyosema. Hata hivyo huu ndio mwanzo wa mwisho.
D.Cameron kasema anashughulikia matatizo ya Wales, northern Irelanda.
Cameron akasema, England imeachwa katika mjadala wa kitaifa na ni wakati nao wasipuuzwe kama wanavyopuuzwa Watanganyika.
Kwa kadri CCM inavyowafanya wananchi majuha, muungano unakaribia sana kuvunjika.
Kwasasa hoja si Zanzibar, ni kurejea kwa Tanganyika katika hadhi yenye mamlaka, utamaduni na value zake kama ambavyo Cameron ameonyesha njia kwa Wales, England na N.Ireland.
Kinyume cha uwepo wa Tanganyika ni kuvunjika muungano.Hilo si mjadala tena ni suala la wakati.