Sasa ni Kanda ya Ziwa na Kusini Basi

Sasa ni Kanda ya Ziwa na Kusini Basi

Kweni mtu kwenda kwao maana yake waTanzania wengine siyo wa kwake?kwanza we mtoa mada kwenu wapi na ulienda lini kwa mala ya mwisho?misiba ya huko kwenu hua unahudhuria?tukikuchunguza tutakuta wewe ni mtu unatoa kibanzi cha jicho la mwenzio
 
Salaam Wakuu.
Takribani ni Mwaka mmoja toka Serikali ya Awamu ya 5 ishike hatamu naona Trip za Wakubwa zaidi kwanzia PM zaidi ya 90% ni Kusini, yaani Lindi na Mtwara, mathalani PM baada ya Kutoka tu Arusha Juma lililopita kapitiliza Mtwara na leo hii Ruangwa ambako ndiyo jimbo lake, ni zaidi ya mara 3 anashinda huko wakati kuna Mikoa hajakanyaga Kusikiliza Kero za Wananchi wao wenyewe maana ndiyo inatia Uzito. Ikumbukwe ni Waziri Mkuu na si Mbunge wa kawaida.

Naye Mkulu toka State House ndiyo Kabisaaa, ameenda Chato naye si Chini ya Mara 3 na leo yupo huko kwa kisingizio eti kaenda Msibani.Mbona Bukoba walikufa Watanzania na wengi zaidi na jirani na Chato ila hajawahi Kanyaga?

Kama wewe si wa Kusini ama Kanda ya Ziwa hususani Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Geita nje na Dar es Salaam utasubiri saana.Kumbuka Ukweli hisia huja zaidi baada ya Kujionea.

Aliyoyakataza Muasisi wa Taifa hili la Tanznaia Hayati; Mwl. JK Nyerere yaani, Ukabila, Ukanda na Udini yanarejea kwa Kasi ya Ajabu saana, kwa Pamoja wapenda Tanzania tuyapinge kwa nguvu zetu zote.
Utakwenda jela kama Lema endelea tuone
 
Labda 2020 kudanganya wakati wa Kuomba Kura.
Tatizo la Nchi hii ni wapiga Kura wasio na elimu na tume ya uchaguzi. Kimsingi watu wengi wamesha mkinai na kwahakika hawata mpa kura 2020 ila tume watasoma matukio kinyumenyume.
 
Unafikiri Angela Kairuki ni Mhaya!? Kalagabaho ubaki na Ubaguzi wako.
Ukitaka uzimie fuatilia wakurugenzi wa Halmashauri karibu asilimia 70 wanatoka kanda pendwa yaani karibu na inakotoka kofia. Mungu awape nini awamu hii?
 
nakumbuka kijamaa kilisema kinazunguka nchi nzima kuwashukuru waliompigia kura,alianza kanda ya ziwa akahusisha na baadhi ya mikoa along mwanza dar road tu..zenji alienda kumwaga sumu za fitna..
sijui mbeya tulikomzomea 2015 atakuja lini kutushukuru wapiga kura ?
Usihofu bado ana miaka 4 atakuja tu.
 
Mara 10 ya hyo
Mh. Pm muda wako, tupe raha wana kusin. Kusin oyeeee..!! KILWA hometown.
Me@raiahuru tz, Tabora 1 now.
 
Huu utawala ni wa fitina na ubaguzi lakini kamwe hii laana haitawaacha
 
Acheni kulalamika. Mlichagua wenyewe. Ukweli mimi sitaki tena kumlalamikia Rais. Watanzania walimchagua. Na hivyo walikubaliana nae. Tuwe wavumilivu tu. Inatia akili hiyo. Inafundisha pia usichague tu bila kufikiri. Next time mtatia akili kabla ya kuamua.
 
Pamoja na kua mimi sitoki huko kwenye hizo kanda natoka Kaskaz inayotupiwa mawe daily hapa jamvini ni ujinga kufikiri kua Rais na PM kwenda huko makwao ndio kupendelea,ukweli ni kua Rais hajaenda msibani bali yupo ktk mapumziko ya mwisho wa mwaka na Chato ndio nyumabani ulitaka akapumzike kwenu?vyombo vya habar vinasema toka hajaondoka so andiko lako ni uchochezi,pili PM nae yupo mapumzikoni huko Ruangwa ambapo ndio nyumbani vp ulitaka akapumzike Mbeya,acha uongo mkuu,mbona wachaga sisi tunaenda makwetu klm nyakati hizi na sio pengine?Lowassa akiwa PM alikua anaenda mapumzikoni Monduli na wamasai wote wanahamia kwake kuchinja wewe ulikua huoni au umeona mwaka huu,the same to Jakaya alikua anakwenda kupumzika Msoga kila mwisho wa mwaka vp unasemaje?au unafikiri ukishakua na cheo ndio kwenu huendi,na as long as washakua viongozi wetu lazma tukubali kubeba gharama hizo so acha kuwachonganisha viongozi na wananchi fanya kazi
 
Mkuu wewe ni typical mtanzania, yaani kichwa kigumu kuelewa na kujiongeza. Teuzi zimekuwa na uelekeo wa upande mmoja, ziara ndio huko unakosema, majanga ya wakulima na wafugaji hayajasemewa, tetemeko limetelekezwa, wengine wamebomolewa nyumba bila hata kauli ya kuwafariji ila machinga wa Mwanza waliotolewa waliko kinyume na sheria wakazuiliwa kuondolewa na viongozi wakaonesha wanajua hadi eneo la Kiloleli hakuna biashara. Hapo haujongelea fedha ya nini sijui ikajenge rami huko. Barabara niliyopita 1990 kule mbeya wakati naenda kuanza form one hadi leo tunabanana humo humo yaani toka Simike hadi Nzovwe kama una ka Vitz halafu kako chini kananata barabarani matairi yanabaki yanaelea. Nchi ina wenyewe saizi wanalipiza kaskazini walivyokula bata kwa hiyo kama hauko Ntwara Lindi, hauko Kaskazini ambako wameshiba tayari na hauko Ziwa ambako ndio zamu yao kula, ishia kuchekea chooni tu
Umeandika uongo uliopitiliza,hawa watu hawapo ziarani acheni kupotosha kwa maksudi wapo likizo,wewe xmass umeenda kwenu ulitaka wakiwa likizo waje kwako acha umbea
 
Salaam Wakuu.
Takribani ni Mwaka mmoja toka Serikali ya Awamu ya 5 ishike hatamu naona Trip za Wakubwa zaidi kwanzia PM zaidi ya 90% ni Kusini, yaani Lindi na Mtwara, mathalani PM baada ya Kutoka tu Arusha Juma lililopita kapitiliza Mtwara na leo hii Ruangwa ambako ndiyo jimbo lake, ni zaidi ya mara 3 anashinda huko wakati kuna Mikoa hajakanyaga Kusikiliza Kero za Wananchi wao wenyewe maana ndiyo inatia Uzito. Ikumbukwe ni Waziri Mkuu na si Mbunge wa kawaida.

Naye Mkulu toka State House ndiyo Kabisaaa, ameenda Chato naye si Chini ya Mara 3 na leo yupo huko kwa kisingizio eti kaenda Msibani.Mbona Bukoba walikufa Watanzania na wengi zaidi na jirani na Chato ila hajawahi Kanyaga?

Kama wewe si wa Kusini ama Kanda ya Ziwa hususani Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Geita nje na Dar es Salaam utasubiri saana.Kumbuka Ukweli hisia huja zaidi baada ya Kujionea.

Aliyoyakataza Muasisi wa Taifa hili la Tanznaia Hayati; Mwl. JK Nyerere yaani, Ukabila, Ukanda na Udini yanarejea kwa Kasi ya Ajabu saana, kwa Pamoja wapenda Tanzania tuyapinge kwa nguvu zetu zote.
Huu uzi umeandikwa kinafiki sana. Kaka Kassim alikuwa Arusha ambapo amekaa wiki nzima akishughulikia suala la faru John na mengine ya kiserikali. Ina maana Arusha ndipo alipozaliwaa waziri mkuu?.
 
Pm amezuru kwao mara 4 ndani ya mwaka 1.
> mara ya kwanzai....akatoa kauli ya kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa.
>mara ya pili ...akakagua shule ya sekondari iliyo ungua.
>mara ya 3 ...akafungua duka la msd
>mara ya 4 ndo sasa.

mbona mikoa mingine hajakanyaga hata mara 1?
Halafu wajinga wajinga wanasapoti ujinga kama huu. Ukanda na Ukabila vitatugawa hakika.
 
Back
Top Bottom