Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,200
- 10,948
Kila siku zinavyokwenda mashambulizi ya Houth dhidi ya Israel na washirika wake yanazidi kupamba moto.
Hali hiyo inaongeza mashaka juu ya uwezo na athari ya yale mashambulio ya kila mara yanayofanywa na meli za kivita za Marekani na Uiengereza.
Meli kubwa ya mizigo iliyopigwa Jumatatu inakisiwa kuwa imezama tayari.
Siku mbili baadae hapo mapema leo meli nyengine ya mizigo ambayo nayo ina uhusiano na Uiengereza imepigwa na kuwaka moto.
Uwezo wa kurusha makombora ya ballisitic wa Houth haujatetereka hata kidogo kwani kombora la leo limeweza kupenya mpaka mji wa kusini wa bandari wa Israel wa Eliot.
Israel imetangaza kuliwahi kombora hilo angani kwa mfumo wake wa ulinzi wa angani.
Siku za mwanzo za kuanza kwa mashambulizi ya Houth mfumo wa ulinzi wa anga wa Saudia uliwahi kuyatungua makombora hayo ya Houth yasielekee Israel.
Makombora ya Houth kuelekea Israel ni lazima yatambao magharibi mwa Saudi Arabia au yaruka juu yake.
Hata hivyo Katika siku za karibuni kazi ya kupambana na makombora hayo imeachiwa Israel ifanye peke yake.
Muhimu katika mabadiliko haya na ukali unaopanda wa wanamgambo wa Houth katika kuitetea Palestina ni kuwa ama meli za kivitaj baharini haziwezi kupigana kikamilifu na mbabe yeyote anayepigana kutoka ardhini.
Au meli hizo zimeishiwa na zana za kuendelea na vita na au vyenginevyo Houth ameanza kupokea misaada ya silaha kutoka mataifa mengine hasimu na Marekani mbali na misaada ya kutoka Iran.
Uwezekano wa mwisho ni kuwa nchi kama Saudi Arabia na Misri zimeanza kuunga mkono juhudi za Houth katika namna za sirij ikiwemo kutoshughulishwa na mashambulizi yao dhidi ya Israel na Marekani pindi yanapofanyika.
Hali hiyo inaongeza mashaka juu ya uwezo na athari ya yale mashambulio ya kila mara yanayofanywa na meli za kivita za Marekani na Uiengereza.
Meli kubwa ya mizigo iliyopigwa Jumatatu inakisiwa kuwa imezama tayari.
Siku mbili baadae hapo mapema leo meli nyengine ya mizigo ambayo nayo ina uhusiano na Uiengereza imepigwa na kuwaka moto.
Uwezo wa kurusha makombora ya ballisitic wa Houth haujatetereka hata kidogo kwani kombora la leo limeweza kupenya mpaka mji wa kusini wa bandari wa Israel wa Eliot.
Israel imetangaza kuliwahi kombora hilo angani kwa mfumo wake wa ulinzi wa angani.
Siku za mwanzo za kuanza kwa mashambulizi ya Houth mfumo wa ulinzi wa anga wa Saudia uliwahi kuyatungua makombora hayo ya Houth yasielekee Israel.
Makombora ya Houth kuelekea Israel ni lazima yatambao magharibi mwa Saudi Arabia au yaruka juu yake.
Hata hivyo Katika siku za karibuni kazi ya kupambana na makombora hayo imeachiwa Israel ifanye peke yake.
Muhimu katika mabadiliko haya na ukali unaopanda wa wanamgambo wa Houth katika kuitetea Palestina ni kuwa ama meli za kivitaj baharini haziwezi kupigana kikamilifu na mbabe yeyote anayepigana kutoka ardhini.
Au meli hizo zimeishiwa na zana za kuendelea na vita na au vyenginevyo Houth ameanza kupokea misaada ya silaha kutoka mataifa mengine hasimu na Marekani mbali na misaada ya kutoka Iran.
Uwezekano wa mwisho ni kuwa nchi kama Saudi Arabia na Misri zimeanza kuunga mkono juhudi za Houth katika namna za sirij ikiwemo kutoshughulishwa na mashambulizi yao dhidi ya Israel na Marekani pindi yanapofanyika.