Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Asante Nguruvi3

ilimu mujarabu hii, wanaopotosha acha waendelee kupotosha, siku ukweli ukijidhihirisha watatafuta pa kujisitiri
 
Mkuu Nguruvi3,hakika umenena, uzi huu ni shule tosha haswaaa kuhusu muungano wetu,
Back Tanganyika##
 
Last edited by a moderator:
mkuu nguruvi3 umefanya uchambuz wa kimataifa hakika mwil unasisimka kwa unayoelez na yanyotokea,asante sana nimeelika zaid ya vile nilivyofokiri ubarikiwe sana.
 
Asante Nguruvi3

ilimu mujarabu hii, wanaopotosha acha waendelee kupotosha, siku ukweli ukijidhihirisha watatafuta pa kujisitiri
Uingereza walijaribu kuficha ficha, ukweli ulipoanza kutimia, wao wameamua kukimbia mbele ili kuzuia madhara zaidi.

Kwasasa England, Wales na Scotland zinajipanga.
Kuna mawili, ima ziendelee kivyao na kuwatenga Scotland au kudai haki kama Scotland

Hapa nyumbani watu wanaficha ukweli kana kwamba hakuna tatizo.

Sasa hivi hoja si Zanzibar, bali ni Tanganyika.

Ukisoma rasimu ya Sitta na CCM, wamejaribu sana kuwapendeza wazanzibar kwa gharama za Watanganyika.

Watanganyika ndio wenye muungano, hakika ukweli hauna muda mrefu utatimia.

Ya Scotland yalitosha kabisa kuwa somo. Wendawazimu wakafunga macho na masikio.

Ni suala la muda tu
 
Nakubaliana na nguruvi kasoro uhalali wa tume ya warioba...labda tungeanza na kura ya maoni...
The Boss , wewe ni 'veteran' hapa jamvini. Nadhani unakumbuka si mara moja au mbili, tumewaeleza serikali na CCM kuhusu kura ya maoni. Nakumbuka niliandika gazetini na kusema katiba itavurugwa na suala la muungano.

Tulipaswa kwanza ku settle suala la muungano kama walivyofanya Uingereza. Baada ya hapo ndipo tuamue tunakwenda mbele kwa muundo gani. Hilo lilikuwa litokee kwa wazanzibar kama Scotland.
Hakuna kiongozi aliyefikiria wala kusikiliza, wakaamua kuteka mchakato ili wafanye uhuni waliozoea.

Hawakuelewa kuwa zama zinabadilika na kila zama na kitabu chake.
Wakaunda tume ya Warioba wakijua wataweza kuchakachua kwa kutumia tume.

Tume ilijaa wazee wa busara ambao yale waliyonena ndiyo David Cameron kayasema.
Kama utakumbuka Warioba alisema, njia muafaka ni kusikiliza matatizo ya pande zote.

Prof Palamagamba akafafanua walichokiona katika kukusanya maoni yao.
Akasema, Watanganyika wana yao moyoni siku wakiyatoa itakuwa tabu.

Leo Sitta na CCM wameamua kuunda tume yao ya Sitta kukutana na watu 23 na kusema ni maoni.
Wametoa katiba yao ya mafichoni tuliyoieleza siku nyingi ili watubambikizie.

Pengine watafaulu kwa muda mfupi, kitakachotokea baada ya hapo ni kile Cmaeron alichokisema.
Kwamba, washirika wengine England, Wales na Ireland lazima wasikilizwe na Watendewe haki kama Scotland

Leo Watanganyika wamedharauliwa. Hatari kubwa ni kuwa hawa Watanganyika ndio waliobeba muungano.
Ipo siku na si muda mrefu yatawakifu mioyoni, watayatoa kama Palamagamba alivyosema.

Kitakachofuata si kujadili muungano tena, bali kugawana mbao baada ya jahazi kuvunjwa.

Tunaweza kusema, kama CCM walidhamiria kuvunja muungano kwa kumtumia Samwel Sitta, hakika wamefanikiwa.
Muungano utavunjika kama glass iliyojaa maziwa na kubwagwa chini.

David Cameron ameliona hilo mapema, amechukua hatua za kuzuia uharibifu ulioanza kujitookeza.

Sisi viongozi wetu wanasubiri waondoke mwakani, ili nchi ikiingia katika machafuko wao wanaelekea hazina kuchukua pesa za kutibiwa nje na familia zao. Huko nje watakuwa wanaangalia BBC huku wakitoa matamko ya pande husika kukaa pamoja.

Tanzania si masikini, bali tuna umasikini wa viongozi wasioweza kuona, kutambua na kufikiri. Sote tutalipa gharama za uzmebe huu kama hatatuchakua hatua za lazima, halali na makusudi.
 
Kuna mmoja hapa anajaribu ku-spin kilichotokea: Union hatters learn from Scottish vote

Ila ukisoma speech ya Cameron, alisema kuwa suala siyo tuu Scotland, Wales na Northern Ireland tuu, bali pia interests za England ndani ya UK.

England ikiwa na maana ya interests za Tanganyika ndani ya Muungano. Wale wanaolazimishia Muungano ndiyo wanatakiwa wajifunze kutoka Scotland.

Kama wana gusts badala ya kutumia polisi kuzima opinions za raia wafanye kama iliyofanyika Scotland kwa kuwapa raia haki ya kupiga kura ya NDIYO au HAPANA juu ya Muungano.
 
Tatizo letu kubwa ni kutopata elimu yenye uhakika kuhusu masuala ya elimu ya siasa na hasa sheria za mwananchi husika.Na pili rushwa,umaskini unaotumika sana na watawala wetu,na tukumbuke kuwa hatuna viongozi bali tunawatawala.Viongozi walishakufa wote.Hakuna UZALENDO tukauona bali kuna uzalendo wa maneno matamu ambayo sababu ya elimu duni za watu wetu tunakosa kwenda mbele bali kurudi nyuma.Na mbaya zaidi watakuja kushtuka pale balaa la vurugu na mauaji ya wenyewe kwa wenyewe yakianza na sababu ya wao wanapesa watatukimbia wao na familia zao na sisi tukabaki kwenye vurugu letu.Kama tuonavyo leo SUDAN kusini kinachotokea.Watawala wamekosa uvumilivu kisiasa,utashi,busara na weledi.Wote wapo kwa kujinufaisisha zaidi wao na familia zao.wametuacha watanzania tukiendelea kuw amaskini wakutupwa.Na nina uhakika wanajua kuwa likitokea la kutokea wao na familia zao watakimbia na kukaa ughaibuni.

Watu kama Nguruvi na Mchambuzi mngeweza kutusaidia kama mnaweza kupata vipindi kwenye TV ili tuweze kujifunaza zaidi,maana mara nyingi hoja zenu zina mshiko kuliko kawaida.

Asanteni sana.

Tetty naungana na wewe sema pia kwa uwezo hawa jamaa walionao siku wakijiexpose bado maisha yao yatakuwa hatarini..

Tusisahau sisi hatuna viongozi ila tuna watawala.
Mtawala anaua na kuharibu yoyote asiyefuata matakwa yake! poor Tanzania.
 
Last edited by a moderator:
Nimeipenda! Ungeiandikia kajitabu tena kwa lugha hii hii ya Kiswahili ili wakati wa kupiga kura za maoni watu waweze kujielimisha badala ya kusubiri kudanganywa na hawa wadanganyifu wa siku zote.
 
Tetty naungana na wewe sema pia kwa uwezo hawa jamaa walionao siku wakijiexpose bado maisha yao yatakuwa hatarini..

Tusisahau sisi hatuna viongozi ila tuna watawala.
Mtawala anaua na kuharibu yoyote asiyefuata matakwa yake! poor Tanzania.
Absolutely right, hatuna viongozi tuna watawala.

Viongozi wanaongoza, watawala wanatumia FFU na mbinu za kilaghai ili kuendelea kutawala.

Ndio maana nasema, sisi si masikini, ni masikini wa viongozi.

Cameron ameonyesha uongozi, je viongozi wetu wameonyesha nini tofauti na uzezeta?
 
Kuna mmoja hapa anajaribu ku-spin kilichotokea: Union hatters learn from Scottish vote

Ila ukisoma speech ya Cameron, alisema kuwa suala siyo tuu Scotland, Wales na Northern Ireland tuu, bali pia interests za England ndani ya UK.

England ikiwa na maana ya interests za Tanganyika ndani ya Muungano. Wale wanaolazimishia Muungano ndiyo wanatakiwa wajifunze kutoka Scotland.

Kama wana gusts badala ya kutumia polisi kuzima opinions za raia wafanye kama iliyofanyika Scotland kwa kuwapa raia haki ya kupiga kura ya NDIYO au HAPANA juu ya Muungano.
Mkuu , leo hii tungekuwa tunasema Cameron ameiga kutoka Tanzania. Mbona mambo yote tuliyaweka hapa jamvini tena bila kununua?

Viongozi wetu wanaongozwa na fikra za zama za FFU.

Leo masilahi ya Tanganyika hayasemwi, hata jina wanalazimisha lifutike.
England. Wales, Scotland, Northen Ireland hakuna hata nchi moja iliyopoteza utaifa, utamaduni au value zake na bado ni taifa moja.


Hao CCM wanadanganya wananchi kuwa Scotland ni mfano wa kuigwa kwa kukataa kujitenga.
Mazingira yetu na Scotland yana tofauti katika kauli ya kujitenga. Nadhani Tanganyika na Zanzibar wanakubaliana katika muungano.

Kinyume chake tungewahi kuwa na hoja ya wznz kujitenga. Wao hawapo hivyo wanachosema ni kutoa mamlaka zaidi.

Sasa unapotoa mamlaka kwa znz kama Scotland, huwezi hata siku moja ku ignore Tanganyika kama ambavyo Cameron amezungumzia England, Wales na Ireland. Tena akaweka msisitizo lazima mageuzi ya Scotland yaende samba na washirika.

Alichojaribu kuepusha ni England kusubiri na kuchukua hatua zake.
Na hilo ndilo CCM wanalitaka, kwamba Tanganyika wachoke wachukue hatua.

Ndio maana nasema, kama CCM wamedhamiria kuua muungano basi njia wanayotumia ni muafaka sana.
Swali, ni je wanatambua kuwa wanalipeleka taifa machakani?
 
Absolutely right, hatuna viongozi tuna watawala.

Viongozi wanaongoza, watawala wanatumia FFU na mbinu za kilaghai ili kuendelea kutawala.

Ndio maana nasema, sisi si masikini, ni masikini wa viongozi.

Cameron ameonyesha uongozi, je viongozi wetu wameonyesha nini tofauti na uzezeta?

Tena ni uzezeta uliokomaa, Mkuu watu kama nyie mnahitajika sana katika jamii hii iliyojaa watu wenye elimu duni na fikra finyu..

Nikisoma maandiko yako kwa makini zaidi, naelewa kabisa na ninapata picha ni dhahiri bado tungali chini ya mkoloni hatuna uhuru, haswa kwenye kujiamulia mambo yetu wenyewe.

Vijana hata wazee tunaishi kwa woga sana, hakika hii ni dhambi.
Huwa najisemea moyoni Ole wetu sisi tunaoujua ukweli wa mambo, tunaofahamu sababu za hawa wanyonyaji wetu kutumia nguvu nyingi kuziba na kukandamiza matwaka yetu halafu tukakaa kimya.
 
Ndugu,
Tatizo la watu kama wewe mnaziangalia siasa za Uingereza mkiwa nje na kuanza kujenga hoja ambazo hazina ukweli kiuharisia na kimantiki. Unatakiwa uzichambue kwanza katika historia yake na hali ilivyo kwa sasa.

Bila kufanya uchambuzi fasaha unajenga hoja kama hii hapa chini kutaka kuwaaminisha wanaJF,
HOJA POTOFU ZA WATANZANIA
Kwamba, Scotaland imemua kubaki katika muungano.
Ukweli ni kuwa imeabaki kwa masharti ya kutimiziwa madai yao ikiwa ni kuwapa mamlaka kamili

Mamlaka hayo ndiyo yatabadili muundo wa muungano wa Uingereza kutoka
Unitary system kwenda quasi federalism na kuelekea katika federation kamili
Waliokuwa wanataka uhuru kamili ni viongozi wa SNP ambao walijiunga na wananchi wengine katika mwanvuli wa harakati wanaouita Scottish nationalism.

Hoja ya Mamlaka kamili ilikataliwa na wananchi wengi katika kura ya maoni. Wewe bado unaongelea Mamlaka Kamili.

Hoja yako haitofautiani na madai ambayo yamekuwa yanatolewa na baadhi ya wanasiasa nchini walionukuliwa katika mikutano ya hadhara wakidai wanataka Zanzibar na Tanganyika zipewe MAMLAKA KAMILI.

Baadhi ya wanasiasa wa kikundi kinachojiita UKAWA walinukuliwa wakisema,

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA na UKAWA katika mkutano wa Aprili 30, 2014, pamoja na mambo mengine, alinukuliwa na gazeti la Mwananchi la Mei mosi, 2014 akiwaeleza wananchi wa Zanzibar kuwa: "Ni jambo la hatari katika mchakato wa Katiba ya wananchi kuwa na woga au hofu…Lazima tuwe tayari kuwaonyesha watawala kuwa tuna umoja imara, tunapigania mataifa huru ya Tanganyika na Zanzibar".

Katika mkutano huo huo, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA na mjumbe muhimu wa UKAWA, Tundu Lissu, alinukuliwa na gazeti la Tanzania Daima la Mei mosi, 2014 akiwaambia wananchi kuwa: "Kwa sababu Zanzibar haijawa huru na Tanganyika haijawa huru na ukitaka kujua ukweli wa hili angalia vitabu, kuna jina Tanganyika limefutwa ili kuitawala Zanzibar, sasa inabidi tuseme ili kuleta uhuru wetu". Lissu aliendelea kusema; "Zanzibar inatakiwa kuwa mamlaka kamili".

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alinikuliwa pia na gazeti la Tanzania Daima la Mei mosi, 2014 akisema kuwa atawashawishi wananchi kutetea mfumo wa serikali mbili iwapo kutakuwa na Zanzibar huru na Tanganyika huru.
Kuanza kujenga hoja katika msingi wa kitaifa na kuondoa uchama kwenye siasa za Uingereza ni kupotosha au kutokuzifahamu siasa za Uingereza.

David Cameron hakukubali kufanyika Kura ya maoni kwa sababu ya kusukumwa na mstakabali wa kitaifa bali kwa sababu ya kupambana na chama cha Labour.

Chama cha Labour ambao ni waanzilishi wa devolution nchini Scotland hawakutaka kufanya kura ya maoni badala yake waliamua kuwapa madaraka zaidi lakini waendelee kuwa sehemu ya Muungano kwa sababu Scotland ni ngome yao katika maamuzi ya Westminster.

Kwanza lazima uelewe kuwa chama cha conservative kina mbunge mmoja tu anayetoka Scotland katika Bunge (Westminister) wakati Labour wana Wabunge kama 40, kwa maana kuwa chama cha conservative hakikubaliki Scotland.

Kujitenga kwa Scotland kungenufaisha chama cha Conservative katika bunge la Westminister zaidi ya Labour Party, ndiyo maana kwa sasa unamsikia David Cameron akisema anapenda kuwepo na English votes for English laws, kwa maana kuwa, masuala ya England yawe yanaamuliwa na wabunge wa England ambao kiuharisia, wabunge zaidi ya 40 wa Labour kutoka Scotland hawataruhusiwa kuamua masuala hayo. Kama hili litakubaliwa, basi chama cha Labour hakitakuwa na wabunge wengi watakao weza kupitisha maamuzi ya serikali itakayoundwa na chama cha Labour.

Chama cha Conservative kilikuwa na win win situation katika matokeo ya Kura ya Maoni na siyo kusema kilisimama katika msingi wa utaifa. Conservative walisimama katika msingi wa kichama, vivyo hivyo, Labour nao walisimama katika msingi wa Uchama ndiyo maana wanasiasa kutoka Labour ndiyo walikuwa wanapigana kihoja kwa hali na mali ili Scotland ibakie katika Muungano huku wanasiasa wa Conservative wakiwa wamekaa pembeni wakichekelea mtifuano.

Kinachofanyika katika suala la Scotland ni party politics ambazo kwa mtu asiye chambua kwa undani hawezi kuelewa.

Unafahamu kinachoendelea kwa sasa kuhusu suala hili kwenye Mkutano Mkuu wa Labour huko Manchester?
 
Tatizo lililopo ni kuwa bado Watz hawajaweza kujitawala mpk leo wanataka waendelee kutawaliwa.

Leo akitokea kiongozi wa ulaya na kuisema Tz ifanye nini au ichukue hatua gani kuhusu katiba mpya utaona kitakachoendelea.

Ama kwa sasa tusubiri tuone vyama vikuu vimeanza kuwa na waasi na hujuma za hapana pale pia hilo linaweza kuleta mabadiliko lakini sio kwa kumsubiri 6 atake hilo ni never.
 
Nguruvi3,
Mkuu wangu wewe na Mchambuzi mumeamua kuwapotosha wananchi vibaya sana na kwa sababu hawaelewi wamekubali kuwa misukule wakitumikia wasichokielewa.

Swala la Scotland linafanana sana na swala letu kwa madai ya nchi ya Scotland japo sisi tuko mbele yao kidogo na hivyo ni serikali ya England kujifunza kutoka kwetu. Changes zitakazo fanyika sisi tayari zimekwisha fanyika na ndizo zinawatpa taabu kwa sababu Scotland walichotaka ni kuondosha mamlaka ya serikali kuu kukusanya kodi badala yake wapewe wao kisha wachangie mfuko wa taifa.

Scotland walichotaka pia ni wao kuwa wasimamizi wa shughuli zote zinazohusiana na huduma za wananchi wake (social welfare) mamlaka ambayo yapo chini ya serikali kuu hivyo hizi changes hazina mahusiano yoyote na kuundwa kwa serikali ya shrikisho ama kuwa na serikali 5 zinazounda UK. Na kwa nini Scotland wametaka hivyo? - ni kutokana na kuwepo mafuta na gas nchi mwao hivyo wanachokitaka kwa kila pato la kodi zao mfano corporate tax wawe na asilimia yao, halafu wachangie mfuko wa Taifa badala ya fedha zote kuwa mfuko wa Muungano kisha wakatiwe baada ya kuzingatia mahitaji ya nchi nne zilizopo katika muungano. Na haya ndio pia yalopelekea Zanzibar kuendeleza madai zaidi juu ya mapato yatokanayo na gas na mafuta jambo ambalo wao wanadai hawapewi kitu kutoka bara.

Nimekwisha kukwambia ni rahisi sana kuwalalamikia Zanzibar kwa haya lakini haya yalifanyika baada ya makubaliano baina ya CCM na serikali ya Zanzibar kupewa mamlaka hayo (kina Cameron wetu) jambo ambalo sisi tulitakiwa kulizungumzia toka mwaka 2010 bungeni na sio vinginevyo. Na wala matatizo yake hayakuanza jana ila toka mwaka 1984 tulipobadilisha mfumo wa kiuchumi kutoka Ujamaa kwenda Ubepari tukapotea kuunda mfuko wa pamoja kukusanya mapato ya taifa, hivyo Zanzibar wasingeweza kuchangia kitu ambacho hakipo wala hakuna sheria inayosema watachangia asilimia ngapi ya makusanyo yao.

Tofauti na sisi Ungereza wakifanya hivyo wataweka tofauti ya mifuko hivyo Scotland watalazimika kuchangia moja kwa moja mfuko huo wa pamoja kwa silimia itakayo wekwa na vile vile yawezekana likaondolewa ktk sheria mama ili kila upande utakusanya kodi zake na kuchangia mfuko wa Pamoja ni swala la maridhiano kwa washirika wote yatafuatia. Na hakuna kigumu hapa kabisa ikiwa kesho bunge letu la katiba litakubaliana kuweka asilimia fulani kwa kila kodi kuingia mfuko wa pamoja halafu kila upande utajadili na kupanga asilimia yake.

Tuacheni hizi habari za Siasa kutumia jukwaa hili kutangaza vitu ambavyo vitawapotosha wananchi na kuwa misukule ya chama badala ya kutazama mustakabali wa Taifa letu. Tujifunze kwa mema badala ya kuzua uhasama usokuwa na maana kabisa kwani kesho maneno haya yatakuja wahukumu nyie mlowalisha wananchi haramu hizi.
 
Ukiacha unazi na husda haya ndiyo mambo ya kujifunza Pongenzi kwako Nguruvi3, Mchambuzi ............Uzalendo wa kweli ndiyo silaha pekee kwa muungano wetu.........tusemezane................tuambiane ukweli...................unawatisha wenzako wasiseme ukweli ili iweje na kwa faida ya nani.....? nina uchungu sana............................!!!!Kwenye historia ya siasa maandiko yenu ni dhahabu iliyo wazi..............
 
Tuacheni hizi habari za Siasa kutumia jukwaa hili kutangaza vitu ambavyo vitawapotosha wananchi na kuwa misukule ya chama badala ya kutazama mustakabali wa Taifa letu. Tujifunze kwa mema badala ya kuzua uhasama usokuwa na maana kabisa kwani kesho maneno haya yatakuja wahukumu nyie mlowalisha wananchi haramu hizi.

Mkuu wangu Mkandara, kwa Tanzania bila ya Tanganyika na zanzibar kuwepo ni kujipa faraja ambayo ndani ya nafsi unajua kabisa ni bomu linaloweza lipuka wakati wowote.........Hili linahitaji marekebisho.......Uwepo wa Tanganyika utakuwa dhambi mkuu.......?
 
Mkuu wangu Mkandara, kwa Tanzania bila ya Tanganyika na zanzibar kuwepo ni kujipa faraja ambayo ndani ya nafsi unajua kabisa ni bomu linaloweza lipuka wakati wowote.........Hili linahitaji marekebisho.......Uwepo wa Tanganyika utakuwa dhambi mkuu.......?
Kuwepo wa Tanganyika ni swala la sisi wenyewe kujitangaza kama England inavyofanya. Tuwe na wana michezo wetu, ligi yetu iitwe ligi ya Tanganyika, taifa Stars ijulikane kama ni ya Tanganyika na mengineyo mengi ambayo tunaweza kuyatenganisha kiasi kwamba wewe kesho ukiulizwa unatoka wapi sema Tanganyika. Lakini tukubali pia Wazanzibar wawe na timu zao na wanamichezo wao kuiwakilisha Zanzibar kama tunaona ni sifa kwetu.

Mbona Waingereza (England) wameweza wakati hawana serikali yao kiasi kwamba huku duniani tunaiita UK nzima ni Uingereza, Sisi tunashindwa nini hadi kudai serikali kana kwamba serikali ndio kutupa jina. Nani huko Bongo anajua kuna serikali ya Wyoming Marekani? sii mpaka wapekue ramani..na hata ukiijua nani mwenye kutaka kuijua na ili iwe nini? Jina Marekani linatosha ni jina kubwa zaidi ya nchi zake..
Kama Wazanzibar wanajiita wao Wazanzibar, am good with Mtanzania maana ndiyo yenye jina kubwa huko nje kuliko Zanzibar ama Tanganyika, am proud of it - Mtanganyika limekaa kama Mgagagigikoko! lol!
 
Ndugu,
Tatizo la watu kama wewe mnaziangalia siasa za Uingereza mkiwa nje na kuanza kujenga hoja ambazo hazina ukweli kiuharisia na kimantiki. Unatakiwa uzichambue kwanza katika historia yake na hali ilivyo kwa sasa.

Bila kufanya uchambuzi fasaha unajenga hoja kama hii hapa chini kutaka kuwaaminisha wanaJF,

Waliokuwa wanataka uhuru kamili ni viongozi wa SNP ambao walijiunga na wananchi wengine katika mwanvuli wa harakati wanaouita Scottish nationalism.

Hoja ya Mamlaka kamili ilikataliwa na wananchi wengi katika kura ya maoni. Wewe bado unaongelea Mamlaka Kamili.

Hoja yako haitofautiani na madai ambayo yamekuwa yanatolewa na baadhi ya wanasiasa nchini walionukuliwa katika mikutano ya hadhara wakidai wanataka Zanzibar na Tanganyika zipewe MAMLAKA KAMILI.

Baadhi ya wanasiasa wa kikundi kinachojiita UKAWA walinukuliwa wakisema,



Kuanza kujenga hoja katika msingi wa kitaifa na kuondoa uchama kwenye siasa za Uingereza ni kupotosha au kutokuzifahamu siasa za Uingereza.

David Cameron hakukubali kufanyika Kura ya maoni kwa sababu ya kusukumwa na mstakabali wa kitaifa bali kwa sababu ya kupambana na chama cha Labour.

Chama cha Labour ambao ni waanzilishi wa devolution nchini Scotland hawakutaka kufanya kura ya maoni badala yake waliamua kuwapa madaraka zaidi lakini waendelee kuwa sehemu ya Muungano kwa sababu Scotland ni ngome yao katika maamuzi ya Westminster.

Kwanza lazima uelewe kuwa chama cha conservative kina mbunge mmoja tu anayetoka Scotland katika Bunge (Westminister) wakati Labour wana Wabunge kama 40, kwa maana kuwa chama cha conservative hakikubaliki Scotland.

Kujitenga kwa Scotland kungenufaisha chama cha Conservative katika bunge la Westminister zaidi ya Labour Party, ndiyo maana kwa sasa unamsikia David Cameron akisema anapenda kuwepo na English votes for English laws, kwa maana kuwa, masuala ya England yawe yanaamuliwa na wabunge wa England ambao kiuharisia, wabunge zaidi ya 40 wa Labour kutoka Scotland hawataruhusiwa kuamua masuala hayo. Kama hili litakubaliwa, basi chama cha Labour hakitakuwa na wabunge wengi watakao weza kupitisha maamuzi ya serikali itakayoundwa na chama cha Labour.

Chama cha Conservative kilikuwa na win win situation katika matokeo ya Kura ya Maoni na siyo kusema kilisimama katika msingi wa utaifa. Conservative walisimama katika msingi wa kichama, vivyo hivyo, Labour nao walisimama katika msingi wa Uchama ndiyo maana wanasiasa kutoka Labour ndiyo walikuwa wanapigana kihoja kwa hali na mali ili Scotland ibakie katika Muungano huku wanasiasa wa Conservative wakiwa wamekaa pembeni wakichekelea mtifuano.

Kinachofanyika katika suala la Scotland ni party politics ambazo kwa mtu asiye chambua kwa undani hawezi kuelewa.
Unafahamu kinachoendelea kwa sasa kuhusu suala hili kwenye Mkutano Mkuu wa Labour huko Manchester?
MwanaDiwani,

Kwanza, Usichanganye Watu kwa kujadili suala la kudai "mamlaka kamili" Kama vile ni sawa na suala la kutaka "kujitenga". Hivi ni vitu viwili tofauti Kabisa. Kaeni mkidanganyana Huko huko kwenye vikao vya chama, sio kutuletea upuuzi huu Kama vile kila mwananchi ni mjinga. Suala la "mamlaka kamili" ndani ya shirikisho sio tatizo, badala yake it's an asset to a federation kwani wananchi get to experience the best of both worlds, on the one hand, "shared Ruled" chini ya a national government, and on the other hand, "self rule", chini ya subnational government(s). Kwa mama nyingine Rahisi, ndani ya mfumo wa shirikisho, kila mshirika Anakuwa na mamlaka yake kamili Katika mambo ambayo hayapo Katika ushirikiano. Hii Ndio maana ya:

1. Fiscal autonomy.
2. Policy autonomy.
3. Political autonomy.


Tukiangalia Hapa kwetu, mshirika mmoja wa muungano yani- Zanzibar, tofauti na mshirika mwenza (Tanganyika), Zanzibar amepewa autonomy Katika maeneo haya. Kwa mfano, Zanzibar Ina:

1. Bajeti yake nje ya bajeti ya muungano.
2. Ina national Economic plan and policies nje ya muungano (mfano MKUZA vis a vis MKUKUTA)
3. Ina Dira yake ya taifa - vision 2020, tofauti na Ile ya muungano (na Tanganyika) ya vision 2025.
4.Ina chagua viongozi na wawakilishi wao nje ya siasa na chaguzi za muungano.

Etcetera.

Scotland iliyapigiania haya na kupewa serikali yake na bunge lake mwisho wa miaka ya tisini. Je tatizo likawa wapi hadi kupeleka kura ya maoni? Tutaelimishana:

Kama ulikuwa haujui, ujio wa kura ya maoni Scotland ulishaonekana miaka zaidi ya kumi iliyopita. Fanya utafiti, usipotoshe Watu. Pamoja na devolution kutokea Katika maeneo husika, Scotland bado hawakuridhika Kwa sababu kuu Mbili:

1. Uncertain future ya UK in the EU. Na utata juu ya Hilo unaweZa kuzaa Tena kura nyingine ya maoni Scotland muda sio mrefu, hasa iwapo UK wataamua kutojiunga na EU. Tuna tatizo Kama Hilo ndani ya muungano wetu kuhusiana nchi washirika and regional intergrarion but let's save this discussion for next time.

2. Pili ni Kwamba pamoja na Devolution to Scotland (serikali na bunge), bado kukawa na tatizo kwani it was more like a self-governing colony arrangement, kufikia kiwango cha kuwa na judicial appeals to the Privy Council katika masuala ya kikatiba. Hata ndani ya muungano wetu, tuna mgogoro mkubwa sana kuhusiana na judiciary issues but also on this one, leta save it for some other day.

Kutokana na haya, lakini hasa hili la pili, mgogoro mkubwa in the union UK was imminent. Lakini kwa vile wenzetu wana uongozi bora (sio sisi wenye bora uongozi) na wanaweka Maslahi ya nchi Mbele, haiku chukua muda mrefu, Wanasiasa wengi wa UK bila ya kujalisha itikadi zao za vyama, wakaanza kuona kwamba ‘an independent Scotland’ was a real possibility kupitia kura ya maoni, na hii ilikuwa miaka kumi iliyopita. Again, the referendum for independence was noted over ten years ago. Ndio maana viongozi wakaanza kulifanyia kazi suala Hilo na kuambulia 55% "NO". Lakini Kama alivyojadili mleta mada, no vote didn't mean no to change Kama mnavyopotosha.

Katika suala la misimamo ya chama juu ya devolution ya Scotland, hili nalo unapotosha. Kumbuka, viongozi wa upinzani wakati wa Utawala wa Labour Party - 1997 to 2010, (wapinzani wakiwa ni Conservatives), awali they voted against devolution of scotland, lakini baada ya kusoma alama za nyakati, wakaamua kuachana na itikadi na badala yake kuweka utaifa mbele, na wakaamua kuungana na chama cha Labour kuhakikisha kwamba muungano unadumishwa through more devolution. Ni kwa mantiki hii, suala la devolution limekuwa a bipartisan issue Katika siasa za Uingereza. Hata katika elections manifestos za vyama vinavyounda coalition government ya sasa, suala la devolution lilikuwa at the fire front. Nenda kafanye utafiti utaona Hilo. Vyama vyote Vikuu nchini Uingereza vina msimamo mmoja, nao ni Kwamba muungano wa UK utadumishwa kwa kutoa mamlaka kamili kwa washirika wa muungano Katika masuala nje ya muungano - fiscal, policy and political autonomy.

Acha porojo zako juu ya nini kinaendelea Manchester. Hakuna chama kinachopinga "devolution", wanachopishana pengine ni the means to get there, basi.










Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: ral
Kuwepo wa Tanganyika ni swala la sisi wenyewe kujitangaza kama England inavyofanya. Tuwe na wana michezo wetu, ligi yetu iitwe ligi ya Tanganyika, taifa Stars ijulikane kama ni ya Tanganyika na mengineyo mengi ambayo tunaweza kuyatenganisha kiasi kwamba wewe kesho ukiulizwa unatoka wapi sema Tanganyika. Lakini tukubali pia Wazanzibar wawe na timu zao na wanamichezo wao kuiwakilisha Zanzibar kama tunaona ni sifa kwetu.

Mbona Waingereza (England) wameweza wakati hawana serikali yao kiasi kwamba huku duniani tunaiita UK nzima ni Uingereza, Sisi tunashindwa nini hadi kudai serikali kana kwamba serikali ndio kutupa jina. Nani huko Bongo anajua kuna serikali ya Wyoming Marekani? sii mpaka wapekue ramani..na hata ukiijua nani mwenye kutaka kuijua na ili iwe nini? Jina Marekani linatosha ni jina kubwa zaidi ya nchi zake..
Kama Wazanzibar wanajiita wao Wazanzibar, am good with Mtanzania maana ndiyo yenye jina kubwa huko nje kuliko Zanzibar ama Tanganyika, am proud of it - Mtanganyika limekaa kama Mgagagigikoko! lol!
Bulicheka..................umenikumbusha mbali sana............................!
 
Back
Top Bottom