Sasa ni rasmi: Serikali Imeishiwa

Sasa ni rasmi: Serikali Imeishiwa

Serikali kupitia TRA wanawapa wafanyabiashara tax demand notes za miaka ya nyuma mno. Nimeona kwa macho yangu mtu "anadaiwa" kodi (na kuongezewa riba na adhabu juu) kuanzia alipofungua kampuni 2006.

Nchi hii inaelekea kubaya zaidi ya Zimbabwe ya Mugabe.
Kama kweli hawajalipa lazima walipe tu, kama uliuwa mtu miaka ya 70 au 80 na ikajulikana ulifanya huo unyama lazima ushtakiwe tu, haijalishi kama ni miaka ya nyuma au mbele..
 
Kama kweli hawajalipa lazima walipe tu, kama uliuwa mtu miaka ya 70 au 80 na ikajulikana ulifanya huo unyama lazima ushtakiwe tu, haijalishi kama ni miaka ya nyuma au mbele..

Kama angekuwa ni kweli hajalipa unadhani angelalamika?
 
I doubt kuwa unajua public entities zinafanyaje kazi nchi hii. Unajua kisheria limit ya kudai (assuming kweli kuna deni la kudaiwa) ni miaka mingapi? Unajua limit ya kuweka rekodi?
Deni la mzungu (wa kukamata ndege) ni la miaka mingapi vile!?
 
Tatizo la humu mkuu watoto ni wengi sana,. Utawajua kwa uchanga wa akili zao,. Hata kujua kwa nini unapewa Tax clearance hilo nalo kwao ni tatizo,
Ulichoonge ni kweli kuna watu hawajui kitu wao ni kushabikia tu ni ajabu MTU hajui maana ya tax clearance
 
Tatizo lako mleta mada hutaki kuheshimu maoni ya wengine. Unataka kila mtu awe na mtazamo wako. Sasa kama unajua kila kitu unalalamika nini si utumie ujuaji kutatua hilo tatizo?

Kila kitu kina taratibu zake. Mimi nilipewa tax bill ya ajabu. Nilikaa nao tukaongea,tukagombana tukaelewana na tukafikia kiwango ambacho niliafiki na ninakilipa kwa awamu.

Nilivyokusoma unasema anaedaiwa ni mteja wako ina maana wewe ni auditor wake au mhasibu unajua tatizo liko wapi. Mara nyingine nyinyi ndio msingi wa matatizo ya Kodi ya wafanyabiashara wengi.

Na mbaya zaidi mtoa mada ni mbishi na inaonekana haelewi hii mambo. Anaongelea limit ya madeni na wakati huohuo anatoa mfano wa mkulima Stein aliyekopa enzi sijui za mwalimu huko na anakuja kudai leo, sasa sijui argument yake anaielewa kweli?
 
Alaaniwe alieuwa elimu ya kweli nchi hii hadi kufikia kupata watu waliokaririshwa. Hivi umeshindwa japo ku-google ukajionea kuwa huwa kuna statutory limit ya kumdai mtu? Tofautisha claims zilizofanywa na zinazofanywa. Kwa akili yako Mkulima Stein amewasilisha claims zake mwaka jana?
Kwa sheria za nchi hii; ikipita miaka 6 bila kudai deni limekufa.

Inaonekana wewe hatakuielewa sheria unayoiongelea huielewi. Kwa msaada nimekuwekea google snapshot ya hiyo unayoisema hapa “statutory limit ya deni” tena from the certain dispute,
Adjustments.JPG
soma kwanza na uielewe then uone kama ina reflect kile ulichokiandika na kukitetea hapa.
There’s a big difference in statutory limit of a debt when there is a contract/agreement and when there isnt.
 
Am sorry; but you have written here like an idiot. Mtu ana tax clearance kwa miaka yote hiyo utasemaje kuwa hakuwa analipa kodi? Acheni upumbavu wenu; nchi imeshawashinda.
Simple; nimemshauri mteja afunge kampuni. Mtamfanya nini sasa? Hata provisional tax yake (na huwa analipa minimum ya 15m) hatalipa akifunga biashara.

Wewe Mfiaukweli! Ukishaanza kutukana watu mitandaoni ndipo hoja yako inakuwa ya nguvu? Mwenzio katoa hoja yake kistaarabu wewe unajibu na kutukana eti ‘idiot’! Yaani umekuwa kama kijana ambaye hajapata balehe. Umeshindwa na wewe kujibu kistaarabu? Sasa ukishaanza kuporomosha tusi kama hivyo, unategemea humu ndani tukueleweje wewe? Hebu tujadiliane kwa staha mara zote jamani.
 
Inaonekana wewe hatakuielewa sheria unayoiongelea huielewi. Kwa msaada nimekuwekea google snapshot ya hiyo unayoisema hapa “statutory limit ya deni” tena from the certain dispute, View attachment 1332681soma kwanza na uielewe then uone kama ina reflect kile ulichokiandika na kukitetea hapa.
There’s a big difference in statutory limit of a debt when there is a contract/agreement and when there isnt.

Sasa kwenye situation niliyoileta hapa kuna contract gani? Tax payer amekuwa ana file returns miaka yote, TRA wamekuwa wanamfanyia tax audit muda wote na hakuna demand waliyompa all those years; so why demand anything now?

Na ulichokileta hapa kinahusiana vipi na tax management? Hebu soma hapa chini halafu urudi kutoa ufafanuzi.

Statute of limitations
There is a five-year time limit for the TRA to adjust an income tax return filed by a taxpayer. The five years runs from the due date of filing the final tax return
 
Wewe Mfiaukweli! Ukishaanza kutukana watu mitandaoni ndipo hoja yako inakuwa ya nguvu? Mwenzio katoa hoja yake kistaarabu wewe unajibu na kutukana eti ‘idiot’! Yaani umekuwa kama kijana ambaye hajapata balehe. Umeshindwa na wewe kujibu kistaarabu? Sasa ukishaanza kuporomosha tusi kama hivyo, unategemea humu ndani tukueleweje wewe? Hebu tujadiliane kwa staha mara zote jamani.

Nilitegemea Mkuu Msulushi uanze na huyo niliemjibu. Nina kawaida moja; namjibu mtu kulingana na alivyoniijia. Kuna watu humu wapo kujaribu kuzuia taarifa sahihi zisiwafikie watu; nisamehe sana lakini kwangu mimi hao watu hawastahili heshima kwa kuwa wao wenyewe wameamua kujidhalaurisha.
 
Mzungu alitupeleka mahakamani kisa deni la nyuma kabla ya jpm na watz waka comment dawa ya deni kulipa..kwann tumaowadai wasilipe?sheria ya kodi ipo tangu enzi za kale..kama hukulipa its on you not the government..
Serikali kupitia TRA wanawapa wafanyabiashara tax demand notes za miaka ya nyuma mno. Nimeona kwa macho yangu mtu "anadaiwa" kodi (na kuongezewa riba na adhabu juu) kuanzia alipofungua kampuni 2006.

Nchi hii inaelekea kubaya zaidi ya Zimbabwe ya Mugabe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nonsense..... Kwann Watanzania hatupendi kulipa kodi? Afu ni lini TRA walitunga sheria za kodi? Wakulaumiwa ni BUNGE wao hutunga then TRA hufata. Tuache lawaza bhana watu hatulali kukusanya pesa ili mpate hizo barabara na shule lakini kuna kundi la watu huona kama hakuna kifanyikacho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza kurudia kusoma utumbo wako ulioandika , kuna mtu anakataa kulipa kodi au mazingira ya kodi ni mabovu na kodi ni kandamizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na mbaya zaidi mtoa mada ni mbishi na inaonekana haelewi hii mambo. Anaongelea limit ya madeni na wakati huohuo anatoa mfano wa mkulima Stein aliyekopa enzi sijui za mwalimu huko na anakuja kudai leo, sasa sijui argument yake anaielewa kweli?

Ninakujibu kwa mara ya mwisho kwa sababu moja tu: naamini kuna mtu/watu anae/wanaofuatilia hii issue (kwa kuwa ame/wamekutana nayo). Na uzoefu wangu binafsi umenifanya nitambue kuwa serikali kupitia idara na taasisi zake zinawaonea watu kwa kuwa wanajua watu wengi hawajui haki zao. Na bahati mbaya zaidi watu wanaoonewa wanaamini kila kitu wanachoambiwa na waonezi wao.

Hata huku mtaani huwa nawasaidia watu wengi (wakati mwingine free of charges) ili wapate haki zao lakini kwa wao kutimiza wajibu wao pia kwa matakwa ya kisheria.

Obviously; WEWE ni mmoja wa wale wanao mislead watu. Hapa ama ni kweli hujui au unajifanya huelewi tofauti ya essence kati ya deni la mkulima Stein kwa serikali na TRA kumdai mlipakodi kinyume cha sheria. I will explain kwa manufaa ya anaefuatilia kwa nia ya kujua (and on this I am 110% certain kuwa ndivyo sheria ilivyo unless ibadilishwe):

Mtu (hata taasisi) ikiwasilisha madai ya kulipwa deni lake within time limits huwa hakuna limitations ya hilo deni kulipwa mpaka litakapokuwa settled kwa namna ambayo wahusika wameridhia. Mkulima Stein aliwasilisha madai yake ndani ya muda, serikali haikuwahi kumlipa deni lake; kwa hiyo limitation ya kudai deni HAIPO. Lakini asingedai within stipulated time leo hii HAKUNA mahakama ambayo inge-entartain madai yake.

Kwa upande wa tax management ya nchi hii mlipakodi anaetakiwa ku-file returns anapaswa kufanya hivyo within six months tangu afunge hesabu zake za mwaka husika. Hesabu hizo zitawezesha computation ya tax liability (kama alipata faida kwa mwaka husika). Asipofanya hivyo kuna penalty na interests anazopaswa kulipa. Mlipakodi asipowasilisha returns zake na ama kulipa au kuingia makubaliano jinsi ya kulipa kodi inayotakiwa HAWEZI KUPATA TAX CLEARANCE.

Lakini TRA wana haki ya kukagua hesabu zilizowasilishwa na mlipakodi husika ili kujiridhisha kuwa hesabu zilikuwa sahihi (na kama kuna material omissions basi TRA watatoa additional assessment ambako pia kunaweza kuhusisha penalties na interests). Lakini TRA wapo limited kufanya tax audit ndani ya miaka 5 tangu returns zilipofanyika. Na ndio maana mfanyabiashara anapaswa kutunza source documents zake (invoices, receipts, contracts etc) kwa angalau miaka 5 kwa kuwa anaweza kudaiwa kuzionyesha anytime ndani ya miaka hiyo mitano (unless ni payroll related information maana hizo zina time limits tofauti).

Katika mazingira ya namna hii; aniambie mtu hapa (mie mbumbumbu) TRA wamepata wapi uhalali wa kumdai mtu "kodi" ya 2006 (miaka 14 iliyopita) ambae:
(a) amekuwa ana-file returns consistently miaka yote
(b) amekuwa anafanyiwa tax audit miaka yote na hajawahi kudaiwa chochote
(c) amekuwa anapata tax clearance kwa miaka yote.
 
Serikali kupitia TRA wanawapa wafanyabiashara tax demand notes za miaka ya nyuma mno. Nimeona kwa macho yangu mtu "anadaiwa" kodi (na kuongezewa riba na adhabu juu) kuanzia alipofungua kampuni 2006.

Nchi hii inaelekea kubaya zaidi ya Zimbabwe ya Mugabe.
Kweli aisee yani hata mishahara ya january hadi leo bado haijalipwa....
Hali ni tete

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo jamaa achaneni nae, kichwa yake mbovu. Nimeshatambua uwezo wake wa kuelewa unaishia wapi, so nakushauri Ngorunde achana na huyu mleta mada

Mimi "kichwa mbovu" nitaendelea kuwa "kichwa mbovu" kila kukicha (as long Mungu Jehovah ananipa uhai) ili niwaelimishe Watanzania wenzangu wajue haki zao.
Kwa hili NIMEJITOLEA.
 
Mimi "kichwa mbovu" nitaendelea kuwa "kichwa mbovu" kila kukicha (as long Mungu Jehovah ananipa uhai) ili niwaelimishe Watanzania wenzangu wajue haki zao.
Kwa hili NIMEJITOLEA.

Waelimishe basi ukweli usiwapotoshe mzee.
Tax limit ipo kisheria iwapo mdai (TRA) na mdaiwa (biznesman) watakuwa wameshaingia makubaliano ya kulipana na malipo yakaanza kufanyika. Sasa unapowaambia watu humu kuwa kuna limit ya kudai mtu (6yrs) na kwamba ikishapita huwezi kudai hapo ndipo unapopotosha mzee baba. Na ndio maana nikakupa mfano kwamba mbona wazee wa iliyokuwa East African community wanaidai serikali mpaka leo.. au yule mkulima mbona kaja kukamata ndege zetu ilhali deni lake lilishapita zaidi ya miaka hiyo 6?? Au serikali kulipa malimbikizo ya madeni ya watu mbalimbali hata zaidi ya 10 yrs, kwani hiyo sheria ni ya upande mmoja tu?
Kama mteja wako alifanyiwa tax audit na akawa cleared, lakini leo kaletewa deni kwanini umshauri afunge biashara ilhali anao ushahidi wa malipo ya kodi? TRA officers ni binadamu kama wewe au huyo mteja wako, so mshauri atoe nyaraka zake zote wakae chini na TRA, mbona mbivu na mbichi zitajulikana tuu.
Sasa kuendelea kubishana humu kwa jambo ambalo lipo wazi unaonekana unatetea bila mantiki. Lakini kama hiyo ndiyo jadi yako kiasili na unaipenda, basi mimi nanyanyua mikono juu niseme umeshinda wewe.
 
Waelimishe basi ukweli usiwapotoshe mzee.
Tax limit ipo kisheria iwapo mdai (TRA) na mdaiwa (biznesman) watakuwa wameshaingia makubaliano ya kulipana na malipo yakaanza kufanyika. Sasa unapowaambia watu humu kuwa kuna limit ya kudai mtu (6yrs) na kwamba ikishapita huwezi kudai hapo ndipo unapopotosha mzee baba. Na ndio maana nikakupa mfano kwamba mbona wazee wa iliyokuwa East African community wanaidai serikali mpaka leo.. au yule mkulima mbona kaja kukamata ndege zetu ilhali deni lake lilishapita zaidi ya miaka hiyo 6?? Au serikali kulipa malimbikizo ya madeni ya watu mbalimbali hata zaidi ya 10 yrs, kwani hiyo sheria ni ya upande mmoja tu?
Kama mteja wako alifanyiwa tax audit na akawa cleared, lakini leo kaletewa deni kwanini umshauri afunge biashara ilhali anao ushahidi wa malipo ya kodi? TRA officers ni binadamu kama wewe au huyo mteja wako, so mshauri atoe nyaraka zake zote wakae chini na TRA, mbona mbivu na mbichi zitajulikana tuu.
Sasa kuendelea kubishana humu kwa jambo ambalo lipo wazi unaonekana unatetea bila mantiki. Lakini kama hiyo ndiyo jadi yako kiasili na unaipenda, basi mimi nanyanyua mikono juu niseme umeshinda wewe.

Sishindani na wewe, (na sihitaji kushindana na mtu yeyote yule). Ila nitaendelea kuelimisha ukweli ninaoujua. As long as am alive and as long there are people who will be smart enough to understand what they should basi nimejitolea kufanya ninayoyafanya.
Tukubaliane kutokubaliana lakini Jehovah anajua nani anafanya haki kati yetu. Na anaesema UONGO hapa kwa kukusudia laana inayomstahili impate yeye na uzao wake WOTE hata kizazi cha tatu na cha NNE.
 
Ninakujibu kwa mara ya mwisho kwa sababu moja tu: naamini kuna mtu/watu anae/wanaofuatilia hii issue (kwa kuwa ame/wamekutana nayo). Na uzoefu wangu binafsi umenifanya nitambue kuwa serikali kupitia idara na taasisi zake zinawaonea watu kwa kuwa wanajua watu wengi hawajui haki zao. Na bahati mbaya zaidi watu wanaoonewa wanaamini kila kitu wanachoambiwa na waonezi wao.

Hata huku mtaani huwa nawasaidia watu wengi (wakati mwingine free of charges) ili wapate haki zao lakini kwa wao kutimiza wajibu wao pia kwa matakwa ya kisheria.

Obviously; WEWE ni mmoja wa wale wanao mislead watu. Hapa ama ni kweli hujui au unajifanya huelewi tofauti ya essence kati ya deni la mkulima Stein kwa serikali na TRA kumdai mlipakodi kinyume cha sheria. I will explain kwa manufaa ya anaefuatilia kwa nia ya kujua (and on this I am 110% certain kuwa ndivyo sheria ilivyo unless ibadilishwe):

Mtu (hata taasisi) ikiwasilisha madai ya kulipwa deni lake within time limits huwa hakuna limitations ya hilo deni kulipwa mpaka litakapokuwa settled kwa namna ambayo wahusika wameridhia. Mkulima Stein aliwasilisha madai yake ndani ya muda, serikali haikuwahi kumlipa deni lake; kwa hiyo limitation ya kudai deni HAIPO. Lakini asingedai within stipulated time leo hii HAKUNA mahakama ambayo inge-entartain madai yake.

Kwa upande wa tax management ya nchi hii mlipakodi anaetakiwa ku-file returns anapaswa kufanya hivyo within six months tangu afunge hesabu zake za mwaka husika. Hesabu hizo zitawezesha computation ya tax liability (kama alipata faida kwa mwaka husika). Asipofanya hivyo kuna penalty na interests anazopaswa kulipa. Mlipakodi asipowasilisha returns zake na ama kulipa au kuingia makubaliano jinsi ya kulipa kodi inayotakiwa HAWEZI KUPATA TAX CLEARANCE.

Lakini TRA wana haki ya kukagua hesabu zilizowasilishwa na mlipakodi husika ili kujiridhisha kuwa hesabu zilikuwa sahihi (na kama kuna material omissions basi TRA watatoa additional assessment ambako pia kunaweza kuhusisha penalties na interests). Lakini TRA wapo limited kufanya tax audit ndani ya miaka 5 tangu returns zilipofanyika. Na ndio maana mfanyabiashara anapaswa kutunza source documents zake (invoices, receipts, contracts etc) kwa angalau miaka 5 kwa kuwa anaweza kudaiwa kuzionyesha anytime ndani ya miaka hiyo mitano (unless ni payroll related information maana hizo zina time limits tofauti).

Katika mazingira ya namna hii; aniambie mtu hapa (mie mbumbumbu) TRA wamepata wapi uhalali wa kumdai mtu "kodi" ya 2006 (miaka 14 iliyopita) ambae:
(a) amekuwa ana-file returns consistently miaka yote
(b) amekuwa anafanyiwa tax audit miaka yote na hajawahi kudaiwa chochote
(c) amekuwa anapata tax clearance kwa miaka yote.

Mfiaukweli, ungekuwa umeanzisha uzi huu kwa maelezo haya ungepata uungwaji mkono mzuri tu na hata wakosoaji wasingekuwa wengi, mimi mwenyewe nikiwemo. Tatizo ulianzisha uzi kwa maelezo ambayo sio sahihi na ndio maana kila msomaji anaeelewa haya mambo hakukubalina nawe.
Btw kwa hoja hii sasa umejirekebisha na kutoa maelezo yenye mantiki ambayo nayaunga mkono kwa asilimia fulani 80% kwa kuwa hoja yako ni ya upande mmoja na hizo zilzobaki ni za upande wa TRA; maswali yangu ni haya:
1). Je ni kweli kuwa TRA walimpa tax clearance mteja wako throughout?
2). Je TRA hawakuwahi kumpa tax invoice mteja wako at any one time before the preceding clearances?
3). Kwanini sasa umshauri mteja wako afunge biashara ilhali anazo nyaraka zake za ukaguzi na malipo ya kodi? Unajua kabisa kuwa deni linatokana na audit iliyofanyika na si kwamba TRA wamekuja kutaka kufanya audit tena baada ya 14 bali wamemletea deni ambalo naamini lilitokana na auditing fulani lakini deni hilo halijalipwa

Maswali hapa ni mengi sana lakini nakushauri mwambie mteja wako awasilishe nyaraka zake kwa TRA na awaonyeshe kila kitu maana sitaki kuamini kama TRA watazikana hizo documents zao wenyewe (labda ziwe fake..)
Usimwambie afunge biashara manake inawezekana ana familia inayotegemea hiyo biashara na maendeleo ya kweli yanaletwa na biashara (katika nyanja zote)
 
Mhhhh
Sishindani na wewe, (na sihitaji kushindana na mtu yeyote yule). Ila nitaendelea kuelimisha ukweli ninaoujua. As long as am alive and as long there are people who will be smart enough to understand what they should basi nimejitolea kufanya ninayoyafanya.
Tukubaliane kutokubaliana lakini Jehovah anajua nani anafanya haki kati yetu. Na anaesema UONGO hapa kwa kukusudia laana inayomstahili impate yeye na uzao wake WOTE hata kizazi cha tatu na cha NNE.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfiaukweli, ungekuwa umeanzisha uzi huu kwa maelezo haya ungepata uungwaji mkono mzuri tu na hata wakosoaji wasingekuwa wengi, mimi mwenyewe nikiwemo. Tatizo ulianzisha uzi kwa maelezo ambayo sio sahihi na ndio maana kila msomaji anaeelewa haya mambo hakukubalina nawe.
Btw kwa hoja hii sasa umejirekebisha na kutoa maelezo yenye mantiki ambayo nayaunga mkono kwa asilimia fulani 80% kwa kuwa hoja yako ni ya upande mmoja na hizo zilzobaki ni za upande wa TRA; maswali yangu ni haya:
1). Je ni kweli kuwa TRA walimpa tax clearance mteja wako throughout?
2). Je TRA hawakuwahi kumpa tax invoice mteja wako at any one time before the preceding clearances?
3). Kwanini sasa umshauri mteja wako afunge biashara ilhali anazo nyaraka zake za ukaguzi na malipo ya kodi? Unajua kabisa kuwa deni linatokana na audit iliyofanyika na si kwamba TRA wamekuja kutaka kufanya audit tena baada ya 14 bali wamemletea deni ambalo naamini lilitokana na auditing fulani lakini deni hilo halijalipwa

Maswali hapa ni mengi sana lakini nakushauri mwambie mteja wako awasilishe nyaraka zake kwa TRA na awaonyeshe kila kitu maana sitaki kuamini kama TRA watazikana hizo documents zao wenyewe (labda ziwe fake..)
Usimwambie afunge biashara manake inawezekana ana familia inayotegemea hiyo biashara na maendeleo ya kweli yanaletwa na biashara (katika nyanja zote)

Utakuwa unaishi Tanzania tofauti na ninayoishi mimi (kwa mantiki hiyo TRA yako inafanya kazi rationally na kwa mujibu wa sheria zilizopo).
Lakini Tanzania niishiyo mimi (from practical point of view) TRA wanawabambikia taxpayers madai ya kodi ambayo siyo realistic. Na sio kuwa hawajui au ni bahati mbaya (ingekuwa nimeona kwa mtu mmoja wala nisinge-raise hii alarm lakini nimeona madai ya ajabu sana kwa watu wengi tu na yenye mwelekeo wa kufanya hivyo kwa makusudi).
Unauliza kuwa "nina uhakika TRA wamekuwa wanatoa tax clearance throughout", sasa ningekuwa na hoja gani kama hilo halikufanyika? Kwa nini nizushe jambo kama hilo? Ili nifaidike na nini kwa uzushi huo?
Kungekuwa na tax demand (iliyotolewa zamani), msingi wa hoja yangu ungekuwa nini sasa?

Kwamba nisimshauri mteja kufunga biashara "ila apeleke nyaraka TRA", unadhani hilo sijawahi kulifikiria kabla? (Kumbuka hii ni kazi yangu na ninaifanya siku nyingi tu na huo ndio utaratibu wa mwanzo kabisa).
Utakata rufaa kwa mtu yule yule aliekuonea halafu kukawa na uamuzi tofauti? Kama uonevu haukufanywa deliberately, ungefanyika in the first place?

Fact is: TRA wanafanya haya mambo kwa makusudi kwa kuwa sheria inasema hivi: mlipa kodi akiwa assessed na asiporidhika na hiyo assessment INAMBIDI alipe one third ya hiyo disputed amount ili objection yake iweze kusikilizwa. Kwa mantiki hiyo, mteja huyu "anaedaiwa" kodi ya kutoka 2006 (ambayo kwa kuwa HAIKUWAHI kudaiwa -hata kama ni kweli ilitakiwa kulipwa, na kusema ukweli kwa kesi hii HAKUNA any outstanding tax liability- KISHERIA HALIPO) anapaswa kulipa one third ili objection yake isikilizwe.
"Unamdai" mtu bilioni 2 wakati annual revenue yake haijawahi kufikia milioni 400 ataipata wapi one third ya hiyo amount?

Nielekeze option iliyopo zaidi ya kufunga biashara. Na kusema ukweli nimeshuhudia biashara nyingi tu zikifungwa kwa sababu hii. Don't take my words; kama unamfahamu mtu anaefanya kazi bank muulize idadi ya akaunti zinazofungwa sasa hivi vs zinazofunguliwa. Kama upo TRA fanya uchunguzi kidogo tu utajionea mwenyewe barua za kufunga biashara zinazowasilishwa (binafsi nimepeleka mbili tangu mwaka huu uanze peke yake).
 
Back
Top Bottom