Sasa ni Kanda ya Ziwa na Kusini Basi

Sasa ni Kanda ya Ziwa na Kusini Basi

Tatizo ni kwamba hata hawa wanaopinga jpm kwenda kupumzika kwao ni wale ambao hawana utamaduni wa kwenda kutembelea ndugu zao huko vijijini walikotoka. Mtu ana uwezo lakini anakaa Dar miaka 15 hajawahi kwenda kwao kusalimia kisa yupo Dar utadhani kwao dar kumbe ni wa kuja tu kwao hukoooo! Hata marais wa Marekani na nchi nyingine zilizoendelea rais kwenda kwao kwa ajili ya mapumziko ya sikukuu hasa za kidini pamoja na mwaka mpya ni jambo la kawaida sana. Hata Nyerere mwenyewe alikuwa anakwenda kwao butuama mara kwa mara kupumzika pale alipokuwa anapata nafasi ya kufanya hivyo. Mzee wa msoga ndio usiseme mara nyingi tu alikuwa anazuka msoga kusalimia. MBONA JAMBO LA KAWAIDA SANA SISI MIAFRIKA BWANA NDIO MAANA TUNAZIDI KUWA MASKINI KWA SABABU YA ROHO MBAYA NA CHUKI ZISIZO NA SABABU!
Ni wa kusamehewa bure hujui ulichokiandika ni kama ukeandikiwa vile. Jaribu kujiuliza mpaka sasa huyo Rais ni maeneo gani kaenda zaidi pia PM na wakati kuna maeneo hata hajakanyaga.
 
Kumbe bukoba hakuwahi kabisa kwenda kuwafariji wale wahanga dah..,any way labda akitoka chato ataenda
Thubutuuu! Haendi ng'o huko, labda akisoma comment hii kwaajili ya aibu.
 
Miaka 9 gani tena hiyo? Mbona unaongea kama una matatizo kichwani mkuu? Katiba gani inasema Rais ataongoza miaka 10 mfululizo? Hopeless kabisa wewe kiumbe.
Kwan katika historia ya Tanzania kuna rais yeyote ambaye amekaa madarakani miaka 5
Wote waliopita wamekaa miaka kumi
Au unadhan ye hapapendi ikulu
 
Kwan katika historia ya Tanzania kuna rais yeyote ambaye amekaa madarakani miaka 5
Wote waliopita wamekaa miaka kumi
Au unadhan ye hapapendi ikulu
Acha kuota mchana. Hakuna linalodumu milele.
 
Pm amezuru kwao mara 4 ndani ya mwaka 1.
> mara ya kwanzai....akatoa kauli ya kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa.
>mara ya pili ...akakagua shule ya sekondari iliyo ungua.
>mara ya 3 ...akafungua duka la msd
>mara ya 4 ndo sasa.

mbona mikoa mingine hajakanyaga hata mara 1?
 
Thamani ya bodaboda mia mbili na Ambulance 50 unaonaje ulinganifu wake?
Raisi tunampenda tutampa tena kura na mpasuke!! Yanajengwa madly dar huoni nongwa MTU kwenda kwao mnapata ajenda!!!!!!
 
Pm amezuru kwao mara 4 ndani ya mwaka 1.
> mara ya kwanzai....akatoa kauli ya kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa.
>mara ya pili ...akakagua shule ya sekondari iliyo ungua.
>mara ya 3 ...akafungua duka la msd
>mara ya 4 ndo sasa.

mbona mikoa mingine hajakanyaga hata mara 1?
Mcheza kwao hutunzwa
 
Raisi tunampenda tutampa tena kura na mpasuke!! Yanajengwa madly dar huoni nongwa MTU kwenda kwao mnapata ajenda!!!!!!
Kwel kabsaa yaan hawa mtu kwenda kwao hata akienda mara mia si ni kwao
Mcheza kwao Hutunzwa
Rais wetu yuko tatizo walkuwa wamezoea kudeka
 
74771e74e6f3cbca1b2f9b5ca2a7d0fd.jpg
Mods huyu apigwe ban mwaka
 
Hivi kuna Waziri , Naibu Waziri toka Arusha NA Kilimanjaro
Mkoa wa Arusha na Kilimanjaro karibu majimbo yote yako upinzan sasa atachaguaje mawazir ama manaibu waziri ambao sio chama chake si kinyume na katiba?, but anyway toka nchi hii ipate Uhuru ukanda wa kaskazin from manyara, arusha plus Kilimanjaro wamekuwa wakitoa mawazir na manaibu wengi tu tena uwaziri mkuu ndio tusiseme utadhan nafasi hiyo ilikuwa preserved rasmi kwa watu wa ukanda huo tu. Mbona kipindi chote hicho watz hawakulalamika pale mikoa ama wilaya zao hazikupata mawazir ama manaibu ? Kwa sasa ndio m naona mnaonewa? Si shabiki wa ccm but UKWELI ubaki ulivyo mm ni mzalendo ambaye nilikuwa naumia sana baadhi ya mikoa ilipokuwa inapuuzwa huku mingine ikipewa kipaumbele
 
nakumbuka kijamaa kilisema kinazunguka nchi nzima kuwashukuru waliompigia kura,alianza kanda ya ziwa akahusisha na baadhi ya mikoa along mwanza dar road tu..zenji alienda kumwaga sumu za fitna..
sijui mbeya tulikomzomea 2015 atakuja lini kutushukuru wapiga kura ?
Kijamaa gani hicho mkuu?

Lugha sio ya kistaarabu. Huyo unayemzodoa hapa kwa kejeli ni Rais wetu...kama humtaki ni vema ukanyamaza...
 
Back
Top Bottom